Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 4

“Viumbe Vyenye Uzima Vyenye Viko na Nyuso Ine” Ni Nani?

“Viumbe Vyenye Uzima Vyenye Viko na Nyuso Ine” Ni Nani?

EZEKIELI 1:15

WAZO KUBWA: Viumbe vyenye viko na uzima na mambo yenye vinatufundisha

1, 2. Juu ya nini Yehova alitumia wakati fulani vitu vyenye kuonekana juu ya kufundisha watumishi wake wa ku dunia kweli fulani?

WAZIA familia yenye kuwa na watoto kidogo wenye kukaa kuzunguka meza ya mafiga yao na wako wanajifunza Biblia. Juu ya kusaidia watoto waelewe kweli moja hivi ya Biblia, baba anawaonyesha michoro fulani. Watoto wanaonyesha uso wa furaha na wanatoa maelezo ya kufurahisha, ile inaonyesha kama Baba ameweza kabisa. Kwa kutumia picha wakati anazungumuza nao, anasaidia watoto wake waelewe mafundisho kuhusu Yehova yenye hawangeweza kuelewa kwa sababu miaka yao ingali kidogo.

2 Vilevile, Yehova ametumia vitu vyenye kuonekana juu ya kusaidia watoto wake wa kibinadamu waelewe mambo yenye haionekane yenye hawawezi kuelewa mu njia ingine. Kwa mufano, juu ya kufasiria kweli fulani nzito kuhusu yeye mwenyewe, Yehova alionyesha Ezekieli maono yenye kujaa picha za kushangaza. Mu sura yenye ilitangulia ya kitabu hiki, tulizungumuzia picha moja ya vile. Kwa sasa, tukazie uangalifu sehemu moja ya ile maono ya kushangaza sana na tuone namna kuelewa maana yake kunaweza kutusaidia tumukaribie Yehova zaidi.

“Niliona . . . Kitu Chenye Kilifanana na Viumbe Ine Vyenye Uzima”

3. (a) Kulingana na Ezekieli 1:4, 5, Ezekieli aliona nini mu maono? (Ona picha ku mwanzo wa habari.) (b) Unatambua nini kuhusu namna ya Ezekieli ya kuandika mambo yenye aliona?

3 Soma Ezekieli 1:4, 5. Ezekieli anaeleza kama “kitu chenye kilifanana na viumbe ine vyenye uzima” kilikuwa na uso wa malaika, wa mutu, na wa nyama. Ona kile Ezekieli aliandika kabisa kuhusu mambo yenye aliona, alisema kama aliona “kitu chenye kilifanana na” viumbe vyenye uzima. Wakati utasoma maono yote yenye kupatikana mu Ezekieli sura ya 1, utatambua kwamba nabii huyu anatumia sana maneno kama vile “-onekana kama,” “-kuwa kama,” “-fanana na.” (Eze. 1:13, 24, 26) Ile inaonyesha kama, Ezekieli alitambua kwamba aliona mambo yenye kufanana tu, ao picha tu, ya mambo yenye haionekane yenye iko mbinguni.

4. (a) Ile maono ilikuwa na matokeo gani juu ya Ezekieli? (b) Inawezekana Ezekieli alijua nini kuhusu makerubi?

4 Ezekieli alipaswa kushangaa sana juu ya mambo yenye aliona na kusikia mu ile maono. Vile viumbe ine vyenye uzima vilionekana kama “makaa ya moto yenye kuwaka.” Mwendo wa haraka wa vile viumbe ulifanana na “umeme wa radi.” Mabawa ya vile viumbe ilitosha sauti “kama sauti ya maji yenye kuteremuka haraka” na mwendo wa vile viumbe ulikuwa “kama sauti ya jeshi.” (Eze. 1:13, 14, 24-28; ona kisanduku “Nilikuwa Ninaangalia Viumbe Hivyo Vyenye Uzima.”) Mu maono yenye alipata kisha, Ezekieli alionyesha kama vile viumbe ine vyenye uzima ni “makerubi,” ao viumbe vyenye nguvu, ni kusema, malaika. (Eze. 10:2) Juu alikomalia mu familia ya kikuhani, bila shaka Ezekieli alijua kama makerubi wanapatikana karibu na Yehova na wanamutumikia wakiwa wajumbe wake.​—1 Ny. 28:18; Zb. 18:10.

