Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wateteaji wa Kweli ya Biblia

Wateteaji wa Kweli ya Biblia

Wanafunzi wa Somo la 132 la Masomo ya Gileadi Wanapewa Diplome Zao

Wateteaji wa Kweli ya Biblia

TAREHE 10, mwezi wa 3, 2012, ilikuwa siku ya pekee sana kwenye mahali pakubwa pa mafundisho, mahali panapotumiwa na Mashahidi wa Yehova huko Patterson, New York. Maelfu ya watu wenye kuvalia vizuri, na wageni kutoka inchi mbalimbali, walikuja kuhuzuria programu ya kutolea wanafunzi wa somo la 132 la Masomo ya Biblia ya Gileadi diplome. Watu wengi walikusanyika katika jumba kubwa huko Patterson; na wengine walifuata pia programu hiyo kwenye Beteli zingine ambako ilionyeshwa kwenye televizyo. Watu wote waliohuzuria programu hiyo walikuwa 9042.

Watu walingojea programu hiyo kwa hamu sana. Masomo hayo yalikuwa tofauti na masomo mengine ya Gileadi ambayo yamekwisha kufanyika. Wanafunzi wote wa masomo hayo walikuwa tayari katika aina fulani ya utumishi wa wakati wote: wamoja walikuwa wametumika kwenye Beteli, wengine mapainia wa pekee, waangalizi wanaosafiri, na kuna wale ambao walikuwa wamisionere​—ijapokuwa walikuwa bado hawajahuzuria masomo ya Gileadi. Wanafunzi hao wenye uzoefu wangeambiwa nini?

Bila kukawia, wale waliohuzuria walipata jibu la ulizo hilo. Gerrit Lösch, ndugu anayetumikia katika Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, ndiye aliyekuwa musimamizi wa programu hiyo na ni yeye aliyetoa hotuba ya kwanza. Aliuliza ulizo hili lenye kumufanya mutu afikiri, “Je, Wewe Ni Muteteaji?” Alieleza kama Wakristo ni wateteaji wa kweli ya Biblia, wanatetea mafundisho yote ya Kikristo. Kutetea ile kweli hakumaanishe tu kufundisha watu kweli, lakini kunamaanisha pia kuwasaidia waipende.

Ndugu Lösch aliuliza hivi: “Namna gani tunajua kama sisi tuna ile kweli?” Alionyesha kama si hesabu ya watu wanaokubali ile kweli ndiyo inayoonyesha kama tuna ile kweli. Alionyesha kama ijapokuwa leo watu wengi sana wameikubali ile kweli, wakati wa Pentekoste mwaka wa 33, ni watu wachache tu ndio walioikubali. Alitaja njia tano zinazotusaidia kujua kama sisi tuna ile kweli: (1) Tunaendelea kufuata mafundisho ya Yesu, (2) tunapendana, (3) tuna mwenendo unaopatana na kanuni za juu za Mungu, (4) hatujiingize katika mambo ya ulimwengu huu, na (5) sisi ndio watu ambao Mungu amechagua ili kuitwa kwa jina lake.

“Muendelee Kufuata Maagizo na Kutii”

Kisha, ndugu Geoffrey Jackson anayetumikia pia katika Baraza Linaloongoza alipanda kwenye jukwaa akiwa na valize, na wahuzuriaji walijiuliza ikiwa atasema nini! Hotuba yake ilikuwa na kichwa “Muendelee Kufuata Maagizo na Kutii;” hotuba hiyo ilitegemea Isaya 50:5. Unabii wa andiko hilo unaozungumuzia Yesu Kristo unasema hivi: ‘Nami kwa upande wangu sikuwa muasi. Sikugeuka upande ulio kinyume.’

Ndugu Jackson aliwashauria wanafunzi wawe tayari kutambua muongozo ao maagizo ambayo Yehova anatoa kupitia roho yake takatifu, Biblia, na tengenezo lake. Katika mufano wa talanta unaopatikana katika andiko la Mathayo 25:14-30, tunaweza kusema kama watumwa wote walipewa sawasawa kwa sababu kila mutumwa alipewa kulingana na uwezo wake. Kila mumoja alitazamiwa kutumia uwezo wake wote. Bwana wao aliwapongeza watumwa wawili na kusema kama ni watumwa “wema na waaminifu.” Mutu haitwe muaminifu kwa sababu tu ya matokeo anayopata, lakini pia kwa sababu ya kufuata muongozo ao maagizo anayopewa.

