Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 13

Je, Sikukuu Zote Zinamufurahisha Mungu?

Je, Sikukuu Zote Zinamufurahisha Mungu?

“Muendelee kuhakikisha ni nini yenye kukubaliwa kwa Bwana.”​—WAEFESO 5:10.

1. Tunapaswa kufanya nini ili kuhakikisha kama ibada yetu inamufurahisha Yehova, na sababu gani?

YESU alisema hivi: “Waabudu wa kweli watamuabudu Baba kwa roho na kweli, kwa maana, kwa kweli, Baba anatafuta watu wa namna hiyo ili wamuabudu.” (Yohana 4:23; 6:44) Kila mumoja wetu anapaswa ‘kuendelea kuhakikisha ni nini yenye kukubaliwa kwa Bwana.’ (Waefeso 5:10) Haiko mwepesi kufanya vile sikuzote. Shetani anajaribu kutudanganya ili tufanye mambo yenye haimufurahishe Yehova.​—Ufunuo 12:9.

2. Fasiria mambo yenye ilifanyika karibu na Mulima Sinai.

2 Namna gani Shetani anajaribu kutudanganya? Njia moja yenye anatumia ni kutuvuruga ili tusijue tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na mambo yenye haiko sawa. Fikiria jambo lenye lilipata watu wa taifa la Israeli wakati walipiga kambi karibu na Mulima Sinai. Musa alikuwa ameenda ku mulima, na watu walikuwa wanamungojea arudie mu kambi. Mwishowe, walichoka kumungojea na walimuomba Haruni awafanyie mungu. Alifanya mungu wa zahabu mwenye kufanana na kitoto-dume cha ngombe. Kisha watu walifanya sikukuu. Walicheza na wako wanazunguka kitoto-dume cha ngombe na kukiinamia. Waliwaza kama kwa kuinamia kitoto-dume cha ngombe, walikuwa kabisa wanamuabudu Yehova. Lakini kuona tu ile tukio kuwa “sikukuu kwa ajili ya Yehova” hakukuifanya ikuwe ya muzuri. Yehova aliona ile jambo kuwa ibada ya sanamu, na watu wengi kati yao walikufa. (Kutoka 32:1-6, 10, 28) Tunapata somo gani? Usijiache udanganywe. ‘Usiguse kitu chochote kichafu,’ na uache Yehova akufundishe tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na mambo yenye haiko sawa.​—Isaya 52:11; Ezekieli 44:23; Wagalatia 5:9.

3, 4. Juu ya nini inafaa kuchunguza namna sikukuu mingi zenye kupendwa sana zilianza?

3 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alifundisha wanafunzi wake waonyeshe mufano kwa kufanya ibada yenye kuwa safi. Kisha kifo chake, mitume waliendelea kufundisha wanafunzi wapya kanuni za Yehova. Lakini kisha kifo cha mitume, walimu wa uongo walianza kuingiza mawazo ya uongo, desturi na sikukuu za kipagani mu kutaniko. Hata walibadilisha majina ya sikukuu fulani za kipagani ili zionekane kuwa za Kikristo. (2 Watesalonike 2:7, 10; 2 Yohana 6, 7) Sikukuu mingi kati ya hizo zingali zinapendwa na watu wengi, na zingali zinaendeleza mafundisho ya uongo na ibada ya roho waovu. *​—Ufunuo 18:2-4, 23.

4 Leo mu ulimwengu, watu wanaona kama kufanya sikukuu ni jambo la maana mu maisha. Lakini, kadiri unaendelea kujifunza kuhusu namna Yehova anaona mambo, unaweza kutambua kama uko na lazima ya kubadilisha mawazo yako kuhusu sikukuu fulani. Kufanya vile haiwezi kuwa mwepesi, lakini unaweza kuwa hakika kama Yehova atakusaidia. Tuzungumuzie basi namna sikukuu fulani zenye kupendwa sana zilianza. Ile inaweza kutusaidia kuelewa namna Yehova anajisikia kuhusu zile sikukuu.

SIKUKUU YA NOELI ILIANZA NAMNA GANI?

5. Ni mambo gani yenye kuonyesha kama Yesu hakuzaliwa tarehe 25 Mwezi wa 12?

5 Mu sehemu mingi za dunia, sikukuu ya Noeli inafanywa tarehe 25 Mwezi wa 12, na watu wengi wanawaza kama ni siku yenye Yesu alizaliwa. Biblia haituambie siku ao hata mwezi wenye Yesu alizaliwa, lakini inatuambia jambo fulani kuhusu ni wakati gani katika mwaka alizaliwa. Luka aliandika kama wakati Yesu alizaliwa Betlehemu, “wachungaji walikuwa wanaishi inje,” wakichunga makundi yao ya wanyama. (Luka 2:8-11) Mu Mwezi wa 12, muji wa Betlehemu unakuwaka na baridi, mvua na teluji (ao, neige) na wachungaji hawangeikaa inje pamoja na makundi yao wakati wa usiku. Ile inatufundisha nini? Yesu alizaliwa wakati hali ya hewa ilikuwa muzuri, hapana mu Mwezi wa 12. Ushuhuda wa Biblia na wa historia unaonyesha kama Yesu alizaliwa siku fulani mu mwezi wenye tunajua leo kuwa Mwezi wa 9 na wa 10.

