Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 14

“Hii Ndiyo Sheria ya Hekalu”

“Hii Ndiyo Sheria ya Hekalu”

EZEKIELI 43:12

WAZO KUBWA: Maono ya hekalu​—somo mbalimbali zenye watu wa siku za Ezekieli walipata na maana ya ile maono kwetu leo

1, 2. (a) Tulijifunza nini kuhusu maono ya Ezekieli ya hekalu mu sura yenye ilitangulia? (b) Tutazungumuzia maulizo gani mbili mu sura hii?

EZEKIELI hakuonaka hekalu kubwa la kiroho lenye mutume Paulo alizungumuzia miaka mingi kisha. Tuliona vile mu sura yenye ilitangulia. Tuliona pia kama ile maono ilitolewa juu ya kufundisha watu wa Mungu kama ni jambo la lazima kufuata kanuni za Mungu za ibada safi. Watu wangefurahia tena uhusiano mupya na Yehova kama tu wangetii zile kanuni. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini Yehova alikazia mara mbili wazo hili la maana mu andiko moja: “Hii ndiyo sheria ya hekalu.”​—Soma Ezekieli 43:12.

2 Sasa ni muzuri tuchunguze maulizo ingine mbili. Ya kwanza: Wayahudi wa siku za Ezekieli walipata somo gani mbalimbali kuhusu kanuni za Yehova kwa ajili ya ibada safi mu ile maono ya hekalu? Jibu ya ile ulizo itatusaidia kujibia ulizo yetu ya pili: Ile maono iko na maana gani kwetu mu siku hizi za mwisho zenye kujaa muvurugo?

Ile Maono Ilipatia Watu Fundisho Gani mu Wakati wa Zamani?

3. Hekalu lenye lilionwa mu maono lilikuwa juu ya mulima murefu, namna gani ile ilifanya watu wasikie haya?

3 Juu ya kujibia ulizo ya kwanza, acha tuchunguze sehemu za maana za maono hii ya hekalu. Mulima murefu. Inaonekana watu waliona kama kuko upatano kati ya fasi kwenye kulikuwa hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono na unabii wenye kutia moyo wa Isaya kuhusu kurudishwa kwa ibada safi. (Isa. 2:2) Lakini kuona nyumba ya Yehova ku mulima murefu kuliwafundisha nini? Kuliwafundisha kama ibada safi inapaswa kuinuliwa, kuwekwa juu, kupandishwa juu kuliko kitu kingine chochote. Ni kweli kwamba, ibada safi inakuwaka tu yenye kuinuliwa, sababu ni mupango wa Ule mwenye ‘kuinuliwa juu zaidi kuliko miungu mingine yote.’ (Zb. 97:9) Lakini watu njo hawakukuwa wanafanya ile walipaswa kufanya. Mu miaka mingi, walifanya tena na tena ibada safi isiheshimiwe, iachwe, na ichafuliwe. Kuona namna nyumba takatifu ya Mungu ilikuwa imeinuliwa, namna ilikuwa imepandishwa kufikia hali ya utukufu na heshima yenye ilistahili, kulipaswa kabisa kufanya watu wenye moyo muzuri wasikie haya.

4, 5. Milango mikubwa ya murefu ya hekalu ilipaswa kupatia wasikilizaji wa Ezekieli somo gani?

4 Milango mikubwa ya murefu. Ku mwanzo-mwanzo wa maono, Ezekieli aliona namna malaika mwenye alikuwa anamuongoza alikuwa anapima milango mikubwa. Ile milango mikubwa ilikuwa na urefu wa metre 30 hivi! (Eze. 40:14) Walinzi wa vyumba walikuwa ku kila muingilio. Ile yote ilipaswa kupatia wazo gani wale wenye walijifunza plani ya hekalu? Yehova aliambia Ezekieli: “Kaza sana uangalifu kuhusu njia ya kuingilia ya hekalu.” Juu ya nini? Juu, watu walikuwa wanaleta wale wenye “hawatahiriwe katika moyo na katika mwili” na kuwaingiza mu nyumba takatifu ya Mungu ya ibada. Matokeo? “Wanachafua hekalu langu,” ni vile Yehova alisema.​—Eze. 44:5, 7.

5 Wale wenye walikuwa “hawatahiriwe katika . . . mwili” walikuwa wameshindwa kutii amri ya Mungu yenye iko wazi yenye ilitolewa tangu wakati wa Abrahamu. (Mwa. 17:9, 10; Law. 12:1-3) Lakini wale wenye walikuwa “hawatahiriwe katika moyo” walikuwa na shida kubwa sana. Walikuwa waasi wenye kiburi, wenye hawakutii maagizo na muongozo wa Yehova. Watu wa namna ile hawakupaswa kuruhusiwa kuingia mu nyumba takatifu ya Yehova ya ibada! Yehova anachukia unafiki, lakini watu wake walikuwa wameacha unafiki ujae mu nyumba yake. Kwa hiyo, milango mikubwa na walinzi wa vyumba wa hekalu lenye lilionwa mu maono, ile yote ilitoa fundisho hii: Makosa ya vile haipaswe tena kufanyika! Kanuni za juu ili kuingia mu nyumba ya Mungu zilipaswa kuheshimiwa. Ni kwa kufanya vile tu njo Yehova angebariki ibada ya watu.

6, 7. (a) Yehova anatumia namna gani ukuta wenye kuzunguka majengo ya hekalu juu ya kupatia watu wake fundisho fulani? (b) Mu siku za mbele, watu wa Yehova walitendea nyumba yake namna gani? (Ona maelezo.)

6 Ukuta wenye kuzunguka eneo la hekalu. Jambo lingine la maana kuhusu hekalu lenye lilionwa mu maono ni ukuta wenye ulizunguka eneo lote la hekalu. Ezekieli anasema kama kila upande wa ukuta ulikuwa na urefu wa matete 500, ao metre 1 555, ao kilometre 1.6! (Eze. 42:15-20) Lakini, majengo ya hekalu na viwanja vilifanyiza eneo la pande ine zenye ziko sawasawa la mikono 500 tu, ao metre 259, kila upande. Kwa hiyo kulikuwa eneo kubwa kuzunguka hekalu, na lilizungukwa na ukuta wa inje. * Juu ya nini?

7 Yehova alisema: “Sasa acha watie ukahaba wao wa kiroho na mizoga ya wafalme wao mbali na mimi, na nitakaa kati yao milele.” (Eze. 43:9) Inaonekana “mizoga ya wafalme wao” ilimaanisha ibada ya sanamu. Kwa hiyo, ni kama vile Yehova alitumia ile ukuta ya mukubwa yenye kuzunguka eneo la hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono juu ya kusema: “Ile uchafu yote ibakie kule mbali. Musipime hata kuileta karibu.” Kama wangeendelea kulinda ibada yao ikiwa safi, Yehova angewabariki kwa kuishi katikati yao.

8, 9. Mashauri mazito yenye Yehova alipatia wanaume wenye madaraka ilipaswa kufundisha watu nini?

8 Mashauri mazito kwa wanaume wenye madaraka. Yehova alitoa pia mashauri mazito lakini ya upendo kwa wanaume wenye walikuwa na madaraka makubwa kati ya watu wake. Alikaripia kwa uzito Walawi wenye walijitenga naye wakati watu walizama mu ibada ya sanamu, lakini alipongeza wana wa Sadoki, “wenye walifanya kazi za patakatifu [pake] wakati Waisraeli walienda mbali.” Alitendea kila kikundi kwa haki na rehema, kufuatana na matendo yao. (Eze. 44:10, 12-16) Vilevile, wakubwa wa Israeli walikaripiwa kwa uzito.​—Eze. 45:9.

9 Kwa kufanya vile, Yehova alionyesha waziwazi kama wanaume wenye wako na mamlaka na daraka la kusimamia mambo walipaswa kutoa hesabu juu ya namna walitumia madaraka yao. Wao pia walikuwa na lazima ya mashauri, karipio, na nizamu. Na ni wao njo walipaswa kuwa mifano mu kushika kanuni za Yehova!

10, 11. Ni nini inaonyesha kama wahamishwa fulani wenye walirudia mu inchi yao walitumikisha somo mbalimbali zenye walipata mu maono ya Ezekieli?

