Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tabia za Mubaya

Tabia za Mubaya

Wakristo wanapaswa kuepuka tabia gani za mubaya?

Kasirani

Zb 37:​8, 9; Mez 29:22; Kol 3:8

Ona pia Mez 14:17; 15:18

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 37:​18, 19, 23, 24, 31-35—Ndugu za Yosefu wanamushambulia, wanamuuzisha mu utumwa, na wanamudanganya Yakobo kama munyama wa pori ameua mutoto wake mupendwa

    • Mwa 49:​5-7—Simeoni na Lawi wanapata laana juu ya kasirani yao kali

    • 1Sa 20:​30-34—Juu ya kasirani, Mufalme Sauli anamutukana mutoto wake Yonatani na anajaribu kumuua

    • 1Sa 25:​14-17—Nabali anatukana wanaume wa Daudi na anajitia mu hatari yeye na watu wa nyumba yake

Ugomvi

Woga

Kutendea wengine kwa ukali

Kum 15:​7, 8; Mt 19:8; 1Yo 3:17

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 42:​21-24—Ndugu za Yosefu wanakumbuka kwa huzuni namna walimutendea Yosefu kwa ukali

    • Mk 3:​1-6—Yesu anaumizwa sana na ukali wa Wafarisayo

Kukosa heshima

Ona “Kukosa Heshima

Kujiona kuwa wa maana

Gal 5:26; Flp 2:3

Ona pia Mez 3:7; 26:12; Ro 12:16

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Sa 15:​1-6—Absalomu anajionyesha na anapenda kufanya watu wamufuate yeye kuliko kumufuata Mufalme Daudi, baba yake

    • Da 4:​29-32—Mufalme Nebukadneza iko na kiburi, na ile inafanya Yehova amupatie nizamu

Tamaa; wivu

Ro 13:9; 1Pe 2:1

Ona pia Gal 5:26; Tit 3:3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 26:​12-15—Yehova anabariki Isaka mwenye kutumika kwa bidii, na Wafilisti wanaanza kumusikilia wivu

    • 1Fa 21:​1-19—Mufalme muovu Ahabu anatamani shamba ya Naboti, na ile inafanya akamate mipango ya kumuua

Kuogopa watu

Zb 118:6; Mez 29:25; Mt 10:28

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Hes 13:​25-33—Wapelelezi kumi Waisraeli wanaogopa na wanafanya wengine waogope

    • Mt 26:​69-75—Juu ya kuogopa wanadamu, mutume Petro anafikia kumukana Yesu mara tatu

Tamaa

Ona “Tamaa

Chuki

Unafiki

Ona “Unafiki

Wivu

Ona “Wivu

Uvivu

Kupenda makuta na vitu vya kimwili

Mt 6:24; 1Ti 6:10; Ebr 13:5

Ona pia 1Yo 2:​15, 16

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yob 31:​24-28—Hata kama iko tajiri, Yobu anaepuka mutego wa kupenda vitu vya kimwili

    • Mk 10:​17-27—Juu anapenda sana vitu vyenye iko navyo, mwanaume moya tajiri anashindwa kuviacha juu ya kumufuata Yesu

Uchungu wenye uovu

1Sa 30:6; Efe 4:31; Kol 3:19

Ona pia Yak 3:14

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Oba 10-14—Mungu anahukumu Waedomu juu walitendea ndugu zao, Waisraeli, kwa uchungu wenye uovu

Kimbelembele

Ona “Kimbelembele

Kiburi; majivuno

Ona “Kiburi

Kupenda ugomvi

Mez 26:20; 1Ti 3:​2, 3; Tit 3:2

Ona pia Mez 15:18; 17:14; 27:15; Yak 3:​17, 18

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 13:​5-9—Ugomvi unatokea kati ya wachungaji wa mifugo ya Abrahamu na wa mifugo ya Loti, lakini Abrahamu anafanya amani

    • Amu 8:​1-3—Watu wa Efraimu wanatafuta ugomvi na Muamuzi Gideoni, lakini unyenyekevu wa Gideoni unasaidia kukuwe amani

Uasi

Kuwa mwenye haki kupita kiasi

Muh 7:16; Mt 7:​1-5; Ro 14:​4, 10-13

Ona pia Isa 65:5; Lu 6:37

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mt 12:​1-7—Yesu anaonyesha wazi mwelekeo wa Wafarisayo wa kuwa wenye haki kupita kiasi

    • Lu 18:​9-14—Yesu anatumia mufano juu ya kuonyesha kama wenye kuwa wenye haki kupita kiasi hawawezi kukubaliwa na Yehova

Kuwa kichwa-nguvu

Yer 13:10

Ona pia Yer 7:​23-27; Zek 7:​11, 12

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Ny 36:​11-17—Sedekia anajionyesha kuwa mufalme muovu na mwenye kichwa-nguvu, na ile inafanya watu wake wateseke

    • Mdo 19:​8, 9—Mutume Paulo anaachana na watu wenye wanakatala kuamini habari njema juu ya kichwa-nguvu

Kukosa usawaziko

Mk 7:​21-23; Efe 5:17

Ona pia 1Pe 2:15

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 8:​10-20—Waisraeli wanajibia nabii Samweli bila usawaziko wakati anawaambia juu ya nini haiko jambo ya hekima kuwa na mufalme mwanadamu

    • 1Sa 25:​2-13, 34—Nabali anakatala kukubali ombi yenye usawaziko ya musaada; ile inaletea watu wote wa nyumba yake matatizo

Kuwazia mutu mubaya na kumushitaki kwa uongo

Yob 1:​9-11; 1Ti 6:4

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • 1Sa 18:​6-9; 20:​30-34—Mufalme Sauli anamuwazia Daudi mubaya; anawaza kama haiko mushikamanifu, na anajaribu kufanya Yonatani amuchukie Daudi