Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 32

Namna Mungu Alimulinda Yesu

Namna Mungu Alimulinda Yesu

WAKATI fulani Yehova anafanyaka mambo ya kushangaza juu ya kulinda viumbe vyake vyenye haviyakomala na vyenye haviwezi kujilinda. Kama unatembea mu pori, utaona namna Yehova anafanyaka vile. Pengine ku mwanzo hautaelewa mambo yenye iko napitikana.

Unaona ndege inashuka karibu na weye, inaonekana sawa vile imelumia. Wakati unapima kuikaribia, inakokota bawa yake moya na inaenda mbali. Wakati unaendelea kuifuata, inaendelea kuenda mbali na weye. Kisha mara moya inaruka. Haikukuwa nalumia hata kidogo. Unajua juu ya nini ilifanya vile?​—

Ilikuwa imeficha vitoto vyake karibu na pale kwenye ilishukia. Ile ndege ilikuwa naogopa kama utaona vitoto vyake na kuviumiza. Kwa hiyo ilijifanya sawa vile inalumia juu ikupeleke mbali. Unajua nani njo anaweza kutulinda sawa vile ndege inalindaka vitoto vyake?​—Biblia inafananisha Yehova na ndege mwenye kuitwa tai, ile ndege inasaidiaka vitoto vyake.​—Kumbukumbu la Torati 32:11, 12.

Ndege iko nafanya nini juu ya kulinda vitoto vyake?

Mutoto mupendwa sana wa Yehova ni Yesu. Wakati Yesu alikuwa mbinguni, alikuwa kiumbe wa roho mwenye nguvu sana sawa Baba yake. Angeweza kujilinda. Lakini wakati alizaliwa sawa mutoto ku dunia, hakukuwa na nguvu na alikuwa na lazima ya mutu wa kumulinda.

Juu Yesu atimize mambo yenye Mungu alimutuma afanye ku dunia, iliomba akomale akuwe mutu muzima mwenye kuwa mukamilifu. Lakini Shetani alijaribu kumuua wakati alikuwa angali mutoto. Namna Shetani alijaribu kumuua Yesu na namna Yehova alimulinda, ni hadisi yenye kufurahisha sana. Unapenda kuisikia?​—

Wakati fulani kisha Yesu kuzaliwa, Shetani alifanya kitu fulani yenye kufanana na nyota ionekane mu anga mu eneo ya mashariki. Wanaume wenye kujifunza nyota walifuata ile nyota na ikawapeleka Yerusalemu. Wakati walifika, waliuliza ni wapi njo mufalme wa Wayahudi alipaswa kuzaliwa. Wakati wale wenye kujua mambo yenye Biblia inasema waliulizwa, walijibia hivi: “Katika Betlehemu.”​—Matayo 2:1-6.

Kisha watu wenye kujifunza nyota kumutembelea Yesu, Mungu aliwapatia onyo gani yenye iliokoa uzima wa Yesu?

Wakati Herode, mufalme mubaya wa Yerusalemu, alisikia kama kuko mufalme mwenye alikuwa amezaliwa mu muji wa Betlehemu wenye ulikuwa karibu, aliambia wale watu wenye kujifunza nyota hivi: “Mutafute kwa uangalifu ule mutoto mudogo, na wakati mutamupata, muniletee habari.” Unajua juu ya nini Herode anapenda kujua kwenye Yesu iko?​— Ni juu iko na wivu na anapenda kumuua!

Mungu alifanya nini juu ya kulinda Mwana wake?​— Wakati wale watu wenye kujifunza nyota walimupata Yesu, walimupatia zawadi. Kisha Mungu akawaonya mu ndoto wasirudie kwa Herode. Kwa hiyo, wakarudia kwao bila kupita Yerusalemu. Wakati Herode alipata habari kuwa wale watu wenye kujifunza nyota wamerudia kwao, alikasirika sana. Sasa juu aue Yesu, aliomba watoto wote wanaume wa Betlehemu wenye kuwa chini ya miaka mbili wauawe. Lakini Yesu hakukuwa tena Betlehemu.

Unajua namna Yesu aliponyoka?​— Wakati wale watu wenye kujifunza nyota walirudia kwao, Yehova aliambia Yosefu, bwana ya Maria, atoke Betlehemu na wakimbilie Misri. Kule Herode hangeweza kumutendea Yesu mubaya. Kisha miaka fulani, wakati Yosefu na Maria walirudia kutoka Misri pamoya na Yesu, Mungu aliambia tena Yosefu jambo ya kufanya. Alimuambia waende Nazareti juu kule Yesu angekuwa salama.​—Matayo 2:7-23.

