Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Barua Kutoka kwa Baraza Lenye Kuongoza

Barua Kutoka kwa Baraza Lenye Kuongoza

Kwa wale wenye kumupenda Yehova Mungu na Neno lake, Biblia:

Yesu alisema hivi: “Mutajua kweli, na kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Fikiria namna ulijisikia wakati ulijua kwa mara ya kwanza kweli yenye iko mu Biblia! Ilikuwa jambo lenye kufurahisha sana kujua kama mu ulimwengu wenye kujaa uongo, tunaweza kujifunza kweli.​—2 Timoteo 3:1.

Yehova Mungu anapenda tujue kweli. Na kwa kuwa tunapenda watu, tunapenda kuzungumuza nao kuhusu ile kweli. Lakini kumutumikia Mungu kunatia ndani mambo mingi. Tunapaswa kufanya nguvu yetu yote ili kuishi kama Wakristo juu tunaheshimia sana kanuni za Yehova. Yesu alizungumuzia jambo moja la maana lenye tunaweza kufanya ili kuonyesha kama tunamupenda Mungu. Alisema hivi: “Kama munashika amri zangu, mutabakia katika upendo wangu, kama vile mimi nilishika amri za Baba na ninabakia katika upendo wake.”​—Yohana 15:10.

Yesu anamupenda kabisa Baba yake, na anafanya kila jambo lenye Baba yake anamuomba afanye. Kama tunamuiga Yesu katika namna yetu ya kuishi, Yehova atatupenda na tutakuwa na furaha kabisa. Yesu alisema, “Kama munajua mambo haya, ninyi ni wenye furaha ikiwa munayatenda.”​—Yohana 13:17.

Tunatumaini kama kitabu hiki kitakusaidia kujifunza kuishi kulingana na kweli yenye iko mu Biblia na kitakusaidia ukuwe rafiki ya Mungu. Tunasali uendelee kukomaa katika upendo wako kwa Mungu na ubakie “katika upendo wa Mungu . . . [upate] uzima wa milele.”​—Yuda 21.

Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova