Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MAFUNDISHO YA UONGO AMBAYO YANAFANYA WATU WASIMUPENDE MUNGU

Fundisho la Uongo Ambalo Limemufanya Mungu Kuwa Hana Jina

Fundisho la Uongo Ambalo Limemufanya Mungu Kuwa Hana Jina

MAMBO AMBAYO WATU WENGI WANAAMINI:

“Hatukufikia makubaliano ikiwa tunaweza hata kusema juu ya ‘lile’ jina la Mungu, na ikiwa ni hivyo, hilo linaweza kuwa jina gani.”​— David Cunningham, Mwalimu wa Masomo ya Juu, Theological Studies.

KWELI YA BIBLIA:

Mungu alisema: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.” (Isaya 42:8) Yehova ni jina la Kiebrania ambalo linamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.”​—Mwanzo 2:4.

Yehova anataka tutumie jina lake. Biblia inasema hivi: “Liitieni jina lake. Tangazeni matendo yake kati ya vikundi vya watu. Semeni kwamba jina lake limeinuliwa juu.”​—Isaya 12:4.

Yesu alitumia jina la Mungu. Katika sala, Yesu alimuambia Yehova hivi: “Nami nimewajulisha [wanafunzi wa Yesu] jina lako nami nitalijulisha.” Sababu gani Yesu aliwajulisha wanafunzi wake jina la Mungu? Yesu aliendelea kusema hivi: “Ili upendo ulionipenda nao [wewe Mungu] upate kuwa ndani yao nami katika muungano pamoja nao.”​—Yohana 17:26.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Walter Lowrie ambaye ni mwalimu wa dini, aliandika hivi: “Mutu ambaye hajue jina la Mungu hamujue Mungu kuwa mutu anayeishi kwelikweli, na hawezi kumupenda ikiwa anamujua kuwa nguvu fulani tu.”

Mwanaume anayeitwa Victor alikuwa anaenda kwenye kanisa kila juma, lakini hakujisikia kuwa alimujua Mungu kwelikweli. Anasema hivi: “Kisha nilijifunza kwamba jina la Mungu ni Yehova, na ilikuwa kama nilijitambulisha kwake. Nilijisikia kama vile nilikutana mwishowe na Yule ambaye nilikuwa nimesikia mambo mengi juu yake. Nilifikia kumuona kuwa Mutu anayeishi kwelikweli na nilifanya urafiki pamoja naye.”

Yehova pia anawakaribia wanadamu ambao wanatumia jina lake. Kuhusu “wale wanaolifikiria jina lake,” Mungu anaahidi hivi: ‘Nami nitawaonyesha huruma, kama vile mwanaume anavyomuonyesha huruma mwana wake ambaye anamutumikia.’ (Malaki 3:16, 17) Pia Mungu anawapa zawadi wale ambao wanaliitia jina lake. Biblia inasema hivi: ‘Kila mutu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.’​—Waroma 10:13.