Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 17

“Nitapigana na Wewe, Ee Gogu”

“Nitapigana na Wewe, Ee Gogu”

EZEKIELI 38:3

WAZO KUBWA: Maana ya “Gogu” na “inchi” yenye atashambulia

1, 2. Ni vita gani kubwa yenye iko inakuja, na tunaweza kujiuliza maulizo gani kuhusu ile vita? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

MU MIAKA mingi, dunia hii imechafuliwa na damu za watu wenye wanakufa mu vita, bila kusahau damu mingi yenye ilimwangika wakati wa vita mbili za ulimwengu za mu karne ya 20 (1901-2000). Lakini vita kubwa zaidi ya historia ya wanadamu iko inakuja. Ile vita haitakuwa kati ya wanadamu na wanadamu, taifa na taifa, juu tu ya kutafuta faida za kichoyo. Tofauti na ile, vita yenye iko inakuja itakuwa “vita ya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu. 16:14) Adui fulani mwenye kujiona sana ataanzisha ile vita na atashambulia inchi ya samani sana ku macho ya Mungu; ile shambulizi itafanya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova amwange juu ya dunia uharibifu mukubwa, wenye hauyakuwaka.

2 Ile inatokeza maulizo fulani: Ule adui ni nani? Inchi yenye atashambulia, ni inchi gani? Atashambulia ile inchi wakati gani, juu ya nini, na namna gani? Ile matukio ya wakati wenye kuja inatuhusu sisi waabudu wa kweli wa Yehova hapa ku dunia, njo maana ni muzuri tupate majibu. Majibu iko mu unabii wenye kupendeza wenye unapatikana mu Ezekieli sura ya 38 na 39.

Ule Adui Ni Gogu wa Magogu

3. Fasiria kwa kifupi unabii wa Ezekieli kuhusu Gogu wa Magogu.

 3 Soma Ezekieli 38:1, 2, 8, 18; 39:4, 11. Kwa kifupi, ile unabii inasema hivi: “Katika kipindi cha mwisho cha miaka,” adui mwenye kuitwa “Gogu wa . . . Magogu” anashambulia “inchi” ya watu wa Mungu. Lakini shambulizi lake linafanya “kasirani kali” ya Yehova iwake, na Yehova anakamata ile mambo na anamushinda Gogu. * Kisha kupata ushindi, Yehova anatoa adui wake mwenye ameshindwa na wote wenye walikuwa naye “kuwa chakula cha kila namna ya ndege wenye kuwinda na wanyama wa pori.” Ku mwisho, Yehova anapatia Gogu “kaburi.” Juu tuelewe namna ile unabii itatimia mu wakati wenye unakaribia, tunapaswa kwanza kujua maana ya Gogu.

4. Tunaweza kusema kama Gogu wa Magogu ni nani?

4 Kwa hiyo basi, Gogu wa Magogu ni nani? Kufuatana na maelezo ya Ezekieli, tunaweza kusema kama Gogu ni adui wa waabudu wa kweli. Je, Gogu ni jina la kiunabii la Shetani, adui mukubwa zaidi kati ya maadui wote wa ibada ya kweli? Mu miaka mingi, vichapo vyetu vilikuwa vinasema vile. Lakini, kisha kuchunguza tena unabii wa Ezekieli, ilionekana wazi kama iliomba kubadilisha namna yetu ya kuelewa mambo. Munara wa Mulinzi ulifasiria kama jina Gogu wa Magogu halimaanishe kiumbe cha kiroho chenye hakionekane, lakini linamaanisha adui wa kibinadamu mwenye kuonekana, ni kusema, muungano wa mataifa yenye itashambulia ibada safi. * Mbele tuone sababu zenye zinatufanya tuseme vile, acha tuchunguze mawazo mbili mu unabii wa Ezekieli yenye inaonyesha kama Gogu haiko kiumbe cha kiroho.

5, 6. Ni mambo gani mu unabii wa Ezekieli yenye inaonyesha kama Gogu wa Magogu haiko kiumbe fulani cha kiroho?