6, 7. (a) Desturi mingi za Noeli zenye kupendwa sana na watu wengi zilianza namna gani? (b) Ni nini yenye inapaswa kutuchochea kutoa zawadi?

6 Kwa hiyo, Noeli ilianza namna gani? Ilitokana na sikukuu za kipagani, sikukuu kama ile ya Saturnalia ya Waroma, yenye ilifanywa kwa ajili ya Saturne, mungu wa kilimo. Kitabu The Encyclopedia Americana kinasema hivi: “Desturi mingi za kujifurahisha zenye kufuatwa wakati wa Noeli zinatokana na Saturnalia, sikukuu ya Waroma yenye ilifanywa katikati ya Mwezi wa 12. Kwa mufano, desturi za kufanya mapambo wakati wa karamu, za kutoleana zawadi na za kuwasha mishumaa (ao, bougie), zilitokana na ile sikukuu.” Pia, sikukuu ya Mithra, mungu-jua wa Waajemi ilifanywa tarehe 25 Mwezi wa 12.

7 Lakini leo, watu wengi wenye wanafanya sikukuu ya Noeli hawafikirie jambo la kuwa ilitokana na sikukuu za kipagani. Wanaona tu kama Noeli ni wakati wa kuwa pamoja na familia, kufurahia kula chakula cha muzuri na kupatiana zawadi. Ni kweli kwamba tunapenda watu wa familia yetu na marafiki, na Yehova anapenda watumishi wake waonyeshane ukarimu. Na andiko la 2 Wakorinto 9:7 linatuambia kuwa, “Mungu anapenda mutu mwenye anatoa kwa furaha.” Yehova hapendi tutolee watu wengine zawadi wakati fulani tu wa pekee. Watu wa Yehova wanafurahia kutoa zawadi na kuwa pamoja na marafiki na watu wa familia wakati wowote katika mwaka, na hawatazamie watu wengine pia wawarudishie kitu. Ni juu wanawapenda wengine njo maana wanawatolea zawadi.​—Luka 14:12-14.

Kujua namna sikukuu zilianza kunaweza kutusaidia tujue ni sikukuu gani yenye tutaepuka

8. Wanajimu walimutolea Yesu zawadi muda mufupi tu kisha kuzaliwa kwake? Fasiria.

8 Ili kutegemeza wazo la kutoa zawadi wakati wa Noeli, watu wengi wanasema kama wale watu watatu wenye hekima walimuletea Yesu zawadi kisha tu kuzaliwa kwake, na kama walifanya vile wakati alikuwa fasi ya kukulishia wanyama. Ni kweli kwamba kikundi cha wanaume walimutembelea Yesu na walimuletea zawadi. Mu wakati wa zamani, ilikuwa jambo la kawaida kuletea zawadi mutu wa maana. (1 Wafalme 10:1, 2, 10, 13) Je, ulijua kama Biblia inasema wale wanaume watatu walikuwa wanajimu, watu wenye walitumia uchawi na wenye hawakumuabudu Yehova? Pia, hawakumutembelea Yesu wakati alikuwa mu nafasi ya kuchungia wanyama, muda mufupi tu kisha kuzaliwa kwake. Walimutembelea nyuma, wakati alikuwa “mutoto mudogo” na iko anaishi mu nyumba.​—Matayo 2:1, 2, 11.

BIBLIA INASEMA NINI JUU YA SIKUKUU ZA KUZALIWA?

9. Ni sikukuu gani za kuzaliwa zenye Biblia inazungumuzia?

9 Siku yenye mutoto anazaliwa ni siku ya furaha. (Zaburi 127:3) Lakini ile haimaanishe kama tunapaswa kufanya sikukuu za kuzaliwa. Waza kidogo: Ni sikukuu mbili tu za kuzaliwa njo zenye Biblia inazungumuzia. Sikukuu moja ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Farao wa Misri, na ingine ilikuwa ya kuzaliwa kwa Mufalme Herode Antipa. (Soma Mwanzo 40:20-22; Marko 6:21-29.) Wale watawala wote wawili hawakumutumikia Yehova. Kwa kweli, mu Biblia hakuna fasi yenye tunasoma kama mutumishi fulani wa Yehova alifanya sikukuu ya kuzaliwa.

