Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Barua Kutoka ku Baraza Lenye Kuongoza

Barua Kutoka ku Baraza Lenye Kuongoza

Ndugu na Dada Wenye Kumupenda Yehova:

Ilikuwa mwaka wa 1971. Wenye walihuzuria Mukusanyiko wa Eneo “Jina la Mungu” wenye ulifanywa ile mwaka walifurahi sana kupokea vichapo vya mupya. Watu walisema kama “hakuna mutu aliwaziaka kupata vile vichapo.” Kuhusu kichapo kimoja kati ya vile vyenye vilitolewa, ndugu moja alisema: “Hatujapataka kichapo chenye kinatuonjesha kabisa mambo yenye itakuja sawa hiki!” Alikuwa anazungumuzia kichapo gani? Ilikuwa kitabu “Mataifa Itajua Kwamba Mimi Ni Yehova”​—Namna Gani? (cha Kiingereza) Lakini juu ya nini ile kitabu ilimufanya awaze vile? Juu, ilikuwa na mafasirio ya sasa ya maunabii yenye inapatikana mu kitabu cha Biblia cha Ezekieli​—maunabii yenye inahusu wakati wenye kuja wa wanadamu wote.

Mu miaka yenye ilifuata tangu kutolewa kwa kitabu “Mataifa Itajua Kwamba Mimi Ni Yehova,” hesabu ya watu wa Mungu imeongezeka sana​—kutoka watu milioni 1.5 hivi kufikia watu zaidi ya milioni 8. (Isa. 60:22) Ile mamilioni ya watumishi wa Yehova wanazungumuza zaidi ya luga 900. (Zek. 8:23) Wengi hawajapataka nafasi ya kujifunza kitabu chenye kinafasiria kwa urefu maunabii yenye iliongozwa na roho ya Mungu yenye iliandikwa na nabii Ezekieli.

Zaidi ya ile, tangu 1971, namna yetu ya kuelewa kweli mingi za Biblia imeendelea kurekebishwa kadiri mwangaza wa kiroho unaendelea kuongezeka. (Mez. 4:18) Mu mwaka wa 1985, tulianza kuona waziwazi namna “kondoo wengine” wanatangazwa kuwa wenye haki na kuwa marafiki wa Mungu. (Yoh. 10:16; Ro. 5:18; Yak. 2:23) Kisha, mu mwaka wa 1995, tulielewa kwa mara ya kwanza kwamba hukumu ya mwisho ya “kondoo” na “mbuzi” itakuwa wakati wa “taabu kubwa” yenye kuja. (Mt. 24:21; 25:31, 32) Ile marekebisho yote imebadilisha namna yetu ya kuelewa kitabu cha Ezekieli.

“Mwana wa binadamu, angalia kwa uangalifu, sikiliza muzuri, na ukazie uangalifu kila kitu chenye ninakuonyesha, kwa maana uliletwa hapa kwa sababu hiyo.”​—EZEKIELI 40:4

Mu miaka ya nyuma kidogo, mwangaza wa kiroho umeendelea kuongezeka kabisa. Fikiria somo zenye tumepata mu mifano ya Yesu. Kwa sasa, somo mingi kati ya zile zenye tumepata zimekuwa wazi sana mu akili na moyo wetu. Hesabu kubwa ya ile mifano inahusu mambo yenye itatokea wakati wa taabu kubwa yenye inakaribia sana. Kwa hiyo, namna tulikuwa tunaelewa maunabii yenye kupatikana mu kitabu cha Ezekieli imerekebishwa. Kwa mufano, maunabii kuhusu Gogu wa Magogu (sura ya 38 na 39), kazi ya mwanaume mwenye kuwa na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino (sura ya 9), na bonde la mifupa yenye kukauka na kuunganishwa kwa mufano kwa vipande mbili vya muti (sura ya 37). Ile miangaza yote mipya inabadilisha mambo yenye iliandikwa zamani mu kitabu “Mataifa Itajua Kwamba Mimi Ni Yehova.”

Njo maana, watumishi wengi wa Yehova wameuliza, “Ni siku gani tutapataka kitabu chenye kinatoa mafasirio ya sasa juu ya maunabii ya Ezekieli?” Kitabu chenye kiko na ile mafasirio ni hiki: Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena! Wakati utasoma sura zake 22 na kufikiri sana juu ya picha za muzuri zenye kuwa ndani, utashangaa juu ya utafiti wenye ulifanywa kwa uangalifu ili kutayarisha kitabu hiki. Sala mingi zilitolewa pamoja na kufikiri sana juu ya kutafuta kuelewa sababu gani Yehova alitoa kitabu cha kushangaza sana cha Ezekieli. Maulizo kama hii ilifikiriwa sana: Kitabu cha Ezekieli kilikuwa na somo gani kwa ajili ya watu wa mu wakati wa Ezekieli na kiko na somo gani kwa ajili yetu leo? Ni maunabii gani yenye inazungumuzia matukio yenye ingali mbele? Je, inaomba kutafuta vifananishi na vifananishwa mu maunabii ya Ezekieli? Majibu ku ile maulizo yote inatusaidia tuelewe muzuri zaidi kitabu hiki cha Biblia chenye sisi wote tunapenda.

Wakati utakuwa unasoma kitabu cha Ezekieli kuanzia mwanzo mupaka mwisho, utashangaa sana juu ya sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Yehova. Bila shaka utashangaa pia juu ya kanuni za juu zenye Yehova ameweka kwa ajili ya wale wenye wanataka kumuabudu mu namna anakubali, ikuwe mbinguni ao duniani. Kitabu Ibada Safi kitakusaidia ufurahie zaidi mambo yenye Yehova alishafanyia watu wake na ile yenye atawafanyia sasa hivi. Utavumbua kama kitabu hiki kinakazia mambo mbili tena na tena. Kwanza, kusudi tumufurahishe Yehova, tunapaswa kumujua na kumukubali kuwa Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi wa Ulimwengu Wote Muzima. Pili, tunapaswa kumuabudu Yehova mu namna yenye anakubali, na kupatanisha maisha yetu na kanuni zake za juu.

Tunatumaini kama kitabu hiki kitakusaidia uazimie kabisa kumuabudu Yehova mu namna yenye inaheshimisha jina lake kubwa na takatifu. Tena, tunapenda kikutie moyo uendelee kungojea wakati wenye mataifa yote italazimika kujua kwamba yeye ni Yehova.​—Eze. 36:23; 38:23.

Tunasali Baba yetu mwenye upendo, Yehova, abariki sana namna utajikaza kuelewa kitabu chenye roho yake iliongoza Ezekieli aandike.

Ndugu zenu,

Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova