Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 17

Bakia Katika Upendo wa Mungu

Bakia Katika Upendo wa Mungu

“Mujijenge ninyi wenyewe juu ya imani yenu takatifu zaidi . . . Mubakie katika upendo wa Mungu.”​—YUDA 20, 21.

1, 2. Tunaweza kufanya nini ili kubakia katika upendo wa Mungu?

SISI wote tunapenda kuwa wenye nguvu na wenye afya ya muzuri. Kwa hiyo tunajikaza kula chakula ya muzuri, kufanya mazoezi kwa ukawaida, na kuhangaikia mwili wetu. Hata kama inaomba kujikaza, tunafurahia matokeo ya muzuri yenye tunapata, kwa hiyo hatuchoke. Lakini tunapaswa pia kuwa wenye nguvu na wenye afya ya muzuri mu njia ingine.

2 Hata kama tumekwisha kuweka musingi muzuri kwa kufikia kumujua Yehova, tunapaswa kufanya uhusiano wetu uendelee kuwa wenye nguvu zaidi. Wakati Yuda alitia moyo Wakristo, “Mubakie katika upendo wa Mungu,” alifasiria namna wangeweza kufanya vile. Aliwaambia hivi: “Mujijenge ninyi wenyewe juu ya imani yenu takatifu zaidi.” (Yuda 20, 21) Kwa hiyo, tunaweza kufanya nini ili imani yetu ikuwe yenye nguvu?

ENDELEA KUTIA NGUVU IMANI YAKO

3-5. (a) Shetani anapenda ujisikie namna gani kuhusu kanuni za Yehova? (b) Unajisikia namna gani kuhusu sheria na kanuni za Yehova?

3 Ni jambo la maana wewe mwenyewe ukuwe hakika kama njia za Yehova ni za muzuri zaidi. Shetani anapenda ufikiri kama ni nguvu sana kuishi kulingana na kanuni za Mungu na kama utakuwa mwenye furaha zaidi ikiwa unajiamulia mwenyewe mema na mabaya. Tangu bustani ya Edeni, Shetani amejaribu kufanya watu waamini ile jambo. (Mwanzo 3:1-6) Na angali anajikaza sana kufanya vile leo.

4 Je, Shetani anasema kweli? Kanuni za Yehova zinatubana sana? Hapana. Kwa mufano, wazia uko unatembea mu shamba la wanyama la muzuri sana. Unaona ukuta murefu wenye unakuzuia kuenda sehemu fulani. Pengine unaweza kujiuliza, ‘Juu ya nini huu ukuta unanifungia njia?’ Lakini ile wakati, unasikia simba anangurumia ule upande mwingine wa ukuta. Sasa, utajisikia namna gani juu ya ule ukuta? Utafurahi sana juu unakulinda ili simba asikukule! Kanuni za Yehova ziko kama ule ukuta, na Ibilisi iko kama ule simba. Neno la Mungu linatuonya hivi: “Mulinde akili zenu, mukuwe macho! Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba mwenye kunguruma, akitafuta kumumeza mutu.”​—1 Petro 5:8.

5 Yehova anapenda tukuwe na maisha ya muzuri zaidi. Hapendi Shetani atudanganye. Njo maana ametupatia sheria na kanuni ili kutulinda na kutufanya tukuwe wenye furaha. (Waefeso 6:11) Yakobo aliandika hivi: “Ule mwenye anaangalia katika sheria kamilifu ya uhuru na anaendelea kuwa katika hiyo . . . atafurahia kile chenye anafanya.”​—Yakobo 1:25.

6. Namna gani tunaweza kuwa hakika kama njia za Mungu ni za muzuri zaidi?

6 Wakati tunafuata muongozo wa Yehova, maisha yetu inakuwa ya muzuri zaidi na urafiki wetu pamoja naye unakuwa wenye nguvu zaidi. Kwa mufano, tunapata faida wakati tunakubali mualiko wake wa kusali kwake kila mara. (Matayo 6:5-8; 1 Watesalonike 5:17) Tunapata furaha wakati tunatii muongozo wake wa kukusanyika pamoja ili kumuabudu na kutiana moyo na wakati tunajitoa sana mu kazi ya kuhubiri na ya kufundisha. (Matayo 28:19, 20; Wagalatia 6:2; Waebrania 10:24, 25) Wakati tunafikiria namna ile mambo imetusaidia kufanya imani yetu ikuwe yenye nguvu, tunakuwa hakika zaidi kama njia za Yehova ni za muzuri zaidi.

7, 8. Ni nini inaweza kutusaidia tusiogope majaribu yenye inaweza kutupata wakati wenye kuja?

7 Tunaweza kuogopa kama wakati wenye kuja tutapata majaribu ya imani yenye itakuwa nguvu sana kuvumilia. Kama unajisikia vile, ukumbuke hii maneno ya Yehova: “Mimi, Yehova, niko Mungu wako, Mwenye anakufundisha ili ujipatie faida, Mwenye anakuongoza katika njia yenye unapaswa kutembea ndani yake. Kama tu ungesikiliza amri zangu! Basi amani yako ingekuwa kama vile muto na haki yako kama mawimbi ya bahari.”​—Isaya 48:17, 18.

8 Wakati tunamutii Yehova, amani yetu itakuwa kama muto wenye haukauke, na haki yetu itakuwa kama mawimbi yenye kuendelea kujipiga pembeni ya bahari. Hata tupatwe na hali gani mu maisha yetu, tunaweza kubakia waaminifu. Biblia inatuahidi hivi: “Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.”​—Zaburi 55:22.

‘SONGA MBELE KUELEKEA UKOMAVU’

9, 10. Kuwa mukomavu maana yake nini?

9 Ukiendelea kutia nguvu uhusiano wako pamoja na Yehova, ‘utasonga mbele kuelekea ukomavu.’ (Waebrania 6:1) Kuwa mukomavu maana yake nini?

10 Hatukuwe Wakristo wakomavu kwa sababu tu ya miaka yenye tuko nayo. Ili kuwa wakomavu, tunapaswa kumufanya Yehova kuwa Rafiki yetu wa sana na kujikaza kuona mambo kama vile anaiona. (Yohana 4:23) Paulo aliandika hivi: “Wale wenye wanaishi kulingana na mwili wanakaza akili zao kwenye mambo ya mwili, lakini wale wenye wanaishi kulingana na roho wanakaza akili zao kwenye mambo ya roho.” (Waroma 8:5) Mutu mwenye kukomaa hakaze akili juu ya raha ao vitu vya kimwili mu maisha yake. Lakini, anakaza akili juu ya kumutumikia Yehova na anakamata maamuzi yenye hekima mu maisha. (Mezali 27:11; soma Yakobo 1:2, 3.) Hajiache achochewe kufanya mambo ya mubaya. Mutu mwenye kuwa mukomavu anajua mambo yenye kuwa sawa na anaazimia kuifanya.

11, 12. (a) Mutume Paulo alisema nini juu ya ‘nguvu za utambuzi’ za Wakristo? (b) Ni katika njia gani kuwa Mukristo mukomavu ni kama kuwa muchezaji?

11 Inaomba kujikaza ili kufikia kuwa Mukristo mukomavu. Mutume Paulo aliandika hivi: “Chakula kigumu ni cha watu wakomavu, wale wenye kwa kutumia nguvu zao za utambuzi wamezizoeza kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.” (Waebrania 5:14) Neno “wamezizoeza” linaweza kutufanya tufikirie mazoezi ya watu wenye kucheza michezo mbalimbali.

12 Wakati tunaona namna fundi wa muchezo fulani iko anacheza muchezo wake, tunajua kama iliomba wakati na mazoezi ili afikie kuwa fundi. Hakuzaliwa vile. Wakati mutoto anazaliwa, hajuake kabisa namna ya kutumia mikono na miguu yake. Lakini vile wakati uko unapita, anajifunza namna ya kukamata vitu na namna ya kutembea. Kupitia mazoezi, anaweza kufikia kuwa muchezaji. Vilevile, inaomba wakati na mazoezi ili tufikie kuwa Wakristo wakomavu.

13. Ni nini itatusaidia kufikiri kama vile Yehova anafikiri?

13 Katika kitabu hiki, tumeona namna tunaweza kufikiri kama vile Yehova anafikiri na kuona mambo kama vile anaiona. Tumejifunza kufurahia kanuni za Yehova na kuzipenda. Wakati tunakamata maamuzi, tunajiuliza: ‘Ni sheria ao kanuni gani za Biblia zinaweza kutumika katika hali hii? Namna gani ninaweza kuzitumikisha? Yehova angependa nifanye nini?’​—Soma Mezali 3:5, 6; Yakobo 1:5.

14. Ili kutia nguvu imani yetu, tunapaswa kufanya nini?

14 Hatuwezi kuacha kuendelea kutia nguvu imani yetu katika Yehova. Kama vile tu kula chakula chenye kujenga kunatusaidia tukuwe na mwili wenye nguvu, kujifunza juu ya Yehova kunatusaidia kuwa na imani yenye nguvu. Wakati tulianza kujifunza Biblia, tulijifunza kweli za musingi juu ya Yehova na njia zake. Lakini vile wakati uko unapita, tunapaswa kuelewa mambo mazito. Ni ile njo Paulo alimaanisha wakati alisema: “Chakula kigumu ni cha watu wakomavu.” Wakati tunatumikisha mambo yenye tunajifunza, tunapata hekima. Biblia inatuambia hivi: “Hekima ndilo jambo la maana zaidi.”​—Mezali 4:5-7; 1 Petro 2:2.

15. Juu ya nini ni jambo la maana tumupende kabisa Yehova na ndugu na dada zetu?

15 Mutu anaweza kuwa mwenye nguvu na mwenye afya ya muzuri, lakini ili abakie vile, anajua kama anapaswa kuendelea kujihangaikia muzuri. Vilevile, Mukristo mukomavu anajua kama anapaswa kujikaza sana ili aendelee kuwa na uhusiano wenye nguvu pamoja na Yehova. Paulo anatukumbusha hivi: “Muendelee kujijaribu ili kuona kama muko katika imani; muendelee kuhakikisha namna ninyi wenyewe muko.” (2 Wakorinto 13:5) Lakini, zaidi ya kutia nguvu imani yetu, kuko jambo lingine lenye tunapaswa kufanya. Upendo wetu kwa Yehova na kwa ndugu na dada zetu unapaswa kuendelea kukomaa. Paulo alisema hivi: “Kama niko na . . . ujuzi wote, na kama niko na imani yote ya kuweza kuhamisha milima, lakini sina upendo, mimi ni bure.”​—1 Wakorinto 13:1-3.

KAZA AKILI JUU YA TUMAINI LAKO

16. Shetani anapenda tujisikie namna gani?

16 Shetani anapenda tufikiri kama hatuwezi hata kidogo kumufurahisha Yehova. Anaweza kupenda tuvunjike moyo na tuwaze kama matatizo yetu haiwezi kuisha. Hapendi tutumainie Wakristo wenzetu, na hapendi tukuwe wenye furaha. (Waefeso 2:2) Shetani anajua kama mawazo yenye haifae inaweza kutuvunja moyo na kuharibu uhusiano wetu pamoja na Mungu. Lakini Yehova ametupatia jambo fulani ili kutusaidia kupiganisha mawazo yenye haifae. Ametupatia tumaini.

