Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 7

Mataifa “Yatalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”

Mataifa “Yatalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”

EZEKIELI 25:17

WAZO KUBWA: Mambo yenye tunajifunza kutokana na uhusiano wenye Israeli alifanya na mataifa yenye kuzarau jina la Yehova

1, 2. (a) Ni nini inaonyesha kama Israeli alikuwa sawa vile kondoo mwenye kuwa peke yake kati ya imbwa wa pori? (Ona picha ku mwanzo wa habari.) (b) Waisraeli na wafalme wao waliacha mambo gani itokee?

MU MIAKA mingi, Israeli alikuwa sawa vile kondoo mwenye iko peke yake kati ya kundi la imbwa wa pori. Waamoni, Wamoabu, na Waedomu walisumbua Israeli ku mupaka wake wa mashariki. Wafilisti, maadui wa siku mingi wa Israeli, walikuwa upande wa mangaribi. Ku upande wa kaskazini kulikuwa muji wa Tiro, muji tajiri na mahali pa maana pa biashara kubwa. Ku upande wa kusini kulikuwa taifa la zamani la Misri, lenye liliongozwa na mufalme Farao, mwenye alionwa kuwa mungu.

2 Wakati Waisraeli walimutegemea Yehova, aliwalinda kutokana na maadui wao. Lakini, mara mingi, watu wake na wafalme wao waliacha mataifa yenye kuwazunguka iwapotoshe. Mufalme Ahabu ni mufano moja tu wa watu wenye waliacha wengine wawachochee juu wasishikamane na Yehova. Aliishi wakati moja na Mufalme Yehoshafati wa Yuda, na alitawala ufalme wa makabila kumi wa Israeli. Alioa binti ya mufalme wa Sidoni mwenye alitawala muji tajiri wa Tiro. Ule mwanamuke, mwenye kuitwa Yezebeli, aliendelesha kwa bidii ibada ya Baali mu Israeli na alichochea bwana yake achafue ibada safi mu njia yenye haiyakuwaka.​—1 Fa. 16:30-33; 18:4, 19.

3, 4. (a) Sasa Ezekieli alikazia uangalifu wake juu ya nani? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

3 Yehova alikuwa ameonya watu wake kuhusu matokeo ya kukosa kushikamana naye. Sasa, uvumilivu wake ulifikia mwisho. (Yer. 21:7, 10; Eze. 5:7-9) Mu mwaka wa 609 M.K.Y., jeshi la Babiloni lilirudia mu Inchi ya Ahadi kwa mara ya tatu. Miaka karibu kumi ilikuwa imepita tangu shambulizi lao la mwisho. Mara hii, walibomoa kuta za Yerusalemu na kuponda-ponda watu wenye waliasi Nebukadneza. Wakati Yerusalemu ilianza kuzungukwa kwa ajili ya vita na maneno ya unabii ya Ezekieli ikatimia mu njia ya kuhuzunisha, nabii Ezekieli alikazia uangalifu wake juu ya mataifa yenye ilikuwa pembeni-pembeni ya Inchi ya Ahadi.

Mataifa yenye ilizarau jina la Yehova haingeponyoka matokeo ya matendo yao

4 Yehova alifunulia Ezekieli kama maadui wa Yuda watafurahi sana wakati Yerusalemu itaharibiwa na watatesa wale wenye wataponyoka. Lakini ile mataifa yenye ilizarau jina la Yehova na kutesa ao kupotosha watu wake haingekosa kupata matokeo ya matendo yao. Uhusiano wenye Israeli alifanya na ile mataifa unaweza kutupatia somo gani? Na namna gani maunabii ya Ezekieli kuhusu ile mataifa inatupatia tumaini leo?

Watu wa Jamaa ya Israeli Wenye Walimutendea kwa “Zarau Kamili”

5, 6. Kulikuwa uhusiano gani kati ya Waamoni na Waisraeli?

