Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA MICHANGO YAKO INATUMIWA

Kutolea Musaada Wale Wenye Walipatwa na Musiba

Kutolea Musaada Wale Wenye Walipatwa na Musiba

Tarehe 1 Mwezi wa 2, 2021

 Mu mwaka wa 2020 kulikuwa misiba mingi ya asili, na mwanzo wa coronavirus wenye kuwa mu dunia yote. Mashahidi wa Yehova walisaidia namna gani wale wenye walipatwa na ile hali?

 Mu mwaka wa utumishi wa 2020, * Halmashauri ya Waratibu ya Baraza Yenye Kuongoza, ilikubali dolare milioni 28 itolewe * ili kusaidia wale wenye walipatwa na misiba. Ile musaada ilitegemeza wale wenye walipatwa na misiba. Misiba yenye ilitokea ilikua zaidi ya 200, kutia ndani ugonjwa wa coronavirus, upepo mukali mbalimbali wenye ulitokea, maji yenye kuyala sana mu maeneo fulani ya Africa, ukosefu wa chakula mu inchi ya Venezuela, na ukame mu inchi ya Zimbabwe. Ile misaada ilisaidia kuuza chakula, maji, fasi ya kulala, manguo, na kulipia matunzo, na pia ilisaidia kujenga upya, kutengeneza, na kusafisha. Fikiria mifano fulani ya kazi yenye ilifanywa ili kusaidia.

 Coronavirus. Mu dunia yote, ule ugonjwa ulifanya ndugu na dada wakuwe na magumu ya afya kiakili na magumu ya kupata makuta. Juu ya kuwasaidia, zaidi ya Halmashauri 800 ziliwekwa mu dunia yote. Ndugu wa zile Halmashauri, walijua mahitaji ya ndugu zetu na walituma ripoti kwa ndugu wa Halmashauri ya waratibu, na ile iliwasaidia wajue muzuri zaidi namna ya kuongoza kazi ya kutoa misaada.

 Mu ile mwaka, zile Halmashauri za kutoa misaada, zilisaidia wengi kupata chakula, maji, mambo fulani juu ya usafi, na dawa. Mu maeneo fulani, zile Halmashauri zilitumika pia pamoya na wazee wa ile eneo, ili kusaidia ndugu wapate misaada ya serikali.

 Wenye hawako Mashahidi waliona kazi yetu ya kutoa misaada. Kwa mufano, Field Simwinga mwenye ni musimamizi wa wilaya ya Nakonde, mu inchi ya Zambia, aliambia hivi ndugu zetu: “Tunawashukuru sana kwa musaada wenye kufaa wenye mulitolea familia zenye zilikuwa nayo lazima kabisa.”

 Ukosefu wa Chakula mu Angola. Kwa sababu ya Coronavirus, chakula ilikuwa kidogo sana mu Angola, na tena ikakuwa bei sana. Ndugu na dada zetu wengi walikuwa na magumu sana ya kuuza chakula.

Colis za chakula zilitoka Brazili kuenda Angola

 Waliomba tawi ya Brazili itumie ndugu wa Angola chakula. Juu ya kutumia muzuri zaidi michango kwa ajili ya misaada, ndugu walitafuta kwa uangalifu njia ya muzuri zaidi ya kuuza na kutuma chakula. Juu ya kuuza na kusafirisha kila colis ya munene, iliomba tu dolare 22 na ile colis ilikuwa na kilo 20 hivi na ndani ya kila colis mulikuwa chakula sawa vile muchele, maharagi na mafuta ya kupika nayo. Kufikia leo 33 544 Colis za munene zilishasafirishwa, ile yote ilifanyiza tone 654. Tukichanga na chakula yenye iliuziwa mu inchi ya Angola, ile ilisaidia kukulisha watu zaidi ya 50 000!

 Ndugu na dada wanajisikia namna gani kuhusu musaada wenye walipata? Alexandre, mwenye anaishi mu eneo fulani ya mbali mu inchi ya Angola, anasema hivi: “Naona ile kuwa ushuhuda kama Yehova ananipenda na kama siko miye peke. Kumbe na miye najulikana mu tengenezo ya Yehova!” Mariza, mwenye iko anakomalisha watoto wake yeye peke, anasema hivi: “Yehova alisikia kilio yangu. Namushukuru sana na pia nashukuru tengenezo yake!”

