Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 6

Namna Tunaweza Kuchagua Mambo ya Kujifurahisha

Namna Tunaweza Kuchagua Mambo ya Kujifurahisha

“Mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.”​—1 WAKORINTO 10:31.

1, 2. Juu ya nini tunapaswa kuwa waangalifu wakati tunachagua mambo ya kujifurahisha nayo?

WAZIA kuwa unataka kula tunda, kisha unatambua kama sehemu moja ya tunda hilo ni yenye kuoza. Utafanya nini? Utaamua tu kuikula? Utaitupa? Ao utakata ile sehemu yenye kuoza na kula sehemu ya muzuri?

2 Kwa njia fulani, mambo ya kujifurahisha inafanana na ile sehemu yenye kuoza ya tunda. Mambo fulani ya kujifurahisha ni ya muzuri, lakini mambo mingi ya kujifurahisha ni yenye kuoza juu ni machafu, iko na jeuri, ao iko na uhusiano na pepo wachafu. Kwa hiyo wakati unachagua mambo yenye utajifurahisha nayo, unasemaka kama: “Ile inaniangalia tu mimi. Ninaweza kuchagua mambo yoyote ya kujifurahisha yenye ninapenda”? Ao unasemaka kama: “Mambo yote ya kujifurahisha nayo ni ya mubaya”? Ao unachagua kwa uangalifu mambo ya kujifurahisha, kwa kuepuka ya mubaya na kufurahia ya muzuri?

3. Tunapaswa kujiuliza ulizo gani wakati tunachagua mambo ya kujifurahisha nayo?

3 Sisi wote tuko na lazima ya kufanya mambo fulani ili kupitisha tu wakati na kujifurahisha, na tunapenda kuchagua muzuri. Lakini ni muzuri tujiulize: ‘Maamuzi yangu juu ya mambo ya kujifurahisha itakuwa na matokeo gani juu ya ibada yangu kwa Yehova’?

“MUFANYE MAMBO YOTE KWA UTUKUFU WA MUNGU”

4. Ni kanuni gani ya Biblia yenye inaweza kutusaidia kuchagua mambo ya kujifurahisha?

4 Wakati tunajitoa kwa Yehova katika sala, tunamuahidi kuwa tutatumia maisha yetu ili kumutumikia. (Soma Muhubiri 5:4.) Tunaahidi kuwa ‘tutafanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu.’ (1 Wakorinto 10:31) Ile inamaanisha kama tuko wenye kujitoa kwa Mungu hata wakati tunapumuzika ao wakati tunajifurahisha, haiko tu wakati tuko ku mikutano ao mu mahubiri.

5. Ni ibada ya namna gani tunapaswa kumutolea Yehova?

5 Kila kitu chenye tunafanya mu maisha kiko na uhusiano na ibada yetu kwa Yehova. Paulo alieleza jambo hilo wakati alisema hivi: “Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu, na yenye kukubalika kwa Mungu.” (Waroma 12:1) Yesu alisema hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Marko 12:30) Sikuzote tunapenda kumutolea Yehova kitu cha muzuri zaidi. Katika Israeli ya zamani, wakati watu walitoa zabihu ya munyama kwa Yehova, walipaswa kutoa munyama mwenye kuwa na afya ya muzuri. Ikiwa zabihu ilikuwa na kasoro ao ulemavu fulani, Mungu aliikataa. (Mambo ya Walawi 22:18-20) Vilevile, Yehova anaweza kukataa ibada yetu. Juu ya nini?

6, 7. Mambo yenye tunachagua ili kujifurahisha nayo inaweza kuwa na matokeo gani juu ya ibada yetu kwa Yehova?

6 Yehova anatuambia hivi: “Munapaswa kuwa watakatifu, kwa sababu mimi ni mutakatifu.” (1 Petro 1:14-16; 2 Petro 3:11) Yehova atakubali ibada yetu ikiwa tu iko takatifu, ao safi. (Kumbukumbu la Torati 15:21) Ibada yetu haiwezi kuwa safi kama tunafanya mambo yenye Yehova anachukia, kama vile mambo machafu, yenye jeuri, ao yenye kuwa na uhusiano na pepo wachafu. (Waroma 6:12-14; 8:13) Lakini Yehova anaweza kuchukizwa pia kama tunatumia mambo ya vile ili kujifurahisha. Ile inaweza kufanya ibada yetu isikuwe safi na Yehova hawezi kuikubali. Tena, ile mambo inaweza kuharibu kabisa uhusiano wetu pamoja naye.

7 Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuchagua kwa hekima mambo ya kujifurahisha? Ni kanuni gani zinaweza kutusaidia kutambua mambo ya kujifurahisha yenye kufaa na yenye haifae?

CHUKIA MAMBO YA MUBAYA

8, 9. Ni mambo gani ya kujifurahisha yenye tunapaswa kuepuka? Juu ya nini?

8 Leo, watu wanaweza kujifurahisha na mambo mingi mbalimbali. Mambo fulani ya kujifurahisha ni yenye kufaa kwa Wakristo, lakini mambo mingi ya kujifurahisha haifae. Kwanza, tuzungumuzie mambo fulani ya kujifurahisha yenye tunapaswa kuepuka.

9 Filme mingi, site za enternete, vipindi vya televizyo, michezo ya video, na nyimbo ziko na mambo machafu, yenye jeuri, ao yenye kuwa na uhusiano na pepo wachafu. Mara mingi mambo ya mubaya inaonyeshwa kwa njia yenye kufanya ionekane kama ni ya muzuri na hata yenye kuchekesha. Lakini Wakristo wanaonyesha uangalifu kwa kukataa mambo ya kujifurahisha yenye haipatane na kanuni safi za Yehova. (Matendo 15:28, 29; 1 Wakorinto 6:9, 10) Wakati tunakataa mambo ya kujifurahisha ya ile namna, tunamuonyesha Yehova kuwa tunachukia mambo ya mubaya.​—Zaburi 34:14; Waroma 12:9.

10. Kuchagua mubaya mambo ya kujifurahisha kunaweza kuwa na matokeo gani?

10 Lakini watu fulani wanawaza kuwa haiko mubaya kujifurahisha na mambo yenye jeuri, machafu, ao yenye kuwa na uhusiano na pepo wachafu. Wanawaza hivi: ‘Kuko ubaya gani? Siwezi hata kidogo kufanya ile mambo.’ Ikiwa tunawaza vile, tunajidanganya sisi wenyewe. Biblia inasema hivi: “Moyo ni mudanganyifu kuliko kitu kingine chochote na uko hatari.” (Yeremia 17:9) Kama tunajifurahisha na mambo yenye Yehova anakataa, tunaweza kusema kabisa kama tunachukia ile mambo? Kadiri tunaendelea kujifurahisha na mambo ya ile namna, ni vile tutaanza kuiona kuwa ya kawaida. Kisha muda fulani, zamiri yetu itakuwa zaifu na itaacha kutuonya wakati tunataka kukamata uamuzi wa mubaya.​—Zaburi 119:70; 1 Timoteo 4:1, 2.

11. Namna gani andiko la Wagalatia 6:7 linaweza kutusaidia kuchagua mambo ya kujifurahisha?

11 Neno la Mungu linatuambia hivi: “Kitu chochote chenye mutu anapanda, ni kile atavuna pia.” (Wagalatia 6:7) Ni wazi kuwa ikiwa tunaamua kujifurahisha na mambo ya mubaya, tunaweza kufikia kuifanya. Kwa mufano, watu fulani wenye walipenda sana kujifurahisha na mambo machafu, walifikia kuifanya. Lakini Yehova anatupatia musaada wenye tuko nao lazima ili tuchague kwa hekima mambo ya kujifurahisha.

