Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 8

“Nitainua Muchungaji Mumoja”

“Nitainua Muchungaji Mumoja”

EZEKIELI 34:23

WAZO KUBWA: Maunabii ine juu ya Masiya na namna ilitimia katika Kristo

1-3. Juu ya nini Ezekieli iko na huzuni sana, na roho ya Mungu inamuongoza aandike nini?

NI MWAKA wa sita tangu Ezekieli aende mu uhamisho. * Iko na huzuni sana kwa sababu Yuda, inchi yao yenye anapenda sana, inatawaliwa mubaya. Ameona wafalme wengi wenye walitawala.

2 Ezekieli alizaliwa katikati ya kipindi cha utawala wa mufalme muaminifu Yosia. Ezekieli alipaswa kufurahi sana wakati alisikia kama Yosia alikuwa anaharibu sanamu zote na kurudisha ibada safi mu Yuda. (2 Ny. 34:1-8) Lakini mambo yenye Yosia alifanya haikuleta mabadiliko ya kuendelea, sababu wafalme wengi wenye walitawala kisha yeye waliendelea kuabudu sanamu. Haishangaze kwamba, wakati wale wafalme wabaya walikuwa wanatawala, taifa lilizama mu matope ya upotovu wa kiroho na wa mwenendo. Je, hakukuwa tena tumaini? Hapana kabisa!

3 Kupitia roho yake, Yehova aliongoza nabii wake muaminifu aandike unabii moja​—wa kwanza kati ya maunabii mingi—​kuhusu Masiya, Mutawala mwenye angekuja na Muchungaji mwenye angerudisha mu njia ya kudumu ibada safi na kuhangaikia kwa upendo kondoo wa Yehova. Ni muzuri tuchunguze ile maunabii kwa uangalifu, kwa sababu kutimizwa kwa ile maunabii kuko na matokeo juu ya wakati wetu wa milele wenye kuja. Acha basi tuchunguze maunabii ine juu ya Masiya, yenye kuwa mu kitabu cha Ezekieli.

“Chipukizi la Teketeke” Linakuwa “Mwerezi Mukubwa”

4. Unabii wa Ezekieli ulionyesha nini, na Yehova aliutoa mu njia gani?

4 Mu mwaka wa 612 hivi M.K.Y., “neno la Yehova” lilikuja kwa Ezekieli, na alieleza unabii moja wenye kuonyesha ukubwa wa utawala wa Masiya na ulazima wa kutumainia Ufalme wake. Yehova alitoa ile unabii kwa kumuongoza Ezekieli aambie wahamishwa wenzake kitendawili cha unabii chenye kilionyesha namna watawala wa Yuda hawakukuwa waaminifu na chenye kilikazia ulazima wa kuwa na Masiya-Mutawala mwenye haki.​—Eze. 17:1, 2.

5. Kwa kifupi, ile kitendawili inasema nini?

5 Soma Ezekieli 17:3-10. Kwa kifupi, ile kitendawili inasema hivi: “Tai mukubwa” anaongoa chipukizi la juu sana la muti wa mwerezi na kulitia “katika muji wa wafanyabiashara.” Kisha ule tai anakamata “mbegu fulani ya inchi” na kuipanda mu shamba lenye mbolea “pembeni ya maji mengi.” Mbegu inaota na kuwa “muzabibu wenye kutambaa.” Kisha, “tai mukubwa” wa pili anatokea. Mizizi ya ule muzabibu inajinyoosha “kwa bidii kumuelekea” ule tai wa pili, inatafuta ule tai aipeleke na kuipanda fasi yenye kumwangiliwa maji muzuri. Yehova anahukumu matendo ya ule muzabibu, anaonyesha kama mizizi yake itaongolewa na ‘itakauka kabisa.’

Tai mukubwa wa kwanza alifananisha Mufalme Nebukadneza wa Babiloni (Ona fungu la 6)

6. Fasiria maana ya ile kitendawili.

6 Ile kitendawili iko na maana gani? (Soma Ezekieli 17:11-15.) Mu mwaka wa 617 M.K.Y., Mufalme Nebukadneza wa Babiloni (“tai mukubwa” wa kwanza) alizunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita. Aliongoa ao kuondoa Mufalme wa Yuda Yehoyakimu (“chipukizi la juu sana”) ku kiti cha ufalme na kumupeleka Babiloni (“muji wa wafanyabiashara”). Nebukadneza alitia Sedekia (mumoja wa “mbegu [ya kifalme] ya inchi”) ku kiti cha ufalme kule Yerusalemu. Huyu mufalme mupya wa Yuda alikuwa ameapishwa katika jina la Mungu, na ile ilimulazimisha akuwe mufalme mudogo, mwenye alikuwa anafuata tu kile Nebukadneza anasema. (2 Ny. 36:13) Lakini Sedekia hakuheshimia kiapo chake; aliasi Babiloni na kuenda kutafuta musaada wa kijeshi kwa Farao, mufalme wa Misri (“tai mukubwa” wa pili), lakini hakupata matokeo ya muzuri. Yehova alilaumu matendo ya kukosa ushikamanifu ya ule muvunja-kiapo, ni kusema, Sedekia. (Eze. 17:16-21) Kwa mwisho, Sedekia alitoshwa ku kiti cha ufalme, na akakufia mu kifungo kule Babiloni.​—Yer. 52:6-11.

7. Ile kitendawili ya unabii inatufundisha nini?

7 Ile kitendawili ya unabii inatufundisha nini? Kwanza, kwa kuwa tuko waabudu wa ibada safi tunapaswa kutimiza mambo yenye tunasema. Yesu alisema, “Muache tu neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana.” (Mt. 5:37) Tukiwaza kama ni lazima tufanye kiapo mbele ya Mungu kwamba tutasema kweli​—kwa mufano wakati watatuomba tutoe ushuhuda ku tribinali—​tunapaswa kuona ile kiapo kuwa jambo nzito sana. Pili, hatupaswe kutumainia kila mutu. Biblia inatupatia angalisho hii: “Musitumainie wakubwa wala mwana wa binadamu, mwenye hawezi kuleta wokovu.”​—Zb. 146:3.

8-10. Yehova anatoa maelezo gani juu ya Masiya-Mutawala mwenye kuja, na namna gani ile unabii inatimia? (Ona kisanduku “Unabii Juu ya Masiya​—Muti Mukubwa wa Mwerezi.”)

8 Lakini, kuko mutawala moja mwenye tunapaswa kabisa kutumainia. Kisha kutoa ile kitendawili kuhusu chipukizi lenye lilienda kupandwa fasi ingine, Yehova anatumia maneno ileile ya mufano juu ya kutoa maelezo fulani kuhusu Masiya-Mufalme mwenye kuja.

9 Mambo yenye ile unabii inasema. (Soma Ezekieli 17:22-24.) Mara hii haiko wale tai wakubwa lakini Yehova mwenyewe njo atatenda. Ataongoa chipukizi la teketeke “kutoka sehemu ya juu ya mwerezi murefu sana na kulipanda, . . . juu ya mulima murefu na wenye kuwa juu sana.” Ile chipukizi itakomaa na kuwa “mwerezi mukubwa” wenye kutolea makao “ndege wa kila namna.” Kisha “miti yote ya shamba” itajua kwamba Yehova mwenyewe njo alifanya ile muti murefu sana ikomae.

10 Namna ile unabii imetimia. Yehova aliongoa ao kuondoa Mwana wake, Yesu Kristo, kutoka mu kizazi cha Daudi (“mwerezi murefu sana”) na kumupanda juu ya Mulima Sayuni wenye kuwa mbinguni (“mulima murefu na wenye kuwa juu sana”). (Zb. 2:6; Yer. 23:5; Ufu. 14:1) Mu ile njia, Yehova alikamata Mwana wake, mwenye maadui wake walimuona kuwa “mwanadamu wa hali ya chini zaidi,” na akamutukuza kwa kumupatia “kiti cha ufalme cha Daudi baba yake.” (Da. 4:17; Lu. 1:32, 33) Sawa vile mwerezi murefu sana, Yesu Kristo, Masiya-Mufalme, atakuwa juu ya dunia yote na atakuwa chemchemi ya baraka kwa raia wake wote. Kusema kweli, huyu njo Mutawala mwenye tunapaswa kutumainia. Chini ya kivuli cha Ufalme wa Yesu, wanadamu watiifu mu dunia yote ‘wataishi kwa usalama na hawatasumbuliwa na woga wa musiba.’​—Mez. 1:33.

