Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

kovop58/stock.adobe.com

MUENDELEE KUKESHA!

Michezo ya Olempike Inaweza Kabisa Kuunganisha Watu?​—Biblia Inasema Nini?

Michezo ya Olempike Inaweza Kabisa Kuunganisha Watu?​—Biblia Inasema Nini?

 Wakati ya Michezo ya Olempike ya 2024, inakadiriwa kama watu miliare tano wataangalia wachezaji kutoka inchi 206 wenye watacheza ile michezo. Thomas Bach, mwenye anaongoza Kamati ya Kimataifa ya Olempike alisema hivi: ”‏Hii ni tukio yenye inaunganisha watu mu dunia na inaleta amani. Tuheshimie basi wazo yenye Michezo ya Olempike inachochea, wazo ya kwamba watu wote wanapaswa kuishi kwa amani na umoja hata kama wako tofauti.”

 Michezo ya Olempike inaweza kabisa kutimiza ile kusudi ya muzuri? Kuko tumaini ya kupata amani ya kweli na umoja?

Michezo ya Olempike itaweza kuleta amani na umoja?

 Michezo ya Olempike ya hii mwaka haichochee tu watu kufikiria mambo ya michezo. Imefanya pia matatizo kati ya watu na matatizo mu mambo ya politike yenye inagawanya watu ionekane wazi. Ile matatizo inatia ndani haki za binadamu, ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa kidini, na watu fulani kuwa maskini sana wakati wengine ni matajiri sana.

 Matukio sawa vile Michezo ya Olempike, yenye inakusanya watu kutoka inchi mingi, inafurahisha watu. Lakini, kuliko kuleta amani na umoja wa kweli, ile matukio inaonyesha na kuchochea mawazo na matendo yenye inaleta migawanyiko.

 Biblia ilitabiri tabia zenye zinafanya ikuwe nguvu leo kwa watu kuishi kwa umoja. (2 Timoteo 3:1-5) Juu ya kujua habari mingi kuhusu ule unabii wa Biblia, soma habari “Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?

Tumaini ya kweli ya kupata amani na umoja

 Biblia njo inatupatia tumaini ya kweli ya kupata amani na umoja wa kweli mu dunia yote. Inaahidi kama watu wa mu dunia yote watakuwa na umoja chini ya utawala wa guvernema ya mbinguni yenye inaitwa “Ufalme wa Mungu.”​—Luka 4:43; Matayo 6:10.

 Yesu Kristo, Mufalme wa ule Ufalme, ataleta amani mu dunia yote. Biblia inasema:

  •   “Mwenye haki atasitawi, na amani itakuwa nyingi.”​—Zaburi 72:7.

  •   “Ataokoa maskini mwenye kulilia musaada . . . Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”​—Zaburi 72:12, 14.

 Hata leo, tayari mafundisho ya Yesu imeunganisha mamilioni ya watu mu maeneo 239. Juu ni Wakristo, Mashahidi wa Yehova wa mu dunia yote wamejifunza kuwa wenye kufanya amani. Ili kujua namna wamefanya vile, soma Munara wa Mulinzi wenye kichwa “Mambo ya Kufanya Juu ya Kuachana na Chuki.”