Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 4A

“Nilikuwa Ninaangalia Viumbe Hivyo Vyenye Uzima”

“Nilikuwa Ninaangalia Viumbe Hivyo Vyenye Uzima”

Bila shaka Ezekieli alikuwa amekwisha kuona sanamu kubwa za kuchongwa za ngombe-dume na simba wenye mabawa na wenye vichwa vya mwanadamu zikisimama kama walinzi mbele ya nyumba za wafalme na mahekalu. Sanamu kama zile zilipatikana katika Ashuru na Babilonia yote ya zamani. Kama vile watu wote wenye walikuwa wanaziona, Ezekieli alipaswa kushangaa vile viumbe vikubwa sana, vimoja vilikuwa na urefu wa karibu metre 6. Lakini, hata kama vilionekana kuwa viumbe vyenye nguvu, havikukuwa na uzima, vilikuwa tu vitu vyenye vilichongwa kutokana na majiwe.

Tofauti na ile, viumbe ine vyenye Ezekieli aliona mu maono vilikuwa “viumbe vyenye uzima.” Ile ni tofauti kubwa sana! Mambo yenye Ezekieli aliona ilimuvutia sana mupaka akatumia maneno “viumbe vyenye uzima” mara 11 mu maneno ya kwanza-kwanza ya unabii wake. (Eze. 1:5-22) Maono ya viumbe ine vyenye uzima vyenye kuenda kwa umoja vikiwa chini ya kiti cha ufalme cha Mungu ilipaswa kumuhakikishia Ezekieli kwamba Yehova anaongoza kabisa uumbaji wake wote. Leo, ile maono inatusaidia kuelewa ukubwa na uwezo wa Yehova na utukufu wa mamlaka yake makubwa zaidi.​—1 Ny. 29:11.