11. Ile unabii juu ya “chipukizi la teketeke” lenye linakuwa “mwerezi mukubwa” inatupatia somo gani ya maana?

11 Somo yenye tunapata mu ile unabii. Unabii wenye kufurahisha sana juu ya “chipukizi la teketeke” lenye linakuwa “mwerezi murefu” unatusaidia kupata jibu la hii ulizo ya maana sana: Tutatumainia nani? Ni kukosa akili kutumainia guvernema za wanadamu na nguvu ya majeshi yao. Kama tunapenda kupata usalama wa kweli, ni jambo la hekima kutumainia kabisa Masiya-Mufalme, ni kusema, Yesu Kristo. Guvernema ya mbinguni yenye iko mu mikono yenye uwezo mukubwa ya Yesu njo tumaini moja tu la wanadamu.​—Ufu. 11:15.

“Ule Mwenye Kuwa na Haki ya Kisheria”

12. Namna gani Yehova alionyesha waziwazi kama hajasahau mapatano yenye alifanyaka na Daudi?

12 Mafasirio yenye Mungu alipatia Ezekieli kuhusu wale tai wawili, ilimusaidia kuelewa kama Sedekia, mufalme mwenye hakukuwa muaminifu na mwenye alikuwa wa kizazi cha kifalme cha Daudi, alipaswa kuondolewa ku kiti cha ufalme na kupelekwa mu utekwa Babiloni. Pengine nabii alijiuliza, ‘Sasa itakuwa je juu ya mapatano yenye Mungu alifanyaka na Daudi, yenye ilionyesha kama kungekuwa mufalme moja wa kizazi cha Daudi mwenye angetawala milele?’ (2 Sa. 7:12, 16) Kama Ezekieli alijiuliza ile ulizo, hakupaswa kuchunga siku mingi juu ya kupata jibu. Mwaka wa 611 hivi M.K.Y., mu mwaka wa saba wa uhamisho, wakati Sedekia alikuwa angali anatawala Yuda, “neno la Yehova likakuja” kwa Ezekieli. (Eze. 20:2) Yehova alimuambia atoe unabii ingine juu ya Masiya, wenye kufasiria waziwazi kama Mungu hajasahau mapatano yenye alifanyaka na Daudi. Lakini, ile unabii ilionyesha kama Masiya-Mutawala mwenye angekuja angekuwa na haki ya kisheria ya kutawala kama muriti wa Daudi.

13, 14. Kwa kifupi, ile unabii yenye kuwa mu Ezekieli 21:25-27 inazungumuzia nini, na namna gani ilitimia?

13 Mambo yenye ile unabii inasema. (Soma Ezekieli 21:25-27.) Kupitia Ezekieli, Yehova anazungumuza waziwazi na “mukubwa muovu wa Israeli,” mwenye wakati wake wa kupewa azabu ulikuwa umefika. Yehova anaambia ule mukubwa muovu kwamba “kilemba” na “taji,” (alama za mamlaka ya kifalme) vitaondolewa kwake. Kisha, mamlaka zenye kutawala zenye zimekuwa “chini” zitainuliwa, na zile zenye zimekuwa “juu” zitashushwa chini. Mamlaka zenye kutawala zitaendelea kutawala, lakini mupaka tu wakati “ule mwenye kuwa na haki ya kisheria atakuja,” na kisha, Yehova atamupatia Ufalme.

