KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 12A
Kuunganishwa kwa Vipande Mbili vya Muti
Yehova aliomba Ezekieli aandike juu ya kipande kimoja cha muti “kwa ajili ya Yuda” na juu ya kingine “kwa ajili ya Yosefu, kipande cha muti cha Efraimu.”
“kwa ajili ya Yuda”
WAKATI WA ZAMANI
Ufalme wa makabila mbili ya Yuda
WAKATI WETU
Watiwa-mafuta
“kwa ajili ya Yosefu, kipande cha muti cha Efraimu”
WAKATI WA ZAMANI
Ufalme wa makabila kumi ya Israeli
WAKATI WETU
Kondoo wengine
“vikuwe kipande kimoja tu cha muti katika mukono wako”
WAKATI WA ZAMANI
537 M.K.Y. Waabudu wa kweli wanarudia kutoka kati ya mataifa, wanajenga upya Yerusalemu, na kufanya ibada wakiwa taifa moja.
WAKATI WETU
Tangu 1919, watu wa Mungu wanapangwa muzuri hatua kwa hatua na wanaunganishwa juu watumike wakiwa “kundi moja.”