Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ujilinde na Tamaa ya Mambo Makubwa!

Ujilinde na Tamaa ya Mambo Makubwa!

Kwa Ajili ya Vijana

Ujilinde na Tamaa ya Mambo Makubwa!

Maagizo: Ufanye mazoezi haya mahali pa utulivu. Unaposoma maandiko, wazia kama unatazama namna matukio hayo yanavyofuatana. Ona matukio hayo akilini mwako. Sikia sauti za watu wanaozungumuziwa na ujisikie namna walivyojisikia. Fanya kama ulikuwa hapo na kuona namna mambo yalivyotendeka.

Watu wanaozungumuziwa sana katika habari hii: Daudi, Absalomu, na Yoabu

Kwa kifupi: Absalomu anajaribu kukamata kwa nguvu ufalme wa baba yake.

1 CHUNGUZA MATUKIO HAYO.​—SOMA 2 SAMWELI 14:25-33; 15:1-17; 18:9-17, 30-33.

Eleza namna unavyowazia sura ya Absalomu. (Soma tena 2 Samweli 14:25, 26.)

․․․․․

Unawazia sura na sauti ya Absalomu vilikuwa namna gani wakati alijaribu kuiba mioyo ya watu waliokuwa wanaleta shida zao mbele ya mufalme? (Soma tena 2 Samweli 15:2-6.)

․․․․․

Unaposoma habari iliyo katika 2 Samweli 14:28-30, unatambua nini juu ya tabia ya Absalomu?

․․․․․

2 TAFUTA KUJUA ZAIDI.

Absalomu alifanya nini ili aweze kukamata ufalme kwa nguvu? (Ili kupata jibu: Soma 2 Samweli 13:28, 29. Amnoni ndiye alipaswa kuriti ufalme kwa sababu alikuwa mutoto wa kwanza wa Daudi.)

․․․․․

Hata ikiwa Absalomu alitamani mambo makubwa na kujitafutia sifa, kufa na kuzikwa kwake kulionyesha kama watu walikuwa na mawazo gani juu yake? (Soma tena 2 Samweli 18:17.)

․․․․․

Unawaza ni nini kilichomufanya Absalomu atamani mambo makubwa? (Ili kulinganisha Absalomu na Diotrefe, soma habari iliyo katika andiko la 3 Yohana 9, 10.)

․․․․․

Matendo ya Absalomu yalimuletea Daudi magumu gani? (Ili kupata jibu: Soma Zaburi ya 3, ambayo Daudi aliandika wakati alikuwa anakimbia kwa sababu ya Absalomu.)

․․․․․

3 TUMIKISHA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA JUU YA . . .

Hatari ya kutamani mambo makubwa.

․․․․․

Magumu ambayo matendo ya mutu yanaweza kuwaletea watu wengine na hata wazazi wake.

․․․․․

NAMNA NYINGINE UNAVYOWEZA KUTUMIKISHA HABARI HII.

Namna gani unaweza kuanguka katika mutego wa kutamani mambo makubwa?

․․․․․

Namna gani unaweza kuepuka kuwa na kiburi?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA HABARI HII YANAYOKUGUSA MOYO SANA, NA SABABU GANI?

․․․․․

Pendekezo: Wazia kama hadisi hii ingeisha namna nyingine. Mambo yangekuwa namna gani ikiwa Absalomu hakutamani mambo makubwa?​—Methali 18:12.

Ufungue www.watchtower.org

Usome Biblia kwenye Internete

Upakue ao kuchapisha habari hii