Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 19

“Kila Kitu Kitaishi Mahali Kwenye Muto Huo Mudogo Unapita”

“Kila Kitu Kitaishi Mahali Kwenye Muto Huo Mudogo Unapita”

EZEKIELI 47:9

WAZO KUBWA: Namna maono ya muto wenye unatoka mu hekalu ilitimia zamani, namna inatimia leo, na namna itatimia mu wakati wenye kuja

1, 2. Kulingana na Ezekieli 47:1-12, Ezekieli anaona nini, na anavumbua nini? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

EZEKIELI anaona jambo lingine la kushangaza mu maono yake ya hekalu: Anaona muto mudogo wenye unatiririka kutoka mu hekalu takatifu! Pima tu kuwazia namna anapita mu ile muto ya maji ya kungara sana. (Soma Ezekieli 47:1-12.) Inateremuka kutoka mu kizingiti cha patakatifu; kisha inaenda kutokea mu majengo ya hekalu karibu na mulango mukubwa wa mashariki. Malaika anamupeleka Ezekieli mbali na hekalu, na iko anapima umbali kadiri wako wanaenda. Malaika anaambia Ezekieli tena na tena apite mu maji, na nabii anatambua kama maji iko inaongezeka mbio, na mu wakati kidogo inafikia kuwa muto mukubwa wenye hawezi kuvuka kama tu haingie ndani na kuogelea!

2 Ezekieli anavumbua kama ile muto inateremuka mupaka kuingia mu Bahari ya Chumvi, na wakati inaingia mu Bahari ya Chumvi, maji ya bahari yenye inajaa chumvi na yenye haina uzima inaponyeshwa, na munakuwa samaki mingi. Ku pembeni-pembeni ya muto, anaona miti mingi ya kila namna. Kila mwezi, ile miti inazaa matunda ya mupya yenye iko na vitu vya kujenga mwili, na inatoa majani ya kuponyesha. Kisha kuona ile yote, moyo wa Ezekieli ulipaswa kujaa amani na tumaini. Lakini, sehemu hii ya maono ya hekalu ilikuwa na maana gani kwake na kwa wahamishwa wenzake? Na iko na maana gani kwetu leo?

Muto Wenye Ezekieli Alionaka mu Maono Ulikuwa na Maana Gani kwa Wahamishwa?

3. Juu ya nini tunasema kwamba Wayahudi hawakuelewa kama muto wenye Ezekieli alionaka mu maono ulikuwa muto wa kweli-kweli?

3 Bila shaka, Wayahudi wa zamani walielewa kama muto wenye Ezekieli alionaka haukukuwa muto wa kweli-kweli. Lakini, inaonekana habari hii ya Maandiko iliwakumbusha unabii ingine kuhusu kurudishwa kwa ibada safi, unabii wenye uliandikwa na nabii Yoeli zaidi ya miaka mia mbili hivi yenye ilikuwa imepita. (Soma Yoeli 3:18.) Wakati wahamishwa Wayahudi walisoma maneno ya Yoeli yenye iliongozwa na roho ya Mungu, hawakutazamia kwamba milima ya kweli-kweli ‘ingetiririka matone-matone ya divai tamu’ ao kwamba vilima ‘vingetiririka maziwa’; wala hawakutazamia kama chemchemi ingetiririka kutoka “katika nyumba ya Yehova.” Vilevile, inawezekana Wayahudi wenzake walielewa kama ujumbe wenye kuwa mu maono ya nabii Ezekieli hauzungumuzie muto wa kweli-kweli kabisa. * Kwa hiyo, Yehova alitaka kuwaambia nini? Maandiko inazungumuzia mambo fulani ya kutusaidia kuelewa sehemu fulani za ile maono. Lakini, tutazungumuzia zaidi sana mauhakikisho tatu yenye kuwa wazi na yenye upendo yenye tunaweza kupata mu habari hii ya unabii.

4. (a) Muto wenye Ezekieli aliona mu maono ulipaswa kufanya Wayahudi watazamie baraka gani za Yehova? (b) Namna Biblia inatumia maneno “muto” na “maji” inatuhakikishia je kama Yehova atabariki watu wake? (Ona kisanduku “Mito ya Baraka Kutoka kwa Yehova.”)

4 Muto wa baraka. Mu Biblia, mito na maji inatumiwa sana juu ya kufananisha baraka za Yehova zenye zinatoa uzima. Ezekieli aliona muto wa vile wenye ulikuwa unatiririka kutoka mu hekalu, ile ilipaswa kufanya watu wa Mungu watazamie kama baraka za kiroho za Yehova zenye kutoa uzima zingemwangika juu yao kadiri wangeendelea kushikamana na ibada safi. Baraka gani? Wangepokea tena mafundisho ya kiroho kutoka kwa makuhani. Na kwa kuwa zabihu zingekuwa zinatolewa ku hekalu, wangeweza tena kuwa hakika kama zambi zao zitafunikwa. (Eze. 44:15, 23; 45:17) Kwa hiyo, wangekuwa safi tena, sawa vile wenye kunawishwa mu maji safi yenye inatoka ku hekalu.

5. Namna gani muto wenye Ezekieli alionaka mu maono unaonyesha kama kungeendelea kuwa baraka za kuenea watu wote?

5 Je, kungeendelea kuwa baraka za kuenea watu wote? Maono inafanya tusikuwe na mashaka yoyote juu inaonyesha namna maji inaendelea kuongezeka mu njia ya muujiza​—muto mudogo unakuwa muto mukubwa wenye urefu wa karibu kilometre moja na nusu tu! (Eze. 47:3-5) Hata kama hesabu ya watu ingeweza kuongezeka mu inchi ya Wayahudi yenye ilirudishwa mu hali ya muzuri, baraka za Yehova pia zingeendelea kuongezeka juu ya kutimiza mahitaji yao. Ile muto ilionyesha kama baraka zingekuwa mingi!

6. (a) Ile maono iko na ahadi gani yenye kutia moyo? (b) Ile maono inatoa pia onyo gani? (Ona maelezo.)

6 Maji ya kutoa uzima. Mu maono ya Ezekieli, muto uliteremuka mupaka mu Bahari ya Chumvi, na ulifanya maji ya bahari ikuwe na uzima. Ona kwamba maji ya ile muto ilifanya kukuwe aina mingi ya samaki mu Bahari ya Chumvi, sawa zile zenye zilikuwa zinapatikana pia mu Bahari Kubwa, ao Bahari ya Mediterania. Na hata biashara ya samaki ilikuwa inafanyika pembeni-pembeni ya Bahari ya Chumvi kati ya miji mbili yenye inaonekana haikukuwa karibu-karibu. Malaika alisema: “Kila kitu kitaishi mahali kwenye muto huo mudogo unapita.” Lakini je, ile inamaanisha kama maji yenye ilikuwa inatoka mu nyumba ya Yehova ilifika ku kila sehemu ya Bahari ya Chumvi? Hapana. Malaika alieleza kama ile maji ya kutoa uzima haitafika ku sehemu fulani za tingitingi. Zile sehemu “zitabakia za chumvi.” * (Eze. 47:8-11) Kwa hiyo, ile maono ya kiunabii ilitoa ahadi yenye kutia moyo yenye inaonyesha kama ibada safi itapatia watu uzima, ni kusema, itawafanya wakuwe na hali ya muzuri. Lakini ilitoa pia onyo fulani: Haiko wote njo wangekubali baraka za Yehova; wala haiko wote njo wangeponyeshwa.

7. Miti yenye ilionwa mu maono pembeni-pembeni ya muto ilipatia wahamishwa Wayahudi uhakikisho gani?

7 Miti ya kutoa chakula na kuponyesha. Tuseme nini juu ya miti ya pembeni-pembeni ya muto? Inafanya maono ipendeze zaidi, hauone vile? Inaongeza pia jambo fulani kuhusu maana ya ile maono. Bila shaka Ezekieli na watu wa inchi yake walifurahia kuwaza juu ya matunda ya butamu yenye ile miti ingezaa, matunda ya mupya kila mwezi! Ile picha yenye kupendeza iliwahakikishia tena kwamba Yehova angewapatia chakula cha kiroho. Lakini, haiko ile tu. Ona kwamba majani ya ile miti “yatakuwa ya kuponyesha.” (Eze. 47:12) Yehova alijua kama, wahamishwa wenye wangerudia mu inchi yao wangehitaji zaidi sana kuponyeshwa kiroho, na aliahidi kama ni vile atafanya. Maunabii ingine ya kurudishwa kwa ibada safi ilizungumuzia namna alifanya vile, sawa vile tuliona mu Sura ya 9 ya kitabu hiki.

8. Ni nini inaonyesha kama maono ya Ezekieli ingetimia mu njia kubwa zaidi?

8 Lakini, sawa vile tulijifunza pia mu Sura ya 9, wahamishwa wenye walirudia mu inchi yao walijionea kwa kiasi kidogo utimizo wa maunabii ya kurudishwa kwa ibada safi. Ni watu njo walifanya ile maunabii itimie kwa kiasi kidogo. Yehova angewabariki je kwa ukamili wakati walikuwa wanarudilia mambo ya mubaya, hawakukuwa wanatii na walikuwa wanazarau sana ibada safi? Waaminifu waliumia sana mu moyo na kukata kitumaini wakati waliona matendo ya Wayahudi wenzao. Lakini, waabudu waaminifu wa Yehova walijua kama ahadi zake hazikosake kutimia; zinatimiaka tu. (Soma Yoshua 23:14.) Kwa hiyo, siku moja maono ya Ezekieli ingetimia mu njia kubwa zaidi. Lakini wakati gani?

Muto Unatiririka Leo!

9. Ni wakati gani maono ya Ezekieli ya hekalu inatimia mu njia kubwa zaidi?

9 Kama vile tuliona mu Sura ya 14 ya kitabu hiki, maono ya Ezekieli ya hekalu inatimia mu njia kubwa zaidi mu “kipindi cha mwisho cha zile siku,” wakati ibada safi inainuliwa mu namna yenye haiyakuwaka. (Isa. 2:2) Ni mu maana gani sehemu hii ya maono ya Ezekieli iko inatimia leo?

10, 11. (a) Ni baraka gani zenye zinatiririka leo juu yetu sawa muto? (b) Namna gani baraka za Yehova zimeendelea kuongezeka juu ya kutimiza mahitaji yenye inaendelea kuongezeka mu siku hizi za mwisho?

10 Muto wa baraka. Maji yenye inatiririka kutoka mu nyumba ya Yehova inatukumbusha baraka gani leo? Bila shaka, inatukumbusha mambo mingi yenye inatusaidia tukuwe na hali ya muzuri ya kiroho na yenye inatuletea faida za kiroho. Ya kwanza kabisa ni nguvu ya kutakasa ya zabihu ya ukombozi ya Kristo, yenye inafanya zambi zetu zisamehewe. Kweli safi za Neno la Mungu zinafananishwa pia na maji yenye inatakasa, yenye inatoa uzima. (Efe. 5:25-27) Namna gani zile baraka zimetiririka mu wakati wetu?

11 Mu 1919, watumishi wa Yehova walikuwa kidogo, na walifurahi sana kupokea chakula cha kiroho chenye walihitaji. Mu miaka ya kufuata, hesabu yao iliendelea kuongezeka. Leo, watu wa Mungu wako zaidi ya milioni munane. Je, maji safi ya kweli imeendelea kuongezeka kadiri wao pia wanaendelea kuongezeka? Ndiyo! Tunafundishwa kweli mingi sana za Biblia. Mamiliare ya Biblia, vitabu, magazeti, broshua, na matrakte imetiririka na kumwangika juu ya watu wa Mungu mu miaka mia moja yenye imepita. Kama vile ile muto yenye Ezekieli aliona mu maono, kweli safi za Biblia zinaendelea kuongezeka sana juu ya kutimiza mahitaji yenye iko inaongezeka ya watu wenye kiu ya kiroho mu dunia yote. Vichapo mingi vyenye kutegemea Biblia vimechapishwa. Na sasa, kupitia site yetu jw.org, vile vichapo vinapatikana mu njia ya kielektroniki mu luga zaidi ya 900! Ile maji yote ya kweli imesaidia je watu wa moyo muzuri?

12. (a) Tumejionea namna gani kwamba ujumbe wa kweli uko unaletea watu uzima na hali ya muzuri ya kiroho? (b) Ni onyo gani yenye kufaa yenye ile maono inatupatia leo? (Ona pia maelezo.)

12 Maji ya kutoa uzima. Ezekieli aliambiwa: “Kila kitu kitaishi mahali kwenye muto huo mudogo unapita.” Fikiria namna ujumbe wa kweli umetiririka juu ya wale wote wenye wameingia mu inchi yetu ya kiroho yenye imerudishwa mu hali ya muzuri. Kweli za Biblia zimepatia mamilioni ya watu wa moyo muzuri uzima na hali ya muzuri ya kiroho. Lakini, maono inatoa pia onyo hii ya maana: Haiko wote njo wanaendelea kusikia ile kweli. Sawa ile maeneo ya maji-maji na tingitingi mu Bahari ya Chumvi yenye Ezekieli aliona mu maono, kuko mioyo yenye haipendi kusikia, yenye inakataa kuitika na kutenda kulingana na kweli. * Tujikaze tusikuwe vile!​—Soma Kumbukumbu la Torati 10:16-18.

13. Miti yenye ilionwa mu maono inaweza kutupatia somo gani?

13 Miti ya kutoa chakula na kuponyesha. Je, miti yenye ilionwa mu maono pembeni-pembeni ya muto iko na somo fulani za kututia moyo leo? Ndiyo! Kumbuka, ile miti ilikuwa inazaa matunda ya mupya na ya butamu kila mwezi, na majani yake ilikuwa inaponyesha. (Eze. 47:12) Ile inatukumbusha kama tunatumikia Mungu mwenye anatukulisha kwa ukarimu na kutuponyesha mu njia ya maana zaidi: njia ya kiroho. Dunia ya leo inagonjwa na iko na njaa ya kiroho. Lakini, fikiria mambo yenye Yehova anatupatia. Je, ulishakajisikia kuwa mwenye kubarikiwa sababu uko na chakula mingi ya kiroho, kwa mufano, kisha kusoma habari fulani mu gazeti, ao kisha kuimba wimbo wa mwisho ku mukusanyiko wa muzunguko ao wa eneo, ao kisha kumaliza kuangalia video ao programu ya kila mwezi ya JW Télédiffusion? Tuko tunakulishwa muzuri sana. (Isa. 65:13, 14) Je, chakula yetu ya kiroho inatusaidia tukuwe na hali ya muzuri ya kiroho? Mashauri ya muzuri yenye tunapata, yenye inategemea kabisa Neno la Mungu, inatusaidia kupigana na maadui wa kiroho sawa vile uasherati, pupa, na ukosefu wa imani. Pia, Yehova amekamata mupango wa kusaidia Wakristo wapone ugonjwa wa kiroho wenye unatokana na zambi nzito. (Soma Yakobo 5:14.) Tumebarikiwa sana, sawa vile maono ya Ezekieli ya miti inaonyesha.

14, 15. (a) Maeneo ya tingitingi yenye haikuponyeshwa mu maono ya Ezekieli inatupatia somo gani? (b) Namna gani muto wenye Ezekieli alionaka mu maono unatuletea faida leo?

14 Maeneo ya tingitingi yenye haikuponyeshwa inaweza pia kutufundisha jambo fulani. Hatupaswe hata kidogo kufungia mulango baraka za Yehova mu maisha yetu. Ni hatari sana kama hatuponyeshwe, sawa vile watu mingi mu dunia hii yenye kugonjwa. (Mt. 13:15) Tofauti na ile, tunafurahi sana kufaidika na muto wa baraka. Wakati tunakunywa kwa hamu maji safi ya kweli mu Neno la Mungu, wakati tunapatia wengine ile maji mu mahubiri, wakati tunapokea muongozo, faraja, na musaada wa wazee wenye wamezoezwa na mutumwa muaminifu, ile yote inatukumbusha muto wenye Ezekieli alionaka mu maono. Ile muto inatoa uzima na inaponyesha kila fasi kwenye inaenda!

15 Sasa, ile unabii ya muto itatimia namna gani wakati wenye kuja? Kama vile tutaona, ile muto itatiririka mu njia kubwa sana mu Paradiso yenye iko inakuja.

Namna Ile Maono Itatimia mu Paradiso

16, 17. (a) Namna gani maji ya uzima itaendelea kuongezeka mu Paradiso? (b) Namna gani muto wa baraka utatuletea faida mu Paradiso?

16 Je, unajiwazia mu Paradiso, marafiki na watu wa familia wako pembeni yako, na uko unafurahia kabisa maisha? Kujifunza maono ya muto yenye Ezekieli alionaka, kunaweza kukusaidia ujiwazie muzuri zaidi mu Paradiso. Juu ya nini tunasema vile? Fikiria tena mambo tatu yenye kuwa wazi na yenye kuonyesha upendo yenye inapatikana mu ile maono.

17 Muto wa baraka. Tunaweza kusema kama ule muto wa mufano, utaongezeka zaidi mu Paradiso, sababu utatuletea faida za kiroho na pia za kimwili. Wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu, Ufalme wa Mungu utasaidia waaminifu kupata faida za bei ya ukombozi mu njia kubwa zaidi. Hatua kwa hatua, watafikia kuwa wakamilifu! Hakutakuwa tena magonjwa, wanganga, hospitali, na asiranse ya matunzo! Maji ya uzima itatiririka juu ya mamilioni ya watu wenye wataokoka Armagedoni, “kundi kubwa la watu” wenye watatoka mu “taabu kubwa.” (Ufu. 7:9, 14) Lakini, baraka za ku mwanzo-mwanzo za ule muto, hata kama zitakuwa kubwa namna gani, zitakuwa tu sawa muto mudogo kwa kuzilinganisha na mambo yenye itakuwa kisha. Kama vile maono ya Ezekieli inaonyesha, ule muto utaongezeka juu ya kutimiza mahitaji makubwa zaidi.

Mu Paradiso, muto wa baraka utafanya kila mutu akuwe kijana na akuwe na afya ya muzuri (Ona fungu la 17)

18. Ni mu maana gani “muto wa maji ya uzima” utakuwa muto mukubwa wakati wa Miaka Elfu?

18 Maji ya kutoa uzima. Wakati wa Miaka Elfu, “muto wa maji ya uzima” utakuwa muto mukubwa. (Ufu. 22:1) Mamilioni mingi, na hata mamiliare ya watu, watafufuliwa na kupewa nafasi ya kuishi milele mu Paradiso! Baraka za Yehova kupitia Ufalme zitatia ndani kupatia uzima hesabu kubwa ya wafu, wanadamu wenye walikuwa wamelala miaka mingi bila uwezo mu mavumbi ya dunia. (Isa. 26:19) Lakini je, wale wote wenye watafufuliwa wataendelea kuishi milele?

19. (a) Ni nini inaonyesha kama kutakuwa maji ya mupya ya kweli za Mungu mu Paradiso? (b) Mu wakati wenye kuja, ni mu maana gani watu fulani watakuwa kama zile sehemu zenye ‘zilibakia za chumvi’?

19 Kila mutu atachagua. Vitabu vipya vya kukunjwa vitafunguliwa ile wakati. Kwa hiyo, maji ya kuburudisha kutoka kwa Yehova itatia ndani kweli za mupya zenye zitafunuliwa, maagizo ya mupya ya kiroho. Je, hauone kama ni jambo la kutia moyo kufikiria ile mambo yenye tunangojea? Lakini, watu fulani watakataa baraka za Yehova, watachagua kumuasi. Watu fulani wanaweza kuasi mu ile Miaka Elfu, lakini hawataruhusiwa kuvuruga Paradiso. (Isa. 65:20) Ile inaweza kutukumbusha maono ya Ezekieli na kutufanya tufikirie zile fasi za tingitingi zenye hazikuzaa, zenye ‘zilibakia za chumvi.’ Wale wenye watakataa kwa kiburi kunywa ile maji yenye samani ya uzima wataonyesha kama hawana akili! Kisha Miaka Elfu, kutakuwa kikundi cha waasi chenye kitajiunga na Shetani. Wale wote wenye watakataa utawala wa haki wa Yehova watafikia mwisho uleule: kifo cha milele.​—Ufu. 20:7-12.

20. Miti yenye Ezekieli alionaka inatukumbusha mupango gani wenye utatuletea faida mu Miaka Elfu?

20 Miti ya kutoa chakula na kuponyesha. Yehova hapendi hata mutu moja kati yetu apoteze uzima wa milele. Juu ya kutusaidia tukamatililie ile uzima yenye anatupatia, atatia tena mupango sawa ule wa miti yenye Ezekieli alionaka. Lakini mu Paradiso, faida zenye Yehova atatoa zitakuwa za kimwili na za kiroho. Mbinguni, Yesu Kristo na watawala wenzake 144 000 watatawala wakiwa wafalme mu Miaka Elfu. Wakiwa kikundi cha makuhani, wale 144 000 watatolea watu faida za zabihu ya ukombozi ya Kristo, na ile itasaidia watu wakuwe wakamilifu. (Ufu. 20:6) Mupango wa kuponyesha watu kimwili na kiroho unatukumbusha miti yenye Ezekieli alionaka pembeni-pembeni ya muto, miti yenye inazaa matunda ya kujenga mwili na yenye iko na majani ya kuponyesha. Maono ya Ezekieli inafanana na unabii ingine ya muzuri, yenye mutume Yohana aliandika. (Soma Ufunuo 22:1, 2.) Majani ya miti yenye Yohana alionaka “yalikuwa ya kuponyesha mataifa.” Mamilioni na mamilioni ya wanadamu waaminifu watafaidika na utumishi wa kikuhani wa wale 144 000.

21. Kufikiri juu ya muto wenye Ezekieli alionaka mu maono kunakusaidia namna gani, na tutazungumuzia nini sasa? (Ona kisanduku “Muto Mudogo Unakuwa Muto Mukubwa!”)

21 Wakati unafikiria muto wenye Ezekieli alionaka mu maono, je, moyo wako haujae amani na tumaini? Mambo ya muzuri iko inatuchunga! Waza kidogo: Miaka mingi mbele, Yehova alitumia maneno ya mufano juu ya kuzungumuzia ile wakati. Alifanya vile juu ya kutualika tukuwe pale na tujionee utimizo mukubwa wa ile maono, wakati itatimia kabisa-kabisa. Utakuwaka pale? Pengine unajiuliza kama utapataka fasi mu Paradiso. Tuzungumuzie sasa namna habari za kumalizia za unabii wa Ezekieli zinatuhakikishia vile.

^ fu. 3 Kwa kuongezea, inawezekana wale wahamishwa Wayahudi wenye walijua muzuri hali za maeneo ya inchi yao walijua kama muto hauwezi kutoka Yerusalemu na kuteremukia mu Bahari ya Chumvi, sababu ingeomba muto upande vilima.

^ fu. 6 Wachunguzi fulani wanaona ile kuwa jambo la muzuri, sababu mu miaka mingi kuokota chumvi juu itumiwe kuchunga vitu ni biashara yenye iko na faida sana mu eneo la Bahari ya Chumvi. Lakini, unabii unasema kama ile maji ya fasi ya tingitingi ‘haitaponyeshwa.’ Haitakuwa na uzima, haitaponyeshwa, sababu maji ya kutoa uzima kutoka mu nyumba ya Yehova haikuigusa. Kwa hiyo, inaonekana kama, wakati unabii unasema kama maeneo ya tingitingi itaendelea kuwa na chumvi, hauzungumuzie jambo la muzuri, lakini jambo la mubaya lenye litapata ile maeneo.​—Zb. 107:33, 34; Yer. 17:6.

^ fu. 12 Fikiria vilevile mufano wa Yesu wa wavu wa kukokotwa. Samaki mingi inakamatwa mu wavu ao makila, lakini yote haiko ya ‘muzuri.’ Samaki zenye hazifae zinapaswa kutupwa. Kupitia ile mufano, Yesu alionya kama wakati fulani, watu mingi wenye wanaingia mu tengenezo la Yehova wanaweza kukosa kuwa waaminifu.​—Mt. 13:47-50; 2 Ti. 2:20, 21.