5 “Nitakufanya kuwa chakula cha kila namna ya ndege wenye kuwinda.” (Eze. 39:4) Mara mingi, wakati Maandiko inasema kama ndege wenye kuwinda wanakula maiti za viumbe, ni juu ya kutoa onyo kuhusu hukumu ya Mungu. Mungu alipatia maonyo ya vile taifa la Israeli na pia mataifa ingine yenye haikukuwa ya Israeli. (Kum. 28:26; Yer. 7:33; Eze. 29:3, 5) Ukiangalia muzuri, utaona kwamba ile maonyo haikupewa viumbe vya kiroho, lakini ilipewa wanadamu wenye wako na nyama na damu. Na inapaswa kuwa vile, juu ndege wenye kuwinda na wanyama wa pori njo wanakulaka nyama, hawakulake viumbe vya kiroho. Kwa hiyo, onyo ya kimungu mu unabii wa Ezekieli inaonyesha kama Gogu haiko kiumbe cha kiroho.

6 “Nitamupatia Gogu kaburi . . . katika Israeli.” (Eze. 39:11) Hakuna fasi kwenye Maandiko inazungumuzia kiumbe cha kiroho chenye kinazikwa ku dunia. Lakini inasema kama, Shetani na mashetani wake watafungwa mu abiso miaka 1 000, na kisha watatupwa mu ziwa la moto la mufano, maana yake wataharibiwa milele. (Lu. 8:31; Ufu. 20:1-3, 10) Kwa kuwa Biblia inasema kama Gogu atapewa “kaburi” ku dunia, tunaweza kusema kama Gogu haiko kiumbe cha kiroho.

7, 8. Ni wakati gani “mufalme wa kaskazini” atafikia mwisho wake, na namna gani ile inafanana na mambo yenye itapata Gogu wa Magogu?

7 Sasa, kama haiko kiumbe cha kiroho, ule Gogu, adui mwenye ataleta shambulizi la mwisho juu ya waabudu wa kweli, ni nani? Fikiria maunabii mbili ya Biblia yenye inatusaidia tujue maana ya Gogu wa Magogu.

8 “Mufalme wa kaskazini.” (Soma Danieli 11:40-45.) Danieli alitabiri guvernema kubwa za dunia zenye zingetokea kuanzia wakati wake mupaka leo. Unabii wake unazungumuzia pia guvernema zenye hazisikilizane na zenye kushindana​—“mufalme wa kusini” na “mufalme wa kaskazini”—​kila mumoja wao amebadilika mu miaka mingi kadiri mataifa ya dunia imeendelea kupigania ukubwa. Kuhusu shambulizi la mwisho lenye mufalme wa kaskazini atafanya mu “wakati wa mwisho,” Danieli alisema: “Ataenda kwa kasirani kali ili kuharibu na kuangamiza watu wengi.” Waabudu wa Yehova njo shabaha ya kwanza ya mufalme wa kaskazini. * Lakini sawa vile Gogu wa Magogu, mufalme wa kaskazini atafikia “mwisho wake” kisha yeye kushindwa kushambulia watu wa Mungu.

9. Ni nini inafanana kati ya mambo yenye itapata Gogu wa Magogu na mambo yenye itapata “wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu”?

9 “Wafalme wa dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Soma Ufunuo 16:14, 16; 17:14; 19:19, 20.) Kitabu cha Ufunuo kilitabiri kama “wafalme wa dunia” watashambulia “Mufalme wa wafalme,” ni kusema, Yesu mwenye iko mbinguni. Lakini hawawezi kushambulia Yesu juu iko mbinguni, kwa hiyo watashambulia wateteaji wa Ufalme ku dunia. Kisha, wafalme wa dunia watashindwa ku vita ya Armagedoni. Ona kwamba watafikia mwisho kisha wao kushambulia watu wa Mungu. Ile inafanana na mambo yenye Biblia inasema kuhusu Gogu wa Magogu. *

10. Tunaweza kusema Gogu wa Magogu ni nani?

10 Kufuatana na yote yenye tumeona, tunaweza kusema Gogu ni nani? Kwanza, Gogu haiko kiumbe cha kiroho. Pili, Gogu anafananisha mataifa ya dunia yenye itashambulia watu wa Mungu sasa hivi. Bila shaka, ile mataifa itafanya muungano, ni kusema, itajiunga pamoja mu njia fulani. Juu ya nini? Kwa kuwa watu wa Mungu wanapatikana mu dunia yote, itaomba mataifa ijiunge pamoja juu iweze kuwashambulia. (Mt. 24:9) Lakini mutu asikudanganye, Shetani njo mwenye atapanga na kuongoza ile shambulizi. Mu miaka mingi, amechochea mataifa ya dunia ipinge ibada ya kweli. (1 Yo. 5:19; Ufu. 12:17) Lakini, maneno ya unabii wa Ezekieli kuhusu Gogu wa Magogu inakazia zaidi sana kile mataifa ya dunia itafanya juu ya kushambulia watu wa Yehova. *

“Inchi”​—Ni Inchi Gani?