5 Amoni, Moabu, na Edomu walikuwa, mu njia fulani, na uhusiano wa damu na Israeli. Ijapokuwa uhusiano wao wa jamaa na historia moja, ile mataifa ilichukia watu wa Mungu kwa muda murefu na iliwatendea kwa “zarau kamili.”​—Eze. 25:6.

6 Fikiria Waamoni. Walitokana na Loti kupitia binti yake mudogo. Loti alikuwa mutoto ya ndugu ya Abrahamu. (Mwa. 19:38) Luga yao ilifanana sana na Kiebrania, na kwa hiyo watu wa Mungu wangeweza kuielewa. Sababu ya ile uhusiano wa jamaa, Yehova aliambia Waisraeli wasianzishe vita na Amoni. (Kum. 2:19) Lakini, mu siku za Waamuzi, Waamoni walijiunga na Egloni, mufalme wa Moabu, juu ya kutesa Israeli. (Amu. 3:12-15, 27-30) Kisha, wakati Sauli alifanywa kuwa mufalme, Waamoni walishambulia Israeli. (1 Sa. 11:1-4) Na mu siku za Mufalme Yehoshafati, walijiunga tena na Moabu juu ya kuvamia Inchi ya Ahadi.​—2 Ny. 20:1, 2.

7. Wamoabu walitendea namna gani watu wa jamaa yao, wazao wa Israeli?

7 Wamoabu pia walikuwa wazao wa Loti, lakini kupitia binti yake mukubwa. (Mwa. 19:36, 37) Yehova aliambia Waisraeli wasipigane na Moabu. (Kum. 2:9) Lakini Wamoabu hawakutendea Israeli kwa wema. Kuliko kusaidia watu wa jamaa yao, wenye walikuwa wanaponyoka utumwa kule Misri, walijaribu kuwazuia wasiingie mu Inchi ya Ahadi. Balaki, mufalme wa Moabu, alilipa Balaamu juu alaani Waisraeli, na Balaamu alifundisha Balaki namna ya kuchochea wanaume wa Israeli wafanye uasherati na pia ibada ya sanamu. (Hes. 22:1-8; 25:1-9; Ufu. 2:14) Mu miaka mingi Wamoabu waliendelea kutesa watu wa jamaa yao, mupaka siku za Ezekieli.​—2 Fa. 24:1, 2.

8. Juu ya nini Yehova alisema kama Edomu alikuwa ndugu ya Israeli, lakini Waedomu walitenda je?

8 Waedomu walikuwa wazao wa Esau, ndugu-pacha wa Yakobo. Uhusiano kati yao na Israeli ulikuwa wa karibu sana kiasi ya kwamba Yehova aliita Waedomu kuwa ndugu za Waisraeli. (Kum. 2:1-5; 23:7, 8) Ijapokuwa ile yote, mara mingi Waedomu walipinga Waisraeli kuanzia wakati walitoka Misri mupaka wakati wa kuharibiwa kwa Yerusalemu mu mwaka wa 607 M.K.Y. (Hes. 20:14, 18; Eze. 25:12) Ile wakati, Waedomu walifurahi sana juu ya mateso ya Israeli, walitia moyo Wababiloni waharibu Yerusalemu na kuifanya kuwa ukiwa, lakini pia walifungia njia Waisraeli wenye walikuwa wanakimbia na waliwatia mu mukono wa adui.​—Zb. 137:7; Oba. 11, 14.

9, 10. (a) Ni nini ilipata Amoni, Moabu, na Edomu? (b) Ni mifano gani inaonyesha kama watu wote wa ile mataifa hawakuchukia Israeli?