10 Je, wahamishwa wenye walirudia mu inchi yao walitumikisha somo mbalimbali zenye maono ya Ezekieli iliwapatia? Kusema kweli, hatujue kwa uhakika mawazo yenye wanaume na wanamuke waaminifu wa ile wakati walikuwa nayo kuhusu ile maono ya ajabu. Lakini, Neno la Mungu linatuambia mambo mingi kuhusu mambo yenye wahamishwa wenye walirudia mu inchi yao walifanya na mawazo yenye walifikia kuwa nayo kuhusu ibada safi ya Yehova. Je, walitumikisha kanuni zenye walijifunza kupitia maono ya Ezekieli? Walifanya vile kwa kiasi fulani​—zaidi sana kama tunawalinganisha na mababu zao waasi wenye waliishi mbele ya uhamisho wa Babiloni.

11 Wanaume waaminifu sawa vile nabii Hagai na Zekaria, kuhani na mwandishi Ezra, na gavana Nehemia, wote walijikaza kufundisha watu kanuni sawa zile zenye maono ya Ezekieli ya hekalu ilionyesha. (Ezr. 5:1, 2) Walifundisha watu kama ibada safi inapaswa kuinuliwa na kutiwa pa nafasi ya kwanza, hapana mambo ya kimwili ao mambo ya kipekee. (Hag. 1:3, 4) Walikazia kama kanuni zenye mutu anapaswa kutii juu astahili kushiriki mu ibada safi zinapaswa kuheshimiwa. Kwa mufano, Ezra na Nehemia walishauria watu kwa uzito wafukuze wanamuke wa kigeni, wenye walikuwa wanafanya hali ya kiroho ya watu ikuwe zaifu. (Soma Ezra 10:10, 11; Ne. 13:23-27, 30) Halafu ibada ya sanamu? Inaonekana kama kisha uhamisho, taifa lilifikia kuchukia sana ile zambi, yenye walikuwa wameangukia ndani tena na tena mu kipindi cha historia yao. Na ilikuwa je kuhusu makuhani na wakubwa? Kama vile maono ya Ezekieli ilionyesha, walikuwa kati ya watu wenye Yehova alipatia mashauri na karipio. (Ne. 13:22, 28) Wengi walikubali ile mashauri kwa unyenyekevu.​—Ezr. 10:7-9, 12-14; Ne. 9:1-3, 38.

Nehemia alifundisha watu kuhusu ibada safi wakati alikuwa anatumika nao (Ona fungu la 11)

12. Ni mu njia gani Yehova alibariki wahamishwa kisha wao kurudia mu inchi yao?

12 Kwa hiyo, Yehova alibariki watu wake. Walikuwa na uhusiano muzuri na Yehova, walikuwa na afya ya muzuri na kulikuwa utaratibu kati yao, mu namna yenye haiyakuwaka zamani. (Ezr. 6:19-22; Ne. 8:9-12; 12:27-30, 43) Juu ya nini vile? Juu, watu walifikia kuanza kutii kanuni za haki za Yehova kuhusu ibada safi. Somo mbalimbali zenye hekalu lenye lilionwa mu maono lilitoa ziligusa mioyo mingi yenye ilikuwa tayari kutii. Kwa kifupi, tunaweza kusema kama maono ya Ezekieli ilisaidia wahamishwa mu njia mbili za maana. (1) Iliwafundisha somo mbalimbali kuhusu kanuni za ibada safi na namna walipaswa kuzitumikisha. (2) Ilitoa uhakikisho fulani wa kiunabii. Ilionyesha kama kuko siku ibada safi ingerudishwa, na tena ilionyesha namna Yehova angebariki watu wake kadiri wangeendelea kumutolea ibada safi. Lakini, sisi pia tunataka kujua: Je, ile maono inatimia leo?

Mambo Yenye Maono ya Ezekieli Inatufundisha Leo

13, 14. (a) Ni nini inatuonyesha kama maono ya Ezekieli ya hekalu inatimia pia wakati wetu? (b) Ile maono inatusaidia mu njia gani leo? (Ona pia kisanduku 13A, “Mahekalu Tofauti, Somo Tofauti.”)

