Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 22

“Abudu Mungu”

“Abudu Mungu”

UFUNUO 22:9

WAZO KUBWA: Kurudilia kwa kifupi mambo makubwa ya kitabu cha Ezekieli na namna inahusu wakati wa leo na wakati wenye kuja

1, 2. (a) Ni uamuzi gani wenye kila mumoja wetu anapaswa kufanya? (b) Malaika moja muaminifu alitenda je wakati alitaka kuabudiwa?

KILA mumoja wetu anapaswa kujibia hii ulizo ya maana sana: Nitaabudu nani? Watu mingi wanaweza kusema ni nguvu kujibu ile ulizo na kama haiko mwepesi kuamua kama utaabudu nani. Lakini, kusema kweli, uamuzi uko wazi na mwepesi: Ao tunaabudu Yehova Mungu ao tunaabudu Shetani Ibilisi.

2 Shetani anapendaka sana kuabudiwa. Ile ilionekana wazi wakati alimujaribu Yesu. Kama vile tuliona mu Sura ya 1 ya kitabu hiki, Shetani aliambia Yesu kama atamupatia jambo fulani la ajabu​—mamlaka juu ya falme zote za dunia. Halafu yeye aliomba apewe nini? Aliomba Yesu ‘amufanyie tendo la ibada.’ (Mt. 4:9) Lakini, malaika mwenye alipatiaka mutume Yohana ufunuo alikataa kuabudiwa. (Soma Ufunuo 22:8, 9.) Wakati Yohana alitaka kuabudu ule malaika, ule mwana wa kiroho wa Mungu mwenye kuwa munyenyekevu alisema hivi: “Usifanye vile!” Kuliko kusema, ‘Uniabudu,’ ule malaika alisema, “Abudu Mungu.”

3. (a) Kitabu hiki kimekuwa na kusudi gani? (b) Tutazungumuzia nini sasa?

3 Kitabu hiki kimekuwa na kusudi la kutusaidia tuazimie kabisa kumuabudu Yehova Mungu peke yake, kama vile ule malaika alisema. (Kum. 10:20; Mt. 4:10) Acha turudilie kwa kifupi mambo yenye maunabii na maono ya Ezekieli imetufundisha kuhusu ibada safi. Kisha, kwa musaada wa Maandiko, tutachungulia juu ya kuona namna mambo itakuwaka wakati kila mumoja wetu mu dunia atapambana na jaribu la mwisho​—jaribu lenye litaonyesha nani ataona namna ibada safi ya Yehova itafikia kurudishwa kwa ukamili, milele na milele.

Mambo Tatu Yenye Kitabu cha Ezekieli Kinakazia Sana

4. Kitabu cha Ezekieli kinakazia sana mambo gani tatu?

4 Kitabu cha Ezekieli kinatufundisha kama ibada safi haiko kufuata-fuata tu desturi fulani. Ibada safi inaomba (1) tushikamane na Yehova tu, (2) tuendelee kuwa na umoja mu ibada safi, na (3) tuonyeshe wengine upendo. Ona namna maunabii na maono yenye inazungumuziwa mu kitabu hiki inakazia sana ile mambo tatu.

Jambo la kwanza: Kushikamana na Yehova tu

5-9. Tumejifunza nini kuhusu kushikamana na Yehova tu?

5 Sura ya 3: * Maono ya kushangaza sana yenye kuonyesha Yehova akiwa amezungukwa na upinde wa mvua na akiwa juu ya viumbe vya roho vyenye nguvu inatufundisha jambo moja la maana kabisa: Mweza-Yote tu njo anastahili ibada yetu.​—Eze. 1:4, 15-28.

6 Sura ya 5: Ilichukiza sana kuona maono yenye ilionyesha namna hekalu la Yehova lilikuwa limechafuliwa! Ile maono inaonyesha kama Yehova haiko kipofu, anaonaka kila kitu. Anaonaka matendo ya kukosa ushikamanifu, kwa mufano wakati watu wake wanaabudu sanamu, hata kama wengine hawaone ile matendo. Matendo ya vile inamuumiza sana na anapatia nizamu wenye kuifanya.​—Eze. 8:1-18.

