Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | SABABU GANI MAMBO MABAYA YANAFIKIA WATU WAZURI?

Mambo Mabaya Yanafikia Watu Wazuri—Sababu Gani?

Mambo Mabaya Yanafikia Watu Wazuri—Sababu Gani?

Kwa kuwa Yehova Mungu * ndiye Muumbaji wa vitu vyote na ni mweza-yote, watu wengi wanafikiri kwamba ni yeye ndiye anatokeza kila kitu kinachofanyika katika ulimwengu na hata mambo yote yaliyo mabaya. Lakini, ona mambo Biblia inasema juu ya Mungu wa kweli:

  • Yehova ni muadilifu [ao mwenye haki] katika njia zake zote.’—Zaburi 145:17.

  • ‘Njia zote [za Mungu] ni haki. Mungu wa uaminifu, ambaye hana ukosefu wowote wa haki; yeye ni muadilifu na munyoofu.’—Kumbukumbu la Torati 32:4.

  • “Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema.”—Yakobo 5:11.

Mungu hachochee mambo mabaya yafanyike. Hata hivyo, je, anachochea wengine wafanye mambo mabaya? Hapana kabisa. Maandiko yanasema hivi: ‘Mutu akiwa chini ya jaribu, yeye asiseme: Mungu ananijaribu.’ Sababu gani? Kwa sababu ‘Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamujaribu yeyote.’ (Yakobo 1:13) Mungu hawezi kujaribu, ao kupima mutu yeyote kwa kumuchochea atende vibaya. Na Mungu hachochee mambo mabaya yafanyike wala kuchochea wengine wafanye mambo mabaya. Kwa hiyo, ni nini, ao ni nani anayefanya mambo mabaya yatufikie?

KUWA MAHALI PASIPOFAA KWA WAKATI USIOFAA

Biblia inaonyesha sababu moja inayofanya watu wateseke. Inasema hivi: ‘Wakati na tukio lisilotazamiwa vinawapata wote.’ (Mhubiri 9:11) Wakati matukio yasiyotazamiwa ao aksidenti zinatokea, ikiwa mutu ataumia ao hapana inategemea sana mahali anapatikana wakati mambo hayo yanatokea. Karibu miaka 2000 iliyopita, Yesu Kristo alisema juu ya musiba ulioua watu 18 wakati munara ulianguka juu yao. (Luka 13:1-5) Hawakukufa kwa sababu ya namna walikuwa wanaishi zamani; walikuwa tu chini ya munara huo wakati ulianguka. Hivi karibuni, tetemeko la inchi lenye kuharibu lilitokea katika inchi ya Haiti katika Mwezi wa 01, 2010; serikali ya Haiti inasema kwamba zaidi ya watu 300000 walikufa. Watu hao wote walikufa bila kuchagua ikiwa walikuwa nani. Magonjwa pia yanaweza kumupata kila mutu wakati wowote.

Sababu gani Mungu hawalinde watu wazuri wasipatwe na mambo mabaya?

Watu fulani wanaweza kuuliza hivi: ‘Mungu hawezi kuzuia misiba kama hiyo yenye kuua isifanyike? Hawezi kulinda watu wazuri wasipatwe na misiba hiyo?’ Ili Mungu afanye hivyo, hilo linaweza kumaanisha kwamba anajua juu ya mambo mabaya mbele yatokee. Hata ikiwa Mungu ana uwezo wa kujua mbele ya wakati mambo ya wakati unaokuja, ulizo tunalopaswa kufikiria ni hili: Je, Mungu anachagua kutumia kwa njia isiyo na mipaka uwezo wake wa kujua mambo kama hayo mbele ya wakati?—Isaya 42:9.