13 Je, tunaweza kusema kama maono ya Ezekieli ya hekalu inatuhusu leo? Ndiyo! Kumbuka jambo lenye kufanana kati ya maono ya Ezekieli ya nyumba takatifu ya Mungu yenye kuwa ku “mulima murefu sana” na unabii wa Isaya wenye kuonyesha kama ‘mulima wa nyumba ya Yehova ungewekwa imara kabisa kwenye kichwa cha milima.’ Isaya anatuambia zaidi sana kwamba unabii wake ungetimia mu “kipindi cha mwisho cha zile siku,” ao “siku za mwisho.” (Eze. 40:2; Isa. 2:2-4; ona pia Mika 4:1-4, maelezo ya chini) Ile maunabii inahusu kipindi cha siku za mwisho kuanzia 1919 wakati ibada safi inainuliwa, inarudishwa mu hali ya muzuri, na kuwekwa ku mulima murefu mu njia ya mufano. *

14 Bila shaka, maono ya Ezekieli inahusu kabisa ibada safi leo. Kama vile ilisaidia sana wahamishwa Wayahudi mu wakati wa zamani, ile maono inatusaidia leo mu njia mbili. (1) Inatuonyesha waziwazi namna tunaweza kushika kanuni za Yehova kuhusu ibada safi. (2) Inatoa uhakikisho wa kiunabii kwamba ibada safi itarudishwa na Yehova atabariki watumishi wake.

Kanuni za Ibada Safi Leo

15. Ni nini hatupaswe kusahau wakati tunatafuta somo mbalimbali kuhusu hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono?

15 Tuzungumuzie sasa sehemu fulani za maono ya Ezekieli. Wazia kama tuko na Ezekieli wakati iko anafanya matembezi mu hekalu kubwa lenye alionaka mu maono. Tusisahau kama ile yenye tunaona haiko njo hekalu kubwa la kiroho; lakini, tuko tu tunatafuta somo mbalimbali zenye zinahusu ibada yetu leo. Ni somo gani zenye tunaweza kujifunza?

16. Vipimo vyote mu maono ya Ezekieli vinaweza kutufundisha nini? (Ona picha ku mwanzo wa habari)

16 Juu ya nini vile vipimo vyote? Kadiri Ezekieli iko anaangalia, ule mwanaume mwenye ni malaika, mwenye kuonekana kwake ni kama kwa shaba anapima sehemu mbalimbali za hekalu, kuta, milango mikubwa, vyumba vya walinzi, viwanja, na mazabahu. Habari ni za mingi na zinaweza kupatia musomaji kizungu-zungu. (Eze. 40:1–42:20; 43:13, 14) Lakini, zile habari zinaweza kutufundisha mambo ya maana. Kupitia zile habari, Yehova anaonyesha kwa mukazo kwamba kanuni zake ni za maana sana. Yeye njo anaziweka, hapana mwanadamu bure. Wenye wanawaza kama mutu anaweza kumuabudu Mungu namna anapenda wanajidanganya kabisa. Tena, kwa kupima kila sehemu ya hekalu, Yehova anahakikisha kama kurudishwa kwa ibada safi ni jambo la hakika kabisa. Utimizo wa ahadi ya Mungu uko hakika namna vile vipimo viko kamili. Mu ile njia Ezekieli anaonyesha kama kurudishwa kwa ibada safi mu siku za mwisho ni jambo la hakika!

Vipimo kamili vya hekalu vinakufundisha nini? (Ona fungu la 16)

17. Ukuta wenye kuzunguka eneo la hekalu unapaswa kutukumbusha nini leo?

17 Ukuta wenye kuzunguka eneo la hekalu. Kama vile tulisema, Ezekieli aliona ukuta kuzunguka eneo lote la hekalu lenye alionaka mu maono. Ile ilimukumbusha kabisa kama watu wa Mungu hawakupaswa kuruhusu uchafu wa dini uingie mu ibada safi, juu usichafue nyumba ya Mungu. (Soma Ezekieli 43:7-9.) Tuko na lazima kabisa ya shauri la vile leo! Kisha watu wa Mungu kukombolewa mu utekwa wa kiroho wa miaka mingi mu Babiloni Mukubwa, Kristo aliweka mutumwa muaminifu na mwenye busara mu mwaka wa 1919. Zaidi sana kuanzia ile wakati, watu wa Mungu wamefanya yao yote juu ya kuachana na mafundisho ya uongo na desturi zenye zinachangana na ibada ya sanamu na upagani. Tunafanya yetu yote juu uchafu wa kiroho usiingie mu ibada safi. Tena, hatufanye biashara mu Jumba letu la Ufalme, juu tusichange mambo ya kimwili na ibada yetu.​—Mk. 11:15, 16.