10. Wakristo wa kwanza-kwanza waliona namna gani kufanya sikukuu za kuzaliwa?

10 Kitabu The World Book Encyclopedia kinasema kama Wakristo wa kwanza-kwanza “waliona kufanya sikukuu ya kuzaliwa kwa mutu yeyote kuwa desturi ya kipagani.” Zile desturi zilitegemea imani za uongo. Kwa mufano, Wagiriki wa zamani waliamini kama kila mutu alilindwa na roho fulani yenye ilikuwa pale wakati wa kuzaliwa kwake. Na waliwaza kama ile roho ilikuwa na uhusiano na mungu fulani mwenye alizaliwa tarehe yenye kupatana na tarehe ya kuzaliwa kwa ule mutu. Zaidi ya zile imani za kipagani, sikukuu za kuzaliwa ziko pia na uhusiano na desturi ya kutabiri matukio kwa kutumia nyota.

11. Yehova anapenda tukuwe na mawazo gani juu ya kuonyesha ukarimu?

11 Watu wengi wanawaza kama siku yao ya kuzaliwa ni siku ya pekee yenye wanapaswa kuonyeshwa upendo na kuonwa kuwa wa maana. Lakini tunaweza kuonyesha upendo watu wa familia yetu na marafiki wakati wowote katika mwaka, kuliko kufanya vile tu siku fulani ya pekee. Yehova anapenda tuonyeshe wema na tukuwe wakarimu wakati wote. (Soma Matendo 20:35.) Kila siku tuko wenye shukrani kwake juu ya zawadi ya maana sana ya uzima, hapana tu wakati wa siku yetu ya kuzaliwa.​—Zaburi 8:3, 4; 36:9.

Wakristo wa kweli wanatolea wengine zawadi juu wanawapenda

12. Namna gani siku ya kufa kwetu inaweza kuwa ya muzuri zaidi kuliko siku ya kuzaliwa kwetu?

12 Andiko la Muhubiri 7:1 linasema hivi: “Jina la muzuri linashindia mafuta ya muzuri, na siku ya kufa inashindia siku ya kuzaliwa.” Namna gani siku ya kufa kwetu inaweza kuwa ya muzuri zaidi kuliko siku ya kuzaliwa kwetu? Wakati tunazaliwa, tunakuwa hatujafanya jambo lolote mu maisha, ikuwe la muzuri ao la mubaya. Lakini, wakati tunatumia maisha yetu ili kumutumikia Yehova na kufanyia wengine mambo ya muzuri, tunajifanyia “jina la muzuri,” ao sifa ya muzuri, na Yehova atatukumbuka hata kisha kifo chetu. (Yobu 14:14, 15) Watu wa Yehova hawafanye sikukuu ya kuzaliwa kwao ao ya kuzaliwa kwa Yesu. Kwa kweli, sikukuu moja tu yenye Yesu aliambia wanafunzi wake waendelee kufanya ni Ukumbusho wa kifo chake.​—Luka 22:17-20; Waebrania 1:3, 4.

PASAKA YENYE WATU WANAONA KUWA YA KIKRISTO ILIANZA NAMNA GANI?

13, 14. Sikukuu ya Pasaka iko na uhusiano na nini?

13 Watu wengi wanaamini kama wakati wanafanya sikukuu ya Pasaka, wanafanya sikukuu ya kufufuka kwa Yesu. Lakini, ukweli ni kwamba, sikukuu ya Pasaka iko na uhusiano na Eostre, mungu wa kipagani wa mapambazuko na wa majira ya kuchipuka kwa majani, mwenye aliabudiwa na Wasaksoni wa zamani wa inchi ya Uingereza. Kitabu The Dictionary of Mythology kinafasiria kama ule mungu alikuwa pia mungu wa uwezo wa kuzaa. Desturi fulani za Pasaka ziko na uhusiano na ibada ya ule mungu. Kwa mufano, kitabu Encyclopædia Britannica kinasema kama mayai “imeonwa sana kuwa alama yenye kuonyesha uzima mupya na ufufuo.” Pia, katika ibada ya kipagani, sungura imetumiwa kwa muda murefu kama alama ya uwezo wa kuzaa. Ni wazi kama Pasaka yenye watu wanaona kuwa ya Kikristo haina uhusiano na ufufuo wa Yesu.

14 Je, Yehova anafurahi wakati anaona watu wanachanga desturi za dini ya uongo na ufufuo wa Mwana wake? Bila shaka hapana. (2 Wakorinto 6:17, 18) Kwa kweli, Yehova hakutuomba tufanye sikukuu ya kufufuka kwa Yesu.