Maandiko yanasema hivi: “Mungu wetu yuko mbinguni; kila kitu ambacho alipendezwa kufanya, amekifanya.” (Zaburi 115:3) Yehova  anafanya mambo anayoona kuwa ya lazima, lakini hafanye kila jambo ambalo ana uwezo wa kufanya. Hilo linahusu pia mambo anayotaka kujua mbele ya wakati. Kwa mufano, kisha maovu kuenea sana katika miji ya zamani ya Sodoma na Gomora, Mungu alimuambia Abrahamu, muzee wa ukoo, hivi: “Mimi nimeazimia kabisa kushuka ili nipate kuona kama wanatenda kabisa kulingana na kile kilio kilicho juu yake ambacho kimenifikia, na ikiwa sivyo, nitajua.” (Mwanzo 18:20, 21) Kwa muda fulani, Yehova hakupenda kujua kiasi cha uovu uliokuwa katika miji hiyo. Vilevile, ni wazi kwamba, Yehova hachague kujua kila kitu mbele ya wakati. (Mwanzo 22:12) Lakini hilo halionyeshe hata kidogo kwamba hakamilike ao kwamba ana uzaifu fulani. Kwa kuwa “kazi zake ni kamilifu,” Mungu anatumia kwa usawaziko uwezo wake wa kujua kimbele mambo ya wakati unaokuja ikiwa hilo linalingana na mapenzi yake; hawalazimishe wanadamu wafuate njia fulani. * (Kumbukumbu la Torati 32:4) Kwa hiyo, tunaweza kusema nini? Kwa kifupi: Mungu anachagua wakati gani na jinsi gani atatumia uwezo wake wa kujua na kupanga mambo mbele ya wakati.

Sababu gani Mungu hawalinde watu wazuri na uuaji?

WANADAMU NDIO WANALETA MAMBO MABAYA?

Sehemu fulani ya mambo mabaya inaletwa na wanadamu. Ona namna Biblia inaonyesha hatua inayoweza kuongoza kwenye matendo mabaya. ‘Kila mutu anajaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe. Kisha tamaa, wakati imetunga mimba, inazaa zambi; nayo zambi, wakati imetimizwa, inaleta kifo.’ (Yakobo 1:14, 15) Wakati wanadamu wanatenda kufuatana na tamaa zisizofaa ao wakati wanashindwa na tamaa mbaya, hilo linaweza kuwaletea matokeo mabaya. (Waroma 7:21-23) Kama vile historia inavyoonyesha, wanadamu wamefanya matendo mabaya sana na kuleta mateso mengi. Zaidi ya hayo, watu waovu wanaweza kuchochea wengine wawe waovu, na kuendeleza mambo mabaya.—Methali 1:10-16.

Wanadamu wamefanya matendo mabaya sana na kuleta mateso mengi

Mungu anapaswa kuingilia mambo na kuzuia watu wasifanye mabaya? Fikiria namna mwanadamu aliumbwa. Maandiko yanasema kwamba Mungu alimuumba mutu kwa sura yake mwenyewe, ni kusema, kwa mufano wake. Kwa hiyo, wanadamu wana uwezo wa kuonyesha sifa za Mungu. (Mwanzo 1:26) Wanadamu walipewa zawadi ya uhuru wa kuchagua na wanaweza kuchagua kumupenda Mungu na kushikamana naye kwa kufanya mambo yaliyo sawa machoni pake. (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20) Ikiwa Mungu angewakaza watu wafuate njia fulani, angeondoa zawadi ya uhuru wa kuchagua, sivyo? Hilo lingefanya wanadamu wakuwe tu kama mashine, wakifanya mambo ambayo wamepangiwa kufanya. Ingekuwa pia hivyo ikiwa kila kitu tunachofanya na kila kitu kinachotufikia kimepangwa mbele ya wakati, ao kuongozwa na majaliwa, ao Kismet. Sisi ni wenye furaha sana kuona kwamba Mungu anatuheshimu kwa kuturuhusu tuchague njia yetu wenyewe! Lakini, hilo halimaanishe kwamba maovu yaliyoletwa na kosa la mwanadamu na uchaguzi mubaya yataendelea kuwatesa wanadamu milele.

 MATESO YETU YANALETWA NA KARMA?

Watu wengi wa dini ya Kihindu ao ya Kibuda wanaamini fundisho la kwamba mutu anapokufa anazaliwa katika mwili mwengine na fundisho la Karma. Karma ni nini? Karma ni fundisho la kwamba matendo mutu alifanya katika maisha yake ya zamani ndiyo yanayofanya akuwe namna iko katika hali ya sasa. Kwa hiyo, ikiwa unamuuliza mutu fulani wa dini ya Kihindu ao ya Kibuda ulizo lililo kwenye ukurasa wa kwanza wa gazeti hili, labda unaweza kusikia jibu hili: “Mambo mabaya yanafikia watu wazuri kwa sababu ya sheria ya Karma. Wanavuna matunda ya mambo waliyofanya katika maisha yao ya zamani.” *