18, 19. (a) Milango mikubwa ya murefu ya hekalu lenye lilionwa mu maono inaweza kutufundisha nini? (b) Tunapaswa kufanya nini wakati mutu fulani anatafuta kushusha ao kuregeza kanuni za juu za Yehova? Toa mufano.

18 Milango mikubwa ya murefu. Tunajifunza nini wakati tunafikiria ile milango mikubwa ya murefu yenye Ezekieli aliona? Bila shaka, milango mikubwa ya murefu yenye ilionwa mu maono ya hekalu ilifundisha wahamishwa Wayahudi kama Yehova iko na kanuni za juu sana za mwenendo. Kama ilikuwa vile wakati wa zamani, halafu leo? Tunaabudu mu hekalu kubwa la kiroho la Yehova. Je, hauone kwamba mwenendo muzuri, wa bila unafiki, ni wa maana hata zaidi leo? (Ro. 12:9; 1 Pe. 1:14, 15) Mu siku hizi za mwisho, Yehova amesaidia watu wake hatua kwa hatua wafuate kwa ukaribu kanuni zake za mwenendo. * Kwa mufano, wakosaji wenye hawatubu wanaondolewa mu kutaniko. (1 Ko. 5:11-13) Zaidi ya ile, walinzi wa vyumba wenye walikuwa ku muingilio wa kila mulango mukubwa wanatukumbusha kama, mutu hawezi kukubaliwa leo mu ibada ya Yehova ikiwa Mungu hamukubali. Kwa mufano, mutu mwenye iko na maisha ya unafiki anaweza kuingia mu Jumba la Ufalme, lakini ile haionyeshe kama Yehova anamukubali. Yehova atamukubali kama tu anafanya mambo yenye anamuomba. (Yak. 4:8) Ile inaonyesha kama ibada safi inalindwa sana mu siku hizi zenye kuharibika, zenye watu wanajiendesha mubaya sana!

19 Biblia ilitabiri kama dunia hii ingeharibika sana mbele mwisho ufike. Tunasoma kama “watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi, wakipotosha watu na kupotoshwa wao wenyewe.” (2 Ti. 3:13) Leo watu mingi sana wanajidanganya kwa kuwaza kama kanuni za juu za Yehova ziko makali-makali, ni za zamani, ao haziko sawa. Je, na wewe utadanganywa? Kwa mufano, ikiwa mutu anapima kukusadikisha kama kanuni za Mungu kuhusu mwanaume kufanya ngono na mwanaume na mwanamuke kufanya ngono na mwanamuke haziko sawa, je, utakubali mawazo yake? Ao je, utakubali mawazo ya Yehova Mungu, mwenye Neno lake linaonyesha waziwazi kama wenye wanafanya matendo ya vile ‘wanatenda mambo machafu’? Mungu anatuonya kama hatupaswe kukubali matendo ya mubaya. (Ro. 1:24-27, 32) Wakati tunajikuta mbele ya mambo ya vile, ni muzuri tuwazie mu akili yetu hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono na ile milango mikubwa ya murefu na kukumbuka hivi: Mikazo ya dunia hii yenye kuharibika haiwezi kumufanya Yehova ashushe ao kuregeza kanuni zake za haki. Je, tunakubali mawazo ya Baba yetu wa mbinguni na kutetea mambo yenye iko sawa?

