KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 7B
Maneno ya Maana Katika Kitabu cha Ezekieli
“Mwana wa Binadamu”
ZAIDI YA MARA 90
Ezekieli anaitwa “mwana wa binadamu” zaidi ya mara 90. (Eze. 2:1) Kwa kumuita vile, Yehova anamukumbusha kwamba hata kama alipokea mapendeleo makubwa, iko tu mutu wa udongo. Inapendeza kwamba, mu habari za Injili, Yesu pia anaitwa “Mwana wa binadamu” karibu mara 80, ile inaonyesha kama alikuwa kabisa mwanadamu na hakukuwa malaika mwenye alikuwa katika umbo ya mutu.—Mt. 8:20.
“. . . Lazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”
ZAIDI YA MARA 50
Zaidi ya mara 50, Ezekieli anaandika maneno ya Mungu ya kuonyesha kwamba watu ‘watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’ ile inaonyesha kwamba Yehova tu njo anastahili kupokea ibada safi.—Eze. 6:7.
“Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova”
MARA 217
Maneno “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova” inapatikana mara 217, inapatia jina la Mungu uzito wenye linastahili na kukazia kama viumbe vyote viko chini ya mamlaka ya Yehova.—Eze. 2:4.