17. Juu ya nini tumaini ni la maana sana?

17 Mu andiko la 1 Watesalonike 5:8, Biblia inalinganisha tumaini letu na kofia ya chuma yenye inalinda kichwa cha askari mu vita, kwa kuita ile kofia ya chuma “tumaini la wokovu.” Kuwa na tumaini katika ahadi za Yehova kunaweza kulinda akili yetu na kutusaidia kupinga mawazo yenye haifae.

18, 19. Namna gani tumaini lenye Yesu alikuwa nalo lilimutia nguvu?

18 Tumaini lenye Yesu alikuwa nalo lilimufanya akuwe mwenye nguvu. Usiku wake wa mwisho hapa ku dunia, alipambana na hali ngumu zenye zilifuatana. Rafiki yake wa karibu alimusaliti. Mwingine hata alimukataa kwa kusema kama hamujue. Wengine walimuacha na kukimbia. Watu wa inchi yake mwenyewe walimugeukia, na waliomba atundikwe ku muti. Ni nini ilimusaidia avumilie ile mambo yenye kuumiza? “Kwa sababu ya furaha yenye iliwekwa mbele yake, alivumilia muti wa mateso, akazarau haya, na amekaa kwenye mukono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Mungu.”​—Waebrania 12:2.

19 Yesu alijua kama kwa kubakia muaminifu, angemuletea Baba yake utukufu na kuonyesha kama Shetani ni muongo. Tumaini hilo lilimuletea furaha kubwa. Alijua pia kama kisha muda mufupi angeweza kuwa tena pamoja na Baba yake mbinguni. Tumaini hilo lilimusaidia kuvumilia. Kama Yesu, tunapaswa kukaza akili juu ya tumaini letu. Ile itatusaidia tuvumilie hata nini itupate.

20. Ni nini inaweza kukusaidia ukuwe na mawazo yenye kufaa?

20 Yehova anaona imani na uvumilivu wako. (Isaya 30:18; soma Malaki 3:10.) Anaahidi kama “atakutimizia tamaa za moyo wako.” (Zaburi 37:4) Kwa hiyo uendelee kukaza akili yako juu ya tumaini lako. Shetani anapenda upoteze tumaini na uwaze kama ahadi za Yehova hazitatimiaka. Lakini haupaswe kuruhusu mawazo yenye haifae iingie mu akili yako! Ikiwa unaona kama tumaini lako linaanza kuregea, umuombe Yehova akusaidie. Ukumbuke maneno yenye kuwa mu Wafilipi 4:6, 7: “Musihangaike juu ya jambo lolote, lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.”

21, 22. (a) Yehova iko na kusudi gani juu ya dunia? (b) Umeazimia kufanya nini?

21 Kila mara ukuwe na wakati wa kufikiri sana juu ya wakati wenye kuja wa muzuri sana. Hivi karibuni, kila mutu mwenye kuishi atamuabudu Yehova. (Ufunuo 7:9, 14) Wazia namna maisha itakuwa mu ulimwengu mupya. Itakuwa ya muzuri sana kuliko jambo lolote lenye tunaweza kuwazia! Shetani, pepo wake wachafu, na uovu wote hautakuwa tena. Hautapatwa na magonjwa, na hautapatwa na kifo. Lakini, utaamuka kila siku ukiwa na nguvu mingi na utafurahia maisha. Watu wote watatumika pamoja ili kufanya dunia ikuwe paradiso. Wote watakuwa na chakula ya muzuri na nafasi ya kuishi yenye kuwa salama. Watu hawatakuwa wakali ao wenye jeuri, lakini wataonyeshana upole wa kweli. Kisha, wanadamu wote ku dunia watakuwa na “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.”​—Waroma 8:21.

22 Yehova anapenda umufanye kuwa Rafiki yako wa sana. Kwa hiyo, ufanye nguvu yako yote ili kumutii Yehova na kumukaribia kila siku. Sisi wote tuendelee basi kubakia katika upendo wa Mungu milele!​—Yuda 21.