“Kila Kimoja cha Viumbe Hivyo Kilikuwa na Nyuso Ine”

5. (a) Juu ya nini makerubi na nyuso zao ine wanaonyesha kama uwezo na utukufu wa Yehova ni mukubwa sana? (b) Juu ya nini sehemu hii ya maono inatukumbusha maana ya jina la Mungu? (Ona maelezo.)

5 Soma Ezekieli 1:6, 10. Ezekieli aliona pia kwamba kila kerubi alikuwa na nyuso ine​—uso wa mwanadamu, wa simba, wa ngombe-dume, na uso wa tai. Kuona zile nyuso ine kulipaswa kufundisha Ezekieli kwamba uwezo na utukufu wa Yehova ni mukubwa sana na hauna mipaka. Juu ya nini tunasema vile? Juu, kila uso ulikuwa wa kiumbe chenye kufananisha ukubwa, nguvu na uwezo. Simba ni munyama mukubwa wa pori, ngombe-dume ni munyama wa kufugwa wa kushangaza, tai ni ndege mwenye nguvu, na mwanadamu njo kazi ya mwisho ya uumbaji wa Mungu ku dunia, na yeye njo mutawala wa viumbe vingine vyote ku dunia. (Zb. 8:4-6) Lakini, mu maono hii, Ezekieli aliona kwamba viumbe ine vyenye nguvu vyenye kufananisha uumbaji, kama vile nyuso ine za kila kerubi zinaonyesha, vilikuwa chini ya kiti cha ufalme cha Yehova, Mutawala Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi. Ile ni njia yenye kufaa kabisa ya kuonyesha kama Yehova anaweza kutumia uumbaji wake juu ya kutimiza kusudi lake! * Kusema kweli, kama vile muandikaji wa zaburi alisema kuhusu Yehova, “ukubwa wake uko juu ya dunia na mbingu.”​—Zb. 148:13.

Viumbe ine vyenye uzima na nyuso ine za vile viumbe vinaonyesha nini kuhusu uwezo, utukufu na sifa za Yehova? (Ona fungu la 5, 13)

6. Pengine ni nini ilimusaidia Ezekieli aelewe kile nyuso ine zinafananisha?

6 Kisha kupita wakati fulani na kisha Ezekieli kufikiri kuhusu mambo yenye aliona, inawezekana alikumbuka kwamba watumishi wa Mungu wenye waliishi mbele ya wakati wake walikuwa wanatumia wanyama fulani juu ya kulinganisha mambo. Kwa mufano, muzee wa ukoo Yakobo alilinganisha mwana wake Yuda na simba na alilinganisha mwana wake Benyamini na imbwa wa pori. (Mwa. 49:9, 27) Juu ya nini? Juu, simba na imbwa wa pori wanafananisha sifa, ao tabia fulani, zenye wale wanaume wangeonyesha mu utu wao. Mu akili yake, Ezekieli alijua ile mifano yenye inatoka mu Maandiko ya Musa yenye iliongozwa na roho ya Mungu, kwa hiyo, inawezekana alifikia kutambua kwamba nyuso za wale makerubi zilifananisha pia sifa fulani ao tabia fulani za pekee. Sifa gani?

Sifa za Yehova na za Familia Yake ya Mbinguni

7, 8. Mara mingi imefasiriwa kwamba nyuso ine za wale makerubi zinafananisha sifa gani?