Kuhusu fundisho la Karma, ni vizuri kuona mambo Biblia inasema juu ya kifo. Katika bustani ya Edeni, kwenye wanadamu walianzia, Muumbaji alimuambia Adamu, mutu wa kwanza hivi: ‘Matunda ya kila muti wa bustani unaweza kula mupaka ushibe. Lakini kuhusu matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya usikule, kwa maana siku utakapokula, utakufa hakika.’ (Mwanzo 2:16, 17) Adamu hangefanya zambi kwa kukosa kumutii Mungu, angeishi milele. Kifo kilimufikia Adamu kama vile malipizi ya kukosa kutii amri ya Mungu. Wakati watoto waliendelea kuzaliwa, “kifo kikaenea kwa watu wote.” (Waroma 5:12) Kwa hiyo, tunaweza kusema kwamba ‘mushahara ambao zambi inalipa ni kifo.’ (Waroma 6:23) Biblia inaeleza pia hivi: ‘Yeye ambaye amekufa ameondolewa hatia ya zambi yake.’ (Waroma 6:7) Kwa maneno mengine, kisha kufa watu hawaendelee kuazibiwa juu ya zambi walizofanya.

Mamilioni ya watu leo wanasema kwamba mateso ya wanadamu yanatokana na Karma. Mara nyingi mutu anayeamini anakubali mateso yake na mateso ya watu wengine bila kuhangaishwa sana nayo. Lakini, kulingana na wazo hilo, hakuna tumaini kwamba mambo mabaya yataisha wakati fulani. Watu wanaamini kwamba kitulizo kimoja tu chenye mutu anaweza kupata ni kuwekwa huru kutokana na hatua za kuzaliwa tena na tena ikiwa anajikaza kuwa na tabia inayokubaliwa na watu wengi na ujuzi wa pekee. Bila shaka, mawazo hayo hayapatane hata kidogo na mambo Biblia inasema. *

SABABU KUBWA INAYOFANYA KUWE MATESO!

Ulijua kwamba sababu kubwa inayofanya watu wateseke ni ‘mutawala wa ulimwengu,’ ni kusema, Shetani Ibilisi?—Yohana 14:30

 

Sababu kubwa inayofanya kuwe mateso haiko wanadamu. Shetani Ibilisi, aliyekuwa malaika muaminifu wa Mungu hapo mwanzo, “hakusimama imara katika kweli” na akaleta zambi katika dunia. (Yohana 8:44) Alianzisha uasi katika bustani ya Edeni. (Mwanzo 3:1-5) Yesu Kristo alimuita ‘yule muovu’ na ‘mutawala wa ulimwengu.’ (Mathayo 6:13; Yohana 14:30) Kwa ujumla, wanadamu wanamufuata Shetani kwa kuitika wakati anawashawishi wapuuze njia nzuri za Yehova. (1 Yohana 2:15, 16) Andiko la 1 Yohana 5:19 linasema hivi: ‘Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu.’ Kuna viumbe wengine wa roho wenye waligeuka kuwa wabaya na wamejiunga na Shetani. Biblia inaonyesha kwamba Shetani na mashetani wake ‘wanaipotosha dunia nzima inayokaliwa’ wakisababisha “ole wa dunia.” (Ufunuo 12:9, 12) Kwa hiyo, Shetani Ibilisi ndiye sababu kubwa ya mambo mabaya.

Ni wazi kwamba, haiko Mungu ndiye analeta mambo mabaya yanayofikia watu; na hafanye watu wateseke. Tofauti na hilo, aliahidi kumaliza mambo mabaya, habari inayofuata itaonyesha jambo hilo.

^ fu. 3 Yehova ni jina la Mungu kama inavyoonyeshwa katika Biblia.

^ fu. 11 Ili kujua sababu gani Mungu ameacha mambo mabaya yaendelee, soma sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ fu. 16 Ili kujua namna ile inayoitwa sheria ya Karma ilianza, soma ukurasa wa 8-12 wa broshua Ni Nini Hutupata Tunapokufa? iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

^ fu. 18 Ili kujua mambo Biblia inafundisha juu ya hali ya wafu na juu ya tumaini kwa ajili ya watu waliokufa, soma sura ya 6 na ya 7 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini?