Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 12

Unaweza Kufanya Nini ili Ukuwe Rafiki ya Mungu?

Unaweza Kufanya Nini ili Ukuwe Rafiki ya Mungu?

1, 2. Taja watu fulani wenye walikuwa marafiki wa Yehova.

UNAPENDA kuwa na rafiki wa namna gani? Mutu mwenye unafurahia. Mutu mwenye unasikilizanaka naye. Mutu mwenye kuwa na tabia za muzuri na sifa zenye unafurahia.

2 Yehova Mungu anachagua wanadamu fulani ili wakuwe marafiki wake. Kwa mufano, Abrahamu alikuwa rafiki ya Yehova. (Isaya 41:8; Yakobo 2:23) Yehova alimupenda Daudi naye. Alisema kama Daudi alikuwa ‘mutu mwenye kufurahisha moyo wake.’ (Matendo 13:22) Na Yehova alimuona nabii Danieli kuwa “mwenye samani [ao, wa maana] sana.”​—Danieli 9:23.

3. Juu ya nini Abrahamu, Daudi, na Danieli walikuwa marafiki wa Yehova?

3 Juu ya nini Abrahamu, Daudi, na Danieli walifikia kuwa marafiki wa Yehova? Yehova alimuambia Abrahamu hivi: “Umesikiliza sauti yangu.” (Mwanzo 22:18) Yehova ni rafiki ya wale wenye wanamutii ao kumusikia kwa unyenyekevu. Hata watu wa taifa lote wangeweza kuwa marafiki wake. Yehova aliambia taifa la Israeli hivi: “Mutii sauti yangu, na nitakuwa Mungu wenu, na ninyi mutakuwa watu wangu.” (Yeremia 7:23) Kwa hiyo, na wewe unapaswa kumutii Yehova kama unapenda kabisa kuwa rafiki yake.

YEHOVA ANALINDA MARAFIKI WAKE

4, 5. Namna gani Yehova analinda marafiki wake?

4 Biblia inasema kama Yehova anatafuta njia za “kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale wenye moyo wao ni kamili kumuelekea yeye.” (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Mu andiko la Zaburi 32:8, Yehova anaahidi marafiki wake hivi: “Nitakupatia ufahamu na kukufundisha katika njia yenye unapaswa kufuata. Nitakupatia shauri jicho langu likikuangalia.”

5 Tuko na adui mwenye nguvu sana mwenye anapenda kuvunja urafiki wetu pamoja na Mungu. Lakini Yehova anapenda kutulinda. (Soma Zaburi 55:22.) Juu tuko marafiki wa Yehova, tunamutumikia kwa moyo wetu wote. Tuko washikamanifu kwake hata wakati wa magumu. Na tuko hakika kama vile muandikaji mumoja wa zaburi mwenye aliandika hivi juu ya Yehova: “Kwa sababu iko kwenye mukono wangu wa kuume, sitatikiswa hata kidogo.” (Zaburi 16:8; 63:8) Shetani anafanya nini ili atuzuie kuwa marafiki wa Mungu?

MAMBO YENYE SHETANI ALISHITAKI

6. Shetani alisema nini juu ya watu?

6 Mu Sura ya 11 tulijifunza kama Shetani alimupinga Yehova kwa kumushitaki kuwa ni musema-uongo na mwenye kukosa haki juu hakuruhusu Adamu na Eva wajiamulie mambo ya muzuri na mambo ya mubaya. Kitabu cha Yobu kinatufundisha kama Shetani anawashitaki pia watu wenye wanapenda kuwa marafiki wa Mungu. Shetani anasema kama wanamutumikia Mungu juu ya mambo yenye anawapatia, lakini haiko juu wanamupenda. Tena Shetani alisema kama anaweza kufanya mutu yeyote aache kumutumikia Mungu. Tuone mambo yenye mufano wa Yobu unatufundisha na namna Yehova alimulinda.

7, 8. (a) Yehova alimuona Yobu namna gani? (b) Shetani alisema nini juu ya Yobu?

7 Yobu alikuwa nani? Alikuwa mutu muzuri mwenye aliishi kumepita miaka 3 600 hivi. Yehova alisema kama, wakati huo hakuna mutu mwingine mwenye alikuwa kama Yobu mu dunia. Alikuwa anamuheshimia Mungu sana, na alichukia mambo ya mubaya. (Yobu 1:8) Kwa kweli, Yobu alikuwa rafiki wa kweli wa Yehova.

8 Shetani alisema kama Yobu alikuwa anamutumikia Mungu juu ya faida zenye alikuwa anapata. Shetani alimuambia Yehova hivi: “Je, haukutia ukuta wa ulinzi kumuzunguka yeye na nyumba yake na kila kitu chenye iko nacho? Umebariki kazi ya mikono yake, na mifugo yake imeenea katika inchi yote. Lakini, ili mambo yabadilike, unyooshe mukono wako na upige kila kitu chenye iko nacho, na hakika atakulaani mbele ya uso wako.”​—Yobu 1:10, 11.

9. Yehova alimupatia Shetani ruhusa ya kufanya nini?

9 Shetani alimushitaki Yobu kama alikuwa anamutumikia Yehova juu tu ya vitu vyenye alikuwa anamupatia. Tena Shetani alisema kama anaweza kumufanya Yobu aache kumutumikia Yehova. Yehova alijua kama Shetani alisema uongo, lakini alimupatia ruhusa ya kumujaribu Yobu. Hilo lingeonyesha ikiwa Yobu alikuwa anamupenda Mungu kabisa.

SHETANI ANAMUSHAMBULIA YOBU

10. Namna gani Shetani alimushambulia Yobu? Yobu alitenda namna gani?

10 Kwanza, Shetani alifanya wanyama wote wa Yobu waibwe ao kuuawa. Aliua watumishi wengi wa Yobu. Yobu alipoteza kila kitu. Katika jaribu la mwisho, Shetani alitumia upepo mukali ili kuua watoto kumi wa Yobu. Lakini Yobu alibakia mushikamanifu kwa Yehova. “Katika mambo haya yote, Yobu hakutenda zambi wala kumulaumu Mungu kwa jambo lolote la mubaya.”​—Yobu 1:12-19, 22.

Yehova alimubariki rafiki yake Yobu juu alibakia mushikamanifu kwake

11. (a) Namna gani Shetani alimushambulia tena Yobu? (b) Yobu alitenda namna gani?

11 Shetani hakuchoka. Alimuchokoza Mungu kwa kusema hivi: “Upige mufupa wake na nyama yake, na hakika atakulaani mbele ya uso wako.” Kwa hiyo, Shetani alimuletea Yobu ugonjwa wenye maumivu sana. (Yobu 2:5, 7) Lakini, Yobu aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova. Alisema hivi: “Mupaka wakati nitakufa, sitaacha uaminifu-mushikamanifu wangu!”​—Yobu 27:5.

12. Namna gani Yobu alionyesha kama Shetani ni musema-uongo?

12 Yobu hakujua jambo lolote juu ya mambo yenye Shetani alimushitaki ao juu ya nini alikuwa anateseka sana. Aliwaza kama Yehova njo alikuwa anamuletea mateso hayo. (Yobu 6:4; 16:11-14) Lakini, Yobu aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova. Sasa, mambo yote yenye Shetani alimushitaki yalipata jibu. Yobu hakukuwa anamutumikia Mungu kwa sababu ya faida fulani. Alikuwa rafiki ya Mungu kwa sababu alimupenda. Mambo hayo yote yenye Shetani alimushitaki yalikuwa ya uongo!

13. Juu ya ushikaminifu wake, Yobu alipata matokeo gani?

13 Hata kama Yobu hakujua mambo yenye yalikuwa yanatendeka mbinguni, aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu na alionyesha kama Shetani alikuwa muovu. Yehova alimubariki rafiki yake Yobu juu ya ushikamanifu wake.​—Yobu 42:12-17.

NAMNA SHETANI ANAKUSHITAKI

14, 15. Ni mambo gani yenye Shetani anashitaki watu wote?