7 Sura ya 7: Hukumu zenye Yehova alitangaza juu ya mataifa jirani yenye ilitendea Israeli kwa “zarau kamili” inahakikisha kwamba Yehova ataomba wale wenye kutendea mubaya watu wake watoe hesabu. (Eze. 25:6) Lakini uhusiano wenye Israeli alifanya na ile mataifa unatufundisha jambo lingine: Tunapaswa kutia ushikamanifu wetu kwa Yehova pa nafasi ya kwanza, kuliko kitu kingine chochote. Hatupaswe kuvunja kanuni za Biblia juu tu ya kufurahisha watu wa jamaa wenye hawamuabudu Yehova; wala kutumainia utajiri ao kuvunja musimamo wetu kwa kupatia guvernema za wanadamu utii wenye Yehova tu njo anastahili.

8 Sura ya 13 na 14: Maono ya hekalu lenye kuwa ku mulima murefu inatufundisha kwamba tunapaswa kuishi kulingana na kanuni za juu za Yehova, na tunapaswa kutambua kama yeye iko juu ya miungu ingine yote.​—Eze. 40:1–48:35.

9 Sura ya 15: Maelezo ya unabii yenye ndani yake Israeli na Yuda wanalinganishwa na makahaba inatukumbusha kama Yehova anachukia sana uzinifu wa kiroho.​—Eze., sura ya 16 na 23.

Jambo la pili: Kuendelea kuwa na umoja mu ibada safi

10-14. Ni maunabii gani yenye inakazia sana ulazima wa kuendelea kuwa na umoja mu ibada safi?

10 Sura ya 8: Maunabii yenye kuahidi kama Yehova angesimamisha “muchungaji mumoja” juu ya kuchunga watu Wake inaonyesha kwamba ni jambo la lazima tutumike mu umoja na amani chini ya uongozi wa Yesu.​—Eze. 34:23, 24; 37:24-28.

11 Sura ya 9: Maunabii ya Ezekieli kuhusu watu wa Mungu wenye walikombolewa mu utekwa wa Babiloni na kisha wakarudishwa mu inchi yao iko na ujumbe fulani kwa ajili ya wale wenye wanapenda kumufurahisha Yehova leo. Waabudu wa kweli wa Yehova wanapaswa kuendelea kujitenga kabisa na desturi na mafundisho yenye kuchafua ya dini ya uongo. Hata kama tulitoka mu dini mbalimbali, hali fulani ya maisha, na hatuko watu wa kabila moja, tunapaswa kulinda umoja wenye unaonyesha kama tuko watu wa Mungu.​—Eze. 11:17, 18; 12:24; Yoh. 17:20-23.

12 Sura ya 10: Habari kuhusu umoja ilizungumuziwa mu maono kuhusu mifupa ya kukauka yenye iliishi tena. Tuko na pendeleo kubwa la kuwa kati ya kikundi cha waabudu wa kweli wenye wanatumika pamoja sawa vile jeshi!​—Eze. 37:1-14.

13 Sura ya 12: Unabii wenye kuzungumuzia vipande mbili vya muti vyenye vinakuwa kipande kimoja cha muti unakazia zaidi sana umoja. Imani yetu inatiwa nguvu wakati tunaona namna watiwa-mafuta na kondoo wengine wanatimiza ile unabii! Hata kama tunaishi mu dunia yenye kugawanyika sababu ya chuki yenye kutokana na dini na politike, upendo na ushikamanifu unaendelea kutuunganisha.​—Eze. 37:15-23.

14 Sura ya 16: Maono ya mwanaume mwenye iko na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino na wanaume wenye wako na silaha za kuponda-ponda inatupatia onyo hii nzito: Ni wale tu wenye wataingia mu “taabu kubwa” na wako waabudu safi njo watapata alama ya wokovu.​—Mt. 24:21; Eze. 9:1-11.

Jambo la tatu: Kuonyesha wengine upendo

15-18. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuonyesha upendo, na namna gani tunaweza kufanya vile?

15 Sura ya 4: Maono ya viumbe ine vyenye uzima ilitufundisha kuhusu sifa za Yehova, na ya kwanza kabisa ni upendo. Wakati tunasema na kutenda kwa upendo, tunaonyesha kama Yehova njo Mungu wetu.​—Eze. 1:5-14; 1 Yo. 4:8.

16 Sura ya 6 na 11: Upendo wa Mungu ulimuchochea kuweka watu fulani kuwa walinzi, kwa mufano Ezekieli. Juu Mungu ni upendo, hataki mutu yeyote aharibiwe wakati ataharibu utawala wa Shetani ku dunia. (2 Pe. 3:9) Tuko na pendeleo la kuonyesha upendo wa Mungu kwa kutimiza daraka letu la kutegemeza kazi ya mulinzi wa leo.​—Eze. 33:1-9.

17 Sura ya 17 na 18: Yehova anajua kama watu wengi watakataa wema wake na watajaribu kumaliza waabudu wake washikamanifu. Upendo utamuchochea Yehova apiganie watu wake wakati “Gogu wa inchi ya Magogu” atashambulia wale wenye wako washikamanifu Kwake. Kupenda wengine kunatuchochea kuonya watu mingi kadiri inawezekana kama Yehova ataharibu wale wenye kutesa watu wake.​—Eze. 38:1–39:20; 2 Te. 1:6, 7.

18 Sura ya 19, 20, na 21: Maono yenye inazungumuzia muto wa maji ya uzima na namna inchi ilipaswa kugawanywa inaonyesha waziwazi kwamba Yehova anapenda watu. Ile maono inaonyesha matokeo ya upendo mukubwa zaidi wenye Yehova alituonyesha, alitoa uzima wa Mwana wake juu zambi zetu zisamehewe na juu tufurahie maisha ya ukamilifu tukiwa sehemu ya familia ya Mungu. Njia moja ya muzuri zaidi ya kuonyesha kama tunapenda watu ni kuwaelezea kuhusu wakati muzuri wenye kuja, wenye Yehova ametayarishia wale wenye kuamini Mwana wake.​—Eze. 45:1-7; 47:1–48:35; Ufu. 21:1-4; 22:17.

Tendo la Kushangaza Sana la Unyenyekevu Kisha Miaka Elfu

19. Yesu atafanya nini mu Utawala wake wa Miaka Elfu? (Ona kisanduku “Jaribu la Mwisho.”)

19 Mu Miaka Elfu ya Utawala wake, Yesu atafufua mamiliare ya watu na kumaliza maumivu yenye “adui [wetu] kifo” analetaka. (1 Ko. 15:26; Mk. 5:38-42; Mdo. 24:15) Historia ya mwanadamu imekuwa sawa vile hadisi ya kuleta huruma yenye inajaa mambo ya huzuni na kupoteza. Lakini kadiri kila kizazi kitakuwa kinafufuliwa, Yesu atakuwa anafuta ile hadisi ya mubaya na kupatia wale wenye wanafufuliwa nafasi ya kuandika historia mupya. Kwa musingi wa zabihu ya bei ya ukombozi, atamaliza mambo yote ya mubaya yenye inatokana na magonjwa, vita, na njaa. Zaidi ya ile, atatusaidia kumaliza kile kinaletaka huzuni, ni kusema, zambi yenye tuliriti kutoka kwa Adamu. (Ro. 5:18, 19) Yesu ‘atavunja kazi za Ibilisi’ kwa ukamili. (1 Yo. 3:8) Kisha kutatokea nini?

Wale wenye watafufuliwa watapewa nafasi ya kuandika historia mupya

20. Namna gani Yesu na wale 144 000 wataonyesha unyenyekevu wa kushangaza sana? Fasiria. (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

20 Soma 1 Wakorinto 15:24-28. Kisha wanadamu wote kuwa wakamilifu, na dunia kuwa Paradiso namna Yehova alipenda tangu mwanzo, Yesu na watawala wenzake 144 000 wataonyesha unyenyekevu wa kushangaza sana: Watamurudishia Yehova Ufalme. Kwa kupenda, na bila kukokotana, watarudisha mamlaka yenye walikuwa nayo mu miaka elfu. Mambo yote yenye Ufalme utakuwa umefanya itadumu milele na milele.

Jaribu la Mwisho

21, 22. (a) Dunia itakuwa je ku mwisho wa miaka elfu? (b) Juu ya nini Yehova atafungua Shetani na mashetani wake?

21 Kisha, Yehova atafanya jambo lingine la ajabu sana, la kuonyesha kama anatumainia sana raia wake wa ku dunia. Ataamuru Shetani na mashetani wafunguliwe kutoka mu abiso mwenye wamefungwa miaka elfu. (Soma Ufunuo 20:1-3.) Dunia yenye wataona itakuwa tofauti na ile yenye walijuaka. Mbele Armagedoni ifike, watu wengi walipotoshwa na Shetani na umoja kati ya watu ulikuwa umegawanyika juu ya chuki na ubaguzi. (Ufu. 12:9) Lakini ku mwisho wa miaka elfu, wanadamu wote watakuwa wanamuabudu Yehova kama familia moja yenye umoja, na yenye upendo. Dunia yote itakuwa Paradiso yenye amani.

22 Juu ya nini Yehova atafungua vile viumbe vibaya sana sawa vile Shetani na mashetani mu dunia yenye kuwa safi? Juu, ushikamanifu wa watu wengi kati ya wale wenye watakuwa wazima ku mwisho wa miaka elfu utakuwa haujajaribiwaka tangu wako waaminifu kwa Yehova. Wengi walikufa bila kumujua Yehova na kisha wakafufuliwa mu Paradiso. Yehova aliwapatia uzima lakini pia aliwatimizia mahitaji yao ya kimwili na ya kiroho. Watakuwa hawajachochewaka na mambo ya mubaya, wameishi na watu wazuri tu. Watakuwa wameishi kati ya watu wenye kumupenda na kumutumikia Yehova. Shetani anaweza kuleta juu ya watu hawa wenye watakuwa wamefufuliwa shitaka ileile yenye aliletaka juu ya Yobu, anaweza kuwashitaki kama wanamutumikia Mungu juu tu anawalinda na kuwabariki. (Yob. 1:9, 10) Kwa hiyo, mbele Yehova aandike majina yetu lote mu kitabu cha uzima, atatupatia nafasi ya kuonyesha kama kweli tuko washikamanifu kwa Baba yetu na Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi.​—Ufu. 20:12, 15.

23. Kila mutu atapaswa kukamata uamuzi gani?

23 Mu wakati kidogo, Shetani atapewa nafasi ya kuchochea watu waache kumutumikia Mungu. Itakuwa je? Hakuna shaka kwamba kila mutu atapaswa kukamata uamuzi wenye unafanana na ule wenye Adamu na Eva walipaswa kukamata​—kukubali kanuni za Yehova, kutegemeza utawala wake, na kumuabudu yeye, ao kumuasi Mungu na kumuunga mukono Shetani.

24. Juu ya nini wale wenye wataasi wanaitwa Gogu na Magogu?

24 Soma Ufunuo 20:7-10. Ya kushangaza ni kwamba, wale wenye wataasi ku mwisho wa miaka elfu wanaitwa Gogu na Magogu. Wako na tabia za kufanana na za waasi wenye Ezekieli alitabiri kuwa wangeshambulia watu wa Mungu wakati wa taabu kubwa. Wale waasi wenye Ezekieli alizungumuzia, ni kusema, “Gogu wa inchi ya Magogu,” ni mataifa mbalimbali yenye ilipinga utawala wa Yehova. (Eze. 38:2) Vilevile, wale wenye wataasi ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo wanaitwa “mataifa.” Wanastahili kabisa kuitwa vile. Juu ya nini? Juu, wakati wa Utawala wa Miaka Elfu, migawanyiko ya kitaifa itakuwa imeondolewa; watu wote watakuwa raia za guvernema moja tu, Ufalme wa Mungu. Sisi wote tutakuwa taifa moja tu la kiroho. Wakati unabii unaita wale waasi kuwa Gogu na Magogu na kusema kama wako “mataifa,” ile inaonyesha kama Shetani ataweza kutokeza migawanyiko kati ya washiriki fulani wa watu wa Mungu. Hakuna mwenye watakaza akuwe upande wa Shetani. Kila mwanadamu mukamilifu atajiamulia.

Wale wenye wataasi wanaitwa Gogu wa Magogu (Ona fungu la 24)

25, 26. Ni wangapi watajiunga na Shetani, na ni nini itawapata?

25 Ni wangapi watajiunga na Shetani? Hesabu ya wenye wataasi itakuwa “kama muchanga wa bahari.” Ile haionyeshe kabisa-kabisa kama hesabu kubwa sana ya watu itaasi. Juu ya nini tunasema vile? Fikiria ahadi yenye Abrahamu alipewa. Yehova alisema kama uzao wake ungekuwa sawa vile “chembe za muchanga pembeni ya bahari.” (Mwa. 22:17, 18) Lakini ku mwisho, hesabu ya wenye kufanyiza uzao wake ilifikia kuwa watu 144 001. (Gal. 3:16, 29) Ni hesabu kubwa, lakini kama tunailinganisha na hesabu ya wanadamu wote, ni watu kidogo tu. Vilevile, hesabu ya watu wenye watajiunga na Shetani inaweza kuwa kubwa, lakini haitakuwa watu wengi sana kabisa. Waasi hawatakuwa hatari kwa watumishi waaminifu wa Yehova.

