Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu Gani Tuzungumuzie Miujiza?

Sababu Gani Tuzungumuzie Miujiza?

Sababu Gani Tuzungumuzie Miujiza?

RICHARD DAWKINS, MWALIMU WA ZAMANI WA SAYANSI KWENYE UNIVERSITÉ YA OXFORD, HUKO ANGLETERRE alisema hivi: “Miujiza, kama inavyoelezwa, inavunja kanuni za sayansi.”

ROBERT LARMER, MWALIMU WA FILOZOFIA KWENYE UNIVERSITÉ YA NEW BRUNSWICK, HUKO CANADA alisema hivi: “Kuamini miujiza ni jambo lenye kupatana na akili. Miujiza haipingane na mafundisho ya dini, lakini inaonyesha upendo wa Mungu kwa watu wake, na inaonyesha kama anaendelea kuwahangaikia.”

“JE, WEWE unaamini miujiza?” Maneno ya walimu hao yanaonyesha kama watu wana mawazo mbalimbali juu ya miujiza. Lakini, namna gani wewe ungejibu ulizo hilo?

Labda unaweza kusita kujibu kama unaamini miujiza. Labda unafikiri kwamba ukikubali kama unaamini miujiza utaonekana kuwa mutu anayeogopa mambo ya uchawi ya kuwazia tu ao utaonekana kuwa mutu ambaye hakusoma. Watu wengi wanafikiri hivyo.

Lakini, labda wewe unasadiki kabisa kama miujiza inafanyika; kama vile miujiza inayozungumuziwa katika Biblia. Kwa mufano, labda unaamini kama Musa aligawanya Bahari Nyekundu. Labda unaamini pia kama miujiza inafanyika wakati wetu. Kitabu fulani (The Cambridge Companion to Miracles) kilichoandikwa na Graham Twelftree mwalimu kwenye université ya Virginia Beach, huko États-Unis, kinasema kama uchunguzi fulani uliofanywa hivi karibuni ulionyesha kama “sehemu kubwa ya wakaaji wa inchi za Ulaya na Amerika, ni kusema karibu 75 % ya wakaaji wa États-Unis na 38 % ya wakaaji wa Angleterre wanaamini miujiza.” Tena, usifikiri kama ni Wakristo tu ndio wanaoamini miujiza. Kitabu fulani (Britannica Encyclopedia of World Religions) kinasema kama “karibu dini zote zinaamini miujiza.”

Ao unaweza kuwa kama wale watu wengine wanaosema: “Sijue, miujiza iwe ao isiwe hainiangalie! Miujiza haijanifikia!” Lakini, sababu gani unapaswa kuzungumuzia miujiza?

Fikiria hali hii: Wazia una ungojwa usiopona. Ikiwa unasoma gazeti fulani la kiganga lenye kutumainika linalozungumuzia dawa mupya ambayo inaweza kukuponyesha, je, unafikiri ni kupoteza wakati ikiwa unajikaza kutumia wakati kidogo ili kujua ukweli wa jambo hilo? Vilevile, Biblia inatuahidi kama hivi karibuni miujiza fulani yenye kushangaza itafanyika. Miujiza hiyo itabadilisha maisha ya kila mutu hapa duniani. Je, hauone kama kuchunguza ikiwa ahadi hiyo ni ya kweli, si kupoteza wakati?

Lakini, mbele ya kuchunguza miujiza hiyo ambayo Biblia inaonyesha kama itafanyika, tujibu kwanza maulizo matatu ambayo watu wanauliza kwa ukawaida ili kupinga miujiza.

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

MUUJIZA NI NINI?

Muujiza ni jambo fulani linalotukia, ambalo linashinda uwezo wote wa kufikiri wa mwanadamu ao ambalo linashinda nguvu za asili, na kwa hiyo, inaonekana kama jambo hilo limetokea kwa sababu ya nguvu fulani zisizo za mwanadamu.