11. Unabii wa Ezekieli unatoa maelezo gani kuhusu “inchi” yenye Gogu atashambulia?

11 Kama vile tulijifunza mu  fungu la 3, Gogu wa Magogu atalamusha kasirani kali ya Yehova wakati atashambulia inchi ya samani ku macho ya Yehova. Ni inchi gani? Acha turudie ku unabii wa Ezekieli. (Soma Ezekieli 38:8-12.) Unabii unasema kama Gogu ‘atashambulia inchi yenye watu wake wamerudishwa’ na wenye ‘wamekusanywa kutoka katika mataifa.’ Ona pia mambo yenye ile unabii inasema kuhusu waabudu wenye wamerudishwa mu hali ya muzuri wenye wanaishi mu ile inchi: ‘Wanakaa kwa usalama’; makao yao “hayalindwe na kuta, mapingo, wala milango mikubwa”; na “wanajikusanyia utajiri.” Ni mu ile inchi njo waabudu wa kweli wa Yehova wanaishi. Ni nini inatusaidia kuijua?

12. Namna gani inchi ya Israeli ilirudishwa mu hali ya muzuri mu wakati wa zamani?

12 Ni muzuri tuchunguze kurudishwa kwa inchi ya Israeli ya zamani, kwenye watu wa Mungu waliishi, walitumikia, na kuabudu mu miaka mingi. Wakati Waisraeli hawakukuwa waaminifu, Yehova aliongoza Ezekieli atabiri kama inchi yao ingeharibiwa na kuachwa ukiwa. (Eze. 33:27-29) Lakini Yehova alitabiri kama siku moja mabaki wenye kutubu wangerudia kutoka mu uhamisho wa Babiloni na wangerudisha ibada safi mu inchi yao. Kwa sababu ya baraka yenye Yehova angeleta, inchi ya Israeli ingebadilika, ingekuwa mu hali ya muzuri “kama bustani ya Edeni.” (Eze. 36:34-36) Ile ilitokea kuanzia mwaka wa 537 M.K.Y. wakati wahamishwa Wayahudi walirudia Yerusalemu juu ya kurudisha ibada ya kweli mu inchi yao yenye walikuwa wanapenda sana.

13, 14. (a) Inchi ya kiroho ni nini? (b) Juu ya nini Yehova anaiona kuwa ya samani?

13 Leo, waabudu wa kweli wa Mungu wamerudishwa pia mu hali ya muzuri. Kama vile tulijifunza mu Sura ya 9 ya kitabu hiki, kufikia mwaka wa 1919, watu wa Mungu walikombolewa kutoka mu utekwa wa siku mingi mu Babiloni Mukubwa. Ile mwaka, Yehova alirudisha waabudu wake mu hali ya muzuri na kuwaingiza mu inchi ya kiroho. Ile inchi njo paradiso ya kiroho​—fasi ya usalama, kwenye kuko hali ya muzuri ya kiroho, ao fasi ya kufanyia mambo ya kiroho, kwenye tunaabudu Mungu wa kweli. Mu ile inchi, tunaishi pamoja kwa usalama, na tuko na amani ya akili na ya moyo. (Mez. 1:33) Tunapokea chakula mingi ya kiroho, na tuko na mambo mingi ya kufanya mu kazi ya kufurahisha ya kutangaza Ufalme wa Mungu. Kusema kweli, tuko tunajionea ukweli wa mezali hii: “Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri, Naye haongeze maumivu yoyote pamoja nayo.” (Mez. 10:22) Ikuwe tunaishi wapi mu dunia hii, tuko mu ile inchi​—paradiso ya kiroho—​wakati tunaendelea kutegemeza kwa bidii ibada safi kwa maneno na matendo.

