Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 2A

Habari za Kujua Ili Kuelewa Maunabii ya Ezekieli

Habari za Kujua Ili Kuelewa Maunabii ya Ezekieli

UNABII NI NINI?

Mu Biblia, tendo la Kiebrania na·vaʼʹ, lenye kutafsiriwa “kutoa unabii,” linamaanisha kwanza kutangaza ujumbe wenye uliongozwa na roho, kutangaza hukumu, fundisho kuhusu mwenendo, ao amri kutoka kwa Mungu. Linaweza pia kumaanisha kutoa ujumbe kutoka kwa Mungu wa jambo fulani lenye litatokea. Maunabii ya Ezekieli inatia ndani zile aina zote za ufunuo mbalimbali kutoka kwa Mungu.​—Eze. 3:10, 11; 11:4-8; 14:6, 7; 37:9, 10; 38:1-4.

NAMNA UNABII ULITOLEWA

  • MAONO

  • MIFANO

  • MAONYESHO

Kitabu cha Ezekieli kiko na maono, mifano, na maonyesho ya ujumbe mbalimbali wa unabii.

UTIMIZO

Maunabii yenye Ezekieli alitoa haiko tu na utimizo moja. Kwa mufano, maunabii kuhusu kurudishwa kwa ibada safi ilitimizwa kwa kiasi fulani wakati watu wa Mungu walirudia mu Inchi ya Ahadi. Lakini kama vile Sura ya 9 ya kitabu hiki inaonyesha, maunabii mingi kuhusu kurudishwa kwa ibada safi inatimia leo na itatimia tena mu siku zenye kuja.

Zamani, tulifasiria mambo mingi mu maunabii ya Ezekieli kwa kutumia vifananishi na vifananishwa. Lakini, kitabu hiki hakizungumuzie mutu, kitu, fasi, ao tukio fulani kuwa kifananishi cha kiunabii chenye kiko na kifananishwa fulani cha sasa kama hakuna musingi wa Maandiko wa kufanya vile. * Kuliko kufanya vile, kinaonyesha utimizo mukubwa zaidi wa maunabii mingi ya Ezekieli. Tena, kinazungumuzia mambo yenye tunaweza kujifunza kutokana na ujumbe wa Ezekieli, na pia kutokana na watu, fasi na matukio yenye alizungumuzia.

^ fu. 12 Ili kupata habari zaidi juu ya vifananishi na vifananishwa, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 3, 2015, uku. 9-11, fu. 7-12; na sehemu “Maulizo ya Wasomaji Wetu,” uku. 17-18 wa ile gazeti.