KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 18A
Yehova Anaonya Watu Juu ya Vita Kubwa Yenye Iko Inakuja
Biblia iko na maunabii mingi yenye inaonya kuhusu vita kubwa yenye Yehova atatumia juu ya kumaliza wote wenye wanamupinga yeye na watu wake. Maunabii fulani inaonyeshwa hapa chini. Ona mambo yenye inafanana kati ya ile maonyo, na uone namna Yehova amehakikisha kwamba watu wote wanapewa nafasi ya kuisikiliza na kutenda.
MU SIKU ZA ISRAELI YA ZAMANI
EZEKIELI: “‘Nitaita upanga juu yake [Gogu] kwenye milima yangu yote,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”—Eze. 38:18-23.
YEREMIA: “[Yehova] mwenyewe atahukumu wanadamu wote. Na ataharibu waovu kwa upanga.”—Yer. 25:31-33.
DANIELI: “Mungu wa mbinguni atasimamisha ufalme wenye . . . utaponda na kumaliza falme hizi zote.”—Dan. 2:44.
MU KARNE YA KWANZA (1-100) K.K.Y.
PAULO: “Yesu . . . pamoja na malaika wake wenye nguvu . . . ataleta kisasi juu ya wale wenye hawamujue Mungu.”—2 Te. 1:6-9.
PETRO: “Siku ya Yehova itakuja kama mwizi, . . . na dunia na kazi zenye ziko ndani yake vitafunuliwa.”—2 Pe. 3:10.
YOHANA: “Kutoka katika kinywa chake [Yesu] upanga murefu mukali unachomoka, wenye utatumiwa kupiga mataifa.”—Ufu. 19:11-18.
MU WAKATI WETU
Biblia njo kitabu chenye kutafsiriwa na kugawanywa sana kupita vitabu vingine
WATUMISHI WA YEHOVA WA WAKATI WETU . . .
-
Wanagawanya mamiliare ya vichapo vyenye kutegemea Biblia mu luga mingi
-
Wanapitisha mamilioni ya masaa kila mwaka mu mahubiri