Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anachukia Ukosefu wa Haki

Yehova Anachukia Ukosefu wa Haki

Umukaribie Mungu

Yehova Anachukia Ukosefu wa Haki

‘MWANADAMU amemutawala mwanadamu kwa kumuumiza.’ (Mhubiri 8:9) Maneno hayo, yaliyoandikwa kumepita karibu miaka 3 000, yanaeleza waziwazi hali ya ulimwengu wa leo. Watu wanatumia vibaya mamlaka yao, iwe wao ni nani ao wanaishi wapi. Mara nyingi wanaonea wenzao wasio na mutu wa kuwasemea na wale wa hali ya chini. Namna gani Yehova anaona ukosefu wa haki kama huo? Tunapata jibu katika andiko la Ezekieli 22:6, 7, 31.​—Soma.

Katika Sheria aliyowapatia Waisraeli, Yehova alionyesha wazi kama wale walio na mamlaka hawakupaswa kutumia vibaya mamlaka yao. Angebariki taifa hilo ikiwa tu viongozi walitendea watu wa hali ya chini na masikini kwa wema na kuwahangaikia. (Kumbukumbu la Torati 27:19; 28:15, 45) Lakini, wakati wa Ezekieli, wakubwa wa muji wa Yerusalemu na Yuda walitumia mamlaka yao vibaya sana. Ni mambo gani yaliyokuwa yakitendeka?

Wakubwa walikuwa wanatumia ‘mukono wao ili kumuanga damu.’ (Mustari wa 6) Neno “mukono” linamaanisha uwezo ao mamlaka. Tafsiri nyingine inasema hivi: ‘Wakubwa wa Israeli . . . wametumia uwezo wao ili kumuanga damu.’ Namna gani kungekuwa haki wakati ambapo viongozi, ambao walipaswa kutii sheria na kutia wengine moyo waitii pia, walikuwa wanatumia vibaya mamlaka yao na kuua watu wasio na kosa?

Kisha kusema maneno yaliyo katika mustari wa 6, Ezekieli aliwalaumu viongozi na pia wale waliowaiga kwa kukosa kutii Sheria ya Yehova. Ezekieli alisema hivi: ‘Wamemutendea zarau baba na mama.’ (Mustari wa 7) Kwa sababu watu walizarau daraka ambalo Yehova aliwapatia wazazi, walivunja musingi wa taifa ambao ni familia.​—Kutoka 20:12.

Watu hao wabaya walionea wale wasio na mutu wa kuwasemea. Kila mara walipovunja Sheria, walionyesha kama hawakuheshimu Sheria ya Mungu iliyochochea roho ya upendo. Kwa mufano, Sheria ya Mungu iliwaamuru Waisraeli wawahangaikie kwa njia ya pekee watu wasio Waisraeli ambao walikaa katika inchi yao. (Kutoka 22:21; 23:9; Mambo ya Walawi 19:33, 34) Lakini, wao ‘walimutendea kwa upunjaji’ mukaaji mugeni.​—Mustari wa 7.

Tena watu waliwatendea vibaya wale ambao hawakuwa na mutu wa kuwasemea— ‘muvulana asiye na baba na mujane.’ (Mustari wa 7) Yehova anahangaikia sana mahitaji ya wale wanaofiwa na muzazi, bibi ao bwana. Aliahidi kama yeye mwenyewe atawahukumu wale wanaomutesa yatima ao mujane.​—Kutoka 22:22-24.

Kwa kuwatesa mayatima na wajane na kufanya mambo mengine mabaya, Waisraeli katika wakati wa Ezekieli walivunja Sheria ya Mungu iliyochochea roho ya upendo. Yehova angefanya nini? Aliahidi hivi: ‘Nitamuanga shutuma zangu juu yao.’ (Mustari wa 31) Kupatana na ahadi yake, aliwaruhusu Wababiloni wauharibu muji wa Yerusalemu na kuwapeleka wakaaji katika utumwa mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu.

Maneno ya Ezekieli yanatufundisha mambo haya mawili juu ya Yehova na juu ya ukosefu wa haki: Jambo la kwanza, Yehova anachukia ukosefu wa haki; jambo la pili, anawasikilia huruma wale wanaotendewa isivyo haki. Mungu hajabadilika. (Malaki 3:6) Anaahidi kama hivi karibuni ataondoa ukosefu wa haki na wale wanaotendea wengine isivyo haki. (Methali 2:21, 22) Sababu gani usijifunze mengi zaidi juu ya Mungu ‘mupenda haki’ na namna unavyoweza kumukaribia zaidi?​—Zaburi 37:28.

Tafazali, mwezi huu wa 8, soma Maandiko haya katika Biblia:

Ezekieli sura ya 21 mupaka sura ya 38

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 27]

Yehova alionyesha wazi kama wale walio na mamlaka hawakupaswa kutumia vibaya mamlaka yao