Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Inawezekana Kufuatia Haki Katika Dunia Hii Yenye Kujaa Rushwa?

Je, Inawezekana Kufuatia Haki Katika Dunia Hii Yenye Kujaa Rushwa?

Je, Inawezekana Kufuatia Haki Katika Dunia Hii Yenye Kujaa Rushwa?

“Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”​—WAEBRANIA 13:18.

IJAPOKUWA hali yetu ya zambi, ulimwengu ambamo tunaishi, na ijapokuwa Ibilisi anaweza kutuchochea sana tusifuatie haki, tunaweza kushinda vishawishi hivyo! Namna gani? Kwa kumukaribia Mungu na kutumikisha kanuni za Neno lake Biblia ambazo zimeonekana kuwa zenye faida sikuzote. Fikiria kanuni hizi mbili.

KANUNI YA BIBLIA: ‘Acheni kufanyizwa kulingana na mufumo huu wa mambo.’—Waroma 12:2.

Mufano: Guilherme ni mufanya-biashara mwenye matokeo mazuri anayekaa katika inchi ya Brezil. Anakubali kama si vyepesi kufuatia haki. Anasema hivi: “Mufanya​-biashara anaweza kwa vyepesi kuambukizwa na tabia za udanganyifu, labda kwa sababu anataka kutimiza miradi ya kazi ao kuendeleza biashara yake kati ya watu wenye roho ya kushindana. Watu wengi wanaona kama tabia ya kutoa na kupokea rushwa (kata-midomo) ni jambo la kawaida. Ikiwa mutu ni mufanya-biashara mukubwa, ni vigumu zaidi kwake kufuatia haki.”

Hata hivyo, Guilherme ameshinda kabisa jaribu hilo la kutenda kwa udanganyifu. Anaendelea kusema: “Hata katika hali ambamo wafanya​-biashara wanaruhusiwa kutenda kwa udanganyifu, inawezekana kufuatia haki. Ni lazima kuwa na kanuni nzuri za mwenendo. Biblia imenisaidia kuona faida za kufuatia haki. Mutu mwenye kufuatia haki ana zamiri safi, moyo mutulivu, na ni mwenye kujiheshimu. Na anaweza kuwasaidia wengine wafuate mufano wake.”

KANUNI YA BIBLIA: ‘Wanaotaka kutajirika huanguka katika vishawishi na mitego na tamaa nyingi zenye upumbavu na zenye kuleta hasara, nazo zinawazamisha wanadamu katika uharibifu na upotevu. Kwani tamaa ya feza ndio muzizi wa mabaya yote.’​—1 Timotheo 6:9, 10, Verbum Bible.

Mufano: André ana kompani yake inayosaidia kutilia watu vyombo vya ulinzi. Kompani yake inatumikia pia kikundi cha wacheza-kabumbu. Siku moja, kisha muchezo mukubwa, André alienda kwenye biro ili kuomba feza kwa ajili ya kazi waliyofanya. Wale wanaohusika na mambo ya feza walikuwa wangali na kazi nyingi sana ya kuhesabia feza walizopata. Kwa sababu saa ilikuwa imepita, musimamizi alianza kulipa watu haraka​-haraka.

André anasema hivi: “Nilipokuwa nikirudi nyumbani, nilivumbua kama musimamizi alinilipa feza nyingi zaidi kuliko zile alizopaswa kunilipa. Nilijua kama ilikuwa vigumu musimamizi huyo ajue ni nani aliyepokea feza nyingi kati yetu. Lakini nilijua tena kama alipaswa kulipa feza zilizopotea! Kwa hiyo, niliamua kurudia ili kumuona. Nilijikaza sana ili kupata njia katikati ya watu wengi sana waliokuwa wakitoka kutazama muchezo wa kabumbu, na nilipomuona, nikamurudishia feza za ziada. Musimamizi huyo alishangaa sana na kusema kama hakuna mutu mwengine ambaye amekwisha kumurudishia feza alizopoteza.”

André anaendelea kusema: “Tendo hilo la kufuatia haki lilifanya musimamizi huyo aniheshimu sana. Ni kompani yangu tu ndiyo inaendelea kutumikia kikundi hicho cha wacheza​-kabumbu. Ninamushukuru sana Mungu kwa sababu kutumikisha kanuni za juu za Biblia kumenifanya niheshimiwe.”

Ni jambo lenye kututia moyo sana kujua kwamba, kwa musaada wa Mungu, tunaweza kushinda vishawishi vya kutoa na kupokea rushwa. Lakini, hatuwezi hata kidogo kuondoa kabisa rushwa kwa nguvu zetu wenyewe. Ni vigumu kabisa kwa watu wasio wakamilifu kumaliza rushwa. Je, hilo linamaanisha kama rushwa haitaisha hata siku moja? Habari ya mwisho katika sehemu hii ina jibu lenye kutia moyo ambalo Biblia inatutolea.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 6]

“Biblia imenisaidia kuona faida za kufuatia haki.”​—GUILHERME

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 6]

“Ninamushukuru sana Mungu kwa sababu kutumikisha kanuni za juu za Biblia kumenifanya niheshimiwe.”​—ANDRÉ