Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 52

Juu ya Nini Tunapaswa Kufikiria Namna Yetu ya Kuvala na Kujipamba?

Juu ya Nini Tunapaswa Kufikiria Namna Yetu ya Kuvala na Kujipamba?

Kila mutu iko na namna yake ya kuvala na kujipamba yenye anafurahiaka. Kuko kanuni fulani za Biblia zenye zinaweza kutusaidia kuvala na kujipamba mu njia yenye itatufurahisha, lakini yenye itamufurahisha pia Yehova. Tuone zile kanuni.

1. Tunapaswa kufikiria kanuni gani wakati tuko nachagula manguo yenye tutavala na namna tutajipamba?

Tunapaswa kuchagula “nguo zenye kufaa, kwa kiasi na akili ya muzuri.” Tunapaswa kuwa safi kila siku juu wengine waone kama ‘tunashikamana na Mungu.’ (1 Timoteo 2:9, 10) Fikiria hizi kanuni ine: (1) Nguo zetu zinapaswa kuwa zenye “kufaa.” Vile umeona ku mikutano ya kutaniko, watu wa Yehova hawakuwake na namna ileile ya kuvala na kujipamba. Lakini namna yetu ya kuvala na kutengeneza nywele inaonyesha kama tunaheshimia Mungu mwenye tunaabudu. (2) Kuvala “kwa kiasi” inamaanisha kuepuka kuvala manguo yenye inaweza kulamusha tamaa ya ngono, ao kufanya wengine watuangalie sana. (3) Tunaonyesha kama tuko na “akili ya muzuri” wakati tunaepuka kufuatilia kila namna ya kuvala na kujipamba yenye inatokea. (4) Namna yetu ya kuvala na kujipamba inapaswa kuonyesha kama ‘tunashikamana na Mungu,’ ni kusema, inapaswa kusaidia wengine waone kama tunamuabudu Mungu wa kweli.​—1 Wakorinto 10:31.

2. Juu ya nini tunapaswa kufikiria ndugu na dada zetu wakati tunachagula manguo yenye tutavala na namna tutajipamba?

Tuko huru kuchagula manguo yenye tutavala na namna tutajipamba. Hata vile, tunapaswa kujiuliza hivi: Maamuzi yangu itafanya wengine wajisikie namna gani? Tunapaswa kujikaza juu tusikwaze mutu. Kila mumoja wetu anapaswa ‘kumupendeza jirani yake kwa faida yake, ili kumujenga.’​—Soma Waroma 15:1, 2.

3. Namna yetu ya kuvala inaweza kufanya watu wakuwe na hamu ya kufanya nini?

Tunajikazaka kuvala muzuri kila wakati, lakini zaidi sana wakati tunaenda ku mikutano na mu mahubiri. Hatupendi watu waanze njo kutuangalia, kuliko kusikiliza habari ya maana yenye tunawaletea. Tunapenda namna yetu ya kuvala isaidie watu wakuwe na hamu ya kujifunza kweli juu ya Mungu na ‘ipambe mafundisho ya Mwokozi wetu.’​—Tito 2:10.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye inaweza kutusaidia tuvale na kujipamba kwa njia yenye inafaa.

Namna yetu ya kuvala na kujipamba, inaweza kuonyesha kama tunaheshimia wenye mamlaka ao hapana. Hata kama Yehova anaangaliaka njo moyo, namna yetu ya kuvala na kujipamba, inapaswa kuonyesha pia kama tunamuheshimia

4. Wakati tunavala na kujipamba muzuri, tunaonyesha kama tunamuheshimia Yehova

Ni sababu gani kubwa yenye inafanya tufikirie namna yetu ya kuvala na kujipamba? Musome Zaburi 47:2, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Namna yetu ya kuvala inaweza kufanya watu wapende kujifunza juu ya Yehova ao hapana?

  • Unawaza ni lazima tukuwe nachunguza namna yetu ya kuvala wakati tunaenda ku mikutano ao mu mahubiri? Juu ya nini unawaza vile?

5. Tuchagule muzuri manguo yenye tutavala na namna tutajipamba

Muangalie VIDEO.

Ikuwe tunavala manguo ya bei sana ao ya bei chini, inapaswa kuwa safi na yenye inapatana na hali. Musome 1 Wakorinto 10:24 na 1 Timoteo 2:9, 10. Kisha, muzungumuzie juu ya nini tunapaswa kuepuka kuvala manguo ya ovyo-ovyo na ya kujiachilia sawa vile . . .

  • ya kubana sana.

  • ya kuonyesha sehemu za mwili zenye hazipaswe kuonekana, na ya kulamusha tamaa ya ngono.

Haiko lazima Wakristo wafuate Sheria ya Musa, lakini mambo yenye iko mu ile Sheria inaweza kuwasaidia wajue mawazo ya Yehova. Musome Kumbukumbu la Torati 22:5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini tunapaswa kuepuka kuvala na kujipamba mu namna yenye inafanya wanaume waonekane sawa vile wanamuke na wanamuke waonekane sawa vile wanaume?

Musome 1 Wakorinto 10:32, 33 na 1 Yohana 2:15, 16, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini tunapaswa kuchunguza ikiwa namna yetu ya kuvala na kujipamba inaweza kukwaza watu fasi kwenye tunaishi ao ndugu na dada mu kutaniko?

  • Fasi kwenye unaishi, watu wanazoea kuvala na kujipamba namna gani?

  • Kuko namna fulani ya kuvala na kujipamba yenye unaona kama haiko muzuri kwa Wakristo? Juu ya nini unasema vile?

Kuko namna mingi ya kuvala na kujipamba yenye inamufurahisha Yehova

WATU FULANI WANASEMAKA: “Niko na haki ya kuvala vile ninapenda.”

  • Na weye unawaza vile? Juu ya nini?

KWA KIFUPI

Tukichagula muzuri manguo ya kuvala na namna ya kujipamba, tutaonyesha kama tunaheshimia Yehova na wengine.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini Yehova anapenda tuchagule muzuri manguo yenye tutavala na namna tutajipamba?

  • Ni kanuni gani zitatusaidia tuchagule muzuri manguo ya kuvala na namna ya kujipamba?

  • Namna yetu ya kuvala na kujipamba inaweza kufanya wengine waone namna gani ibada ya kweli?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mawazo yenye wengine wanaweza kuwa nayo juu yako wakati wanaona namna yako ya kuvala.

“Ninaonekana Namna Gani?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona juu ya nini unapaswa kuwaza sana mbele ya kujichanja alama ku mwili..

“Biblia Inasema Nini Juu ya Mutu Kujichanja Alama Kwenye Mwili?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona kanuni zingine zenye zinaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri.

“Muvalio Wako Unamutukuza Mungu?” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 9, 2016)

Ona mambo yenye ilisaidia mwanamuke fulani, mwenye alipenda kumufurahisha Mungu, ajifunze kukubali maamuzi ya wengine juu ya mambo ya kuvala na kujipamba.

“Namna ya Kuvala na Kujipamba ya Wengine Ilikuwa Nanikwaza” (Amuka!, 22 Mwezi wa 12, 2003)