Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 14A

Somo Zenye Tunajifunza mu Maono ya Ezekieli ya Hekalu

Somo Zenye Tunajifunza mu Maono ya Ezekieli ya Hekalu

Ibada Safi Inainuliwa na Kulindwa

Hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono lilikuwa limeinuliwa juu ya “mulima murefu sana” (1). Je, tulishainua ibada safi, kwa kuipatia nafasi ya juu ao ya kwanza kabisa mu maisha yetu?

Ukuta (2), wenye ulikuwa unazunguka majengo ya hekalu katikati ya eneo kubwa (3), unatukumbusha kama hatupaswe hata kidogo kuacha kitu chochote kichafue ibada yenye tunamutolea Yehova. Ikiwa vitu vya “matumizi ya kawaida” vinapaswa kutiwa mbali na ibada safi, je, hauone kama muabudu wa Yehova leo anapaswa kuondoa kabisa-kabisa mwenendo muchafu ao mubaya mu maisha yake?​—Eze. 42:20.

Baraka za Milele

Muto mudogo unateremuka kutoka patakatifu pa hekalu, unaenda ukinenepa kufikia kuwa muto mukubwa na unaletea inchi uzima na mbolea (4). Zile baraka zitazungumuziwa mu Sura ya 19 ya kitabu hiki.

Kanuni Zilezile kwa Ajili ya Wote

Milango mikubwa ya murefu ya inje (5) na milango mikubwa ya ndani (9) inatukumbusha kama Yehova iko na kanuni za juu za mwenendo zenye watu wote wenye wanashiriki mu ibada safi wanapaswa kufuata. Ona kwamba milango mikubwa ya inje na ya ndani, yote iko na vipimo sawasawa. Inapaswa kuwa vile, sababu kanuni za haki za Yehova ni zilezile kwa ajili ya watumishi wake wote, hazifuate cheo ao madaraka yenye wako nayo.

Kukula na Yehova

Vyumba vya kukulia chakula (8) vinatukumbusha kama wakati wa zamani, watu walikuwa wanakula sehemu ya zabihu zenye walileta ku hekalu, ni sawa vile walikuwa wanakula na Yehova. Mambo haiko vile mu hekalu la kiroho kwenye Wakristo wanaabudu leo, sababu “zabihu moja” imekwisha kutolewa. (Ebr. 10:12) Lakini, tunatoa zabihu yetu ya sifa.​—Ebr. 13:15.

Uhakikisho wa Kimungu

Vipimo mbalimbali vyenye kuzungumuziwa mu maono vinaweza kupatia mutu kizungu-zungu. Lakini vinatoa wazo hili la lazima sana: Vinahakikisha kama kusudi la Yehova la kurudisha ibada safi ni jambo la hakika kabisa, liko kamili na haliwezi kubadilika sawa vile vipimo. Hata kama Ezekieli hakusema kama aliona mwanadamu fulani mu maono yake, aliandika mashauri mazito yenye Yehova alipatia makuhani, wakubwa, na watu. Watumishi wote wa Mungu wanapaswa kushika kanuni zake za haki.