Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA MICHANGO YAKO INATUMIWA

Nyimbo Zenye Zinatusaidia Kumukaribia Mungu

Nyimbo Zenye Zinatusaidia Kumukaribia Mungu

TAREHE 1, MWEZI WA 11, 2021

 Muziki ni zawadi ya muzuri kutoka kwa Yehova. Inaweza kabadilisha mawazo yetu, hisia yetu, na inaweza kutuchochea. Ile njo mambo inamufikiaka mutu kama anasikiliza nyimbo zetu za pekee. Zaidi ya ile, zinaweza kutusaidia kumukaribia Yehova.

 Tangu 2014, nyimbo za pekee zaidi ya 70 zimetolewa. Na sasa, karibu wimbo moya unapatikana mu zaidi ya luga 500! Lakini, unaweza kujiuliza, “Nani anafanyaka zile nyimbo, na zinatolewaka namna gani?’

Namna Ndugu Wanafanyaka Zile Nyimbo

 Ndugu na dada wa mu Idara ya Audio-video njo wanafanyaka ile kazi. Ile Idara inasimamiwa na Halmashauri ya Ufundishaji ya Baraza Yenye Kuongoza. Kuko kikundi ya ndugu na dada 13 wenye wanatunga, wanapanga muziki, na mambo ingine. Zaidi ya ile, Halmashauri ya Ufundishaji imekubali wajitoleaji mu dunia yote wasaidie ku ile kazi. Kati yao kuko wenye kutunga muziki, wapiga-muziki, na waimbaji. Wale ndugu na dada wanatumia kwa unyenyekevu uwezo wenye wako nao, bila kutafuta kujulikana ao kusifiwa.

 Wimbo wa pekee unafanywa namna gani? Kwanza, Halmashauri ya Ufundishaji inaamua wimbo utategemea andiko gani, na namna mutu anaweza kujisikia wakati anasikia wimbo. Kisha, ile kikundi inachagua wenye watatunga muziki na wenye wataandika maneno. Rekodi ya kwanza inafanywa. Halmashauri ya Ufundishaji inaichunguza na kuleta mapendekezo zaidi. Kisha ile kikundi inafanya marekebisho fulani na rekodi ya mwisho inafanywa. Zile nyimbo zinarekodiwa fasi mbalimbali, sawa vile mu biro za tawi, ao mu nyumba za watu wenye wako na vyombo vya kurekodia.

 Kwa mufano, juu ya kutunga na kurekodi nyimbo za pekee, ndugu zetu wanatumia ordinatere za kukamata sauti, programu ya kuandika alama za muziki, na mukusanyo wa sauti. Inaomba pia kutumia vyombo vya muziki, vyombo vya kuchanga sauti, vikuza-sauti, na mikrofone. Mikrofone inaweza kuwa na bei ya dolare 100 mupaka zaidi ya dolare 1 000. Mu 2020, tulitumia dolare 116 000 juu ya kuuza vyombo vya kurekodi muziki.

 Nini inafanywa juu yakutumia muzuri michango? Kuliko kutumia ndugu na dada wengi mu mambo ya muziki ku Beteli, tunatumia wajitoleaji wengi wa inje. Zaidi ya ile, kuliko kutia pamoja wapiga muziki wengi juu ya kurekodi wimbo fulani, mara mingi ndugu zetu wanatunga na kutoa muziki kwa kutumia ordinatere.

“Zinanisaidia Kuwa na Imani ya Nguvu”

 Ndugu na dada wanapendaka kusikiliza nyimbo za pekee. Tara, mwenye kuishi Alemanye, anasema hivi: “Nyimbo za pekee zinanisaidiaka kutulia wakati niko na mahangaiko. Kuzisikia mu luga yangu ya kizalikio inafanyaka nisikie sawa vile Yehova ananikumbatia.” Dmitry, ndugu wa Kazakstan, anasema hivi: “Napendaka kusikiliza zile nyimbo juu sina lazima ya kujiuliza kama zinapatana na kanuni za Biblia ao hapana. Zaidi ya ile, zinanisaidia kukaza akili juu ya mambo ya kiroho.”

 Delia, wa mu Afrika ya Kusini, anaonyesha mawazo yenye iko nayo juu ya nyimbo za pekee: “Zimenisaidia nikuwe na imani ya nguvu. Wakati ninavunjika moyo ao niko na magumu fulani, sikosake wimbo fulani wenye unapatana kabisa na hali yangu. Mara mingi kusikiliza tu wimbo fulani wa pekee kunabadilishaka namna najisikia.”

 Kuko nyimbo fulani zenye watu wanapendaka zaidi. Lerato, mwenye anaishi pia Afrika ya Kusini, anasema hivi: Wimbo wenye kichwa ‘Iko Karibu Sana’ na ‘Dunia Mupya Yenye Kuja’ unanisaidiaka kuwazia siku yenye nitakaribishaka tena mama yangu mupendwa. Kila wakati kama nasikiliza zile nyimbo, naonaka sawa vile mama yangu iko nakuya kunikumbatia.”

 Kuko wimbo fulani wa pekee wenye ulisaidia sana kijana fulani wa mu Sri Lanka. Anasema hivi: “Mwalimu wangu wa sayansi alinifokea sana mbele ya wanafunzi wenzangu juu niko Shahidi wa Yehova. Niliogopa, na sikujua niseme nini. Wakati nilirudia ku nyumba, mama yangu alinitia moyo nisikilize wimbo wenye kichwa Étudier rend fort.’ Ule wimbo ulinisaidia kuona ulazima wa kufanya utafiti na kutayarisha jibu. Kesho yake nilizungumuza na mwalimu wangu. Alinisikiliza na alisema kama anaelewa sasa muzuri mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanaamini. Nashukuru tengenezo ya Yehova kwa kutupatia nyimbo zenye kutia moyo.”

 Tunapataka wapi makuta ya kutusaidia kufanya zile nyimbo? Tunatumia michango yenye inatolewa kwa ajili ya kazi ya mu dunia yote. Michango mingi inatolewaka kupitia njia zenye kuonyeshwa ku donate.pr418.com. Tunakushukuru sana kwa michango yako ya kujipendea.