9 Yehova alihukumu ile mataifa yote yenye ilikuwa na uhusiano wa damu na Israeli kuhusu namna ilitendea watu Wake. Alisema: ‘Nitatoa . . . Waamoni kuwa mali ya watu wa Mashariki, ili Waamoni wasikumbukwe kati ya mataifa.’ Alisema tena hivi: “Nitafanya hukumu katika Moabu, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Eze. 25:10, 11) Miaka tano hivi kisha Yerusalemu kuanguka, ile maunabii ilianza kutimia wakati Wababiloni walishinda Amoni na Moabu. Kuhusu Edomu, Yehova alisema kama ‘ataondoa ndani yake mwanadamu na mifugo’ na kama ‘ataifanya ikuwe ukiwa.’ (Eze. 25:13) Kama vile ilitabiriwa, Amoni, Moabu, na Edomu ilifikia mwisho, na haikukuwa tena.​—Yer. 9:25, 26; 48:42; 49:17, 18.

10 Lakini, haiko kusema kama watu wote wa ile mataifa walichukia watu wa Mungu. Kwa mufano, Seleki Mwamoni na Itma Mumoabu, wanatajwa kati ya wapiganaji-vita wenye nguvu wa Mufalme Daudi. (1 Ny. 11:26, 39, 46; 12:1) Na Rutu Mumoabu alifikia kuwa muabudu mushikamanifu wa Yehova.​—Rut. 1:4, 16, 17.

Usijiachilie hata kidogo

11. Uhusiano wenye Israeli alifanya na Amoni, Moabu, na Edomu unaweza kutupatia somo gani?

11 Uhusiano wenye Israeli alifanya na ile mataifa unaweza kutupatia somo gani? Kwanza, wakati Israeli alikosa kuwa muangalifu, aliambukizwa na desturi zenye kupotosha za dini ya uongo ya watu wa jamaa yake, kama vile ibada ya mungu wa Moabu mwenye kuitwa Baali wa Peori na ya Moleki mungu wa Waamoni. (Hes. 25:1-3; 1 Fa. 11:7) Hali kama ile inaweza kutufikia. Watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi wanaweza kutuchochea tutende tofauti na vile tunaamini. Kwa mufano, wanaweza kushindwa kuelewa juu ya nini hatufanyake Pasaka, juu ya nini hatupatianake zawadi siku ya Noeli, ao kufanya desturi zingine zenye kupendwa sana zenye zinapatana na imani ya dini ya uongo. Bila kuwa na nia ya mubaya, wanaweza kujaribu kutufanya tuvunje kanuni zetu, hata kwa kiasi kidogo. Lakini, ni muzuri tusijiachilie hata kidogo! Kama vile historia ya Israeli inaonyesha, kujiachilia hata kwa kiasi kidogo tu kunaweza kuharibisha urafiki wetu na Yehova.

12, 13. Ni nani wanaweza kutupinga, lakini itakuwa namna gani kama tunaendelea kuwa washikamanifu?

12 Uhusiano wenye Israeli alifanya na Amoni, Moabu, na Edomu unaweza kutupatia somo ingine. Watu wa familia wenye hawako Mashahidi wanaweza kutupinga. Yesu alionya kama wakati fulani ujumbe wenye tunahubiri unaweza “kuleta mugawanyiko, kati ya mwana na baba yake, kati ya binti na mama yake.” (Mt. 10:35, 36) Yehova aliagiza Waisraeli wasipigane na watu wa jamaa yao, na sisi pia hatupaswe kutafuta mihali ao ugomvi na watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi. Lakini hatupaswe kushangaa wakati kunakuwa upinzani.​—2 Ti. 3:12.

13 Hata kama watu wa jamaa yetu hawapinge moja kwa moja ibada yenye tunamutolea Yehova, hatupaswe kuwaacha wakuwe na uvutano mukubwa juu yetu kuliko Yehova. Juu ya nini tunasema vile? Juu, Yehova njo anastahili kuchukua nafasi ya kwanza mu moyo wetu. (Soma Matayo 10:37.) Tena, kama tunaendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova, watu fulani wa jamaa yetu wanaweza kuwa kama Seleki, Itma, na Rutu na kujiunga na sisi mu ibada safi. (1 Ti. 4:16) Kisha wao pia watapata furaha ya kumutumikia Mungu moja tu wa kweli na yeye atawapenda na kuwalinda.

Maadui wa Yehova Walipata “Azabu Kali”

14, 15. Wafilisti walitendea Waisraeli je?

