Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Kwa kweli, ni nani mwenye kuitawala dunia hii?

Ikiwa Mungu ndiye mwenye kutawala dunia, sababu gani inajaa mateso?

Watu wengi wanaamini kwamba Mungu wa kweli ndiye mutawala wa dunia hii. Lakini ingekuwa hivyo, je, dunia ingejaa mateso? (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Kulingana na Biblia, dunia inatawaliwa na mutu fulani muovu.—Soma 1 Yohana 5:19.

Namna gani mutu muovu alifikia kuwa mutawala wa wanadamu? Kwenye mwanzo wa historia ya wanadamu, malaika mumoja alimuasi Mungu na akamuchochea mwanaume na mwanamuke wa kwanza wamuasi pia Mungu. (Mwanzo 3:1-6) Mwanaume na mwanamuke huyo walichagua kumutii malaika huyo muasi, Shetani, na kumufanya kuwa mutawala wao. Mungu Mweza-Yote ndiye peke yake Mutawala anayefaa, lakini anataka watu wachague utawala wake kwa sababu wanamupenda. (Kumbukumbu la Torati 6:6; 30:16, 19) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu wengi wamedanganywa na wamechagua vibaya kama mwanaume na mwanamuke wa kwanza.—Soma Ufunuo 12:9.

Ni nani atakayemaliza magumu ya watu?

Je, Mungu atamuacha Shetani aendelee na utawala wake muovu? Hapana! Mungu atamutumia Yesu ili kuondoa uovu wote ambao Shetani ametokeza.—Soma 1 Yohana 3:8.

Kwa nguvu za Mungu, Yesu atamuharibu Shetani. (Waroma 16:20) Kisha, Mungu atatawala wanadamu na kuwarudishia maisha ya furaha na amani yenye alikusudia wawe nayo tangu mwanzoni.—Soma Ufunuo 21:3-5.