7 Waandikaji wa Biblia wenye waliishi mbele ya wakati wa Ezekieli walikuwa wanafikiri kwamba simba, tai, na ngombe-dume wanaonyesha sifa gani? Ona mistari hii ya Biblia: “Mwanaume hodari mwenye moyo wake uko kama wa simba.” (2 Sa. 17:10; Mez. 28:1) “Tai anapanda juu,” na “macho yake yanaona mbali sana.” (Yob. 39:27, 29) “Nguvu za ngombe-dume zinaleta mavuno mengi.” (Mez. 14:4) Kufuatana na ile maandiko, vichapo vyetu vimefasiria mara mingi kwamba uso wa simba unafananisha haki yenye uhodari; uso wa tai, hekima yenye kuona mbali; uso wa ngombe-dume, nguvu yenye haiwezi kuzuiwa.

8 Lakini, tuseme nini kuhusu “uso wa mutu”? (Eze. 10:14) Unapaswa kufananisha sifa yenye haiwezi kuonyeshwa na munyama fulani, lakini yenye inaweza kuonyeshwa na wanadamu, wenye waliumbwa kwa mufano wa Mungu. (Mwa. 1:27) Ile sifa​—yenye wanadamu tu njo wako nayo hapa ku dunia—​inaonyeshwa katika amri hizi za Mungu: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote” na “unapaswa kumupenda mwenzako kama wewe mwenyewe.” (Kum. 6:5; Law. 19:18) Wakati tunatii amri hizi kwa kuonyesha upendo wenye hauna choyo, tunaonyesha upendo wa Yehova mwenyewe. Kama vile mutume Yohana aliandika, “sisi tunapenda, kwa sababu alitupenda kwanza.”(1 Yoh. 4:8, 19) Kwa hiyo, “uso wa mutu” unafananisha upendo.

9. Sifa zenye kufananishwa na nyuso za wale makerubi ine ni za nani?

9 Zile sifa zote ni za nani? Kwa sababu nyuso ni za makerubi, zile sifa ni za wale wote wenye wale makerubi wanafananisha, ni kusema, familia ya mbinguni ya Yehova ya viumbe viaminifu vya roho. (Ufu. 5:11) Zaidi ya ile, kwa sababu Yehova njo Chanzo cha uzima wa wale makerubi, yeye pia njo Chanzo cha sifa zao. (Zb. 36:9) Kwa hiyo, nyuso za wale makerubi zinaonyesha sifa za Yehova mwenyewe. (Yob. 37:23; Zb. 99:4; Mez. 2:6; Mik. 7:18) Ni mu njia gani Yehova anaonyesha zile sifa za pekee?

10, 11. Ni mu njia gani tunapata faida kutokana na namna Yehova anaonyesha zile sifa ine kubwa?

10 Haki. Kwa sababu yeye ni Mungu mwenye “anapenda haki,” Yehova “hamutendee mutu yeyote kwa upendeleo.” (Zb. 37:28; Kum. 10:17) Kwa hiyo, kila mutu, akuwe wa hali gani ao wa inchi gani, anaweza kuwa na kuendelea kuwa mutumishi wake na kupata baraka za milele. Hekima. Kwa sababu yeye ni Mungu “mwenye hekima katika moyo,” Yehova ametupatia kitabu chenye kujaa “hekima yenye kutenda.” (Yob. 9:4; Mez. 2:7) Kutumikisha mashauri ya Biblia yenye hekima kunatusaidia kupambana na magumu ya maisha ya kila siku na kunatusaidia tuishi maisha yenye kusudi. Nguvu. Kwa sababu yeye ni Mungu “mwenye nguvu nyingi,” Yehova anatumia roho yake takatifu juu ya kutupatia “nguvu zenye kupita zile za kawaida.” Roho yake inatupatia uwezo wa kupambana na majaribu yoyote makali na ya kuumiza yenye tunaweza kupata.​—Nah. 1:3; 2 Ko. 4:7; Zb. 46:1.