Mutumwa wa tatu aliitwa mutumwa ‘muovu na goigoi’ na “asiyefaa kitu.” Mutumwa huyo alikuwa na tatizo gani? Alizika talanta yake. Talanta haikuwa sarafu, lakini kilikuwa kipimo cha uzito kinacholingana na dinari 6 000, ambazo zilikuwa na uzito wa kilo 20. Huo ndio uzito ambao mutu anaruhusiwa kuwa nao katika valize yake anaposafiri kwa avion. Inaomba mutu awe na nguvu ili azike kitu kilicho na ukubwa wa valize. Hilo ndilo jambo ambalo mutumwa huyo alifanya; alizika talanta yake, lakini Bwana wake hakumuambia afanye hivyo. Vilevile, misionere anaweza kuwa mwenye kazi nyingi. Lakini hiyo inaweza kuwa kazi gani? Labda kuandikia watu wa jamaa yake na marafiki barua ndefu-ndefu, kutafuta-tafuta habari kwenye Internete, kujifurahisha pamoja na marafiki, ao kujiingiza katika mambo ya biashara. Misionere huyo anaweza kuchoka kabisa mwishoni mwa siku kisha kufanya kazi hizo, lakini je, hizo ndizo kazi alizoagizwa kufanya? Ndugu Jackson alimalizia kwa maneno haya: “Muendelee kufuata maagizo na kutii!”

“Muondoe Mashaka Katika Akili Zenu”

Hicho kilikuwa kichwa cha hotuba iliyotolewa na ndugu Anthony Morris, anayetumikia pia katika Baraza Linaloongoza. Ndugu Morris alionyesha kwamba “Biblia haiseme hata kidogo kama imani na mashaka vinapatana.” “Imani inaondoa mashaka.” Shetani aliweza kutia mashaka katika akili ya Eva, mwanamuke mukamilifu. Kwa hiyo, anaweza pia kutia mashaka katika akili yenu. Ndugu Morris aliwaambia wanafunzi hivi: “Muendelee kulisha imani yenu, na mashaka yataisha.” Alizungumuzia habari ya Petro, ‘aliyetembea juu ya maji’ lakini, ‘alipoitazama ile zoruba ya upepo,’ akaogopa na akaanza kuzama. Kisha kumushika mukono, Yesu alimuuliza hivi: “Kwa nini umekuwa na shaka?” (Mathayo 14:29-31) “Kwa kuwa ninyi wamisionere mutakuwa na kazi nyingi katika utumishi wa wakati wote, watu wengine wanaweza kushangaa kwa sababu ya mambo munayofanya, ni sawa vile munatembea juu ya maji, lakini zoruba ya upepo inapotokea, musiwe na mashaka.”

Ndugu Morris aliendelea kuonyesha kama, wakati mwengine inaweza kuwa vigumu kushindana na nyakati ngumu zilizo kama zoruba ya upepo, lakini mwishowe upepo huo utatulia. Kuhusu nyakati ngumu, aliwashauri wanafunzi wafikirie kile Paulo na Sila walifanya walipokuwa katika gereza huko Filipi. Andiko la Matendo 16:25 linasema hivi: ‘Karibu na katikati ya usiku Paulo na Sila walikuwa wakisali na kumusifu Mungu kwa wimbo; ndiyo, wafungwa walikuwa wakiwasikia.’ Ona kama Paulo na Sila hawakusali tu lakini waliimba pia. Wafungwa wengine waliwasikia kwa sababu waliimba kwa sauti kubwa sana. Ndugu Morris alieleza kama wengi kati yetu hatuna sauti nzuri za kuimba, lakini hatupaswe kusita kuimba, zaidi sana tunapopambana na magumu. Ndugu Morris alimalizia hotuba yake kwa kusoma katika kitabu cha nyimbo maneno ya Wimbo 135 wenye kichwa “Kuvumilia Mpaka Mwisho.”

Hotuba Zingine Zenye Kutia Moyo

“Je, Utapenda Kuishi Siku Nyingi?” Hicho ndicho kilikuwa kichwa cha hotuba iliyotolewa na Robert Luccioni, wa Biro Inayohusika na Kununua Vitu. Kichwa cha hotuba yake kilitegemea maneno ya Mufalme Daudi yaliyo katika andiko la Zaburi 34:12. Hotuba ya Ndugu Luccioni ilizungumuzia namna mutu anaweza kushindana na nyakati ngumu na bado aendelee kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova. Tunaweza kujifunza mambo mengi kutokana na habari inayozungumuziwa katika 1 Samweli sura ya 30. Daudi, watumishi wake, na familia zao walipokuwa wakimukimbia Mufalme Sauli, waliishi uhamishoni huko Siklagi. Familia zao zilipobebwa na wavamizi kutoka Amaleki, watumishi wa Daudi walimukasirikia na walitaka kumupiga majiwe. Daudi alifanya nini? Hakuvunjika moyo lakini “akajitia nguvu kwa Yehova Mungu wake.” (1 Samweli 30:6) Alimuomba Yehova muongozo, akatenda kulingana na muongozo huo, na akawakomboa watu hao waliochukuliwa mateka. Ndugu Robert aliwahakikishia wanafunzi kama, ikiwa wanamutumainia Yehova na kufuata muongozo wake kama Daudi, watapenda kuishi siku nyingi ili kuona mema. Watafurahia maisha na kuendelea na pendeleo nzuri ambalo wamepewa.