TUMIA KANUNI ZA BIBLIA ILI KUKAMATA MAAMUZI

12. Ni nini inaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri kuhusu mambo ya kujifurahisha?

12 Ni mwepesi kutambua kama mambo fulani ya kujifurahisha inamuchukiza Yehova, na tunajua kuwa tunapaswa kuiepuka. Lakini tutafanya nini kama hatutambue waziwazi? Yehova hatupatie oroza ao liste ya sheria kuhusu mambo yenye tunapaswa kuangalia, kusikiliza, ao kusoma. Lakini, anapenda tutumie zamiri yetu yenye kuzoezwa na Biblia. (Soma Wagalatia 6:5.) Yehova anatupatia kanuni, ni kusema, kweli za musingi zenye kutufundisha namna Yehova anaona mambo. Kanuni hizo zinatusaidia kuzoeza zamiri yetu. Zinatusaidia kujua “mapenzi ya Yehova” ili tuweze kukamata maamuzi yenye inaweza kumufurahisha.​—Waefeso 5:17.

Kanuni za Biblia zinatusaidia kuchagua mambo ya kujifurahisha

13. Sababu gani Wakristo hawakamate maamuzi yenye kufanana juu ya mambo ya kujifurahisha? Lakini Wakristo wote wanapaswa kuongozwa na nini?

13 Mara mingi, mambo ya kujifurahisha yenye Mukristo fulani anachagua inakuwa tofauti na yenye Mukristo mwingine anachagua. Juu ya nini? Ni juu kila mutu iko na mambo yenye anapendaka. Pia, jambo lenye mutu fulani anapenda, pengine mutu mwingine hawezi kulipenda. Lakini, ili kukamata maamuzi ya muzuri, Wakristo wote wanapaswa kuongozwa na kanuni za Biblia. (Wafilipi 1:9) Kanuni hizo zitatusaidia kuchagua mambo ya kujifurahisha yenye Mungu anakubali.​—Zaburi 119:11, 129; 1 Petro 2:16.

14. (a) Ni jambo gani la maana la kufikiria juu ya namna tunatumia wakati? (b) Ni shauri gani Paulo alitolea Wakristo?

14 Jambo lingine la kufikiria ni wakati wenye tunapitisha mu mambo ya kujifurahisha. Ile inaweza kuonyesha ni kwa kadiri gani mambo ya kujifurahisha ni ya maana kwetu. Tukiwa Wakristo, utumishi wetu kwa Yehova njo jambo la maana zaidi mu maisha yetu. (Soma Matayo 6:33.) Lakini bila kujua, mambo ya kujifurahisha inaweza kukamata wakati wetu mwingi. Paulo alishauria Wakristo hivi: “Muendelee kuwa waangalifu sana ili namna munatembea isikuwe kama watu wenye hawana hekima lakini kama watu wenye hekima.” (Waefeso 5:15, 16) Kwa hiyo, tunapaswa kuweka mipaka juu ya wakati wenye tunapitisha mu mambo ya kujifurahisha na kuhakikisha sikuzote kama utumishi wetu kwa Yehova unakamata nafasi ya kwanza mu maisha yetu.​—Wafilipi 1:10.

15. Tunaweza kufanya nini ili kujilinda na mambo ya kujifurahisha yenye inaweza kuharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova?

15 Ni wazi kuwa, tunapaswa kukataa mambo ya kujifurahisha yenye tunajua kuwa Yehova hakubali. Lakini tutafanya nini kama tunakuwa na mashaka juu ya mambo fulani ya kujifurahisha? Je, ni lazima tu tukuwe waangalifu? Fikiria jambo hili. Kama uko unatembea mu njia yenye inapita ku mulima, na pembeni ya ile njia kuko shimo ya murefu, unaweza kutembelea ku mwisho-mwisho ya ile njia? Hapana. Kama unaona uzima wako kuwa wa maana, utaepuka hatari. Ni vile pia kuhusu maamuzi yetu juu ya mambo ya kujifurahisha. Neno la Mungu linatuambia hivi: “Epusha miguu yako na mambo ya mubaya.” (Mezali 4:25-27) Kwa hiyo hatuepuke tu mambo yenye tunajua kuwa ni ya mubaya, lakini pia tunakataa mambo yoyote ya kujifurahisha yenye tuko nayo mashaka kuwa haiko ya muzuri kwetu na kuwa inaweza kuharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova.

