Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kushoto: Olena Yefremkina/stock.adobe.com; katikati: lunamarina/stock.adobe.com; kuume: Rido/stock.adobe.com

MUENDELEE KUKESHA!

Ni Nani Unaweza Kutumainia?​—Biblia Inasema Nini?

Ni Nani Unaweza Kutumainia?​—Biblia Inasema Nini?

 Watu wanavunjika moyo wakati wale wenye wanaonwa kuwa wenye kutumainika hawawahangaikie. Watu wengi hawatumainie tena . . .

  •   wakubwa wa politike wenye wanahangaikia kwanza faida zao kuliko kuhangaikia mambo yenye watu wako nayo lazima.

  •   vyombo vya habari vyenye havitoe habari zenye kutumainika na za kweli.

  •   wanasayansi wenye kusudi yao haiko kusaidia watu.

  •   viongozi wa dini wenye wanategemeza viongozi wa politike kuliko kusaidia watu wamutumikie Mungu.

 Watu wako na sheria ya kuona kama haiko kila mutu njo wa kutumainia. Biblia inatupatia hii angalisho:

  •    “ Musitumainie wakubwa wala mwana wa binadamu, mwenye hawezi kuleta wokovu.”​—Zaburi 146:3.

Ule mwenye unaweza kutumainia

  Biblia inatuonyesha ule mwenye tunaweza kutumainia: Yesu Kristo. Yesu haiko tu mwanaume muzuri mwenye aliishi ku dunia kumepita miaka mingi. Mungu alimuweka Yesu kuwa “Mufalme . . . , na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (Luka 1:32, 33) Yesu ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu, ni kusema guvernema yenye iko natawala sasa mbinguni.​—Matayo 6:10.