Mungu alifanya nini tena juu ya kumuokoa Yesu?

Unaona vile Yehova alilinda Mwana wake?​— Unaweza kusema ni nani njo iko sawa vitoto vya ndege vyenye mama yao alificha ao sawa vile Yesu wakati alikuwa mutoto? Ni weye, hauone vile?​— Na weye kuko watu wenye wanapenda kukutendea mubaya. Unajua ni nani?​—

Biblia inasema kama Shetani iko sawa vile simba mwenye kunguruma mwenye anapenda kutumeza. Sawa vile simba anashambuliaka wanyama wa kidogo-kidogo, Shetani na mashetani wake wanashambuliaka watoto. (1 Petro 5:8) Lakini, Yehova iko na nguvu kuliko Shetani. Yehova anaweza linda watoto wake ao kuondoa kitu yoyote ya mubaya yenye Shetani anawafanyia.

Vile tulijifunza mu sura ya 10 ya hii kitabu, unakumbuka jambo yenye Shetani na pepo wake wachafu wanajaribu kutuchochea tufanye?​— Njo vile, wanajaribu kutuchochea tufanye ngono yenye Yehova anakataza. Nani tu njo wanapaswa kufanya ngono?​— Njo vile, mwanaume na mwanamuke wenye kukomala wenye wameoana.

Lakini, inahuzunisha kuona kama kuko watu wenye kukomala wenye wanapenda kufanya ngono na watoto. Wakati wale watu wenye kukomala wanafanya vile, watoto wanaume na watoto wanamuke wanaweza kuanza kufanya mambo ya mubaya yenye wale watu wenye kukomala walikuwa wanafanya. Wanaweza pia kuanza kutumia viungo vyao vya uzazi mu njia ya mubaya. Njo vile mambo ilikuwaka zamani sana mu muji wa Sodoma. Biblia inasema kama watu wa kule Sodoma, “kuanzia kijana mwanaume mupaka muzee,” walijaribu kufanya ngono na wanaume wenye walitembelea Loti.​—Mwanzo 19:4, 5.

Sawa vile Yesu alikuwa na lazima ya mutu wa kumulinda, na weye uko na lazima ya mutu wa kukulinda juu kuko watu wazima na hata watoto wengine wenye wanaweza kujaribu kufanya ngono na weye. Mara mingi wale watu watajifanya sawa vile ni marafiki wako. Wanaweza hata kukupatia zawadi kama unaitika kuwa hautaambia mutu mwingine mambo yenye wanapenda kufanya na weye. Lakini wale watu wanajifikiria tu wao wenyewe, sawa vile Shetani na pepo wake wachafu. Wanapenda tu kujifurahisha kwa kufanya ngono na watoto. Ile ni mubaya sana!

Unajua wanaweza kufanya nini juu wajifurahishe?​— Wanaweza kujaribu kugusa-gusa viungo vyako vya uzazi. Ao wanaweza hata kupitisha viungo vyao vya uzazi ku viungo vyako vya uzazi. Lakini haupaswe kuacha mutu yeyote achezee kiungo yako ya uzazi. Hata akuwe kaka yako ao dada yako ao mama yako ao baba yako. Vile viungo ni vyako weye peke.

Unaweza kusema nini ao kufanya nini wakati mutu anajaribu kukugusa fasi yenye hapaswe kukugusa?

Unaweza kufanya nini juu wale watu wabaya wasikutendee mubaya?​— Kwanza, usiache mutu yoyote acheze na viungo vyako vya uzazi. Kama mutu anapima kufanya vile, useme hivi kwa sauti kubwa na bila kuogopa: “Niache, nitakuchongea.” Na kama ule mutu anasema kama mambo yenye ilifanyika ni kosa yako, usiitike mambo yenye anasema, ile haiko kweli. Umuchongee tu hata akuwe nani! Unapaswa tu kumuchongea hata kama anasema kama mambo yenye ilifanyika ni siri yenu nyie wawili. Na hata akisema kama atakupatia zawadi ao anakuogopesha, unapaswa tu kumuchongea.

Haupaswe kuogopa, lakini unapaswa kuwa muangalifu. Kama wazazi wako wanakuambia uepuke watu fulani ao fasi fulani zenye zinaweza kuwa hatari, uwasilikize. Kama unafanya vile itakuwa nguvu ukutane na watu wenye wanaweza kukutendea mubaya.

Tusome Mwanzo 39:7-12; Mezali 4:14-16; 14:15, 16; 1 Wakorinto 6:18; na 2 Petro 2:14 juu tuone mambo yenye unaweza kufanya juu ya kuepuka ngono yenye Mungu anakataza.