Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mafasirio Ingine

Mafasirio Ingine
  1.  Babiloni Mukubwa Ni Nani?

  2.  Masiya Angetokea Wakati Gani?

  3.  Matunzo Yenye Inaomba Kutumia Damu

  4.  Kutengana

  5.  Sikukuu

  6.  Magonjwa ya Kuambukiza

  7.  Mambo ya Biashara na ya Sheria

 1. Babiloni Mukubwa Ni Nani?

Nini njo inatusaidia kujua kama “Babiloni Mukubwa” anafananisha dini zote za uongo? (Ufunuo 17:5) Ona mambo fulani:

  • Anapatikana mu dunia yote. Biblia inasema kama Babiloni Mukubwa anaikala juu ya “watu wengi na mataifa.” Na kama iko na “ufalme juu ya wafalme wa dunia.”​—Ufunuo 17:15, 18.

  • Haiko tengenezo fulani ya politike ao ya biashara. Juu Biblia inasema kama “wafalme wa dunia” na “wafanyabiashara” hawataharibiwa wakati yeye ataharibiwa.​—Ufunuo 18:9, 15.

  • Anamuzaraulisha Mungu. Biblia inamuita kahaba juu anafanya mapatano na guvernema za wanadamu juu apate makuta na faida zingine. (Ufunuo 17:1, 2) Anadanganya watu wa mataifa yote. Ameuisha watu wengi.​—Ufunuo 18:23, 24.

Rudia ku somo ya 13 nukta ya 6

 2. Masiya Angetokea Wakati Gani?

Biblia ilisemaka kama Masiya angetokea kisha majuma 69.​—Soma Danieli 9:25.

  • Ile majuma 69 ilianza wakati gani? Ilianza mu mwaka wa 455 M.K.Y. Ile wakati, Gavana Nehemia alifika Yerusalemu juu ya “kurudisha na kujenga upya” muji.​—Danieli 9:25; Nehemia 2:1, 5-8.

  • Ile majuma 69 ilikuwa na urefu gani? Mu maunabii fulani ya Biblia, siku moja inafananisha mwaka moja. (Hesabu 14:34; Ezekieli 4:6) Ni kusema kila juma ni miaka saba. Mu hii unabii, majuma 69 ni miaka 483 (majuma 69 x siku 7).

  • Ile majuma 69 iliisha wakati gani? Kama unahesabia miaka 483 kuanzia mwaka wa 455 M.K.Y, ile itakufikisha mu mwaka wa 29 K.K.Y. a Ni mu ile mwaka njo Yesu alibatizwa na kuwa Masiya!​—Luka 3:1, 2, 21, 22.

Rudia ku somo ya 15 nukta ya 5

 3. Matunzo Yenye Inaomba Kutumia Damu

Kuko matunzo mingi yenye inaombaka kutumia damu ya mugonjwa. Kwa mufano, mutu anaweza kutolea wengine damu yake ao anaweza kuamua damu yake iwekwe, juu itumiwe wakati atafanyiwa upasuaji. Lakini Wakristo hawapaswe kufanya vile.​—Kumbukumbu la Torati 15:23.

Kuko matunzo ingine yenye pengine Mukristo anaweza kukubali. Kwa mufano, kupima damu, hémodialyse, hémodilution, ao récupération du sang épanché ao kutumia mashini yenye kufanya kazi pa nafasi ya moyo na mapafu. b Kila Mukristo anapaswa kuamua yeye mwenyewe namna damu yake itatumiwa wakati ya upasuaji, wakati ya kupima damu, ao wakati iko natunzwa kwa kutumia ufundi fulani. Kila munganga anakuwaka na namna yake ya kutunza. Njo maana mbele ya kukubali upasuaji, kupimwa damu, ao aina fulani ya matunzo, Mukristo anapaswa kutafuta kujua namna damu yake itatumiwa. Anaweza kujiuliza hii maulizo:

  • Kama damu yangu inatoshwa ndani ya mwili wangu na pengine inaacha hata kutembea mu mwili kwa wakati fulani, zamiri yangu itaona kama ile damu ingali sehemu ya mwili wangu, ao itaona kama inapaswa ‘kumwangwa kwenye udongo’?​—Kumbukumbu la Torati 12:23, 24.