UONE MAMBO KAMA YEHOVA

16. (a) Ni mambo gani fulani yenye Yehova anachukia? (b) Namna gani tunaonyesha kuwa tunachukia mambo yenye Yehova anachukia?

16 Muandikaji mumoja wa zaburi aliandika hivi: “Enyi wenye kumupenda Yehova, muchukie mambo ya mubaya.” (Zaburi 97:10) Biblia inatusaidia kujua mawazo ya Yehova na namna anajisikia. Ujiulize namna mambo yenye unajifunza inaweza kukusaidia kuona mambo kama Yehova. Kwa mufano, tunajifunza kuwa Yehova anachukia “ulimi wa uongo, na mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa, moyo wenye kufanya mipango ya uovu, na miguu yenye kukimbilia haraka kwenye uovu.” (Mezali 6:16-19) Tunajifunza kuwa tunapaswa kuepuka “uasherati, . . . ibada ya sanamu, kupashana habari na pepo wachafu, . . . wivu, milipuko ya kasirani, . . . kutamani, ulevi, karamu za kupitisha mipaka, na mambo kama hayo.” (Wagalatia 5:19-21) Je, unaona namna kanuni hizo za Biblia zinaweza kukusaidia kuchagua mambo ya kujifurahisha? Tunapenda kufuata kanuni za Yehova mu sehemu zote za maisha yetu, wakati tuko peke yetu na wakati tuko pamoja na wengine. (2 Wakorinto 3:18) Kwa kweli, maamuzi yenye tunafanya wakati tuko peke yetu mara mingi inaonyesha sisi tuko watu wa namna gani.​—Zaburi 11:4; 16:8.

17. Mbele ya kuchagua mambo ya kujifurahisha, tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

17 Kwa hiyo, wakati unachagua mambo ya kujifurahisha, ujiulize hivi: ‘Uamuzi wangu utakuwa na matokeo gani juu ya uhusiano wangu pamoja na Yehova? Utakuwa na matokeo gani juu ya zamiri yangu?’ Tuchunguze basi kanuni fulani zenye zinaweza kutusaidia wakati tunachagua mambo ya kujifurahisha nayo.

18, 19. (a) Paulo alitolea Wakristo shauri gani? (b) Ni kanuni gani zitatusaidia kuchagua mambo ya kujifurahisha?

18 Wakati tunachagua mambo ya kujifurahisha, tunachagua mambo ya kujaza mu akili yetu. Paulo aliandika hivi: “Mambo yoyote yenye kuwa ya kweli, mambo yoyote yenye kuwa ya hangaiko nzito, mambo yoyote ya haki, mambo yoyote yenye kuwa safi, mambo yoyote yenye kustahili kupendwa, mambo yoyote yenye kusemwa muzuri, tabia zozote za muzuri, na mambo yoyote yenye kustahili sifa, muendelee kufikiria mambo hayo.” (Wafilipi 4:8) Wakati tunajaza akili yetu na mambo ya muzuri kama hayo, tunaweza kusema hivi: “Maneno ya kinywa changu na kufikiri sana kwa moyo wangu vikupendeze wewe, Ee Yehova.”​—Zaburi 19:14.