Tunatoa “zabihu ya sifa” wakati tunashiriki mu ibada safi

20. Washiriki wa “kundi kubwa” wanapata vikumbusho gani vyenye kutia moyo mu maono ya Ezekieli?

20 Viwanja. Wakati Ezekieli aliona kiwanja kikubwa cha inje cha hekalu, ile ilipaswa kumufanya afikirie waabudu wengi wa Yehova wenye furaha wenye wangeweza kukusanyika pale. Leo, Wakristo wanafanya ibada mu fasi yenye iko takatifu zaidi. Washiriki wa “kundi kubwa” wenye wanaabudu Yehova mu kiwanja cha inje cha hekalu la kiroho wanapata vikumbusho vyenye kutia moyo mu maono ya Ezekieli. (Ufu. 7:9, 10, 14, 15) Ezekieli aliona kwamba pembeni-pembeni ya vile viwanja kulikuwa vyumba vya kukulia chakula kwenye waabudu wangeweza kukulia sehemu ya zabihu za ushirika zenye walileta. (Eze. 40:17) Mu njia ya mufano, wangeweza kula chakula na Yehova Mungu​—ile ni alama ya urafiki wenye amani! Leo, hatutoe zabihu sawa vile Wayahudi walikuwa wanafanya chini ya Sheria ya Musa. Lakini, tunatoa “zabihu ya sifa” wakati tunashiriki mu ibada safi, kwa mufano, wakati tunatoa maelezo ku mikutano yetu na kusema maneno yenye kujaa imani na wakati tunahubiri. (Ebr. 13:15) Tunakulishwa pia chakula cha kiroho chenye Yehova anatoa. Bila shaka tunajisikia sawa vile wana wa Kora wenye walimuimbia Yehova hivi: “Siku moja katika viwanja vyako inapita siku elfu moja (1 000) mahali pengine popote!”​—Zb. 84:10.

21. Ukuhani mu maono ya Ezekieli unaweza kupatia Wakristo watiwa-mafuta fundisho gani?

21 Ukuhani. Ezekieli aliona kwamba makuhani na Walawi walikuwa wanaingia mu kiwanja cha ndani kupitia milango mikubwa, na ile milango ilifanana na milango mikubwa yenye makabila yenye haiko ya kikuhani ilikuwa inapitia juu ya kuingia mu kiwanja cha inje. Ile ilikuwa njia ya muzuri ya kukumbusha wanaume wa mu ile kikundi cha makuhani kwamba wao pia walipaswa kushika kanuni za Yehova za ibada safi. Halafu leo? Leo, hakuna watumishi wa Mungu wenye wanariti ukuhani, lakini Wakristo watiwa-mafuta wanaambiwa hivi: “Ninyi ni ‘jamii yenye ilichaguliwa, ukuhani wa kifalme.’” (1 Pe. 2:9) Makuhani wa Israeli ya zamani walikuwa wanafanya ibada mu kiwanja kingine. Leo, Wakristo watiwa-mafuta hawatenganishwe na waabudu wenzao mu njia fulani ya kimwili, lakini Yehova amewafanya kuwa wana wake, kwa hiyo wako na uhusiano wa pekee pamoja naye. (Gal. 4:4-6) Ijapokuwa vile, watiwa-mafuta wanaweza kupata vikumbusho vya maana mu maono ya Ezekieli. Kwa mufano, wanatambua kama, makuhani walipaswa pia kupewa mashauri na nizamu. Ni muzuri Wakristo wote wakumbuke kama tuko “kundi moja” lenye linatumika chini ya uongozi wa “muchungaji mumoja.”​—Soma Yohana 10:16.

22, 23. (a) Mukubwa mwenye kuzungumuziwa mu maono ya Ezekieli anaweza kupatia wazee Wakristo fundisho gani? (b) Ni nini inaweza kutokea mu wakati wenye kuja?

22 Mukubwa. Mu maono ya Ezekieli, mukubwa ni mutu wa maana kabisa. Haiko wa kabila la makuhani, na wakati iko ku hekalu, alipaswa kujitiisha ku uongozi wa makuhani. Lakini, anafanya kazi ya uangalizi kati ya watu na anawasaidia katika kuleta zabihu. (Eze. 44:2, 3; 45:16, 17; 46:2) Kwa hiyo, yeye ni mufano muzuri kwa wanaume Wakristo wenye wanatimiza madaraka fulani leo mu kutaniko. Wazee Wakristo, kutia ndani waangalizi wenye kusafiri, wanapaswa kuendelea kujitiisha kwa mutumwa muaminifu mwenye kutiwa mafuta. (Ebr. 13:17) Wazee wanatumika sana juu ya kusaidia watu wa Mungu watoe zabihu zao za sifa ku mikutano ya Kikristo na mu mahubiri. (Efe. 4:11, 12) Na namna Yehova alikaripia wakubwa wa Israeli juu ya kutumia mubaya mamlaka yao inaweza pia kupatia wazee somo fulani. (Eze. 45:9) Wazee hawapaswe kufikiri kama wao hawana lazima ya kushauriwa na kurekebishwa. Tofauti na ile, wanasamini wakati Yehova anawarekebisha sababu ile inawasaidia wakuwe wachungaji na waangalizi wazuri zaidi.​—Soma 1 Petro 5:1-3.

