Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 12

“Nitawafanya Kuwa Taifa Moja”

“Nitawafanya Kuwa Taifa Moja”

EZEKIELI 37:22

WAZO KUBWA: Ahadi ya Yehova ya kukusanya watu wake pamoja; unabii kuhusu vipande mbili vya muti

1, 2. (a) Juu ya nini wahamishwa walipaswa kuogopa? (b) Lakini, juu ya nini wanashangaa? (c) Tutazungumuzia maulizo gani?

MUNGU aliongoza Ezekieli atolee wahamishwa wenye kuwa Babiloni maunabii mingi kupitia alama zenye kuonekana na macho. Onyesho ya kwanza ya unabii, na ya pili, na ya tatu na maonyesho ingine yenye Ezekieli alifanya ilikuwa na habari ya hukumu. (Eze. 3:24-26; 4:1-7; 5:1; 12:3-6) Kusema kweli, maonyesho yote ya unabii yenye amefanya imeonyesha hukumu kali yenye ingepata Wayahudi.

2 Wazia sasa namna wahamishwa wanapaswa kuogopa wakati Ezekieli anasimama tena mbele yao, na iko tayari kufanya onyesho ingine ya unabii. Pengine wanajiuliza: ‘Anataka tena kutuambia habari gani ya kuogopesha?’ Lakini wanashangaa. Unabii wenye Ezekieli anaanza kutoa kupitia onyesho hauko vile wanawazia. Hauzungumuzie hukumu, lakini ahadi ya muzuri. (Eze. 37:23) Ni habari gani Ezekieli anatolea wahamishwa? Iko na maana gani? Inahusu namna gani watumishi wa Mungu leo? Acha tuone.

“Vitakuwa Kipande Kimoja cha Muti Katika Mukono Wangu”

3. (a) Kipande cha muti “kwa ajili ya Yuda” kilifananisha nini? (b) Juu ya nini “kipande cha muti cha Efraimu” kinafananisha ufalme wa makabila kumi?

3 Yehova aliomba Ezekieli akamate vipande mbili vya muti na aandike juu ya kimoja “kwa ajili ya Yuda” na juu ya kingine “kwa ajili ya Yosefu, kipande cha muti cha Efraimu.” (Soma Ezekieli 37:15, 16.) Vile vipande mbili vya muti vilifananisha nini? Kipande cha muti “kwa ajili ya Yuda” kilifananisha ufalme wa makabila mbili wa Yuda na Benyamini. Wafalme wa kizazi cha Yuda walitawala makabila mbili; pia, kulikuwa uhusiano wa karibu sana kati yao na ukuhani, sababu makuhani walitumika ku hekalu kule Yerusalemu. (2 Ny. 11:13, 14; 34:30) Kwa hiyo, ufalme wa Yuda uliendelesha kizazi cha wafalme wa jamaa ya Daudi na pia ukuhani wa Walawi. “Kipande cha muti kwa ajili ya Efraimu” kilifananisha utawala wa makabila kumi ya Israeli. Juu ya nini kile kipande cha muti kilitajwa kuwa “kipande cha muti kwa ajili ya Efraimu”? Mufalme wa kwanza wa ufalme wa makabila kumi alikuwa Yeroboamu, wa kabila la Efraimu. Kisha, Efraimu ikakuwa kabila la maana zaidi mu Israeli. (Kum. 33:17; 1 Fa. 11:26) Tena, wafalme wa kizazi cha Daudi na makuhani Walawi hawakukuwa sehemu ya utawala wa makabila kumi ya Israeli.

4. Tendo lenye Ezekieli alifanya kwa kutumia vile vipande mbili vya muti lilionyesha nini? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

4 Kisha Ezekieli aliombwa atie pamoja vile vipande mbili vya muti “ili vikuwe kipande kimoja tu cha muti.” Wakati wahamishwa walikuwa wanaangalia Ezekieli na macho ya woga, walimuuliza: “Hautatuambia kama ile yote iko na maana gani?” Alijibu kwa kuwaambia kama tendo lenye alifanya lilionyesha mambo yenye Yehova mwenyewe angefanya. Yehova alisema hivi kuhusu vile vipande mbili vya muti: “Nitavifanya kuwa kipande kimoja cha muti, na vitakuwa kipande kimoja cha muti katika mukono wangu.”​Eze. 37:17-19.

5. Onyesho ya unabii yenye Ezekieli alifanya iko na maana gani? (Ona kisanduku “Kuunganishwa kwa Vipande Mbili vya Muti.”)