  • Kama wakati ya matunzo sehemu ya damu yangu inatoshwa, inarekebishwa, na kurudishwa tena ndani ya mwili wangu, zamiri yangu yenye kuzoezwa na Biblia itanisumbua ao hapana?

Rudia ku somo ya 39 nukta ya 3

 4. Kutengana

Biblia inaambia bibi na bwana kama hawapaswe kutengana. Na inaonyesha waziwazi kama wakati bibi na bwana wanatengana, hakuna mwenye iko na haki ya kuoa ao kuolewa tena. (1 Wakorinto 7:10, 11) Lakini, kuko hali fulani zenye zimefanya Wakristo fulani waamue kutengana na bibi ao bwana yao.

  • Bwana anakatala kimakusudi kutimiza mahitaji ya familia: Bwana anakatala kutimiza mahitaji ya familia yake, mupaka familia inakosa mambo ya lazima sawa vile chakula.​—1 Timoteo 5:8.

  • Bibi ao bwana anatendea mwenzake mubaya sana kimwili: Kutendea mwingine mubaya sana kimwili kunaweza kutia afya ao uzima wake mu hatari.​—Wagalatia 5:19-21.

  • Bibi ao bwana anafanya uhusiano wa mwenzake pamoja na Yehova ukuwe mu hatari sana: Bibi ao bwana anafanya mwenzake asiweze kabisa kumutumikia Yehova.​—Matendo 5:29.

Rudia ku somo ya 42 nukta ya 3

 5. Sikukuu

Wakristo hawafanyake sikukuu zenye Yehova hakubali. Lakini, kila Mukristo anapaswa kutumia zamiri yake yenye kuzoezwa na Biblia juu ya kuamua atafanya nini wakati wengine wako nafanya zile sikukuu. Ona mifano fulani.

  • Mutu anakutakia sikukuu ya muzuri. Unaweza tu kusema, “Aksanti.” Kama ule mutu anapenda kujua mambo mingi zaidi, unaweza kumufasiria juu ya nini haufanyake ile sikukuu.

  • Bibi ao bwana yako, mwenye haiko Shahidi wa Yehova, anakuambia muende kula chakula pamoja na watu wa familia wakati ya sikukuu. Kama zamiri yako inakuruhusu kuenda, unaweza kufasiria mbele ya wakati bibi ao bwana yako kama ikiwa wanafanya desturi fulani za kipagani, weye hautazifanya.

  • Mukubwa wako wa kazi anakupatia matabishi mu kipindi ya sikukuu. Unapaswa kuikatala? Weye njo utajua. Mukubwa wako wa kazi anaona ile matabishi kuwa sehemu ya sikukuu, ao anapenda tu kukushukuru juu ya kazi ya muzuri yenye uko nafanya?

  • Mutu anakupatia zawadi mu kipindi ya sikukuu. Anaweza kukuambia hivi: “Ninajua kama hamufanyake hii sikukuu, lakini ninapenda tu kukupatia hii zawadi.” Pengine ule mutu anapenda tu kukuonyesha roho muzuri. Lakini, inawezekana iko napima imani yako ao kutafuta kukuchochea na weye ufanye ile sikukuu? Kisha kufikiria ile yote, ni weye njo utaamua kama utaitika ile zawadi ao hapana. Hata tukamate maamuzi gani, tunapenda kuendelea kuwa na zamiri ya muzuri na kuwa waaminifu kwa Yehova.​—Matendo 23:1.

Rudia ku somo ya 44 nukta ya 1

 6. Magonjwa ya Kuambukiza

Juu tunapenda watu, tunakuwaka waangalifu juu tusiwaambukize magonjwa. Njoo maana kama tuko na magonjwa ya kuambukiza, ao tunawaza kama tumeambukizwa, tunapaswa kuwa waangalifu sana. Tunafanya vile juu Biblia inatuambia hivi: “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.”​—Waroma 13:8-10.