14 Namna ile unabii imetimia. Mu mwaka wa 607 M.K.Y., wakati Yerusalemu iliharibiwa, ufalme wa “juu” wa Yuda wenye ulikuwa mu Yerusalemu ulishushwa chini wakati Wababiloni waliharibu ile muji na kuondoa Mufalme Sedekia ku kiti cha ufalme na kumupeleka mu utekwa. Kisha, kwa sababu hakukuwa tena mufalme wa kizazi cha kifalme cha Daudi mwenye kutawala Yerusalemu, mamlaka za mataifa zenye zilikuwa “chini” ziliinuliwa juu na kuanza kutawala dunia​—lakini zilitawala mu wakati kidogo tu. Nyakati za Mataifa, ao “nyakati zenye ziliwekwa za mataifa,” zilimalizika mu mwaka wa 1914 wakati Yehova alipatia Yesu Kristo ufalme. (Lu. 21:24) Kwa sababu alitoka mu kizazi cha Mufalme Daudi, Yesu alikuwa kabisa na “haki ya kisheria” ya kuwa mufalme wa Ufalme wa Kimasiya. * (Mwa. 49:10) Kwa hiyo, katika Yesu, Yehova alitimiza ahadi yake ya kupatia Daudi mutu mwenye angeriti Ufalme milele.​—Lu. 1:32, 33.

Yesu iko na haki ya kisheria ya kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu (Ona fungu la 15)

15. Juu ya nini tunapaswa kutumainia kabisa Mufalme, Yesu Kristo?

15 Somo yenye tunapata mu ile unabii. Tunapaswa kutumainia kabisa Mufalme, Yesu Kristo. Juu ya nini? Juu, tofauti na watawala wa dunia wenye wanaweza kuchaguliwa na watu ao kukamata mamlaka kwa nguvu, Yesu yeye alichaguliwa na Yehova na ‘amepewa . . . Ufalme’ wenye iko na haki ya kisheria ya kuongoza. (Da. 7:13, 14) Kwa kweli, Mufalme mwenye Yehova amechagua njo anastahili kutumainiwa!

“Mutumishi Wangu Daudi” Atakuwa “Muchungaji Wao”

16. Namna gani Yehova anatendea kondoo wake, na namna gani “wachungaji wa Israeli” wa siku za Ezekieli walikuwa wanatendea kundi?

16 Yehova, Muchungaji Mukubwa Zaidi, anahangaikia sana hali ya kondoo wake, ni kusema, watumishi wake wenye kuwa mu dunia. (Zb. 100:3) Hata kama anapatia wachungaji wadogo​—wale wenye kuongoza—​daraka la kuchunga kondoo wake, yeye anaangalia sana namna wanatendea kondoo wake. Waza kidogo namna Yehova alijisikia kuhusu “wachungaji wa Israeli” wa siku za Ezekieli. Bila haya, wale viongozi walitawala “kwa ukali na uonevu.” Matokeo? Kundi liliteseka, na ile ilifanya wengi waache ibada safi.​—Eze. 34:1-6.

17. Namna gani Yehova alikomboa kondoo wake?

17 Yehova alifanya nini? Aliambia hivi wale viongozi wabaya: ‘Nitawaomba mutoe hesabu.’ Kisha alitoa ahadi hii: “Nitakomboa kondoo wangu.” (Eze. 34:10) Yehova anatimizaka mambo yenye anasema. (Yos. 21:45) Mu mwaka wa 607 M.K.Y., alikomboa kondoo wake kwa kutumia Wababiloni wenye walivamia Yerusalemu kusudi watoshe wale wachungaji wachoyo ku utawala. Kisha miaka makumi saba, alikomboa waabudu wake wenye kuwa kama kondoo kutoka Babiloni na kuwarudisha mu inchi yao juu warudishe ibada safi. Lakini kondoo wa Yehova waliendelea kuwa mu hatari, sababu wangeendelea kutawaliwa na guvernema za dunia. “Nyakati zenye ziliwekwa za mataifa” zilipaswa kuendelea kwa miaka ingine mingi.​—Lu. 21:24.

18, 19. Ezekieli alizungumuzia unabii gani mu mwaka wa 606 M.K.Y.? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

18 Mu mwaka wa 606 M.K.Y., mwaka moja hivi kisha kuharibiwa kwa Yerusalemu na miaka mingi mbele Waisraeli wakombolewe mu uhamisho kule Babiloni, Yehova aliongoza Ezekieli kupitia roho yake juu atoe unabii moja wenye kuonyesha namna Muchungaji Mukubwa Zaidi anahangaikia sana kondoo wake na anapenda waishi salama milele. Ile unabii inaonyesha namna Masiya-Mutawala atahangaikia kondoo wa Yehova.

