Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Mashahidi wa Yehova wa Nouvelle-Zélande Ni Wakristo Wenye Kufanya Amani na Wanyoofu

Mashahidi wa Yehova wa Nouvelle-Zélande Ni Wakristo Wenye Kufanya Amani na Wanyoofu

Tarehe 21 Mwezi wa 10, 1940 wakubwa wa inchi ya Nouvelle Zélande walisema kama Mashahidi wa Yehova ni “tengenezo ya mubaya na kama iko inatia mu hatari usalama wa watu” Ijapokuwa magumu yenye ilitokana na ile uamuzi, Mashahidi wa Yehova hawakuvunjika moyo. Kwa mufano, waliendelea kukusanyika ili kufanya ibada, hata kama ile ingefanya wakuwe mu hatari ya kufungwa na polisi.

Andy Clarke, mwenye hakukuwa Shahidi, alikuwa bwana ya Mary, mwenye alikuwa Shahidi. Aliona ushikamanifu wa bibi yake wa kuhuzuria mikutano ijapokuwa hatari. Lakini alikuwa anaogopea bibi yake asifungwe wakati wa mikutano. Andy alianza kusindikiza bibi yakeku mikutano hata kama mu hali ya kawadia Andy angefanya vile. Alimuambia hivi bibi yake: “Kama wanapenda kukufunga, na miye batanifunga.” Kuanzia pale, Andy alihuzuria karibu mikutano yote pamoja na bibi yake. Kisha wakati fulani, Andy akakuwa Shahidi wa Yehova. Wakati ya Vita ya Pili ya Ulimwengu, Mashahidi wa Yehova wengi wa Nouvelle-Zélande walibakia washikamanifu sawa Mary hata kama waliteswa.

Wanaendelea kuwa Kuwa Wenye Bidii Hata Kama Wako mu Gereza

Siku moya, polisi walimufunga John Murray, mwenye alikuwa na miaka 78, wakati alikuwa anahubiri nyumba kwa nyumba. Tribinalil ilimuhukumu sababu alikuwa anaunga mukono mambo ya “tengenezo fulani ya mubaya.” Mashahidi wengine wengi walipelekwa ku tribinali. Wamoja walilipa amande, wengine walifungwa kwa muda wa miezi tatu.

Kwa kuheshimia zamiri yao yenye kufundishwa na Biblia, Mashahidi wengi walikatala kufanya kazi ya jeshi. (Isaya 2:4) Juu ya ile, wengi walipata magumu sana wakati walikatala kufanya kazi ya jeshi. Karibu asilimia 80 ya Mashahidi (ao 80%) wenye walikatala kuwa maskari walifungwa muda wote wa vita. Ijapokuwa gereza, kuwatesa na baridi ya nguvu yenye ilikuwa ile wakati, wale wandugu waliendelea kumuabudu Yehova kwa furaha.

Mu fasi mbalimbali kwenye walifungwa, Mashahidi wa Yehova walikamata mipango fulani ya kiroho bila kukawia.. Saa tu vile inakuwaka mu makutaniko, walifanya mikutano na wakachukua mipango ya kuhubiria wafungwa wengine. Mu ma kambi fulani kwenye walifungwa, waliruhusiwa hata kufanya mikutano wakichungwa na mulinzi. Wafungwa fulani walivumbula kweli na wakabatizwa mulemule mu kambi.

Kuhusu Bruce, mutoto mudogo zaidi wa Mary na Andy, wenye tulishazungumuzia, kufungwa ilimusaidia kukomalisha imani yake na kuongeza ujuzi wake wa Biblia. Anakumbuka: “Kwangu miye, ilikuwa sawa vile kuenda ku masomo, juu nilikuwa na nafasi ya muzuri ya kuzungumuza na ndugu wenye uzoefu sana wenye walikuwa mu kambi, na pia kufaidika na ujuzi wao.”

Mu 1944, serikali ilifikiria kutosha Mashahidi fulani wenye walikuwa mu gereza. Lakini wakubwa wa jeshi walikatala ile uamuzi, juu waliamini kama ikiwa Mashahdi wangekuwa huru wangeendelea kutangaza imani yao. Ripoti ya jeshi ilikuwa inasema hivi: “Hata kama wanafungwa kwa muda murefu zaidi ile inaweza kusaidia kwa kiasi fulani, lakini haitafanya waache imani yao.”

Hawatie Usalama wa Watu mu Hatari

Mateso yenye Mashahidi wa Yehova walipata ilifanay watu waseme sana juu yao, na wengine walipenda kujua mengi zaidi kuwahusu. Walivumbula kama Mashahidi hawako hatari, tena ni wenye kufanya amani. Ile ilikuwa na matokeo gani? Mu 1939 hesabu ya Mashahidi wa Yehova mu Nouvelle-Zélande ilikuwa 320. Lakini mu 1945 wakakuwa 536!

Wakubwa fulani wa serikali wenye kuwa na mawazo tofauti na wengine walifikia kusema kama Mashahidi wa Yehova walitendewa mu njia yenye haiko ya haki. Kisha kusikia shitaka yenye walileta juu ya ndugu yetu moja, muamuzi aliona kama ile kesi haitachungwa, na ikabakie vile. Alisema hivi: “Kwangu miye na kulingana na sheria haiko haki kusema kama kazi ya kugawanya Biblia ni kosa.”

Wakati kazi ya kuhuburi iliruhusiwa tena ku mwisho wa vita, Mashahidi wa Yehova waliazimia kabisa kusaidia watu wengi kadiri inawezekana wafikie kujua Ufalme wa Mungu mu Nouvelle-Zélande. Mu 1945, biro ya tawi ilitumia makutaniko yote ya Nouvelle-Zelanda barua. Ile barua ilisema hivi: “Siye wote tukuwe wenye busara, wenye urafiki, na wema kwa watu wote Tuepuka mabishano na kukosana-kosana.. Tusisahau kama watu wenye tunakutana na walishashikilia imani yao . [...] Wengi kati yao ni kondoo za Bwana zenye tunapaswa kupeleka kuongoza kwa Yehova na Ufalme wake.”

Leo, Mashahidi wa Yehova waNouvelle-Zélande wanaendelea kujulisha habari njema kwa wakaaji wa inchi, lakini pia kwa waturiste . Siku moya, mu muji wa Turangi, mu saa kidogo tu, Mashahidi wa Yehova ine walizungumuza pamoja nana watu 67 wenye walikuja kutembelea Nouvelle-Zelande. Na wale watu walitoka mu inchi 17!

Watu wa Nouvelle-Zelande wameelewa kama Mashahidi wa Yehova ni Wakristo weney kufanya amani na pia wanyoofu wenye wanapenda sana kweli zenye kuwa mu Biblia. Kila mwaka,mamia ya watu wanabatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova. Mu 2019, zaidi ya Mashahidi 14 000 walikuwa wanamusifu Yehova kwa furaha mu ile inchi!

Mukutano moja kwa ajili ya kujifunza Biblia wenye ulifanywa kisha kazi yetu kukatazwa mu 1940

Chumba za mutu moja mu kambi ya Kisiwa ya Kaskazini, mu Nouvelle-Zélande

Kambi ya Hautu, ku Kisiwa ya Kaskazini

Mu1949: Kikundi ya Mashahidi wenye walifungwa juu walikatala kujiingiza mu kazi ya jeshi