Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 39

Namna Mungu Anaonaka Damu

Namna Mungu Anaonaka Damu

Damu ni ya maana. Hakuna mutu mwenye anaweza kuishi kama mu mwili yake hamuna damu. Juu Mungu njo alituumba, iko na haki ya kuamua namna damu inapaswa kutumiwa. Alishasema nini juu ya damu? Tunaweza kuikula ao kuitia mu mishipa? Na nini njo inaweza kutusaidia tukamate maamuzi ya muzuri juu ya damu?

1. Yehova anaonaka damu namna gani?

Zamani Yehova aliambiaka hivi watumishi wake: “Uzima wa kila namna ya mwili ni damu yake.” (Mambo ya Walawi 17:14) Yehova anaona kama damu ni uzima. Juu uzima ni kitu kitakatifu na juu ni zawadi yenye Mungu alitupatia, ni kusema damu nayo ni kitu kitakatifu.

2. Mungu anakataza kutumia damu namna gani?

Yehova aliambia watumishi wake wa zamani wasikule damu. (Soma Mwanzo 9:4 na Mambo ya Walawi 17:10.) Na alirudilia ileile amri wakati aliongoza baraza yenye kuongoza iambie Wakristo ‘waendelee kujiepusha . . . na damu.’​—Soma Matendo 15:28, 29.

Kujiepusha na damu maana yake nini? Kama munganga anakuambia ujiepushe na pombe, ni kusema hautaikunywa. Sasa unaweza kuitia mu chakula ao mu mishipa? Hapana. Vilevile, wakati Mungu anatuambia tujiepushe na damu, ni kusema hatupaswe kuikunywa ao kula nyamafu. Tena, hatupaswe kula chakula yoyote yenye waliongeza ndani damu.

Tuseme nini sasa juu ya kutumia damu mu mambo ya matunzo? Matunzo fulani haipatane na sheria ya Mungu. Kwa mufano, kutia mutu damu mu mishipa ao kutumia sehemu kubwa-kubwa ine za damu, ni kusema chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, na plazma. Matunzo ingine haionekane waziwazi kama inavunja sheria ya Mungu. Kwa mufano, matunzo fulani inaombaka kutumia sehemu za kidogo-kidogo zenye zinatoka mu sehemu kubwa za damu. Matunzo ingine inaombaka munganga atumie ileile damu ya mutu wakati iko namutunza. Kila mutu anapaswa kutumia zamiri yake juu ya kuamua ikiwa atakubali zile aina za matunzo. a​—Wagalatia 6:5.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye inaweza kukusaidia kuamua ikiwa utakubali ao utakatala aina fulani ya matunzo.

3. Kamata maamuzi yenye inamufurahisha Yehova

Wakati unapenda kuamua ni aina gani ya matunzo yenye utakubali, namna gani unaweza kukamata maamuzi yenye itamufurahisha Mungu? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie faida ya kufanya mambo yenye kufuata.

  • Uombe Yehova akupatie hekima. ​—Yakobo 1:5.

  • Tafuta kanuni za Biblia na uone namna gani utazitumia.​—Mezali 13:16.

  • Tafuta ni aina gani ya matunzo yenye inapatikana fasi kwenye unaishi.

  • Amua ni aina gani ya matunzo yenye hauwezi kukubali hata kidogo.

  • Hakikisha kama uamuzi wenye utakamata hautachafua zamiri yako.​—Matendo 24:16. b

  • Ujue kama hakuna mutu mwenye anapaswa kukukamatia uamuzi mu mambo ya zamiri, ikuwe bibi ao bwana yako, muzee wa kutaniko, ao mwalimu wako wa Biblia. ​—Waroma 14:12.

  • Andika uamuzi wako.

4. Mashahidi wa Yehova wanatafutaka matunzo ya muzuri

Inawezekana kutii sheria ya Mungu juu ya damu na kupata matunzo ya muzuri yenye haiombe kutumia damu. Muangalie VIDEO.

Musome Tito 3:2, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini tunapaswa kuzungumuza na wanganga kwa heshima na kwa upole?

Hatupaswe kukubali

Ya kujiamulia

A. Plazma

Sehemu za kidogo-kidogo za plazma

B. Chembe nyeupe

Sehemu za kidogo-kidogo za chembe nyeupe

C. Vigandisha-damu

Sehemu za kidogo-kidogo za vigandisha-damu

D. Chembe nyekundu

Sehemu za kidogo-kidogo za chembe nyekundu

 5. Wakati inaomba kutumia sehemu za kidogo-kidogo za damu

Damu iko na sehemu ine kubwa-kubwa: chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, na plazma. Mu zile sehemu kubwa-kubwa munapatikana sehemu zingine za mingi za kidogo-kidogo. c Sehemu fulani za kidogo-kidogo zinatumiwaka mu matunzo juu ya kusaidia kupiganisha magonjwa ao kufanya damu iache kuvuya.

Lakini kuhusu sehemu za kidogo-kidogo za damu, kila Mukristo anapaswa kutumikisha zamiri yake yenye kuzoezwa na Biblia juu ya kuamua kama atazikubali ao atazikatala. Wakristo fulani wanaweza kuamua kukatala matunzo yote yenye inaomba kutumia sehemu za kidogo-kidogo za damu. Lakini, Wakristo wengine wanaona kama zamiri yao inawaruhusu kutumia zile sehemu za kidogo-kidogo za damu.

Wakati unakamata uamuzi, fikiria hii ulizo:

  • Namna gani nitafasiria munganga juu ya nini ninaitika ao ninakatala sehemu fulani za kidogo-kidogo za damu?

KAMA MUTU ANAULIZA: “Ni mubaya kama mutu anaitika wamutie damu mu mishipa?”

  • Weye unawaza nini?

KWA KIFUPI

Yehova hapendi tutumie damu mubaya.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini Yehova anaona damu kuwa kitu kitakatifu?

  • Nini njo inatusaidia kujua kama kujiepusha na damu inamaanisha pia kuepuka kuitia mu mishipa?

  • Nini njo itakusaidia kukamata maamuzi ya muzuri juu ya matunzo yenye inaomba kutumia damu?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Unapaswa kufikiria nini mbele ya kukubali matunzo yenye inaomba kutumia damu yako?

“Maulizo ya Wasomaji Wetu” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 10, 2000)

Unapaswa kufikiria nini mbele ya kuamua ikiwa utakubali matunzo yenye inaomba kutumia sehemu za kidogo-kidogo za damu?

“Maulizo ya Wasomaji Wetu” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 6, 2004)

Nini njo ilisaidia munganga fulani aamini kama Mashahidi wa Yehova wako na mawazo ya muzuri juu ya damu?

“Nilikubali Mawazo ya Mungu Juu ya Damu” (Amuka!, 8 Mwezi wa 12, 2003)

Ona namna wazee wenye wanatumikaka mu Halmashauri ya Uhusiano na Hopitali wanasaidiaka ndugu na dada zao.

Yehova Anasaidiaka Wagonjwa (10:23)

a Ona Somo ya 35, “Namna ya Kukamata Maamuzi ya Muzuri.”

b Ona  nukta ya 5, “Wakati Inaomba Kutumia Sehemu za Kidogo-kidogo za Damu” Mafasirio Ingine ya 3, “Matunzo Yenye Inaomba Kutumia Damu” na Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 11, 2006 uku. 3-6.

c Wanganga fulani wanaonaka kama zile sehemu ine kubwa-kubwa za damu nazo tu ni sehemu za kidogo-kidogo. Njo maana unapaswa kuwafasiria waziwazi kama hautakubali watie mu mishipa yako damu, ao chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, ao plazma.