19 Mambo yenye ile unabii inasema. (Soma Ezekieli 34:22-24.) Mungu ‘atainua muchungaji mumoja,’ na anamuita “mutumishi wangu Daudi.” Maneno “muchungaji mumoja” yenye inatumiwa na neno “mutumishi” inaonyesha kama ule Mutawala hatasimamisha tena kizazi cha wafalme wenye kutokana na Daudi, lakini yeye njo atakuwa muriti wa kudumu wa Daudi. Ule Muchungaji-Mutawala atakulisha kondoo wa Mungu na atakuwa “mukubwa kati yao.” Yehova ‘atafanya agano la amani’ na kondoo wake. “Baraka zitamwangika [juu yao] kama mvua,” na watafurahia usalama wa kweli-kweli, na watapata matokeo ya muzuri mu mambo yote yenye watafanya. Tena, kutakuwa amani kati ya wanadamu lakini pia kati ya wanadamu na wanyama!​—Eze. 34:25-28.

20, 21. (a) Ile unabii juu ya “mutumishi wangu Daudi” ilitimia namna gani? (b) Maneno ya Ezekieli juu ya “agano la amani” inaonyesha nini juu ya wakati wenye kuja?

20 Namna ile unabii imetimia. Kwa kuita huyu Mutawala “mutumishi wangu Daudi,” Mungu alikuwa anazungumuzia Yesu mu njia ya unabii, mwenye alitoka mu kizazi cha Daudi na mwenye iko na haki ya kisheria ya kutawala. (Zb. 89:35, 36) Wakati alikuwa mu dunia, Yesu alionyesha waziwazi kama alikuwa “muchungaji mwema,” kwa kutoa uzima wake “kwa ajili ya kondoo.” (Yoh. 10:14, 15) Lakini sasa yeye ni Muchungaji mbinguni. (Ebr. 13:20) Mu mwaka wa 1914, Mungu aliweka Yesu kuwa Mufalme na alimupatia daraka la kuchunga na kukulisha kondoo wa Mungu wenye kuwa mu dunia. Miaka kidogo tu kisha pale, mu mwaka wa 1919, ule Mufalme mupya aliweka “mutumwa muaminifu na mwenye busara” kusudi akulishe “watumishi wa nyumbani,” ni kusema, waabudu waaminifu wa Mungu wenye kuwa na tumaini la kuishi mbinguni ao duniani. (Mt. 24:45-47) Akiwa chini ya muongozo wa Kristo, ule mutumwa muaminifu amekulisha muzuri kondoo wa Mungu chakula cha kiroho. Ile chakula ya kiroho imewasaidia kuendelesha amani na usalama mu paradiso ya kiroho yenye inaendelea kupanuka.

21 Maneno ya Ezekieli juu ya “agano la amani” na mvua ya baraka inaonyesha nini juu ya wakati wenye kuja? Mu dunia mupya yenye kuja, waabudu wa Yehova watanyeshewa kwa ukamili mvua ya baraka ya ile “agano la amani.” Dunia yote itakuwa paradiso, na mambo sawa vile vita, kutendewa mubaya, njaa, magonjwa, ao wanyama wa pori haitahangaisha tena wanadamu waaminifu. (Isa. 11:6-9; 35:5, 6; 65:21-23) Je, moyo wako haufurahi wakati unafikiria maisha ya milele mu dunia paradiso kwenye kondoo wa Mungu “wataishi kwa usalama, bila mutu wa kuwaogopesha”?​—Eze. 34:28.