14 Wafilisti walikuwa wametoka ku kisiwa cha Krete na kuhamia mu inchi yenye kisha muda fulani Yehova aliahidi kupatia Abrahamu na wazao wake. Abrahamu na Isaka walifanya uhusiano fulani na Wafilisti. (Mwa. 21:29-32; 26:1) Kufikia wakati Waisraeli waliingia mu Inchi ya Ahadi, Wafilisti walikuwa wameongezeka na kuwa taifa lenye nguvu na walikuwa na jeshi la kuogopesha. Waliabudu miungu ya uongo, sawa vile Baal-zebubu na Dagoni. (1 Sa. 5:1-4; 2 Fa. 1:2, 3) Wakati fulani Israeli alijiunga nao kwa kuabudu ile miungu.​—Amu. 10:6.

15 Kwa sababu Israeli alikosa uaminifu, Yehova aliruhusu Wafilisti watawale watu wake mu miaka mingi. (Amu. 10:7, 8; Eze. 25:15) Walitilia Waisraeli sheria za kuwakandamiza * na kuua wengi kati yao. (1 Sa. 4:10) Lakini, wakati Waisraeli walitubu na kumurudilia Yehova, aliwaokoa. Alitokeza wanaume sawa vile Samsoni, Sauli, na Daudi juu ya kuokoa watu Wake. (Amu. 13:5, 24; 1 Sa. 9:15-17; 18:6, 7) Na kama vile Ezekieli alitabiri, Wafilisti walipokea “azabu kali” wakati Wababiloni na baadaye Wagiriki walivamia inchi yao.​—Eze. 25:15-17.

16, 17. Uhusiano wenye Israeli alifanya na Wafilisti unaweza kutupatia somo gani?

16 Uhusiano wenye Israeli alifanya na Wafilisti unaweza kutupatia somo gani? Watu wa Yehova leo wamepambana na upinzani kutoka kwa mataifa yenye nguvu kuliko mataifa yoyote yenye imekwisha kutawala wanadamu. Tofauti na Israeli, sisi tumeendelea kushikamana sana na Yehova. Ijapokuwa vile, wakati fulani inaweza kuonekana kama maadui wa ibada safi wamepata ushindi. Kwa mufano, ku mwanzo wa karne ya 20 (1901-2000), guvernema ya États-Unis ilijaribu kusimamisha kazi ya watu wa Yehova kwa kukatia wale wenye walikuwa wanaongoza tengenezo miaka mingi ya kufungwa mu gereza. Wakati wa vita ya pili ya ulimwengu, chama cha Nazi kule Ujerumani kilitafuta kumaliza watu wa Mungu, kwa kufunga maelfu na kuua mamia kati yao. Kisha ile vita, Muungano wa Sovieti ulianzisha kampanye ya miaka mingi ya kushambulia Mashahidi wa Yehova, kwa kutuma ndugu zetu mu kambi za mateso ao kwa kuwahamishia mu maeneo ya mbali ya inchi.

17 Guvernema zinaweza kuendelea kukataza kazi yetu ya kuhubiri, kufunga watu wa Mungu, na hata kuua wamoja kati yetu. Je, ile inapaswa kutufanya tuogope ao tupoteze imani? Hapana! Yehova atalinda watu wake washikamanifu. (Soma Matayo 10:28-31.) Tulishajionea namna guvernema za nguvu, zenye kutesa watu zinafika ku mwisho, lakini watu wa Yehova wao wanaendelea kuongezeka. Sasa hivi, guvernema zote za wanadamu zitapatwa na kile kilipata Wafilisti​—zitalazimika kumujua Yehova. Na sawa vile Wafilisti, hazitakuwa tena!

“Utajiri Mwingi” Hautoe Ulinzi wa Kudumu

18. Ni biashara ya je yenye Tiro iliongoza?

18 Muji wa zamani wa Tiro * ulikuwa fasi ya maana sana ya biashara kubwa za ulimwengu wa zamani. Ile muji ilikuwa na njia mingi za biashara ku upande wa mangaribi, kuvuka Bahari ya Mediterania. Ku upande wa Mashariki, njia za biashara za Tiro zilipita ku inchi kavu na ziliunganisha Tiro na maeneo ya mbali. Mu miaka mingi, Tiro ilijirundikia utajiri mingi wenye ulitoka mu ile maeneo ya mbali. Wafanyabiashara na wachuruzi wake walifikia kuwa matajiri sana, na ile ilifanya wakuwe na kiburi na kujiona kuwa wakubwa.​—Isa. 23:8.

19, 20. Kuko tofauti gani kati ya wakaaji wa Tiro na wakaaji wa Gibeoni?

19 Wakati wa mufalme Daudi na Sulemani, Israeli alifanya biashara na wakaaji wa Tiro, wenye walituma vitu na mafundi wa kusaidia kujenga nyumba ya kifalme ya Daudi na kisha hekalu la Sulemani. (2 Ny. 2:1, 3, 7-16) Tiro aliona kipindi kizuri cha taifa la Israeli. (1 Fa. 3:10-12; 10:4-9) Waza kidogo: Watiro wengi walikuwa na nafasi ya muzuri ya kujifunza kuhusu ibada safi, kumujua Yehova, na kujionea baraka zenye mutu anapata juu anamutumikia Mungu wa kweli!

20 Hata kama walikuwa na ile nafasi, wakaaji wa Tiro waliendelea na maisha yao ya kutafuta sana vitu vya kimwili. Hawakufuata mufano muzuri wa Gibeoni, muji wa Wakanaani, wenye wakaaji wake walisikia tu kuhusu matendo makubwa ya Yehova na ile ikawachochea wakuwe watumishi wake. (Yos. 9:2, 3, 22–10:2) Tena, wakaaji wa Tiro walifikia kupinga watu wa Mungu na hata waliuzisha wamoja kati yao mu utumwa.​—Zb. 83:2, 7; Yoe. 3:4, 6; Amo. 1:9.

Hatupaswe hata kidogo kuona vitu vya kimwili kuwa ukuta wa kutulinda

21, 22. Ni nini ilipata Tiro, na juu ya nini?

21 Kupitia Ezekieli, Yehova aliambia wale wapinzani hivi: “Angalia, niko juu yako, Ee Tiro, na nitainua mataifa mengi ili yakushambulie, kama vile bahari inainua mawimbi yake. Wataharibu kuta za Tiro na kubomoa minara yake, na nitapalula udongo na kumufanya kuwa mwamba wenye kungaa, wenye kuwa wazi.” (Eze. 26:1-5) Wakaaji wa Tiro walitumaini kama mali yao itawalinda, waliwaza kama iliwapatia usalama sawa ule wenye kuta za muji wao wenye ulikuwa kisiwa ziliwatolea, kuta zenye zilikuwa na urefu wa metre 46. Ingekuwa muzuri kama wangesikiliza kwa uangalifu onyo hii ya Sulemani: “Mali ya tajiri ni muji wake wenye ngome; ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.”​—Mez. 18:11.

22 Wakati Wababiloni na baadaye Wagiriki walitimiza unabii wa Ezekieli, wakaaji wa Tiro walivumbua kama usalama wenye mali ya muji na kuta zake ziliwatolea ulikuwa wa kuwazia tu. Kisha Yerusalemu kuharibiwa, Wababiloni walipigana na Tiro mu miaka 13. (Eze. 29:17, 18) Kisha, mu mwaka wa 332 M.K.Y., Aleksanda Mukubwa alitimiza sehemu ya maana ya maunabii yenye Ezekieli aliandika. * Jeshi lake lilipalula mabomoko ya sehemu kubwa ya inchi kavu ya muji wa Tiro na kutupa majiwe yake, vitu vyake vya mbao, na udongo mu maji, na kwa njia hiyo likajenga njia ya kufika ku ile muji yenye ilikuwa kisiwa. (Eze. 26:4, 12) Aleksanda alitoboa kuta, alibeba vitu vyenye vilikuwa mu ile muji, aliua maaskari wengi na raia, na kuuzisha watu mingi sana mu utumwa. Wakaaji wa Tiro walilazimika kumujua Yehova wakati walijifunza kupitia magumu kwamba “utajiri mwingi” hautoe ulinzi wa kudumu.​—Eze. 27:33, 34.

