Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Namna gani Wayahudi walioishi kati ya mwaka wa 1 na 100 walitayarisha maiti kwa ajili ya maziko?

Wayahudi walikuwa wanazika maiti haraka baada tu ya mutu kufa, kwa kawaida siku hiyohiyo. Kulikuwa sababu mbili zilizowafanya wazike maiti haraka hivyo. Sababu ya kwanza, maiti zinaoza haraka kwa sababu ya hali ya joto ya Mashariki ya Kati. Sababu ya pili, kulingana na mawazo ya watu walioishi wakati huo, kuacha maiti bila kuzikwa kwa siku nyingi kulionyesha kwamba hawaheshimu mutu aliyekufa na pia familia yake.

Vitabu vya Injili na kitabu cha Matendo ya Mitume vinazungumuzia karibu maziko ine yaliyofanywa siku ileile ambayo watu hao walikufa. (Mathayo 27:57-60; Matendo 5:5-10; 7:60–8:2) Mamia ya miaka mbele ya wakati huo, Raheli, bibi mupendwa wa Yakobo, alikufa wakati Yakobo na familia yake walikuwa katika safari. Yakobo hakurudia ili kuzika maiti ya Raheli katika kaburi la familia, lakini alimuzika katika kaburi lililokuwa “njiani kuelekea . . . Bethlehemu.”​—Mwanzo 35:19, 20, 27-29.

Habari za Biblia juu ya matayarisho ya maziko zinaonyesha kwamba Wayahudi walitayarisha maiti kwa uangalifu kwa ajili ya maziko. Watu wa familia na marafiki walinawisha maiti, waliipaka vikolezo na mafuta mazuri, na kisha waliifunga ndani ya nguo. (Yohana 19:39, 40; Matendo 9:36-41) Majirani na watu wengine walikuja ili kuomboleza na pia kuwafariji watu wa familia.​—Marko 5:38, 39.

Je, Yesu alizikwa kama vile Wayahudi wengine walivyokuwa wanazikwa?

Familia nyingi za Wayahudi zilizika watu wao waliokufa katika makaburi yaliyochimbwa katika miamba ao majiwe makubwa yaliyokuwa teketeke ambayo yalipatikana katika sehemu nyingi za Israeli. Kwa kufanya hivyo, walifuata mufano wa wazee wa ukoo. Abrahamu, Sara, Isaka, Yakobo na wengine walizikwa katika makaburi yaliyokuwa katika pango la Makpela karibu na Hebroni.​—Mwanzo 23:19; 25:8, 9; 49:29-31; 50:13.

Yesu alizikwa katika kaburi lililochimbwa ndani ya mwamba. (Marko 15:46) Kwa kawaida, kaburi kama hilo lilikuwa na mwingilio mwembamba. Ndani ya mwamba huo, kila upande wa ukuta, watu walichonga vyumba vidogo-vidogo ambamo maiti za watu wa familia ziliwekwa ao kuingizwa. Kisha mwili kuoza, mifupa iliyokauka ilikusanywa na kutiwa katika sanduku la jiwe lililoitwa sanduku la mifupa, kama ilivyokuwa desturi katika siku za Yesu. Kwa kufanya hivyo, familia ingeweza kupata nafasi ndani ya kaburi hilo ili kuwazika watu wengine wa familia ambao wangekufa baadaye.

Sheria ya Musa iliwakataza Wayahudi kufanya matayarisho kwa ajili ya maziko wakati wa mapumuziko ya siku ya Sabato. Kwa sababu Yesu alikufa karibu saa tatu mbele ya Sabato kuanza, Yosefu wa Arimathea na wengine walimuzika Yesu bila kumaliza kabisa matayarisho ya mwili wake kwa ajili ya maziko. (Luka 23:50-56) Ndiyo sababu, marafiki fulani wa Yesu walienda kwenye kaburi kisha Sabato ili kumaliza matayarisho hayo.​—Marko 16:1; Luka 24:1.