KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 13A
Mahekalu Tofauti, Somo Tofauti
Hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono:
-
Ezekieli njo alilifasiria wahamishwa Wayahudi kule Babiloni
-
Liko na mazabahu kwenye zabihu mingi zinatolewa
-
Linaonyesha kanuni za haki za Yehova kwa ajili ya ibada
-
Linakazia kurudishwa kwa ibada safi kwenye kulianza mu 1919
Hekalu Kubwa la Kiroho:
-
Lilifasiriwa na Paulo, mu barua yenye aliandikia Wakristo Waebrania
-
Liko na mazabahu kwenye zabihu moja tu ilitolewa, “mara moja kwa wakati wote” (Ebr. 10:10)
-
Linafasiria uhalisi wa kiroho wenye tabenakulo na mahekalu ilikuwa inaonyesha tangu zamani—mupango wa Yehova kwa ajili ya ibada safi wenye unategemea zabihu ya ukombozi ya Kristo
-
Linakazia kazi yenye Kristo alifanya akiwa Kuhani Mukubwa Zaidi kuanzia 29 mupaka 33 K.K.Y.