11 Upendo. Kwa sababu yeye ni Mungu “mwenye upendo mwingi mushikamanifu,” Yehova hawezi kuacha hata kidogo waabudu wake waaminifu. (Zb. 103:8; 2 Sa. 22:26) Kwa hiyo, hata kama tuko na huzuni kwa sababu magumu ya afya ao uzee vinatuzuia kufanya mambo mingi mu kazi ya Yehova sawa vile zamani, tunapata kitulizo kwa kujua kama Yehova anaendelea kukumbuka kazi za upendo zenye tulimufanyia zamani. (Ebr. 6:10) Kusema kweli, namna Yehova ameonyesha haki, hekima, nguvu na upendo tayari imetuletea faida, na zile sifa ine kubwa zitaendelea kutuletea faida mu siku zenye kuja.

12. Ni nini hatupaswe kusahau kuhusu uwezo wetu wa kuelewa sifa za Yehova?

12 Lakini, tusisahau kama, juu tuko wanadamu, mambo yenye tunaweza kuelewa kuhusu sifa za Yehova ni “sehemu za pembeni-pembeni tu za njia zake.” (Yob. 26:14) “Hatuwezi kumuelewa kabisa Mweza-Yote,” sababu “ukubwa wake hauchunguzike.” (Yob. 37:23; Zb. 145:3) Kwa hiyo, tunatambua kama hatuwezi kujua hesabu kamili ya sifa za Yehova na hatuwezi kuzipanga mu vikundi-vikundi. (Soma Waroma 11:33, 34.) Maono ya Ezekieli peke yake inaonyesha kwamba sifa za Yehova hazina hesabu wala mwisho. (Zb. 139:17, 18) Ni sehemu gani ya maono yenye inakazia ile jambo?

Nyuso Ine . . . Mabawa Ine . . . Pande Ine”

13, 14. Nyuso ine za makerubi zinafananisha nini, na juu ya nini tunasema vile?

13 Mu maono, Ezekieli aliona kwamba kila kerubi, hakukuwa na uso moja, lakini nyuso ine. Ile inaonyesha nini? Kumbuka kwamba, mu Neno la Mungu, namba ine inatumiwa mara mingi juu ya kufananisha kitu cha kuenea kabisa, chenye kutia ndani kila kitu, ao chenye kuwa kamili. (Isa. 11:12; Mt. 24:31; Ufu. 7:1) Inapendeza kwamba, mu maono hii, Ezekieli anataja namba ine zaidi ya mara 10! (Eze. 1:5-18) Tuseme nini sasa? Kama vile wale makerubi ine wanafananisha viumbe vingine vyote viaminifu vya roho, vilevile, nyuso ine za wale makerubi wakati tunazitia zote pamoja tunaona kwamba zinafananisha, ao zinatia ndani, sifa zote zenye Yehova iko nazo. *

14 Juu ya kuonyesha namna nyuso za wale makerubi ine zinafananisha zaidi ya zile sifa ine, fikiria kwa mufano, kile kinatendeka kuhusu ile magurudumu ine mu maono. Kila gurudumu ni la kushangaza, lakini wakati tunatia ile magurudumu yote pamoja, tunaona kwamba haifanyize magurudumu ine tu ya kushangaza. Lakini, ile magurudumu ine njo musingi wenye ile gari inaikalia. Vilevile, wakati tunatia zile nyuso ine pamoja, tunaona kwamba hazifanyize sifa ine tu za kushangaza. Lakini, zile sifa ine njo musingi wa utu wa Yehova wa kushangaza sana.