Akiwa Muchungaji mbinguni, Yesu anaona namna kondoo wa Mungu wanatendewa (Ona fungu la 22)

22. Namna gani Yesu anatendea kondoo wake, na namna gani wachungaji wadogo wanaiga mufano wake?

22 Somo yenye tunapata mu ile unabii. Sawa vile Baba yake, Yesu anahangaikia sana hali ya kondoo. Huyu Muchungaji-Mufalme anahakikisha kama kondoo wa Baba yake wanakulishwa muzuri kiroho na wanaishi kwa amani na usalama mu paradiso ya kiroho. Kuwa chini ya ulinzi wa Mutawala sawa ule, kunatutuliza sana! Wachungaji wadogo wanapaswa kuiga mufano wa Yesu mu namna wanahangaikia kondoo. Wazee wanapaswa kuchunga kundi “kwa kupenda” na “kwa hamu” na kuwa mifano ya muzuri yenye kondoo wanaweza kuiga. (1 Pe. 5:2, 3) Muzee hapaswe hata kidogo kutendea mubaya kondoo wa Yehova! Usisahau maneno yenye Yehova aliambia wale wachungaji wabaya wa Israeli wa siku za Ezekieli: ‘Nitawaomba mutoe hesabu.’ (Eze. 34:10) Macho ya Muchungaji Mukubwa Zaidi iko juu ya kondoo wake na inaona namna wanatendewa​—na Mwana wake pia anaona vile wanatendewa.

“Mutumishi Wangu Daudi Atakuwa Mukubwa Wao Milele”

23. Ni unabii gani Yehova alitoa kuhusu kuunganishwa tena kwa taifa la Israeli, na namna gani alitimiza ile unabii?

23 Yehova anapenda waabudu wake watumike pamoja mu umoja. Mu unabii moja kuhusu kuunganishwa tena kwa taifa, Mungu aliahidi kwamba angekusanya watu wake​—wawakilishi wa ufalme wa makabila mbili ya Yuda na wale wa ufalme wa makabila kumi ya Israeli—​na kuwaunganisha tena kuwa “taifa moja,” sawa vile kukamata “vipande vya muti” na kuviunganisha juu vikuwe “kipande [kimoja] cha muti” mu mukono wake. (Eze. 37:15-23) Sehemu ya kwanza ya ile unabii ilitimia wakati Mungu alirudisha na kuunganisha tena taifa la Israeli mu Inchi ya Ahadi mu mwaka wa 537 M.K.Y. * Lakini ule umoja ulikuwa tu mufano kidogo wa umoja mukubwa na wa kudumu wenye ungekuja. Kisha kuahidi kwamba angeunganisha tena Israeli, Yehova alipatia Ezekieli unabii kuhusu namna ule Mutawala mwenye angekuja angekusanya waabudu wa kweli pamoja mu dunia yote mu kifungo cha upendo cha milele.

24. Yehova anamuita je ule Masiya-Mutawala, na utawala wake utakuwa wa je?

24 Mambo yenye ile unabii inasema. (Soma Ezekieli 37:24-28.) Mara ingine tena Yehova anatumia maneno “mutumishi wangu Daudi,” “muchungaji mumoja,” na “mukubwa” juu ya kutaja Masiya-Mutawala. Lakini mara hii anatumia neno “mufalme” juu ya kutaja ule Mwenye Aliahidiwa. (Eze. 37:22) Utawala wa huyu Mufalme utakuwa wa je? Utawala wake utadumu. Kutumiwa kwa neno “milele” kunaonyesha kama baraka za utawala wa ule Mufalme hazitakuwaka na mwisho. * Kutakuwa umoja wakati wa utawala wake. Chini ya utawala wa “mufalme [wao] mumoja,” raia washikamanifu watafuata “maamuzi ya hukumu” ileile na “wataishi katika inchi” pamoja. Utawala wake utafanya raia wa Mufalme wamukaribie sana Yehova Mungu. Yehova atafanya “agano la amani” pamoja na wale raia. Yehova atakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wake. Na patakatifu pake patakuwa “katikati yao milele.”

25. Namna gani ile unabii juu ya Masiya-Mufalme imetimia?

25 Namna ile unabii imetimia. Mu mwaka wa 1919, watiwa-mafuta waaminifu waliunganishwa pamoja chini ya “muchungaji [wao] mumoja,” Masiya-Mufalme, Yesu Kristo. Kisha, “kundi kubwa la watu” wenye kutoka mu “mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga” lilifikia kuungana na waamini wenzao watiwa-mafuta. (Ufu. 7:9) Wote pamoja, wamekuwa “kundi moja” chini ya “muchungaji mumoja.” (Yoh. 10:16) Ikuwe tumaini lao ni kuishi mbinguni ao duniani, wote pamoja wanatii maamuzi ya hukumu ya Yehova. Matokeo ni kwamba, wanakaa pamoja mu paradiso ya kiroho wakiwa familia ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada wenye umoja. Yehova amewabariki kwa kuwapatia amani, na patakatifu pake, penye kufananisha ibada safi, pako katikati yao. Yehova ni Mungu wao, nao wanajivunia kuwa waabudu wake​—leo na milele!