19 Ujiulize hivi: ‘Ninajaza akili yangu na mambo gani? Kisha kuangalia filme fulani, ninakuwaka na mawazo ya muzuri na yenye kujenga? Ninakuwaka na amani, na zamiri ya muzuri? (Waefeso 5:5; 1 Timoteo 1:5, 19) Ninajisikiaka huru kusali kwa Yehova? Ao ninajisikiaka mubaya? Mambo yenye nilijifurahisha nayo ilifanya nifikirie mambo machafu ao yenye jeuri? (Matayo 12:33; Marko 7:20-23) Mambo yenye ninachagua ili kujifurahisha inafanya ‘nifinyangwe na mupangilio huu wa mambo’?’ (Waroma 12:2) Majibu yetu yenye kutoka mu moyo inaweza kutusaidia kuona kile tunapaswa kufanya ili uhusiano wetu pamoja na Yehova uendelee kuwa nguvu. Tunapenda kusali kama muandikaji mumoja wa zaburi. Alisali hivi: “Geuzia mbali macho yangu ili yasiangalie mambo yenye hayana mafaa yoyote.” *​—Zaburi 119:37.

MAAMUZI YETU IKO NA MATOKEO JUU YA WENGINE

20, 21. Sababu gani tunapaswa kufikiria zamiri ya wengine wakati tunachagua mambo ya kujifurahisha?

20 Kanuni ingine ya maana ya kukumbuka ni hii: “Mambo yote yanaruhusiwa, lakini haiko mambo yote ndiyo yenye faida. Kila mumoja aendelee kutafuta, hapana faida yake mwenyewe, lakini faida ya ule mutu mwingine.” (1 Wakorinto 10:23, 24) Kuwa tu na uhuru wa kufanya jambo fulani hakumaanishe kuwa tunapaswa tu kulifanya. Tunapaswa kufikiria kwa uangalifu matokeo ya maamuzi yetu juu ya ndugu na dada zetu.

21 Zamiri zinatofautiana. Kwa mufano, zamiri yako inaweza kukuruhusu kufuata programu fulani ya televizyo. Lakini unaweza kusikia kama programu ileile inasumbua zamiri ya ndugu ao dada yako. Utafanya nini? Hata kama uko na haki ya kuifuata, pengine unaweza kuamua kuacha kuifuta. Juu ya nini? Ni juu haupendi ‘kutendea ndugu zako zambi’​—ao hata ‘kumutendea Kristo zambi.’ (1 Wakorinto 8:12) Hatupendi kufanya kitu chochote chenye kinaweza kukwaza Mukristo mwenzetu.​—Waroma 14:1; 15:1; 1 Wakorinto 10:32.

22. Namna gani tunaweza kuonyesha usawaziko juu ya maamuzi ya Wakristo wengine?

22 Kwa upande mwingine, utafanya nini kama zamiri yako haikuruhusu kuangalia, kusoma, ao kufanya jambo fulani lenye mutu mwingine anakubali? Kwa kuwa unamupenda na kumuheshimia ndugu yako, hautamukaza aamue kama wewe. Mutu mwenye kutembeza gari anajua kama watu wengine wanaweza kutembeza mbio zaidi ao polepole zaidi kuliko yeye na wakati uleule wakuwe watembezaji wazuri. Vilevile, wewe na ndugu yako munaweza kuwa munafuata kanuni za Biblia; lakini mawazo yenu inaweza kuwa tofauti kidogo juu ya mambo ya kujifurahisha yenye kukubalika.​—Muhubiri 7:16; Wafilipi 4:5.

23. Ni nini itatusaidia kuchagua muzuri mambo ya kujifurahisha?

23 Kwa hiyo, ni nini itatusaidia kuchagua muzuri mambo ya kujifurahisha? Kama tunatumia zamiri yetu yenye kuzoezwa na kanuni za Biblia na kama tunahangaikia kabisa ndugu na dada zetu, tutakamata maamuzi ya muzuri. Na tutakuwa na furaha kwa sababu tunafanya “mambo yote kwa utukufu wa Mungu.”

^ fu. 19 Tunaweza kupata kanuni zingine zenye zinaweza kutusaidia kuchagua mambo ya kujifurahisha mu andiko la Mezali 3:31; 13:20; Waefeso 5:3, 4; na Wakolosai 3:5, 8, 20.