5 Kisha, Yehova alifasiria maana ya kuunganishwa kwa vile vipande mbili vya muti. (Soma Ezekieli 37:21, 22.) Wahamishwa wa ufalme wa makabila mbili ya Yuda na wahamishwa wa makabila kumi ya Israeli (Efraimu) wangerudishwa mu inchi ya Israeli, na kule wangekuwa “taifa moja.”​—Yer. 30:1-3; 31:2-9; 33:7.

6. Ni maunabii gani ingine inapatikana mu Ezekieli sura ya 37?

6 Sura ya 37 ya Ezekieli iko na maunabii ingine ya kushangaza kabisa kuhusu kurudishwa kwa ibada safi: unabii kuhusu “mifupa yenye kukauka,” na kuhusu vipande mbili vya muti. Yehova ataonyesha kama yeye ni Mungu mwenye kurudisha uzima (mistari ya 1-14) lakini pia mwenye kurudisha umoja (mistari ya 15-28). Ile maunabii mbili iko na habari hii ya kutia moyo: Kifo kinaweza kuondolewa, na mugawanyiko pia unaweza kuondolewa.

Namna gani Yehova ‘Aliwakusanya Pamoja’?

7. Namna gani maelezo ya 1 Mambo ya Nyakati 9:2, 3 inahakikisha kama “kwa Mungu mambo yote yanawezekana”?

7 Ku mawazo ya wanadamu, kukombolewa na kuunganishwa kwa wahamishwa ilionekana kuwa jambo lenye haliwezekane. * Lakini, “kwa Mungu mambo yote yanawezekana.” (Mt. 19:26) Yehova alitimiza unabii wake. Utekwa wa Babiloni uliisha mu mwaka wa 537 M.K.Y., na kisha pale, watu wa zile falme mbili walifika Yerusalemu juu ya kusaidia kurudisha ibada ya kweli. Habari yenye iliongozwa na roho ya Mungu inatoa uhakikisho huu: “Wazao fulani wa Yuda, wa Benyamini, wa Efraimu, na wa Manase walikaa katika Yerusalemu.” (1 Ny. 9:2, 3; Ezr. 6:17) Kwa kweli, sawa vile Yehova alikuwa ametabiri, watu wa ufalme wa makabila kumi ya Israeli waliunganishwa na watu wa ufalme wa makabila mbili ya Yuda.

8. (a) Isaya alitabiri nini? (b) Ni mambo gani mbili ya maana inapatikana mu Ezekieli 37:21?

8 Miaka 200 hivi mbele, nabii Isaya alitabiri mambo yenye ingepata Israeli na Yuda kisha utekwa wao. Alitabiri kama Yehova angeanza kukusanya “watu wa Israeli wenye walisambazwa” na “watu wa Yuda wenye walisambazwa kutoka pembe ine (4) za dunia,” na pia “kutoka Ashuru.” (Isa. 11:12, 13, 16) Na kusema kweli, kama vile Yehova alitabiri, alitosha “Waisraeli katika mataifa.” (Eze. 37:21) Ona mambo hii mbili ya maana: Hapa, Yehova hatumie maneno “Yuda” na “Efraimu” juu ya kuzungumuzia wahamishwa lakini anawaita “Waisraeli”​—kundi moja. Tena, unabii hauseme kama Waisraeli wanatoka mu taifa moja tu, Babiloni, lakini unasema kama wanatoka mu mataifa mingi​—ni kusema, “kutoka kila upande.”

9. Yehova alifanya nini juu ya kusaidia wahamishwa wakuwe mu umoja?

9 Kisha wahamishwa kurudia mu inchi ya Israeli, Yehova alifanya nini juu ya kuwasaidia wakuwe mu umoja? Alitolea Israeli wachungaji wa kiroho, sawa vile Zerubabeli, Kuhani Mukubwa Yoshua, Ezra, na Nehemia. Tena, Mungu alitokeza nabii Hagai, Zekaria, na Malaki. Wale wanaume wote waaminifu walifanya yao yote juu ya kutia moyo taifa lifuate maagizo ya Mungu. (Ne. 8:2, 3) Zaidi ya ile, Yehova alilinda taifa la Israeli kwa kuvunja mipango ya mubaya ya maadui wa watu wa Mungu.​—Est. 9:24, 25; Zek. 4:6.

