Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA

Kuna Mutu Anayeweza Kujua Wakati Unaokuja?

Kuna Mutu Anayeweza Kujua Wakati Unaokuja?

Sisi wote tunafikiri juu ya wakati unaokuja. Tunajiuliza maisha yetu na ya watu tunaopenda yatakuwa namna gani. Tunauliza maulizo kama vile: ‘Watoto wangu wataishi katika dunia nzuri? Dunia itaharibiwa katika musiba? Kuna jambo ninaloweza kubadilisha sasa ili kufanya wakati wangu unaokuja uwe muzuri?’ Ni jambo la kawaida kwetu kupenda kujua wakati unaokuja; kwa kawaida tunapenda kupata uhakikisho, ukweli wa mambo, kuwa na mupango, na kuwa salama. Ikiwa ungekuwa na uhakika juu ya wakati unaokuja, ungeweza kujitayarisha kimwili na moyoni kwa ajili ya wakati huo.

Kwa hiyo, wakati wako unaokuja utakuwa namna gani? Kuna mutu fulani anayeweza kujua? Watu wenye elimu wanajaribu kutabiri wakati unaokuja, matabiri yao fulani yametimia lakini pia mengine mengi hayakutimia. Hata hivyo, inasemekana kuwa Mungu anaweza kutabiri bila kukosea matukio ya wakati unaokuja. Neno lake linasema hivi: “Yeye anayetangaza tangu mwanzo ule mwisho, na kutoka zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa.” (Isaya 46:10) Mambo alitabiri yalitimia kabisa?

MAMBO MUNGU ALITABIRI YALITIMIA BILA KUKOSEA

Sababu gani upende kujua ikiwa mambo Mungu alitabiri zamani yalitimia kabisa? Kwa kweli, ikiwa unaona kwamba mutabiri fulani wa hali ya hewa anasema kweli kila siku kwa kipindi kirefu, unaweza kuvutiwa sana na yeye. Inawezekana utafuata kwa uangalifu mambo aliyosema juu ya hali ya hewa ya siku inayofuata. Kwa njia ileile, ikiwa unajifunza kwamba Mungu ametabiri matukio bila kukosea kabisa, bila shaka utapendezwa na mambo anatabiri juu ya wakati unaokuja.

Ukuta uliojengwa upya katika Ninawi, muji ulioharibiwa zamani

UHARIBIFU WA MUJI MUKUBWA:

Kwa mufano, linaweza kuwa jambo la ajabu sana kutabiri bila kukosea kwamba muji mukubwa, wenye nguvu kwa mamia ya miaka, utaharibiwa karibuni. Kupitia mumoja wa wasemaji  wake, Mungu alitabiri jambo kama hilo, ni kusema, uharibifu wa muji wa Ninawi. (Sefania 2:13-15) Wanahistoria wa ulimwengu waliandika nini juu ya jambo hilo? Katika mwaka wa 632 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, labda miaka 15 hivi kisha Mungu kutabiri uharibifu huo, Wababiloni na Wamedi walishambulia muji wa Ninawi na wakaushinda. Tena, Mungu alionyesha mbele ya wakati kwamba muji wa Ninawi ungefanywa “mahame yenye ukiwa, eneo lisilo na maji kama nyika [ao jangwa].” Tangazo hilo lililosemwa mbele ya wakati lilitimia bila kukosea? Ndiyo. Hata ikiwa labda muji huo na vijiji vilivyouzunguka vilikuwa na kilometa 518 za muraba, wale walioshambulia muji huo hawakuuacha na kutumia vitu vyake, kama inavyoweza kutazamiwa, lakini waliuharibu. Kuna muchunguzi fulani wa kisiasa ambaye angeweza kutabiri matukio hayo bila kukosea?

MIFUPA YA WATU ITATEKETEZWA:

Ni nani angekuwa na ushujaa wa kutangaza, miaka 300 mbele, jina la kwelikweli na ukoo wa mutu atakayeteketeza ao kuchoma mifupa ya watu juu ya mazabahu ao altare, na pia jina la muji kwenye mazabahu hayo yangejengwa? Ikiwa unabii huo usio wa kawaida ungetimia, ungefanya mutu aliyeutabiri ajulikane sana. Musemaji wa Mungu alitangaza hivi: ‘Mwana anayeitwa Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi, na atateketeza mifupa ya watu’ juu ya mazabahu katika muji wa Beteli. (1 Wafalme 13:1, 2) Karibu miaka mia tatu kisha hapo, mufalme anayeitwa Yosia (jina la kibiblia lisilojulikana sana) alitokea katika uzao wa Daudi. Kama tu ilivyotabiriwa, Yosia alituma watu kuichukua ‘mifupa kutoka katika makaburi, akaiteketeza kwa moto juu ya ile mazabahu’ yaliyokuwa katika muji wa Beteli. (2 Wafalme 23:14-16) Namna gani mutu angeweza kutabiri maelezo hayo ya waziwazi bila kuongozwa na nguvu zinazopita za wanadamu?

unabii wa Biblia juu ya kuanguka kwa Babiloni ulitimia bila kukosea

MWISHO WA UTAWALA:

Lingekuwa jambo la kushangaza ikiwa mutu angetabiri bila kukosea jina la mwanaume mwenye angepanga kuanguka kwa serikali kubwa ya dunia, hata kuonyesha njia isiyo ya kawaida yenye angetumia na kutabiri mambo hayo muda murefu mbele ya mwanaume huyo kuzaliwa. Mungu alitangaza kwamba mwanaume anayeitwa Koreshi atapanga namna ya kushinda taifa. Koreshi huyo angewaachilia Wayahudi waliokuwa wamekamatwa kwa nguvu na angetegemeza kujengwa upya kwa hekalu lao takatifu. Tena, Mungu alitabiri kwamba ufundi wa vita wa Koreshi ungetia ndani kukausha maji ya mito na alionyesha kwamba milango ingebakia wazi, na hilo lingewezesha  ushindi. (Isaya 44:27–45:2) Je, maelezo hayo mengi yaliyotajwa katika unabii wa Mungu yalitimizwa bila kukosea? Wanahistoria wanakubali kwamba ushindi huo kupitia Koreshi ulitokea. Jeshi la Koreshi lilitumia ufundi wa hali ya juu wa kugeuza njia ya muto mumoja kati ya mito ya Babiloni​, na hivyo wakakausha maji ya muto huo. Na jambo lingine, jeshi liliingia kupitia milango iliyokuwa imeachwa wazi. Kisha hapo, Koreshi aliwaachilia Wayahudi na akatangaza kwamba wangejenga upya hekalu lao katika muji wa Yerusalemu. Hilo lilikuwa jambo la kushangaza, kwa sababu Koreshi hakuabudu Mungu wa Wayahudi. (Ezra 1:1-3) Ni nani angeweza kutabiri maelezo ya matukio hayo ya kihistoria isipokuwa Mungu tu?

Tumetaja mifano tatu inayoonyesha namna Mungu alitabiri matukio ya wakati unaokuja bila kukosea, na kuna mifano mingine mingi. Yoshua, kiongozi wa taifa la Israeli alitaja jambo moja la hakika lenye wasikilizaji wake walijua sana. Alisema hivi: ‘Munajua vema kwa mioyo yenu yote na kwa nafsi zenu zote kwamba halikukosa kutimia hata neno moja kati ya maneno yote mema ambayo Yehova Mungu wenu amewaambia ninyi. Yote yametimia kwenu. Halikukosa kutimia hata neno moja kati ya hayo.’ (Yoshua 23:1, 2, 14) Watu wa Yoshua hawangeweza kusema kwamba ahadi na unabii mbalimbali wa Mungu havikutimia. Lakini namna gani Mungu anatimiza mambo yote anayotabiri? Kuna tofauti kubwa kati ya njia za Mungu na za wanadamu. Ni lazima ujue jambo hilo, kwa sababu Mungu ametangaza mambo fulani makubwa juu ya wakati unaokuja ulio karibu, mambo hayo yatakuwa na matokeo kabisa katika maisha yako.

UNABII MBALIMBALI WA MUNGU UKO TOFAUTI NA MATABIRI YA WANADAMU

Mambo wanadamu wanatabiri mara nyingi yanategemea mambo kama vile uchunguzi wa kisayansi, uchunguzi wa mambo ya hakika na hali ya mambo, ao hata watu wanaojisema kuwa wana uwezo unaopita wa mwanadamu. Kisha kutabiri, kwa kawaida watu wanangojea tu kile ambacho kitatokea, bila kuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote.—Methali 27:1.

Tofauti na wanadamu, Mungu anajua mambo yote ya hakika. Anaelewa vizuri kabisa hali na mielekeo ya wanadamu; kwa hiyo, ikiwa anachagua kufanya hivyo, anaweza kuona mbele ya wakati namna mutu mumoja-mumoja na mataifa mazima yatatenda. Lakini Mungu anaweza kufanya mengi zaidi ya hayo. Anaweza hata kuongoza na kubadilisha mambo na mielekeo ili kufanya mambo aliyotabiri yatimie. Anasema hivi: “Neno langu linalotoka katika kinywa changu . . . Halitarudi kwangu bila matokeo, . . . na hakika litafanikiwa.” (Isaya 55:11) Nyakati fulani, unabii wa Mungu unatuambia tu mambo atafanya wakati unaokuja. Sikuzote, mambo Mungu anatabiri, yanatimia bila kukosea.

WAKATI WAKO UNAOKUJA

Je, kuna unabii fulani wenye kutegemeka unaohusu wakati wako unaokuja na wakati unaokuja wa watu unaowapenda? Ikiwa unajua mbele ya wakati kwamba kutakuwa upepo mukali, unaweza kujitayarisha ili kuokoa maisha yako. Unaweza kufanya hivyo pia kuhusu unabii wa Biblia. Mungu amesema kwamba mabadiliko makubwa katika dunia nzima yatatokea hivi karibuni. (Soma kisanduku “ Mambo Mungu Amefunua Juu ya Wakati Unaokuja.”) Wakati huo unaokuja ni tofauti kabisa na yale watu wengi wanaoitwa kuwa wenye elimu wanatabiri.

Tunaweza kueleza jambo hilo kwa njia hii: Kuna mupango fulani kuhusu dunia hii. Kupitia unabii mbalimbali wa Biblia, unaweza kujua matokeo ya mwisho ya mupango huo. Mungu anasema kwamba ‘anatangaza tangu mwanzo ule mwisho’ na kwamba ‘shauri lake mwenyewe litasimama na kila jambo ambalo ni mapenzi yake atafanya.’ (Isaya 46:10) Wewe na familia yako munaweza kufurahia wakati muzuri sana unaokuja. Uwaulize Mashahidi wa Yehova juu ya mambo Biblia inasema kuhusu matukio ya wakati unaokuja. Mashahidi wa Yehova si wachawi wanaotabiri wakati unaokuja; na hawaseme kwamba wao wanasikia sauti za roho wala kusema kuwa wana uwezo fulani wa pekee wa kutabiri mambo. Wao ni wanafunzi wa Biblia wanaoweza kukuonyesha mambo mazuri yenye Mungu anakutayarishia kwa ajili ya wakati unaokuja.