Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yesu, Mufano Muzuri wa Maisha Yenye Maana

Yesu, Mufano Muzuri wa Maisha Yenye Maana

JE, KWELI Yesu alikuwa na maisha yenye maana? Ni wazi kwamba Yesu hakukomalia kati ya watu waliokuwa matajiri, na hakuwa na vitu vingi vya kimwili. Kwa kweli, hakuwa na “mahali popote pa kulaza kichwa chake.” (Luka 9:57, 58) Zaidi ya hayo, alichukiwa, alisingiziwa, na mwishowe aliuawa na maadui wake.

Unaweza kufikiri, ‘Maisha kama hayo hayakuwa yenye maana!’ Lakini kuna mambo mengi kuhusu maisha ya Yesu ambayo ni vizuri tufikirie. Acheni tuchunguze hali ine za maisha yake.

1. YESU ALIKUWA NA KUSUDI KATIKA MAISHA​—KUFANYA MAPENZI YA MUNGU.

“Chakula changu ni mimi kufanya mapenzi yake aliyenituma.”​—Yohana 4:34.

Kupitia maneno na matendo yake, Yesu alitafuta kutimiza mapenzi ya Yehova *, Baba yake wa mbinguni. Yesu alipata furaha kubwa katika kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa kweli, alilinganisha kufanya mapenzi ya Mungu na chakula, kama inavyoonyeshwa katika andiko ambalo linatoka kutajwa. Chunguza ni katika hali gani alifanya ulinganifu huo.

Yesu aliposema maneno hayo, ilikuwa karibu katikati ya muchana. (Yohana 4:6) Alikuwa ametembea katika sehemu zenye milima za Samaria asubuhi yote, kwa hiyo, bila shaka alikuwa mwenye njaa. Ndiyo sababu wanafunzi wake walimusihi hivi: “Rabi, kula.” (Yohana 4:31) Kupitia jibu lake, Yesu alionyesha kwamba alijisikia kuwa mwenye kulishwa na mwenye kutiwa nguvu kwa kufanya kazi ya Mungu. Hilo linaonyesha kwamba Yesu ni mutu ambaye alikuwa na maisha yenye maana, sivyo?

2. YESU ALIKUWA NA UPENDO MWINGI KWA BABA YAKE.

‘Ninamupenda Baba.’​—Yohana 14:31.

Yesu alikuwa na urafiki wa sana pamoja na Baba yake huko mbinguni. Upendo mwingi wa Yesu kwa Mungu ulimuchochea ajulishe watu mambo mengi juu ya Baba yake, ni kusema, jina lake, makusudi yake, na sifa zake. Kupitia maneno, matendo, na maoni yake, Yesu alionyesha kwa ukamili sifa za Baba yake hivi kwamba tunamuona Yesu kuwa mufano kabisa wa Baba yake. Ndiyo maana wakati Filipo alimuomba Yesu: “Tuonyeshe Baba,” Yesu alimujibu: ‘Yule ambaye ameniona mimi amemuona Baba pia.’​—Yohana 14:8, 9.

Yesu alimupenda sana Baba yake, ndiyo sababu alikuwa tayari kumutii mupaka kifo. (Wafilipi 2:7, 8; 1 Yohana 5:3) Upendo mwingi kwa Mungu kama huo ndio ulifanya maisha ya Yesu yawe yenye maana.

3. YESU ALIPENDA WATU.

‘Hakuna aliye na upendo mukubwa kuliko huu, kwamba mutu aitoe nafsi yake kwa ajili ya rafiki zake.’​—Yohana 15:13.

Kwa sababu sisi ni wanadamu wasio wakamilifu, kwa kweli hatujue namna gani maisha yetu yatakuwa kesho. Biblia inaeleza hivi: ‘Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.’ (Waroma 5:12) Kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuepuka kifo, ambacho kilitokana na zambi.​—Waroma 6:23.

Jambo la kupendeza ni kwamba, kwa upendo Yehova alitayarisha njia ya kuwatosha wanadamu katika hali hiyo. Alimuruhusu Yesu, Mwana wake mukamilifu na asiye na zambi, ateseke na kufa ili atoe zabihu ya ukombozi iliyohitajiwa ili kukomboa wanadamu kutoka katika utumwa wa zambi na kifo. Upendo kwa Baba yake na kwa wanadamu, ulimuchochea Yesu amutii Mungu bila kulazimishwa na kutoa uzima wake mukamilifu kwa ajili yetu. (Waroma 5:6-8) Upendo kama huo usio na uchoyo ulifanya maisha yake yawe yenye maana. *

4. YESU ALIJUA KWAMBA BABA YAKE ALIMUPENDA NA ALIMUKUBALI.

‘Huyu ni Mwanangu, mupendwa, ambaye nimemukubali.’​—Mathayo 3:17.

Yehova alisema maneno hayo kutoka mbinguni wakati Yesu alibatizwa. Kwa kusema hivyo, Yehova alionyesha waziwazi kwamba alimupenda na kumukubali Yesu, Mwana wake. Ndiyo maana Yesu alisema kwa mukazo hivi: “Baba ananipenda”! (Yohana 10:17) Kujua kwamba Baba yake alimupenda na kumukubali, kulimusaidia Yesu apambane kwa ujasiri na upinzani na kuchambuliwa. Aliendelea kuwa na usawaziko na alipambana na kifo bila woga. (Yohana 10:18) Bila shaka, kujisikia kwamba Baba yake alimupenda na kumukubali kulifanya maisha ya Yesu yawe yenye maana zaidi.

Kwa kweli, Yesu alikuwa na maisha yenye maana. Ni wazi kwamba tunaweza kujifunza mambo mengi juu yake kuhusu namna tunavyoweza kuwa na maisha yenye maana kwelikweli. Habari inayofuata itazungumuzia mashauri fulani yaliyo wazi ambayo Yesu aliwapatia wafuasi wake kuhusu namna ya kuishi.

^ Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.

^ Ili kujifunza mengi zaidi juu ya namna tunavyoweza kufaidika na zabihu ya Yesu ya ukombozi, soma sura ya 5 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.