14 Mambo yenye yalimupata Yobu yanaweza kukufundisha mambo mingi ya maana. Leo, Shetani anatushitaki kama tunamutumikia Yehova juu ya mambo yenye anatupatia. Mu andiko la Yobu 2:4, Shetani alisema hivi: “Mutu atatoa kila kitu chenye iko nacho ili aokoe uzima wake.” Kwa hiyo, Shetani hakumushitaki Yobu tu; alishitaki watu wote kwamba wanamutumikia Mungu juu ya faida zenye wanapata. Miaka mingi kisha Yobu kufa, Shetani alikuwa angali anamutukana Yehova na kushitaki watumishi wake. Kwa mufano, andiko la Mezali 27:11, linasema hivi: “Ukuwe na hekima, mwana wangu, na ufurahishe moyo wangu, ili niweze kumujibu ule mwenye ananichokoza [ao, mwenye ananitukana].”

15 Unaweza kuchagua kumutii Yehova na kuwa rafiki yake mushikamanifu ili uonyeshe kama Shetani ni musema-uongo. Hata kama unapaswa kufanya mabadiliko makubwa mu maisha yako kusudi ukuwe rafiki ya Mungu, huo njo uamuzi wa muzuri zaidi wenye unaweza kukamata mu maisha yako! Huo ni uamuzi wa maana sana. Shetani anasema kama hautaendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu wakati unapata magumu. Anajaribu kutudanganya kusudi tusiendelee kuwa washikamanifu kwa Mungu. Namna gani?

16. (a) Shetani anatumia njia gani ili ajaribu kuzuia watu wasimutumikie Yehova? (b) Namna gani Ibilisi anaweza kujaribu kukuzuia wewe usimutumikie Yehova?

16 Shetani anatumia njia mingi mbalimbali kusudi ajaribu kutuzuia tusikuwe marafiki wa Mungu. Anashambulia “kama simba mwenye kunguruma, akitafuta kumumeza mutu.” (1 Petro 5:8) Usishangae wakati marafiki wako, watu wa familia yako, ao watu wengine wanajaribu kukuzuia ao kukukataza kujifunza Biblia na kukuzuia kufanya mambo yenye kuwa sawa. Unaweza kujisikia kuwa unashambuliwa. * (Yohana 15:19, 20) Tena, Shetani anajigeuza kuwa “malaika wa mwangaza.” Anaweza kujaribu kutudanganya ili tukose kumutii Yehova. (2 Wakorinto 11:14) Njia ingine yenye Shetani anatumia ili atuzuie tusimutumikie Yehova ni kutufanya tuwaze kama hatustahili hata kidogo kumutumikia Mungu.​—Mezali 24:10.

TII AMRI ZA YEHOVA

17. Juu ya nini tunamutii Yehova?

17 Wakati tunamutii Yehova, tunaonyesha kama Shetani ni musema-uongo. Ni nini itatusaidia kuwa wenye kutii? Biblia inasema hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Kumbukumbu la Torati 6:5) Tunamutii Yehova juu tunamupenda. Kadiri upendo wetu kwa Yehova unaendelea kuongezeka, tutapenda zaidi kufanya mambo yote yenye anatuomba. Mutume Yohana aliandika hivi: “Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tushike amri zake; na bado amri zake haziko muzigo muzito.”​—1 Yohana 5:3.

18, 19. (a) Ni mambo gani fulani yenye Yehova anasema kuwa ni ya mubaya? (b) Yehova hatuombe hata kidogo kufanya mambo yenye hatuna uwezo wa kufanya. Ni nini inaonyesha vile?