Yehova Iko Karibu na Watumishi Wake Wote Waaminifu

15. Ni kweli gani ya kutia moyo yenye Ezekieli alijifunza mu maono ya kwanza yenye alipata?

15 Kupitia maono hii ya kwanza, Ezekieli alijifunza kweli fulani ya maana na yenye kutia moyo kuhusu uhusiano wake na Yehova. Kweli gani? Ile kweli inapatikana mu maneno ya kwanza ya kitabu chake cha unabii. Kisha kusema kama alikuwa “katika inchi ya Wakaldayo,” Ezekieli, anaonyesha jambo lenye lilimufikia yeye mwenyewe, kwa kuongeza hivi: “Pale, mukono wa Yehova ukakuja juu yake.” (Eze. 1:3) Ona kama Ezekieli alisema kwamba alipokea maono, hapana kule Yerusalemu, lakini pale​—mu Babiloni. * Kwa hiyo, ile ilisaidia Ezekieli kuelewa nini? Ilimusaidia kuelewa kwamba, hata kama alikuwa muhamishwa wa hali ya chini mwenye alikuwa amepelekwa mbali na Yerusalemu na hekalu lake, hakukuwa amepelekwa mbali na Yehova na ibada Yake. Yehova alimutokea Ezekieli mu Babiloni. Ile ilionyesha kama hata mutu akuwe mu hali gani ao fasi gani anaweza kumutolea Mungu ibada safi. Kuhusu Ezekieli, iliomba tu akuwe na hali ya muzuri ya moyo na tamaa ya kumutumikia Yehova.

16. (a) Ni uhakikisho gani wenye kufariji wenye tunaweza kupata mu maono ya Ezekieli? (b) Ni nini inakuchochea umutumikie Yehova kwa moyo wako wote?

16 Juu ya nini ile kweli yenye Ezekieli alijifunza inatufariji sana leo? Juu, inatuhakikishia kama wakati tunamutumikia Yehova kwa moyo wetu wote, yeye iko karibu na sisi hata tukuwe wapi, hata tuvunjike moyo namna gani, ao tukuwe mu hali gani za maisha. (Zb. 25:14; Mdo. 17:27) Yehova hachokake haraka kutusaidia kwa sababu upendo wake mwingi mushikamanifu unamuchochea kusaidia kila mumoja wa watumishi wake. (Kut. 34:6) Kwa hiyo, Yehova anaweza kukuonyesha upendo wake mushikamanifu hata ukuwe mu hali gani ao fasi gani. (Zb. 100:5; Ro. 8:35-39) Zaidi ya ile, maono hii ya kushangaza yenye kuonyesha utakatifu wa Yehova na uwezo wake mukubwa sana inatukumbusha kama Yehova njo anastahili kupokea ibada yetu. (Ufu. 4:9-11) Kwa kweli, tuko wenye shukrani sana kwa sababu Yehova alitumia maono hii juu ya kutusaidia kuelewa kweli fulani za maana juu yake na juu ya sifa zake! Kuelewa muzuri zaidi sifa za Yehova zenye kupendeza kunatufanya tumukaribie zaidi na kunatuchochea kumusifu na kumutumikia kwa moyo wetu wote na kwa nguvu zetu zote.​—Lu. 10:27.

Yehova anaweza kutuonyesha upendo wake mushikamanifu hata tukuwe mu hali gani ao fasi gani (Ona fungu la 16)

17. Tutazungumuzia maulizo gani mu sura za kufuata?

17 Lakini, ya kuhuzunisha ni kwamba, mu siku za Ezekieli, ibada safi ilichafuliwa na kuzarauliwa. Namna gani ilifikia kuwa vile? Yehova alifanya nini? Na ile matukio ya zamani inaweza kutufundisha nini leo? Tutazungumuzia ile maulizo mu sura za kufuata.

^ fu. 5 Maelezo ya Ezekieli kuhusu vile viumbe inatukumbusha jambo fulani kuhusu jina la Mungu, Yehova, lenye tunaelewa kama linamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” Kama vile sehemu moja ya maana ya ile jina inaonyesha, Yehova anaweza kufanya uumbaji wake ukuwe kitu chochote chenye inaomba juu ya kutimiza kusudi lake.​—Ona Nyongeza A4 mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

^ fu. 13 Mu miaka mingi, vichapo vyetu vimezungumuzia sifa karibu 50 za Yehova.​—Ona Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova chini ya kichwa “Yehova,” kichwa kidogo “Sifa za Yehova.”

^ fu. 15 Neno “pale,” kulingana na mutu moja mwenye kutoa maelezo juu ya Biblia, “linavuta uangalifu sana kuhusu ile wakati kuliko neno lingine lolote. . . . Mungu iko pale mu Babiloni! Ile inafariji sana!”