Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ufufuo wa Yesu Unatuwezesha Kupata Uzima!

Ufufuo wa Yesu Unatuwezesha Kupata Uzima!

HATUWEZI kuona ufufuo wa Yesu kuwa jambo fulani tu lililotokea zamani ambalo halina faida yoyote kwetu leo. Mutume Paulo alionyesha faida ya ufufuo wa Yesu alipoandika hivi: “Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo. Kwa kuwa kifo ni kupitia mwanadamu, ufufuo wa wafu pia ni kupitia mwanadamu. Kwa maana kama vile katika Adamu wote wanakufa, vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.”​—1 Wakorintho 15:20-22.

Yesu alifufuliwa tarehe 16, Mwezi wa Nisani, mwaka wa 33, siku ambayo kila mwaka Wayalitoa matunda ya kwanza ya mazao yao ya kwanza mbele ya Yehova Mungu kwenye patakatifu pa hekalu huko Yerusalemu. Kwa kumuita Yesu matunda ya kwanza, Paulo alimaanisha kwamba kungekuwa pia watu wengine ambao wangefufuliwa kutoka kwa wafu.

Maneno ya Paulo yanayofuata yanaonyesha mambo ambayo ufufuo wa Yesu uliwezesha. Paulo alisema hivi: “Kwa kuwa kifo ni kupitia mwanadamu, ufufuo wa wafu pia ni kupitia mwanadamu.” Sisi wote tunakufa kwa sababu tuliriti zambi na kutokamilika kutoka kwa Adamu. Hata hivyo, kwa kutoa uzima wake mukamilifu kuwa zabihu ya ukombozi, Yesu alifungulia wanadamu njia ya kukombolewa kutoka katika utumwa wa zambi na kifo kupitia ufufuo. Katika andiko la Waroma 6:23, Paulo anazungumuzia vizuri jambo hilo kwa kifupi. Aliandika hivi: ‘Mushahara ambao zambi inalipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu anatoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.’

Yesu mwenyewe alieleza faida ambayo tunapata kupitia kifo chake na ufufuo wake. Alizungumuza juu yake mwenyewe kwa kusema hivi: ‘Mwana wa binadamu atainuliwa, ili kila mutu anayemuamini apate kuwa na uzima wa milele. Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu anayemuamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.’​—Yohana 3:14-16.

Wazia uzima usio na mwisho bila maumivu, mateso, ao huzuni! (Ufunuo 21:3, 4) Hilo ni tumaini nzuri sana, sivyo? Mutu fulani mwenye elimu alisema hivi juu ya jambo hilo: “Hata ikiwa makaburi yanatukumbusha kwamba maisha ni mafupi, ufufuo unatuhakikishia kwamba kifo kina mipaka.” Kwa kweli, ufufuo wa Yesu unatuwezesha kupata uzima!