Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 37

Biblia Inasema Nini Juu ya Kazi na Makuta?

Biblia Inasema Nini Juu ya Kazi na Makuta?

Kuko siku ulishakahangaika sana juu ya kukosa kazi ao makuta? Inaweza kuwa nguvu kupata wakati ya kutafuta makuta ya kutusaidia mu maisha, na wakati ileile kupata wakati ya kumutumikia Yehova. Mu Biblia muko mashauri yenye inaweza kutusaidia.

1. Biblia inasema nini juu ya kazi?

Mungu anapenda tufurahie kazi yetu. Biblia inasema kama “hakuna jambo la muzuri zaidi kwa mutu kuliko . . . kufurahia kazi yake ya nguvu.” (Muhubiri 2:24) Yehova anatumikaka sana. Wakati tunamuiga kwa kutumika kwa bidii, tunamufurahisha, na tunakuwa na furaha.

Kazi ni ya maana. Lakini, hatupaswe kuiona kuwa ya maana sana kuliko kumuabudu Yehova. (Yohana 6:27) Yehova anatuhakikishia kama tukitia ibada yake pa nafasi ya kwanza, atatusaidia kupata mambo yenye tuko nayo lazima.

2. Tunapaswa kuona makuta namna gani?

Ni kweli kama Biblia inasema kuwa “feza ni ulinzi,” lakini inasema tena kama haiwezi kutuletea furaha. (Muhubiri 7:12) Njo maana Biblia inatushauria tusipende feza ao makuta, lakini ‘tutosheke na vitu vya sasa.’ (Soma Waebrania 13:5.) Kama tunatosheka ao kufurahia mambo yenye tuko nayo, hatutakuwa na mahangaiko ya kuwaza kama kuko mambo yenye tungali nakosa. Tutaepuka kukamata madeni wakati haiko lazima kufanya vile. (Mezali 22:7) Na tutaepuka hatari za kucheza michezo ya makuta na za kutafuta kuwa tajiri mbio-mbio.

3. Namna gani tunaweza kuonyesha kama hatuko wachoyo mu namna tunatumia makuta yetu?

JYehova hakuwake muchoyo. Tunamuiga wakati tuko “wakarimu, tayari kushiriki [ao, kuchangia] na wengine.” (1 Timoteo 6:18) Tunaonyesha kama hatuko wachoyo wakati tunatoa michango juu ya kusaidia kutaniko, na wakati tunasaidia wengine wenye wako na lazima ya musaada, zaidi sana Wakristo wenzetu. Jambo yenye Yehova anaangaliaka zaidi, haiko kiasi ya makuta yenye tunatoa, lakini nia yenye inatuchochea kutoa. Wakati tunatoa kwa kujipendea, tutakuwa na furaha, na tutamufurahisha Yehova.​—Soma Matendo 20:35.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone faida ya kuwa na mawazo yenye inafaa juu ya kazi, na tuone faida ya kutosheka.

4. Ufanye kazi mu namna yenye inamutukuza Yehova

Juu tuko marafiki wa Yehova, tunapaswa kuona kazi vile yeye anaionaka. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, Jason alikuwa na mawazo gani juu ya kazi, na alikuwa najiendesha namna gani?

  • Alifanya nini juu kazi isimuzuie kumuabudu Yehova?

Musome Wakolosai 3:23, 24, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini tunapaswa kuwa na mawazo yenye kufaa juu ya kazi?

Kazi ni ya maana. Lakini, hatupaswe kuiona kuwa ya maana zaidi kuliko kumuabudu Yehova

5. Ni muzuri kutosheka

Watu wengi wanajikazaka kuwa na makuta mingi sana. Lakini Biblia inaonyesha kama haiko muzuri kufanya vile. Musome 1 Timoteo 6:6-8, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Biblia inatushauria nini?

Tunaweza kuwa na furaha hata kama hatuna vitu mingi. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Hata kama zile familia hazina makuta mingi, juu ya nini ziko na furaha?

Halafu kama tuko na vitu mingi lakini tunapenda tena tukuwe na vitu mingi zaidi? Kuko hatari. Yesu alileta mufano wenye unaonyesha ile hatari. Musome Luka 12:15-21, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

Musome na mulinganishe Mezali 10:22 na 1 Timoteo 6:10. Kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza nini njo ya maana zaidi, kuwa rafiki ya Yehova ao kuwa na makuta mingi? Juu ya nini unawaza vile?

  • Kutafuta tu kuwa na makuta mingi zaidi kunaletaka magumu gani?

6. Yehova atakusaidia kupata mambo yenye uko nayo lazima

Wakati tunakosa kazi ao makuta, ile inaweza kutusaidia kujua ikiwa tunamutumainia Yehova ao hapana. Muangalie VIDEO juu ya kuona mambo yenye tunaweza kufanya wakati tunakosa kazi ao makuta, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, ule ndugu alikuwa na magumu gani?

  • Alifanya nini juu ya kupiganisha ile magumu?

Musome Matayo 6:25-34, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Yehova anasema kama atafanyia nini watu wenye wanatia ibada yake pa nafasi ya kwanza?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Ninapaswa kutumika sana, juu nipate makuta ya kusaidia familia yangu. Siwezi kuwa nafika ku mikutano kila juma.”

  • Ni andiko gani inakuhakikishia kama inakuwaka tu muzuri kutia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza?

KWA KIFUPI

Kazi na makuta ni mambo ya lazima, lakini haipaswe kutuzuia kumutumikia Yehova.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Nini njo inaweza kukusaidia ukuwe na mawazo yenye inafaa juu ya kazi?

  • Kutosheka kunaweza kukuletea faida gani?

  • Unaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama uko hakika kuwa Yehova atakusaidia upate mambo yenye uko nayo lazima?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Makuta ni kitu ya mubaya? Ona mawazo ya Biblia.

“Makuta Njo Chanzo ya Mambo Yote ya Mubaya?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna tunaweza tumia makuta yetu juu ya kumufurahisha Mungu.

“Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa?” (Inapatikana ku Enternete)

Kuko hatari kama mutu anakuwa nacheza michezo ya feza?

“Mawazo ya Biblia—Michezo ya Feza” (Amuka!, Mwezi wa 3, 2015)

Ona mambo yenye ilisaidia mwanaume fulani aache kucheza michezo ya makuta na aache kuiba.

“Nilikuwa Napenda Sana Mashindano ya Kutembeza Farasi” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 11, 2011)