14 Ile inchi ya kiroho iko ya samani sana ku macho ya Yehova. Juu ya nini? Yehova anaona wakaaji wa ile inchi kuwa “vitu vyenye samani vya mataifa yote,” watu wenye amevuta mu ibada safi. (Hag. 2:7; Yoh. 6:44) Wanajikaza kuvaa utu mupya, wenye unaonyesha sifa za hali ya juu za Mungu. (Efe. 4:23, 24; 5:1, 2) Kwa sababu wao ni waabudu wa kweli, wanajitoa kabisa mu kazi yake, wanafanya vile mu njia yenye inamuletea utukufu na yenye inaonyesha kama wanamupenda. (Ro. 12:1, 2; 1 Yo. 5:3) Tunaweza kuwazia furaha yenye Yehova anasikia mu moyo wake wakati anaona namna waabudu wake wanajikaza sana juu ya kufanya ile inchi ya kiroho ipendeze. Waza kidogo: Wakati unatia ibada safi pa nafasi ya kwanza mu maisha yako, unafanya paradiso ya kiroho ipendeze lakini pia unafurahisha moyo wa Yehova!​—Mez. 27:11.

Ikuwe tunaishi wapi, tuko mu inchi ya kiroho wakati tunaendelea kutegemeza kwa bidii ibada safi (Ona fungu la 13, 14)

Gogu Atashambulia Ile Inchi​—Wakati Gani, Juu ya Nini, na Namna Gani?

15, 16. Ni wakati gani Gogu wa Magogu atashambulia inchi yetu ya kiroho yenye imerudishwa mu hali ya muzuri?

15 Kujua kama muungano wa mataifa ya dunia utashambulia inchi yetu ya kiroho yenye samani, kunafanya tufikiri kwa uzito. Kwa sababu sisi waabudu wa kweli wa Yehova njo tutashambuliwa, ni muzuri tujue mambo mingi kuhusu ile shambulizi. Fikiria maulizo tatu yenye inatokea.

16 Ni wakati gani Gogu wa Magogu atashambulia inchi yetu ya kiroho yenye imerudishwa mu hali ya muzuri? Unabii unajibu: “Katika kipindi cha mwisho cha miaka utashambulia inchi.” (Eze. 38:8) Ile ni wakati wenye uko karibu na mwisho wa mupangilio huu wa mambo. Kumbuka kama taabu kubwa itaanza na kuharibiwa kwa Babiloni Mukubwa, ni kusema, dini zote za uongo. Kisha matengenezo ya dini ya uongo kuharibiwa na mbele Armagedoni ianze, Gogu ataanzisha shambulizi la mwisho kabisa juu ya waabudu wa kweli.

17, 18. Namna gani Yehova ataongoza mambo wakati wa taabu kubwa?

17 Juu ya nini Gogu atashambulia inchi ya waabudu wa kweli wa Yehova yenye imerudishwa mu hali ya muzuri? Unabii wa Ezekieli unafunua sababu mbili​—kwanza, namna Yehova ataongoza mambo, na pili, nia mubaya ya Gogu.

18 Namna Yehova ataongoza mambo. (Soma Ezekieli 38:4, 16.) Ona mambo yenye Yehova anaambia Gogu: ‘Nitatia . . . kulabu katika mataya yako’ na, “nitakuleta ushambulie inchi yangu.” Je, ile inaonyesha kama Yehova atakaza mataifa ishambulie waabudu wake? Hapana kabisa! Hawezi kuletea watu wake jambo la mubaya. (Yob. 34:12) Lakini Yehova anajua muzuri maadui wake​—anajua kama watachukia waabudu wa kweli na kama hawatapitisha nafasi yenye inajitokeza ya kuwaharibu. (1 Yo. 3:13) Yehova ataongoza mambo juu ile matukio itokee kulingana na mapenzi Yake na kwa wakati Wake, kufanya vile ni sawa na kutia kulabu (crochets) mu mataya ya Gogu na kuanza kumuongoza. Wakati fulani kisha Babiloni Mukubwa kuharibiwa, Yehova anaweza mu njia fulani kuchochea mataifa itimize mambo yenye iko tayari mu moyo wao. Kwa kufanya vile, Yehova atakuwa ameongoza mambo juu shambulizi la mwisho lenye litapeleka ku Armagedoni litokee. Armagedoni njo itakuwa vita kubwa zaidi kuliko vita zote zenye zimekwisha kufanyika ku dunia. Kisha, atakomboa watu wake, atatukuza mamlaka yake makubwa zaidi, na kutakasa jina lake takatifu.​—Eze. 38:23.