26 Wale wenye watajiunga na uasi wataharibiwa mara moja. Wao na Shetani wataishia pale​—bila tumaini la kufufuliwa siku moja. Yenye itakuwa inakumbukwa tu ni maamuzi yao ya mubaya na matokeo ya ile maamuzi.​—Ufu. 20:10.

27-29. Ni nini inangojea wale wenye watashinda jaribu la mwisho?

27 Lakini, majina ya wale wenye watashinda jaribu la mwisho itaandikwa milele mu “kitabu cha uzima.” (Ufu. 20:15) Kisha, kama familia yenye umoja, wana na mabinti wote waaminifu wa Yehova watamupatia ibada yenye anastahili kabisa.

28 Fikiria ile wakati. Utakuwa na maisha ya muzuri, kazi ya muzuri na marafiki wazuri. Wewe na wapendwa wako hamutakuwa munateseka tena. Utasimama mbele ya Yehova bila kuwa na lazima ya mupatanishi, na bila zambi yoyote. Kila mutu atakuwa na urafiki wa bila mipaka na Mungu. Na ya maana zaidi, ibada safi itatolewa kwa ukamilifu mbinguni na duniani. Na pale sasa njo ibada safi itakuwa imerudishwa kwa ukamili kabisa!

Wakati utakuwa mukamilifu, utasimama mbele ya Yehova bila kuwa na lazima ya mupatanishi, na bila zambi yoyote (Ona fungu la 28)

29 Je, utakuwaka pale juu ujionee ile wakati ya muzuri sana? Inawezekana, kama unaendelea kutumikisha somo tatu kubwa zenye tunapata mu kitabu cha Ezekieli​—kushikamana na Yehova tu, kuendelea kufanya ibada safi mu umoja na wengine, na kuonyesha wengine upendo. Maunabii ya Ezekieli inatoa somo fulani ya mwisho, na ya musingi. Somo gani?

Wazia namna itafurahisha sana wakati viumbe vyote mbinguni na duniani vitafikia kuungana mu ibada safi (Ona fungu la 27-29)

“Kujua Kwamba Mimi ni Yehova”

30, 31. Maneno “watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova” itamaanisha nini (a) kwa maadui wa Mungu? (b) kwa watu wa Mungu?

30 Mu kitabu chote cha Ezekieli, maneno “watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova” inarudiliwa tena na tena. (Eze. 6:10; 39:28) Kwa maadui wa Mungu, ile maneno itamaanisha vita na kifo. Watalazimika kujua jambo lingine zaidi ya kujua kama Yehova iko. Watajifunza kupitia magumu kama jina lake kubwa linamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” “Yehova wa majeshi” atakuwa “mupiganaji-vita mwenye nguvu” mwenye atapigana nao. (1 Sa. 17:45; Kut. 15:3) Wataelewa kweli hii ya maana juu ya Yehova: Hakuna kitu kinaweza kumuzuia asitimize kusudi lake. Lakini itakuwa kuchelewa sana.

31 Kwa watu wa Mungu, maneno “watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova” itamaanisha amani na uzima. Yehova atafanya tukuwe namna alipenda tukuwe ku mwanzo, ni kusema, wana na mabinti wenye kuonyesha kwa ukamilifu sifa zake. (Mwa. 1:26) Tayari, Yehova amejionyesha kuwa Baba yetu mwenye upendo na Muchungaji mwenye kutulinda. Sasa hivi, atakuwa Mufalme wetu mushindi. Mbele ile wakati ifike, tuchunge mu moyo wetu ujumbe wa Ezekieli. Tuonyeshe kila siku kupitia maneno na matendo yetu kwamba tunajua Yehova ni nani na maana ya jina lake. Tukifanya vile, hatutaogopa wakati pepo za uharibifu za taabu kubwa zitaachiliwa. Lakini, tutainua vichwa vyetu, juu tunajua kama ukombozi wetu unakaribia. (Lu. 21:28) Kwa sasa, tuendelee kusaidia watu fasi yote wamujue na kumupenda Mungu moja tu mwenye anastahili ibada, Mwenye iko na jina kubwa kupita majina yote, ni kusema, Yehova.​—Eze. 28:26.

^ fu. 5 Namba inaonyesha sura za mu kitabu hiki.