Ndugu wa Angola wako wenye shukrani kwa ajili ya musaada wa chakula

 Musaada kwa Ajili ya Zimbabwe juu ya Ukame. Mu mwaka wa utumishi wa 2020, Zimbabwe ilipatwa na ukame wa nguvu sana, na ile ilifanya mamilioni ya watu wateseke sana juu ya njala. Mashahidi wengi wa Yehova wa mu Zimbabwe hawakukuwa na chakula mingi.

 Halmashauri tano ya kutoa misaada ilifanyizwa ili kutolea chakula ndugu zetu. Wahubiri wengi walisaidia kufunga chakula na kupakiza, na walikopesha gari yao juu itumikishwe. * Mu mwaka wa utumishi wa 2020, dolare 691 561 ilitumiwa ili kusaidia zaidi ya watu 22 700!

Ndugu wa Zimbabwe wanapata musaada wa chakula (mbele ugonjwa uanze)

 Mu hali fulani wakati misaada ilifika, tayari ndugu fulani walikuwa walishamaliza chakula yao. Wakati chakula ilifika, ndugu zetu walimusifu Yehova. Wamoja hata walianza kuimba wimbo za Ufalme.

 Mu eneo fulani, wajane wawili Mashahidi walienda ku mukutano wenye ulifanyizwa juu ya kuzungumuzia misaada ya chakula yenye shirika fulani yenye haiko ya serekali ilipenda kuwatolea. Lakini, ule mukutano ulianza kuzungumuzia mambo ya politike, njo maana dada zetu waliamua kukatala kufanya mambo yenye iliombwa ili kupata musaada. Na wakati walikuwa wanatoka ku ule mukutano, waliwacheka na kuwaambia, “Musikuye tena kutafuta chakula huku!” Hata vile kisha tu juma mbili, ndugu zetu walifika mu ile eneo na walipatia dada zetu chakula mbele hata ile shirika ifike!

Prisca anasema hivi: “Yehova haachake watumishi wake”

 Musaada wenye ulitolewa Zimbabwe kwa ajili ya musiba ulitoa pia ushahidi muzuri. Fikiria mufano wa Prisca mwenye kuishi mu kijiji moya ya kidogo. Ijapokuwa magumu ya ukame, Prisca alipenda kuhubiri kila siku ya tatu na siku ya tano, hata mu kipindi ya kulima mashamba. Watu wa mu ile kijiji yakewalimuzarau kwa kusema hivi: “Utatesa familia yako na njala juu ya mahubiri yako.” Prisca aliwajibia hivi: “Yehova haachake watumishi wake.” Muda kidogo kisha pale, alipata musaada wa chakula wenye tengenezo yetu ilitoa. Ile ilishangaza majirani wake fulani, wenye walimuambia Prisca hivi: “Mungu hakuachake kabisa, tunapenda kujua mengi zaidi juu yake.” Kwa sasa, majirani wake saba wako wanasikiliza mikutano yenye inapitishwaka ku radio.

 Kadiri tunakaribia mwisho, ni vile tutaendelea kupambana na misiba ya asili. (Matayo 24:3, 7) Tuko wenye shukrani sana kwa ajili ya michango yenye munatoa kupitia njia mbalimbali yenye kupatikana ku donate.pr418.com Ile michango itatumiwa muzuri ili kutolea misaada wale wenye kuteseka wakati wako nayo lazima.

^ Mwaka wa utumishi wa 2020 ulikamata Mwezi wa 9 2019 mupaka Mwezi wa 8 2020.

^ Dolare zote zenye kuzungumuziwa mu hii habari, inazungumuzia dolare ya Amerika.

^ Juu ya vizuizi vyenye vilitiliwa juu ya coronavirus, iliomba ndugu zetu wapewe ruhusa juu ya kutoa chakula. Walikuwa pia waangalifu juu ya kupunguza hatari ya kuambukizwa na ule ugonjwa.