Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 19A

Mito ya Baraka Kutoka kwa Yehova

Mito ya Baraka Kutoka kwa Yehova

Fikiria maandiko fulani ya Biblia yenye inatumia maneno “muto” na “maji” juu ya kuonyesha baraka zenye zinatiririka kutoka kwa Yehova. Wakati tunatia ile maandiko pamoja, tunaona kama inaonyesha jambo fulani la kutia moyo sana kuhusu namna Yehova anatubariki. Juu ya nini tunasema vile?

YOELI 3:18 Hii unabii inaonyesha chemchemi yenye inatoka patakatifu pa hekalu. Inatiririka na kumwanga maji mu “Bonde la Miti ya Migunga,” lenye kukauka. Kwa hiyo, Yoeli na Ezekieli, wote waliona muto wenye unafanya fasi kwenye hakuzae kitu kukuwe na uzima. Mu hali zote mbili, muto unatoka mu nyumba ya Yehova, ao hekalu.

ZEKARIA 14:8 Nabii Zekaria anaona “maji ya uzima” yenye kutiririka kutoka Yerusalemu. Nusu ya ile maji inateremukia mu bahari ya mashariki, ao Bahari ya Chumvi, na nusu ingine, inateremukia mu bahari ya mangaribi, ao Bahari ya Mediterania. Yerusalemu ilikuwa “muji wa Mufalme mukubwa,” Yehova Mungu. (Mt. 5:35) Kwa kutaja ile muji, Zekaria anatukumbusha kuwa Yehova atatawala dunia yote mu wakati wenye kuja. Tangu zamani, tumeelewa kwamba maji mu hii unabii inaonyesha kama Yehova atabariki vikundi mbili vya wanadamu waaminifu mu Paradiso, wale wenye watapita mu taabu kubwa wakiwa wazima na wale wenye watafufuliwa kisha.

UFUNUO 22:1, 2 Mutume Yohana anaona muto wa mufano wa kufanana sana na muto wenye Ezekieli alionaka. Mara hii, hautoke mu hekalu, lakini unatoka mu kiti cha ufalme cha Yehova. Kwa hiyo, inaonekana kwamba maono hii, sawa ile ya Zekaria, inakazia baraka za utawala wa Mungu wakati wa Miaka Elfu.

Kwa kweli, kuko tofauti moja tu yenye haionekane waziwazi kabisa kati ya baraka zenye zinatokana na utawala wa Yehova na baraka zenye zinafananishwa na muto wenye Ezekieli alionaka mu maono. Zile baraka zote zinatoka kwa Yehova na zinatiririka juu ya watu wote waaminifu.

ZABURI 46:4 Inaonekana andiko hii inazungumuzia mambo mbili: ibada na utawala. Hapa tunaona muto wenye unaleta shangwe mu “muji wa Mungu,” maana yake Ufalme na utawala, na pia unaleta shangwe mu “tabenakulo takatifu na kubwa ya Mwenye Kuwa Juu Zaidi,” maana yake ibada safi.

Wakati tunatia ile maandiko yote pamoja, tunaona kama inatuhakikishia kwamba Yehova atabariki wanadamu waaminifu mu njia mbili. Kwanza, utawala wake utatuletea faida za milele, na pili, mupango wa ibada safi utatuletea faida za milele. Tuazimie basi kuendelea kutafuta “maji ya uzima” kutoka kwa Yehova Mungu na Mwana wake. Ile “maji ya uzima” ni mipango ya upendo yenye wanakamata juu ya uzima wa milele!​—Yer. 2:13; Yoh. 4:10.