Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mukusanyiko wa maana sana mu 1919 ulionyesha waziwazi kama kwa mwisho watu wa Mungu walikuwa wamekombolewa mu utumwa wa Babiloni Mukubwa

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 9B

Juu ya Nini 1919?

Juu ya Nini 1919?

Juu ya nini tunasema kama watu wa Mungu walikombolewa mu utumwa wa Babiloni Mukubwa mu mwaka wa 1919? Unabii wa Biblia na habari fulani za kihistoria vinatusaidia kusema vile.

Unabii wa Biblia na historia vinaonyesha kwa upatano kama Yesu alianza kutawala akiwa Mufalme kule mbinguni mu mwaka wa 1914, na ile ilikuwa mwanzo wa siku za mwisho za mupangilio wa Shetani ku dunia. Yesu alifanya nini kisha tu kuwa Mufalme? Je, mara moja alikomboa watumishi wake wa ku dunia mu utumwa wa Babiloni Mukubwa? Je, aliweka “mutumwa muaminifu na mwenye busara” mu mwaka wa 1914 na kuanza kazi kubwa ya mavuno?​—Mt. 24:45.

Hapana kabisa. Kumbuka kwamba, mutume Petro aliongozwa na roho ya Mungu kuandika kama hukumu ilipaswa “kuanza na nyumba ya Mungu.” (1 Pe. 4:17) Vilevile, nabii Malaki alitabiri kuhusu wakati wenye Yehova angekuja mu nyumba Yake ya ibada akisindikizwa na “mujumbe wa agano,” ni kusema, Mwana wa Mungu. (Mal. 3:1-5) Ile ingekuwa wakati wa kusafisha na kujaribu watu wa Mungu. Je, historia inaonyesha kama ile maelezo ya unabii ilitimia?

Ndiyo kabisa! Kipindi kuanzia 1914 mupaka mwanzo wa 1919 kilikuwa wakati wa majaribu na wa kusafisha Wanafunzi wa Biblia, jina la zamani la Mashahidi wa Yehova. Mu mwaka wa 1914, wengi kati ya watu wa Mungu hapa ku dunia walivunjika moyo wakati mwisho wa ulimwengu haukufika kama vile walikuwa wanatumainia. Walivunjika moyo tena zaidi mu mwaka wa 1916, wakati Charles Russell alikufa, mwenye alikuwa anaongoza mambo kwa bidii kati ya watu wa Mungu. Wamoja wenye walikuwa wanamupenda sana Ndugu Russell walipinga sana mipango ya Joseph Rutherford, mwenye alikamata nafasi ya Russell katika kuongoza mambo. Migawanyiko ilitokea na tengenezo lilikuwa karibu kuvunjika mu mwaka wa 1917. Kisha, mu mwaka wa 1918, inaonekana kwa sababu viongozi wa makanisa walichochea mambo, Ndugu Rutherford na wenzake saba walisambishwa, wakahukumiwa bila haki, na kutumwa mu kifungo. Makao makubwa kule Brooklyn ikafungwa. Ni wazi kama, watu wa Mungu walikuwa hawajakombolewa mu Babiloni Mukubwa!

Lakini, kulitokea nini mu mwaka wa 1919? Kusema kweli, mambo iligeuka haraka sana! Ku mwanzo wa ile mwaka, Rutherford na wenzake walifunguliwa mu gereza. Na mara moja walianza kazi! Mu wakati kidogo, mukusanyiko wa maana sana ulipangwa, na gazeti mupya, L’Âge d’Or, (leo ni Amuka!) ilikuwa inatayarishwa. Ile gazeti ilitayarishwa kusudi itumiwe mu kampanye za mahubiri. Tena, mwangalizi aliwekwa mu kila kutaniko juu ya kupanga mahubiri na kutia watu moyo washiriki mu kazi ya kuhubiri. Mu mwaka ileile, kichapo Bulletin (sasa ni Buku la Mukutano​—Utumishi na Maisha ya Mukristo) kilichapishwa juu kisaidie watu kupanga kazi ya kuhubiri.

Ni nini ilikuwa imetokea? Ni wazi kama, Kristo alikuwa amekomboa watu wake mu utekwa wa Babiloni Mukubwa. Alikuwa ameweka mutumwa wake muaminifu na mwenye busara. Kazi ya mavuno ilikuwa imeanza. Kuanzia ile mwaka ya maana sana ya 1919, kazi imesonga mbele mu njia ya kushangaza sana.