Yehova alitoa wachungaji wa kiroho juu ya kusaidia watu wake wakuwe mu umoja (Ona fungu la 9)

10. Shetani aliweza kufanya nini?

10 Lakini, ijapokuwa ile yote yenye Yehova alifanya juu aliwapenda, Waisraeli mingi hawakushikamana na ibada safi. Matendo yao inaonyeshwa mu vitabu vya Biblia vyenye viliandikwa kisha wahamishwa kurudia mu inchi yao. (Ezr. 9:1-3; Ne. 13:1, 2, 15) Tena, miaka mia moja kisha wao kurudia mu inchi yao, Waisraeli walijitenga sana na ibada safi mupaka Yehova akawaambia: “Munirudilie.” (Mal. 3:7) Kufikia wakati Yesu alikuja ku dunia, dini ya Kiyahudi ilikuwa imegawanyika mu mazehebu mingi yenye ilikuwa inaongozwa na wachungaji wenye hawakukuwa waaminifu. (Mt. 16:6; Mk. 7:5-8) Shetani aliweza kuzuia watu wasikuwe mu umoja kabisa. Ijapokuwa vile, unabii wa Yehova kuhusu kuunganishwa kwa watu wake ungetimia tu. Namna gani?

“Mutumishi Wangu Daudi Atakuwa Mufalme Wao”

11. (a) Yehova alifunua nini kuhusu unabii wake wa kuunganisha watu wake? (b) Shetani alijaribu tena kufanya nini kisha yeye kufukuzwa mbinguni?

11 Soma Ezekieli 37:24. Yehova alifunua kama unabii wake kuhusu kuunganishwa kwa watu wake ungetimia kwa ukamili kisha tu “mutumishi [wake] Daudi,” ni kusema, Yesu, kuanza kutawala akiwa Mufalme, na ile ilitokea mu mwaka wa 1914. * (2 Sa. 7:16; Lu. 1:32) Ile wakati, Waisraeli wa kiroho, wenye kutiwa mafuta, walikuwa wamekamata nafasi ya Waisraeli wa kimwili. (Yer. 31:33; Gal. 3:29) Shetani alianza tena kuvuruga umoja wa watu wa Mungu, zaidi sana kisha yeye kufukuzwa mbinguni. (Ufu. 12:7-10) Kwa mufano, kisha kifo cha Ndugu Russell mu mwaka wa 1916, Shetani aliona ile kuwa nafasi ya kuleta mugawanyiko kati ya watiwa-mafuta kupitia matendo ya waasi-imani. Lakini, kisha wakati kidogo, wale waasi-imani waliacha tengenezo. Shetani aliweza pia kufanya wenye kuongoza mambo ile wakati watupwe mu gereza, lakini hata ile haikumaliza watu wa Yehova. Ndugu watiwa-mafuta wenye walibakia waaminifu kwa Yehova hawakupoteza umoja wao.

12. Juu ya nini mipango ya Shetani ya kuleta migawanyiko mu Israeli wa kiroho imeshindikana?

12 Kwa hiyo, tofauti na ile yenye ilifikia Waisraeli wa kimwili, Waisraeli wa kiroho hawakujiacha washindwe na mipango ya Shetani ya kuleta migawanyiko. Juu ya nini mipango ya Shetani imeshindikana? Juu, watiwa-mafuta wamefanya yao yote ili kushikamana na kanuni za Yehova. Matokeo? Wamelindwa na Mufalme wao, Yesu Kristo, mwenye anaendelea kumushinda Shetani.​—Ufu. 6:2.

Yehova Atafanya Waabudu Wake ‘Wakuwe Kipande Kimoja cha Muti’

13. Unabii kuhusu kuunganishwa kwa vipande mbili vya muti unatufundisha kweli gani ya maana?

13 Unabii kuhusu kuunganishwa kwa vipande mbili vya muti uko na maana gani leo? Kumbuka kama kusudi la ile unabii lilikuwa kuonyesha namna vikundi mbili vingefikia kuwa mu umoja. Na zaidi ya yote, ile unabii inaonyesha kama Yehova njo alileta ile umoja. Basi, unabii kuhusu kuunganishwa kwa vipande mbili vya muti unaonyesha kweli gani ya maana juu ya ibada safi? Kwa kifupi, ni hii: Yehova mwenyewe njo atafanya waabudu wake ‘wakuwe kipande kimoja cha muti,’ ao wakuwe mu umoja.​—Eze. 37:19.