Hata kama Tiro ilionekana kuwa salama kabisa, iliharibiwa, sawa vile Ezekieli alitabiri (Ona fungu la 22)

23. Hali ya wakaaji wa Tiro inaweza kutupatia somo gani?

23 Hali ya wakaaji wa Tiro inaweza kutupatia somo gani? Tusiruhusu hata kidogo “nguvu za udanganyifu wa utajiri” zitufanye tutumainie vitu vya kimwili, kwa kuviona kuwa ukuta wa kutulinda. (Mt. 13:22) Hatuwezi “kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.” (Soma Matayo 6:24.) Ni wale tu wenye kumutumikia Yehova kwa nafsi yao yote njo wako na usalama wa kweli. (Mt. 6:31-33; Yoh. 10:27-29) Maunabii kuhusu mwisho wa ulimwengu huu wa sasa itatimia mu kila nukta kama vile tu maunabii juu ya Tiro ilitimia. Ile wakati, wale wenye kutumainia mali watalazimika kumujua Yehova wakati ataharibu mufumo wa biashara wa ulimwengu huu wenye pupa, wenye kuchochea watu watafute tu faida zao.

Guvernema Yenye Ilikuwa Kama “Unyasi”

24-26. (a) Juu ya nini Yehova aliita Misri “unyasi”? (b) Namna gani Mufalme Sedekia hakutii agizo la Yehova, na matokeo ilikuwa nini?

24 Kuanzia siku za Yosefu mupaka wakati Wababiloni walienda kushambulia Yerusalemu, Misri ilikuwa inaongoza mambo mingi ya politike mu eneo la Inchi ya Ahadi. Sababu Misri ilikuwa imefanya siku mingi, ilionekana kuwa haiwezi kuanguka, kama vile muti wenye umefanya miaka mingi. Lakini mbele ya Yehova, ilikuwa zaifu​—haikukuwa na nguvu, ilikuwa tu sawa “unyasi.”​—Eze. 29:6.

25 Mufalme muasi Sedekia hakutambua kama Misri ilikuwa vile. Kupitia nabii Yeremia, Yehova aliambia Sedekia ajitie mu mukono wa mufalme wa Babiloni. (Yer. 27:12) Sedekia hata alifanya kiapo mu jina la Yehova kama hataasi mamlaka ya Nebukadneza. Lakini kisha, hakutii agizo la Yehova, alivunja kiapo chenye alifanya na Nebukadneza, na aliomba Misri imusaidie kupigana na Wababiloni. (2 Ny. 36:13; Eze. 17:12-20) Lakini, Waisraeli wenye walitegemea uwezo wa guvernema ya Misri walijiletea magumu ya mingi. (Eze. 29:7) Pengine Misri ilionekana kuwa yenye kuogopesha kama vile “munyama mukubwa wa bahari.” (Eze. 29:3, 4) Lakini Yehova alisema kama atatendea Misri sawa vile wawindaji wanafanyaka juu ya kukamata mamba za Muto Nile​—atatia kulabu (crochets) mu mataya yake na kumuharibu. Alifanya vile wakati alituma Wababiloni juu washinde ile Misri ya zamani.​—Eze. 29:9-12, 19.

26 Ni nini ilipata mufalme Sedekia mwenye hakukuwa muaminifu? Sababu alimuasi Yehova, Ezekieli alitabiri kama ule “mukubwa muovu” atapoteza taji lake la kifalme na utawala wake utaharibiwa. Lakini Ezekieli alitoa pia ujumbe wa tumaini. (Eze. 21:25-27) Kupitia Ezekieli, Yehova alitabiri kama mufalme mwenye atatoka mu kizazi cha kifalme, mwenye kuwa na “haki ya kisheria,” atachukua kiti cha ufalme. Mu sura ya kufuata ya kitabu hiki, tutaona kama ule mufalme ni nani.