23 Mu dunia Paradiso yenye iko inakuja, Yehova ataendelea kuweka waangalizi wenye kustahili, na wenye upendo. Kwa kweli, wazee wengi leo wako wanapata mazoezi yenye itawasaidia wakafikie kuwa wachungaji wazuri na wenye kustahili mu Paradiso. (Zb. 45:16) Je, haipendeze sana kufikiria namna wale wanaume watakuwa baraka kwa wengine mu ulimwengu mupya? Kwa wakati wa Yehova wenye kufaa, tunaweza kuelewa mu njia yenye kuwa wazi zaidi maono ya Ezekieli, na maunabii ingine ya kurudishwa kwa ibada safi. Pengine sehemu fulani zitatimia mu njia ya ajabu mu siku zenye kuja, utimizo wenye hatuwezi kuelewa muzuri leo. Tuchunge tu.

Milango mikubwa ya murefu na viwanja vinatufundisha nini kuhusu ibada yetu? (Ona fungu la 18-21)

Baraka za Yehova Juu ya Ibada Safi

24, 25. Namna gani maono ya Ezekieli inaonyesha baraka zenye Yehova atapatia watu wake wakati wataendelea kushikamana na ibada safi?

24 Kwa kumalizia, tufikirie tena tukio kubwa lenye linatokea mu maono ya Ezekieli. Yehova anakuja mu hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono, na anaahidi watu wake kama ataendelea kukaa pale siku zote zenye watashikamana kwa uaminifu na kanuni zake kuhusu ibada safi. (Eze. 43:4-9) Kuwapo kwa Yehova kungekuwa na matokeo gani juu ya watu na juu ya inchi yao?

25 Maono inazungumuzia baraka za Mungu kwa kutumia semi mbili za mufano zenye kutia moyo: (1) Muto unatiririka kutoka mu kiwanja cha hekalu, unatoa uzima na kufanya inchi ikuwe na mbolea; na (2) inchi inagawanywa kwa utaratibu, kwa ukamili, hekalu na viwanja vyake viko katikati kabisa. Zile semi za mufano ziko na maana gani leo? Tunaishi wakati wenye Yehova ametokeza, amesafisha, na kukubali namna ya ibada yenye iko takatifu zaidi, ni kusema, hekalu kubwa la kiroho. (Mal. 3:1-4) Tutazungumuzia zile semi mbili za mufano mu Sura ya 19 mupaka 21 ya kitabu hiki.

^ fu. 6 Mu ile njia, Yehova alikuwa anaonyesha tofauti kati ya namna watu wake walitendea zamani nyumba yake takatifu: “Kwa kutia kizingiti chao karibu na kizingiti changu na mwimo wa mulango wao pembeni ya mwimo wa mulango wangu, tukitenganishwa tu na ukuta kati yangu na wao, walichafua jina langu takatifu kupitia mambo yenye kuchukiza.” (Eze. 43:8) Mu Yerusalemu ya zamani, mulikuwaka ukuta moja tu wenye ulikuwa unatenganisha hekalu la Yehova na nyumba zingine. Wakati watu waliacha kufuata kanuni za haki za Yehova, walileta uchafu wao, ibada yao ya sanamu, juu tu ya kuzaraulisha nyumba ya Yehova. Ile hali haikupaswa kuendelea!

^ fu. 13 Maono ya Ezekieli ya hekalu inahusiana pia na maunabii ingine ya kurudishwa kwa ibada safi yenye imetimia mu siku za mwisho. Kwa mufano, ona mambo yenye inafanana kati ya Ezekieli 43:1-9 na Malaki 3:1-5; Ezekieli 47:1-12 na Yoeli 3:18.

^ fu. 18 Hekalu la kiroho lilianza mu mwaka wa 29 K.K.Y. wakati Yesu alibatizwa na kuanza kazi yake ya Kuhani Mukubwa. Lakini, ibada safi ilipuuzwa sana ku dunia mu miaka mingi kisha kifo cha mitume wa Yesu. Ni zaidi sana kuanzia mwaka wa 1919 njo ibada safi iliinuliwa.