26. Namna gani unaweza kuendelesha umoja wa paradiso ya kiroho?

26 Somo yenye tunapata mu ile unabii. Tuko na pendeleo la kuwa mu umoja katika familia ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada wenye kujitoa kwa ajili ya ibada safi ya Yehova. Lakini ile pendeleo inatupatia daraka fulani​—tunapaswa kuendelesha ile umoja. Kwa hiyo, sisi wote tunapaswa kufanya sehemu yetu juu ya kulinda umoja katika imani na matendo. (1 Ko. 1:10) Kusudi tufanye vile, tunapaswa kula kwa hamu chakula kilekile cha kiroho, kushika kanuni zilezile za Maandiko kuhusu mwenendo, na kufanya kazi ya maana sana ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. Lakini, siri ya umoja wetu ni upendo. Kadiri tunajikaza kukomalisha na kuonyesha sehemu mbalimbali za upendo​—kama vile kujitia pa nafasi ya mwingine, huruma, na musamaha—​tunaendelesha umoja wetu. Biblia inasema “upendo ni kifungo kikamilifu cha umoja.”​—Kol. 3:12-14; 1 Ko. 13:4-7.

Yehova anabariki familia ya ulimwenguni pote ya ndugu na dada wenye kuwa na umoja (Ona fungu la 26)

27. (a) Maunabii juu ya Masiya yenye kuwa mu kitabu cha Ezekieli inakufanya ujisikie je? (b) Tutazungumuzia nini mu sura za kufuata?

27 Tuko wenye shukrani sana kuhusu maunabii juu ya Masiya yenye kuwa mu kitabu cha Ezekieli! Kusoma na kufikiri sana kuhusu ile maunabii juu ya Masiya kunatufundisha kwamba Mufalme wetu mupendwa, Yesu Kristo, anastahili kutumainiwa, iko na haki ya kisheria ya kutawala, anatuchunga kwa upendo, na atatusaidia tuendelee kuwa mu kifungo cha umoja, chenye kitadumu milele. Ndiyo, tuko na pendeleo kubwa sana la kuwa raia wa Masiya-Mufalme! Tusisahau kama ile maunabii juu ya Masiya ni sehemu ya tungo kubwa kuhusu kurudishwa kwa ibada safi yenye kuzungumuziwa mu kitabu cha Biblia cha Ezekieli. Ni kupitia Yesu njo Yehova anakusanya watu Wake na kurudisha ibada safi kati yao. (Eze. 20:41) Mu sura za kufuata za kitabu hiki, tutachunguza ile tungo yenye kuchochea ya kurudishwa kwa ibada safi na namna inazungumuziwa mu kitabu cha Ezekieli.

^ fu. 1 Mwaka wa kwanza wa uhamisho ulianza mu mwaka wa 617 M.K.Y. wakati wahamishwa Wayahudi wa kwanza-kwanza walipelekwa Babiloni. Kwa hiyo, mwaka wa sita ulianza mu mwaka wa 612 M.K.Y.

^ fu. 14 Kizazi cha Daudi mwenye Yesu alitokea ndani kinaonyeshwa muzuri sana mu Vitabu vya Injili vyenye viliongozwa na roho takatifu.​—Mt. 1:1-16; Lu. 3:23-31.

^ fu. 23 Ile unabii ya Ezekieli juu ya vile vipande mbili vya muti na namna ilitimia itazungumuziwa mu Sura ya 12 ya kitabu hiki.

^ fu. 24 Kuhusu neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “milele,” kitabu kimoja kinasema hivi: “Ile neno iko na wazo la muda murefu, lakini pia inaonyesha hali ya kudumu, hali ya kutokuvunjwa, hali ya kutobadilika.”