WIMBO 107
Tuonyeshe Upendo Kama Mungu
-
1. Yehova Mungu alituwekea
Mufano muzuri.
Alionyesha upendo mukubwa
Kwa kutoa Yesu Kristo,
Ili akuye kufunika zambi,
Tukombolewe mu magumu yetu.
Upendo wake ni mukubwa sana
Mungu wetu ni wa ajabu.
-
2. Kama Yehova, tukuwe tayari
Kupenda wengine.
Tuwaonyeshe upendo wa kweli,
Na tukuwe na umoja.
Hatutasema tunapenda Mungu,
Lakini tuko tunachukiana.
Kwa hiyo basi, tuhurumiane.
Tupendane kwa moyo wote.
-
3. Tuko katika familia moja
ya Mungu wa kweli.
Tuko tayari kusaidiana
Mu wakati wa magumu.
Umoja wetu unategemea
Neno ya Mungu pia roho yake.
Basi tupende ndugu zetu wote
Mu maisha ya kila siku.
(Ona pia Ro. 12:10; Efe. 4:3; 2 Pe. 1:7.)