14. Namna gani unabii kuhusu kuunganishwa kwa vipande mbili vya muti umetimia mu njia kubwa zaidi tangu 1919?

14 Tangu 1919, kisha watu wa Mungu kusafishwa kiroho na kisha wao kuanza kuingia mu paradiso ya kiroho, unabii kuhusu kuunganishwa kwa vipande vya muti ulianza kutimia mu njia kubwa zaidi. Ile wakati, hesabu kubwa ya wenye waliunganishwa mu umoja walikuwa na tumaini la kuwa wafalme na makuhani mbinguni. (Ufu. 20:6) Mu njia ya mufano, wale watiwa-mafuta walikuwa sawa vile kipande cha muti “kwa ajili ya Yuda”​—taifa lenye mulikuwa wafalme wa kizazi cha Daudi na makuhani Walawi. Lakini, kadiri wakati ilipita, watu mingi wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia walijiunga na Wayahudi wa kiroho. Wale watu walikuwa sawa vile “kipande cha muti kwa ajili ya Efraimu”​—taifa lenye hamukukuwa wafalme wa kizazi cha Daudi na makuhani Walawi. Vikundi vyote mbili vinatumika kwa umoja vikiwa taifa la Yehova chini ya Mufalme wao mumoja, Yesu Kristo.​—Eze. 37:24.

“Watakuwa Watu Wangu”

15. Namna gani maneno ya unabii yenye inapatikana mu Ezekieli 37:26, 27 iko inatimia leo?

15 Unabii wa Ezekieli unaonyesha kama watu mingi wangefurahia kujiunga na watiwa-mafuta mu ibada safi. Yehova alisema hivi kuhusu watu wake: ‘Nitawafanya . . . wakuwe wengi’ na, “hema yangu itakuwa juu yao.” (Eze. 37:26, 27; maelezo ya chini) Ile maneno inatukumbusha mambo yenye mutume Yohana aliambiwa miaka 700 hivi kisha wakati wa Ezekieli, ya kama, “Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme [angetandika] hema yake” juu ya “kundi kubwa la watu.” (Ufu. 7:9, 15) Leo, watiwa-mafuta na kundi kubwa wanakaa wakiwa taifa moja, watu wa Mungu, chini ya hema ya ulinzi ya Mungu.

16. Zekaria alitoa unabii gani kuhusu kuunganishwa kwa Israeli wa kiroho na wale wenye wako na tumaini la kuishi ku dunia?

16 Kuunganishwa kwa Wayahudi wa kiroho pamoja na wale wenye wako na tumaini la kuishi ku dunia kulitabiriwa pia na Zekaria, yeye mwenyewe alikuwa muhamishwa mwenye alirudiaka mu inchi ya Israeli. Alionyesha kama ‘watu kumi (10) kutoka katika . . . mataifa wangeshika . . . kanzu ya Muyahudi’ na kusema: “Tunataka kuenda pamoja na ninyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu iko pamoja na ninyi.” (Zek. 8:23) Neno “Muyahudi” halimaanishe mutu moja tu, lakini kikundi cha watu, “ninyi,” chenye kinafananishwa leo na mabaki ya watiwa-mafuta, ao Wayahudi wa kiroho. (Ro. 2:28, 29) “Watu kumi (10)” wanafananisha wale wenye wako na tumaini la kuishi ku dunia. ‘Wanashika’ watiwa-mafuta na “kuenda pamoja” nao. (Isa. 2:2, 3; Mt. 25:40) Maneno ‘kushika’ na “kuenda pamoja na ninyi” inaonyesha umoja wenye kuwa kamili kati ya vile vikundi mbili.

17. Yesu alisema nini juu ya kuzungumuzia umoja wenye tuko nao leo?

17 Yesu alijiita kuwa muchungaji, mwenye chini ya uongozi wake, kondoo wake (watiwa-mafuta) na “kondoo wengine” (wale wenye wako na tumaini la kuishi ku dunia) wangekuwa “kundi moja.” Inawezekana ni unabii wa Ezekieli njo Yesu alikuwa nao mu akili wakati alisema vile. (Yoh. 10:16; Eze. 34:23; 37:24, 25) Maneno ya Yesu na ile ya manabii wa zamani inaonyesha umoja wa kiroho wa kushangaza wenye tuko nao leo, ikuwe tumaini letu ni kuenda mbinguni ao kuishi ku dunia! Dini ya uongo imegawanyika mu vikundi-vikundi vyenye havina hesabu, lakini sisi tuko mu umoja, na ile ni muujiza kabisa.