“Endelea Kukazia Macho Wakati Muzuri Unaokuja Kisha Giza.” Hicho ndicho kilikuwa kichwa cha hotuba iliyotolewa na Ndugu Michael Burnett, mumoja wa walimu wa Masomo ya Gileadi. Waisraeli waligawanya usiku katika sehemu tatu kuanzia wakati jua linalala mupaka wakati linaamuka. Kipindi cha mwisho, kilianzia saa 8 ya usiku mupaka saa 12 ya asubuhi. Kipindi hicho kilikuwa ndicho kipindi chenye giza kubwa na baridi kali, na wakati huo ilikuwa vigumu zaidi kukaa macho. Kipindi cha mwisho cha usiku ndio wakati mutunga zaburi alifikiria sana maneno ya Yehova ili asilale usingizi. (Zaburi 119:148) Ndugu Burnett aliwaambia wanafunzi hivi: “Mutahitaji kukaa macho. Mutapambana na nyakati ngumu kama zile mutunga zaburi alizopambana nazo wakati wa usiku. Munapaswa kuamua mbele ya wakati kile ambacho mutafanya ili kushinda mambo hayo yenye kuvunja moyo.” Kisha aliwakumbusha kama, ili waendelee kukaa macho kiroho, wanapaswa kujipangia programu ya kujifunza sana habari mbalimbali zinazopatikana katika Biblia. Ndugu Burnett alitoa mufano unaofuata juu ya jambo hilo: “Kila siku, munasali kwa Yehova kwa sababu munataka awe rafiki yenu. Kwa hiyo, mumuruhusu pia rafiki yenu Yehova, azungumuze nanyi kila siku kupitia Biblia. Nyakati ngumu ambamo tunaishi zitaisha hivi karibuni, kwa hiyo, mupange namna mutakavyotumia siku zinazobaki. Kwa kufanya hivyo, mutaendelea kukazia macho wakati muzuri unaokuja kisha giza.”

“Mumezoezwa kwa Ajili ya Kazi Iliyo Mbele.” Hicho ndicho kilikuwa kichwa cha hotuba iliyotolewa na Mark Noumair, mwalimu mwengine wa masomo ya Gileadi. Kichwa hicho kilitegemea andiko la 1 Petro 5:10. Aliwauliza wanafunzi ulizo hili: “Kwa kuwa ninyi ni wahubiri wenye uzoefu, sababu gani basi muliitwa hapa kwenye Masomo haya ya Gileadi?” Na alijibu hivi: “Ni kwa sababu ninyi ni mafundi katika kazi yenu. Kwa kawaida watu wengi wenye ufundi fulani katika kazi yao wanachukua wakati wao wa mapumuziko ili kuenda kwenye masomo kufanya ufundi wao uwe muzuri zaidi. Katika miezi tano iliyopita, Yehova alikuwa akiwafanya muwe ‘imara’ na ‘wenye nguvu’ kupitia funzo kamili la Neno lake na tengenezo lake, ili muwe na uwezo wa kutimiza madaraka mazito ambayo yanawangojea. Nguzo zinazosimama imara haziwezi kunyauka, kukunjama, ao kuvunjika kwa sababu zinabeba uzito wa nyumba. Matokeo ya mazoezi yenu yataonekana mutakapotumika pamoja na ndugu na dada zenu. Je, magumu yatafanya muache kufuata kanuni za Mungu, ao mutaendelea kushikamana na mambo muliyojifunza katika Neno la Mungu? Kitu chenye nguvu kinaweza kubeba muzigo muzito. Nguvu za muti zinategemea aina ya mbegu iliyozaa muti huo. Vilevile, nguvu zenu zinategemea namna mulivyo kwa ndani. Yehova aliwaleta hapa ili kuwafanya muwe wenye nguvu, wenye kutegemeka na muwe wenye kustahili kwa ajili ya kazi iliyo mbele. Mungu amefanya sehemu yake, kwa hiyo, sala yetu ni kwamba ninyi pia mufanye sehemu yenu na mumuruhusu ‘Mufundishaji wenu Mukubwa’ amalize mazoezi yenu.”

