Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA PILI

“Ni Patakatifu Pangu Ndipo Mulichafua”​—Ibada Safi Inachafuliwa

“Ni Patakatifu Pangu Ndipo Mulichafua”​—Ibada Safi Inachafuliwa

EZEKIELI 5:11

WAZO KUBWA: Wakaaji wa Yuda na Yerusalemu wanapotoka kiroho na mu mwenendo

Yehova alipenda na kuhangaikia Waisraeli kwa sababu walikuwa ‘mali yake yenye alipendezwa nayo sana.’ (Kut. 19:5, maelezo ya chini) Lakini kile wao walimulipa ni kuabudu miungu ya uongo mu hekalu lenye lilijulikana kuwa la Yehova! Walimuhuzunisha sana Yehova na kumuzaraulisha. Juu ya nini Waisraeli walipotoka sana vile? Unabii wa Ezekieli kuhusu kuharibiwa kwa Yerusalemu unaweza kutufundisha nini? Uhusiano wenye Waisraeli walifanya na mataifa yenye ilikuwa inawazunguka unaweza kutupatia somo gani?

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 5

“Uone Mambo Maovu, Yenye Kuchukiza Yenye Wanafanya”

Ezekieli anaona hali za kuchukiza zenye zinaonyesha namna taifa lote lilikuwa limeharibika kiroho.

SURA YA 6

“Sasa Mwisho Uko Juu Yako”

Maonyesho ya unabii ya Ezekieli ilionyesha namna Yehova angeleta hukumu yake kali juu ya Yerusalemu.

SURA YA 7

Mataifa “Yatalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”

Mataifa yenye ilikuwa inasema mubaya juu ya jina la Yehova na kutesa ao kupotosha watu wake haingekosa kupata matokeo ya matendo yao. Uhusiano wenye Israeli alifanya na ile mataifa unaweza kutupatia somo gani?