Mataifa itatafuta kunyanganya ibada safi juu inaichukia na wale wote wenye wanaiendelesha

19. Ni nini itamufanya Gogu ajaribu kunyanganya ibada safi?

19 Nia mubaya ya Gogu. Mataifa ‘itapanga mupango wa uovu.’ Itatafuta kuonyesha kasirani kali ya siku mingi na chuki yenye wako nayo juu ya waabudu wa Yehova, wenye wataonekana kuwa zaifu, sawa vile watu “wenye kukaa katika makao yenye hayalindwe na kuta, mapingo, wala milango mikubwa.” Mataifa itapenda pia “kukamata vitu vingi vyenye vinachukuliwa katika vita na vitu vingi vyenye vinanyanganywa katika vita” kutoka kwa wale wenye “wanajikusanyia utajiri.” (Eze. 38:10-12) “Utajiri” gani? Watu wa Yehova wako na utajiri mukubwa wa kiroho; mali ya samani yenye tuko nayo ni ibada yetu safi, yenye tunamutolea Yehova peke yake. Mataifa itatafuta kunyanganya ibada safi, hapana juu inaiona kuwa ya samani, lakini juu inaichukia na wale wote wenye wanaiendelesha.

Gogu ‘atapanga mupango wa uovu’ juu ya kutafuta kumaliza ibada safi (Ona fungu la 19)

20. Namna gani Gogu atashambulia inchi ya kiroho, ao paradiso ya kiroho?

20 Namna gani Gogu atashambulia inchi ya kiroho, ao paradiso ya kiroho? Pengine mataifa itajaribu kuvuruga maisha yetu na kutuzuia tusifanye ibada yetu. Juu wafikie kufanya vile, pengine watajaribu kuzuia tusiendelee kupata chakula cha kiroho, kutuzuia tusikusanyike pamoja, kuvunja umoja wetu, kutuzuia tusitangaze kwa bidii ujumbe wa Mungu. Ile mambo yote njo inafanyiza paradiso ya kiroho. Kwa sababu ya kuchochewa na Shetani, mataifa itajaribu kumaliza waabudu wote wa kweli​—na pia ibada safi—​ili wasikuwe tena ku dunia.

21. Juu ya nini unafurahi sana kwa kuwa Yehova ametuonya kuhusu mambo yenye iko mbele?

21 Shambulizi lenye kuja la Gogu wa Magogu litagusa waabudu wote wa kweli wenye kupatikana mu inchi ya kiroho yenye Mungu amewapatia. Tunafurahi sana sababu Yehova ametuonya kuhusu mambo yenye iko mbele! Sasa, kadiri tunangojea taabu kubwa ifike, tuazimie kushikamana na ibada safi, kuipatia nafasi ya kwanza mu maisha yetu. Kwa kufanya vile, tutasaidia kufanya inchi yenye imerudishwa ipendeze sasa. Na tutakuwa kati ya watu wenye watajionea sasa hivi jambo fulani la ajabu kabisa: Namna Yehova atasimama juu ya kupigania watu wake na jina lake takatifu ku Armagedoni, sawa vile sura ya kufuata itaonyesha.

^ fu. 3 Mu sura ya kufuata ya kitabu hiki, tutazungumuzia namna gani na wakati gani kasirani kubwa ya Yehova itawaka juu ya Gogu wa Magogu na matokeo yake juu ya waabudu wa kweli.

^ fu. 8 Danieli 11:45 inaonyesha kama mufalme wa kaskazini atashambulia watu wa Mungu, juu inasema kama ule mufalme “atasimamisha mahema yake ya kifalme kati ya bahari kubwa [Mediterania] na mulima mutakatifu wa lile Pambo [kwenye hekalu la Mungu lilikuwaka zamani na kwenye watu wa Mungu walikuwa wanaabudu].”

^ fu. 9 Biblia inazungumuzia pia shambulizi lenye litafanywa na “Mwashuru” wa leo, mwenye atatafuta kumaliza kabisa watu wa Mungu. (Mik. 5:5) Mashambulizi ine yenye ilitabiriwa kama itakuja juu ya watu wa Mungu​—shambulizi la Gogu wa Magogu, shambulizi la mufalme wa kaskazini, shambulizi la wafalme wa dunia, na shambulizi la Mwashuru—​yote inaweza kumaanisha sehemu mbalimbali za shambulizi lilelile lenye linapewa majina tofauti-tofauti.

^ fu. 10 Juu ya kupata mafasirio kuhusu maana ya “Gogu wa Magogu” mwenye anatajwa mu Ufunuo 20:7-9, ona Sura ya 22 ya kitabu hiki.