18 Lakini, ni mambo gani fulani yenye Yehova anasema kuwa ni ya mubaya? Kisanduku chenye kichwa “ Chukia Mambo Yenye Yehova Anachukia,” kinaonyesha mambo fulani kati ya mambo hayo. Mwanzoni, unaweza kuwaza kama mambo fulani kati ya mambo hayo hayako ya mubaya sana. Lakini wakati unasoma maandiko ya Biblia na kuwaza kwa uangalifu juu ya mambo hayo, utaelewa kama ni jambo la hekima sana kutii sheria za Yehova. Unaweza pia kuona kama unapaswa kufanya mabadiliko fulani mu maisha yako. Wakati fulani, inaweza kuwa nguvu kufanya mabadiliko hayo. Lakini kama unafanya vile, utakuwa na amani na furaha juu ya ushikamanifu wako kwa Mungu. (Isaya 48:17, 18) Ni nini inaonyesha kama tunaweza kufanya mabadiliko hayo?

19 Yehova hatuombe hata kidogo tufanye jambo fulani lenye hatuna uwezo wa kufanya. (Kumbukumbu la Torati 30:11-14) Ni Rafiki wa kweli na anatujua muzuri zaidi kupita namna tunajijua. Anajua sifa zetu na uzaifu wetu. (Zaburi 103:14) Mutume Paulo anatutia moyo hivi: “Mungu ni muaminifu, na hatawaacha ninyi mujaribiwe kupita vile munaweza kuvumilia, lakini pamoja na jaribu hilo atafanya pia njia ya kutokea ili muweze kulivumilia.” (1 Wakorinto 10:13) Tunaweza kuwa hakika kama sikuzote Yehova atatupatia nguvu ya kufanya mambo yenye kuwa sawa. Atakupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida” ili akusaidie kuvumilia magumu. (2 Wakorinto 4:7) Kisha Yehova kumusaidia wakati wa magumu, Paulo alisema hivi: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.”​—Wafilipi 4:13.

UJIFUNZE KUPENDA MAMBO YENYE MUNGU ANAPENDA

20. Unapaswa kuiga sifa gani za Yehova, na juu ya nini?

20 Kama tunapenda kuwa marafiki wa Yehova, tunapaswa kuacha kufanya mambo yenye Yehova anachukia. Lakini tunapaswa kufanya jambo lingine. (Waroma 12:9) Marafiki wa Mungu wanapenda mambo yenye anapenda. Mambo hayo yanatajwa mu Zaburi 15:1-5. (Soma.) Marafiki wa Yehova wanaiga sifa zake na wanaonyesha sifa kama vile “upendo, furaha, amani, uvumilivu, fazili, wema, imani, upole, kujizuia.”​—Wagalatia 5:22, 23.

21. Ni nini itatusaidia kuwa na sifa za muzuri?

21 Ni nini itatusaidia kuwa na sifa za muzuri? Unapaswa kujifunza mambo yenye Yehova anapenda kwa kusoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida. (Isaya 30:20, 21) Wakati unafanya vile, upendo wako kwa Yehova utaongezeka, na wakati upendo wako kwake unaongezeka, utapenda kumutii zaidi.

22. Utapata matokeo gani ikiwa unamutii Yehova?

22 Kufanya mabadiliko fulani mu maisha yako, ni kama vile kutosha nguo za zamani na kuvaa nguo za mupya. Biblia inasema kama unapaswa ‘kuvua utu wa zamani’ na kuvaa “utu mupya.” (Wakolosai 3:9, 10) Hata kama inaweza kuwa nguvu, kama tunafanya mabadiliko hayo, na kama tunamutii Yehova, anatuahidi kama atatupatia “zawabu kubwa,” ao atatubariki sana. (Zaburi 19:11) Uchague kumutii Yehova na uonyeshe kama Shetani ni musema-uongo. Usimutumikie Yehova juu ya baraka zenye atatupatia wakati wenye kuja, lakini umutumikie juu unamupenda. Kisha utakuwa rafiki wa kweli wa Mungu!

^ fu. 16 Haiko kusema kama Shetani anaongoza watu wenye wanajaribu kukuzuia kujifunza Biblia. Lakini, Shetani njo “mungu wa mupangilio huu wa mambo,” na “ulimwengu muzima unakaa katika nguvu [zake].” Kwa hiyo, haishangaze kuona watu fulani wanajaribu kutuzuia tusimutumikie Yehova.​—2 Wakorinto 4:4; 1 Yohana 5:19.