Leo, watiwa-mafuta na “kondoo wengine” wanamuabudu Yehova mu umoja wakiwa “kundi moja” (Ona fungu la 17)

“Patakatifu Pangu Patakuwa Katikati yao Milele”

18. Kama vile Ezekieli 37:28 inaonyesha, juu ya nini ni lazima watu wa Mungu wasikuwe “sehemu ya ulimwengu”?

18 Maneno ya mwisho ya unabii wa Ezekieli kuhusu kuunganishwa kwa watu wa Mungu inaonyesha juu ya nini umoja wetu hautavunjikaka. (Soma Ezekieli 37:28.) Watu wa Yehova wako na umoja sababu patakatifu pake, ao ibada safi, pako “katikati yao.” Na patakatifu pake pataendelea kuwa kati yao kama wanaendelea kubakia safi, ao kutokuwa sehemu ya ulimwengu wa Shetani. (1 Ko. 6:11; Ufu. 7:14) Yesu alikazia kama haifae kuwa sehemu ya ulimwengu. Mu sala ya kutoka mu moyo yenye alitoa kwa ajili ya wanafunzi wake, alisema: “Baba Mutakatifu, uwalinde . . . ili wakuwe kitu kimoja . . . Wao hawako sehemu ya ulimwengu . . . Uwatakase kwa njia ya ile kweli.” (Yoh. 17:11, 16, 17) Ona namna Yesu anatia uhusiano kati ya “kitu kimoja” na ‘kutokuwa sehemu ya ulimwengu.’

19. (a) Namna gani tunaonyesha kama tuko “waigaji wa Mungu”? (b) Mangaribi ya mwisho mbele akufe, Yesu alikazia kweli gani ya maana kuhusu umoja?

19 Ni mu hii andiko tu njo Yesu anamuita Mungu kuwa “Baba Mutakatifu.” Yehova njo iko safi na munyoofu kabisa. Zamani, Yehova aliamuru Waisraeli hivi: “Munapaswa kuwa watakatifu, kwa sababu mimi ni mutakatifu.” (Law. 11:45) Kwa kuwa tuko “waigaji wa Mungu,” tunataka kutii ile amri mu mwenendo wetu wote. (Efe. 5:1; 1 Pe. 1:14, 15) Wakati neno “mutakatifu” ao “watakatifu” linatumiwa kuhusu wanadamu, linamaanisha “kutiwa pembeni.” Kwa hiyo, mangaribi ya mwisho mbele akufe, Yesu alikazia kama wanafunzi wake wangeendelea kuwa mu umoja ikiwa wangeendelea kujitenga na ulimwengu huu na roho yake ya migawanyiko.

“Uwalinde kwa Sababu ya Ule Muovu”

20, 21. (a) Ni nini inatusaidia tutumainie sana uwezo wa Yehova wa kutulinda? (b) Unaazimia kufanya nini?

20 Umoja wa pekee wenye unaonekana waziwazi mu dunia yote kati ya Mashahidi wa Yehova unaonyesha kama Yehova alijibu ombi hii ya Yesu: “Uwalinde kwa sababu ya ule muovu.” (Soma Yohana 17:14, 15.) Kwa kweli, kuona namna Shetani ameshindwa kuharibu umoja wa watu wa Mungu kunatusaidia tutumainie sana uwezo wa Mungu wa kutulinda. Mu unabii wa Ezekieli, Yehova alisema kama vipande mbili vya muti vilifikia kuwa kipande kimoja mu mukono wake. Kwa hiyo, Yehova ameunganisha watu wake mu njia ya muujiza chini ya mukono wake wenye kutoa ulinzi​—kwenye Shetani hawezi kufika.

21 Azimio letu linapaswa kuwa nini basi? Azimio letu linapaswa kuwa kuendelea kufanya yetu yote juu ya kuendelesha umoja wa maana sana wenye tuko nao leo. Ni mu njia gani ya maana kila mumoja wetu anaweza kufanya vile? Ni kwa kuendelea kufanya ibada safi mu hekalu la kiroho. Sura za kufuata zitaonyesha namna gani tunaweza kufanya vile kabisa.

^ fu. 7 Miaka mia mbili hivi mbele Ezekieli apokee ile unabii, Waashuru walipeleka wakaaji wa utawala wa makabila kumi (“kipande cha muti cha Efraimu”) mu uhamisho.​—2 Fa. 17:23.

^ fu. 11 Ile unabii inazungumuziwa kwa urefu mu Sura ya 8 ya kitabu hiki.