Mambo Ambayo Wanafunzi Walikutana Nayo Katika Mahubiri na Sehemu za Kuuliza Maulizo

Kwenye programu ya kutolea wanafunzi wa Gileadi diplome zao, sikuzote ni jambo lenye kufurahisha sana kusikia maelezo ya wanafunzi wenyewe, na kama kawaida, wanafunzi walieleza mambo waliyokutana nayo katika mahubiri. Katika sehemu moja ya programu, wanafunzi walicheza upya mambo fulani waliyokutana nayo hivi karibuni katika mahubiri. Kwa mufano, ndugu mumoja na bibi yake walipokuwa wakija kwenye masomo haya ya Gileadi, walipaswa kungojea avion kwa muda wa saa sita. Walipokuwa katika restora kwenye uwanja wa avion, walianzisha mazungumuzo na wanaume wawili waliokuwa wakingojea pia avion. Mwanaume mumoja kati yao aliposema kama alitoka Malawi, walizungumuza naye katika Chichewa. Mwanaume huyo alishangaa na akawauliza namna gani walijua luga yake. Walimuambia kama walikuwa wamisionere huko Malawi. Yule mwengine aliposema kama alikuwa wa Cameroun, walizungumuza naye katika kifaransa, yeye pia alishangaa sana. Wanaume hao waliheshimu sana Mashahidi wa Yehova, na wamisionere hao wakawatolea ushahidi.

Nicholas Ahladis, wa Biro ya Utafsiri aliwauliza maulizo wanafunzi wawili na bibi zao. Mwanafunzi mumoja na bibi yake walitoka Australie na kuhamia katika inchi ya Timor Oriental yenye kusumbuliwa na vita ili kuwa wamisionere huko. Yule mwengine na bibi yake walitoka Corée na kuhamia Hong Kong. Wote walikuwa na hamu kubwa ya kurudia katika migawo yao mipya ili kutumikisha mambo ambayo walijifunza kwenye masomo.

Kisha wanafunzi wote kupewa diplome zao, mwanafunzi mumoja aliyechaguliwa na wengine alisoma barua ya shukurani kwa ajili ya mambo waliyofundishwa. Kisha, Ndugu Lösch alitumia semi fulani nzuri za mufano katika maneno yake ya kumalizia. Alisema hivi: “Kweli ni nzuri kama upinde wa mvua, ni kama chemuchemu ya maji katika jangwa, na kama nanga katika bahari yenye zoruba ya upepo. Kujua ile kweli ni baraka kubwa. Muwe wateteaji wa ile kweli, na muwasaidie wengine pia waitetee.”

[Muchoro/​Karte kwenye ukurasa wa 31]

MAELEZO FULANI JUU YA WANAFUNZI

Hesabu ya inchi walikotoka: 12

Kadirio la miaka yao ya kuzaliwa: 36

Kadirio la miaka katika kweli: 20

Kadirio la miaka katika kazi ya wakati wote: 15

[Karte]

(Ili kuona maelezo hayo, ona kitabu)

Wanafunzi walitumwa katika inchi hizi:

INCHI WALIKOTUMWA

BÉLIZE

BÉNIN

CAMBODGE

CAMEROUN

CAP VERT

CÔTE D’IVOIRE

ÉQUATEUR

ÉTATS-UNIS D’AMÉRIQUE

GABON

GÉORGIE

GUINÉE

HONG KONG

LIBÉRIA

MADAGASCAR

MALAWI

PÉROU

RÉPUBLIQUE DOMINICAINE

SAMOA

SAO TOMÉ-ET PRÍNCIPE

TIMOR ORIENTAL

ZIMBABWE

[Picha katika ukurasa wa 31]

Wanafunzi wa Somo la 132 la Masomo ya Biblia ya Gileadi Wanapewa Diplome zao

Majina ya wanafunzi yanafuatana kuanzia mustari wa kwanza kuenda juu kwenye mustari wa mwisho. Yanaanza na mutu wa kwanza upande wa kushoto.

(1) Iap, Roberto; Iap, Juli; Ng, Ting Wa; Ng, Patricia; Laurino, Franck; Laurino, Blandine; Won, Sang; Won, Stephanie.

(2) Morales, Natan; Morales, Miriam; Zanutto, Jonata; Zanutto, Manuela; Rumph, Inga; Rumph, Jacob; Germain, Delphine; Germain, Nicolas.

(3) Atchadé, Yves; Atchadé, Yvonne; Thomas, Chris; Thomas, Emma; Estigène, Catherine; Estigène, Politzer.

(4) Ehrman, David; Ehrman, Anna; Bray, Joshua; Bray, Amanda; Amorim, Marta; Amorim, David; Seo, Young; Seo, Yong-kee.

(5) Simon, Jean; Simon, Chrystelle; Seale, Christopher; Seale, Dianez; Erickson, Jennifer; Erickson, Ryan.

(6) McCluskey, Daniel; McCluskey, Tanji; Brown, Adam; Brown, Valarie; Mariano, Duane; Mariano, Celia; Loyola, Yolanda; Loyola, Caleb.

(7) Rutgers, Philip; Rutgers, Naomi; Foucault, Philippe; Foucault, Charlotte; Wunjah, Joanie; Wunjah, Ezekiel.