Mutu mwenye iko na ugonjwa wa kuambukiza anaweza kuonyesha namna gani kama anapenda wengine? Anapaswa kuepuka kukaribia sana watu kwa kuwakumbatia ao kuwabusu. Hapaswe kukasirika kama wengine hawamualike mu nyumba zao juu hawapendi kuambukizwa. Na mbele abatizwe, anapaswa kujulisha muratibu wa baraza ya wazee kama iko na ugonjwa wa kuambukiza, juu wazee wakate mipango ya kulinda wengine wenye watabatizwa wasiambukizwe. Mbele ya kuanza uchumba, mutu mwenye alikuwa mu hali yenye ingefanya apate ugonjwa wa kuambukiza, anapaswa kuwa tayari kupimisha damu yake. Ikiwa unafanya vile, unaonyesha kuwa unahangaikia wengine na ‘unaendelea kuangalia, hapana faida zako wewe mwenyewe tu, lakini pia faida za wengine.’​—Wafilipi 2:4.

Rudia ku somo ya 56 nukta ya 2

 7. Mambo ya Biashara na ya Sheria

Kama tunafanya mapatano ya mambo ya makuta, ni muzuri tuandikiane hata kama tunafanya mapatano na Mukristo mwenzetu. Ile inaweza kufanya tuepuke matatizo ya mingi yenye inatokeaka juu ya mambo ya makuta. (Yeremia 32:9-12) Hata vile, wakati fulani Wakristo wanaweza kukosa kuelewana juu ya mambo ya feza ao mambo ingine. Wanapaswa kujikaza kuelewana haraka na kwa amani, na bila kuingiza wengine mu mambo yao.

Lakini tunapaswa kufanya nini kama ni matatizo ya nguvu, kwa mufano mutu anatuiba ao kutusemea uongo? (Soma Matayo 18:15-17.) Yesu alisema tunapaswa kufanya mambo tatu:

  1. Ujikaze juu muelewane kati yenu.​—Ona mustari wa 15.

  2. Kama inashindikana, omba Mukristo mumoja ao wawili wenye kukomala kiroho wakusindikize.​—Ona mustari wa 16.

  3. Kama tu inashindikana, pale sasa njo unaweza kuambia wazee.​—Ona mustari wa 17.

Mu hali za mingi, hatupaswe kupeleka ndugu zetu ku tribinali juu ile inaweza kufanya watu waseme mubaya juu ya Yehova na kutaniko. (1 Wakorinto 6:1-8) Lakini, kuko hali fulani zenye inaweza kuwa lazima zipelekwe ku tribinali, sawa vile kuvunja ndoa, kutafuta haki ya kukomalisha mutoto, kuamua makuta yenye mutu atakuwa anapatia watu wa familia yake juu ya kutimiza mahitaji yao, kushugulikia mambo ya asiranse, biashara kuhomba, ao kuomba testama ikubaliwe kisheria. Kama Mukristo anaenda ku tribinali juu ya kushugulikia ile mambo kwa amani kadiri inawezekana, haende kinyume na mashauri ya Biblia.

Kama ni mambo yenye inahusu kuvunja sheria sawa vile kubaka mutu, kutendea mutoto mubaya kingono, kushambulia mutu, kuibiwa mali ya mingi, ao kuua, Mukristo mwenye anapeleka ile mambo ku serikali, haende kinyume na mashauri ya Biblia.

Rudia ku somo ya 56 nukta ya 3

a Kuanzia mwaka wa 455 M.K.Y. mupaka mwaka wa 1 M.K.Y. kuko miaka 454. Kuanzia mwaka wa 1 M.K.Y. mupaka mwaka wa 1 K.K.Y. kuko mwaka moja (hakuna mwaka zero). Na kuanzia mwaka wa 1 K.K.Y. mupaka mwaka wa 29 K.K.Y. kuko miaka 28. Kama tunakamata miaka 454 + 1 + 28, tunapata miaka 483.

b Ili kupata mafasirio zaidi juu ya zile aina mbalimbali za matunzo, ona “Maulizo ya Wasomaji Wetu” mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 2000.