27. Uhusiano wenye Israeli alifanya na Misri unaweza kutupatia somo gani?

27 Uhusiano wenye Israeli alifanya na Misri unaweza kutupatia somo gani? Leo, watu wa Yehova wanapaswa kuepuka kutumainia guvernema, kwa kuwaza kama guvernema zitaleta usalama wa kudumu. Hatupaswe kuwa “sehemu ya ulimwengu” hata mu mawazo yetu. (Yoh. 15:19; Yak. 4:4) Guvernema fulani inaweza kuonekana kuwa nguvu, lakini kama vile Misri ya zamani, iko zaifu sawa vile tu unyasi. Kutumainia wanadamu wenye wanaweza kufa kuliko kumutumainia Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi wa ulimwengu wote ni kukosa kuona mbali kabisa!​—Soma Zaburi 146:3-6.

Hata wakati tuko peke yetu, tunapaswa kuepuka kuwa upande fulani mu mambo ya politike ya ulimwengu huu (Ona fungu la 27)

Mataifa “Yatalazimika Kujua”

28-30. Kuko tofauti gani kati ya namna mataifa “yatalazimika kumujua” Yehova na namna sisi tunamujua Yehova?

28 Mara mingi mu kitabu cha Ezekieli, Yehova anasema kama mataifa “yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Eze. 25:17) Ile maneno ilitimia zamani wakati Yehova alileta hukumu juu ya maadui wa watu wake. Lakini itatimia mu njia kubwa zaidi mu siku zetu. Namna gani?

29 Kama vile watu wa Mungu wa zamani, sisi pia tunazungukwa na mataifa yenye inatuona kuwa kondoo mwenye kuwa peke yake na mwenye hana mutu wa kumulinda. (Eze. 38:10-13) Kama vile tutaona mu Sura ya 17 na ya 18 ya kitabu hiki, sasa hivi mataifa itashambulia mubaya sana watu wa Mungu. Lakini wakati itafanya vile, pale njo itajua kama haikuwake na nguvu. Italazimika kumujua Yehova​—kutambua mamlaka yake makubwa zaidi​—wakati ataiharibu ku vita ya Armagedoni.​—Ufu. 16:16; 19:17-21.

30 Lakini, Yehova atatulinda salama, na atatubariki. Juu ya nini? Juu, tumetumia nafasi yenye tuko nayo leo juu ya kuonyesha kama tunamujua Yehova kwa kumutumainia, kwa kumutii, na kwa kumutolea ibada safi yenye anastahili.​—Soma Ezekieli 28:26.

^ fu. 15 Kwa mufano, Wafilisti hawakuruhusu mutu yeyote mwenye kufua chuma atumikie mu inchi ya Israeli. Waisraeli walipaswa kuenda kwa Wafilisti juu vyombo vya kulima navyo vinolewe na walilipishwa kiasi cha mushahara wa siku mingi juu vyombo vyao vinolewe.​—1 Sa. 13:19-22.

^ fu. 18 Inaonekana muji wa kwanza wa Tiro ulijengwa ku mwamba wenye ulikuwa pembeni ya bahari, karibu kilometre 50 upande wa kaskazini wa Mulima Karmeli. Kisha, sehemu ingine ya muji ilijengwa ku inchi kavu. Jina la Kisemiti la ule muji ni Suri, maana yake “Mwamba.”

^ fu. 22 Isaya, Yeremia, Yoeli, Amosi, na Zekaria walitoa pia maunabii kuhusu Tiro yenye ilitimia mu kila nukta.​—Isa. 23:1-8; Yer. 25:15, 22, 27; Yoe. 3:4; Amo. 1:10; Zek. 9:3, 4.