TUSEME NINI JUU YA DESTURI FULANI ZA MAZIKO?

15. Juu ya nini Wakristo wa kweli wanakataa kujiingiza mu desturi fulani za maziko?

15 Kuko desturi mingi zenye kufanyika wakati mutu anakufa zenye Wakristo wa kweli wanapaswa kuepuka. Wakati mutu fulani anakufa, watu wanazoea kufanya mambo kama vile kuelekeza kichwa cha mwenye alikufa upande wa mangaribi, kuwasha moto ao mishumaa, na hata kukesha usiku wote. Zile desturi zote zinategemea imani ya kwamba watu hawakufe kabisa na kama wanaweza kusaidia ao kusumbua watu wazima. Zaidi ya ile, kisha maziko, watu wanafanya desturi fulani za kidini kwa ajili ya mutu mwenye alikufa. Siku yenye inafuata watu wanafanya michango ya feza. Desturi kama zile zinafanywa kisha miezi tatu, na kisha mwaka moja, na kisha zinafanywa kila mwaka. Kitabu People of Ceylon, kinasema kama “roho ya mutu mwenye alikufa inaweza kuwa na lazima ya kutendewa vile ili ikuwe na uhuru kwa muda fulani kutokana na hali ya kuteseka.” Kwa kuwa wafu ‘hawajue kitu chochote,’ wale wenye wanapenda kubakia katika upendo wa Mungu wanakataa desturi yoyote yenye kuchochea watu waogope na waheshimie ao wasaidie wafu.​—Muhubiri 9:5, 10.

NDOA ZENYE KUMUFURAHISHA MUNGU

16, 17. Tunapaswa kufikiria nini wakati tunapanga kufunga ndoa?

16 Siku ya ndoa ni siku ya furaha. Katika ulimwengu, ndoa zinafanywa mu njia mingi mbalimbali. Mara mingi watu hawafikirie kujua kama desturi mbalimbali za ndoa zilitoka wapi, kwa hiyo pengine hawawezi kujua kama desturi fulani zinatokana na imani za dini za kipagani. Lakini Wakristo wenye wako wanapanga kufunga ndoa wanahakikisha kama ndoa yao itamufurahisha Yehova. Ikiwa wanajifunza kuhusu namna desturi mbalimbali za ndoa zilianza, watafikia kukamata maamuzi ya muzuri.​—Marko 10:6-9.

17 Watu wengi wanaamini kama desturi fulani za ndoa zinaletea wenye wanafunga ndoa ‘bahati ya muzuri.’ (Isaya 65:11) Kwa mufano, katika sehemu fulani watu wanatupia bibi na bwana muchele ao vitu kama hivyo. Wanawaza kama kufanya vile kutaletea bibi na bwana watoto, furaha, na maisha ya murefu na kama kutawalinda na mambo ya mubaya. Lakini Wakristo wako waangalifu ili kuepuka kila desturi yenye inahusiana na dini ya uongo.​—Soma 2 Wakorinto 6:14-18.

18. Ni kanuni gani zingine za Biblia zenye kutumika kuhusu ndoa?

18 Wakristo wenye wataoana wanapenda siku ya ndoa yao ikuwe yenye furaha na yenye kuheshimika na pia ifurahishe kila mutu mwenye atakuwa pale. Watu wenye wanaalikwa ku karamu ya ndoa ya Kikristo hawatatumia maneno yenye kukosa heshima, yenye kuamusha hamu ya ngono, ao yenye itafanya bibi na bwana wenye kuwa pale wasikie haya. (Mezali 26:18, 19; Luka 6:31; 10:27) Ndoa ya Kikristo haichochee “mutu kujionyesha mali yake katika maisha.” (1 Yohana 2:16) Ikiwa uko unapanga kufanya ndoa, hakikisha kama mambo yenye utakumbuka juu ya ile ndoa itakuletea furaha.​—Ona Mafasirio Ingine ya 28.

NAMNA DESTURI YA KUINUA BILAURI NA KUVIGONGANISHA ILIANZA

19, 20. Desturi ya kuinua na kugonganisha bilauri ilianza namna gani?

19 Desturi fulani yenye kujulikana sana wakati wa karamu za ndoa na karamu zingine za kirafiki ni kuinua bilauri na kuvigonganisha. Wakati wa kugonganisha bilauri mutu mumoja anatakia watu wengine mambo ya muzuri na wengine wanajibu kwa kuinua bilauri yao. Namna gani Wakristo wanapaswa kuona ile desturi?

20 Kitabu International Handbook on Alcohol and Culture kinasema kama pengine desturi ya kuinua na kugonganisha bilauri inatokana na desturi ya kipagani ya zamani yenye ‘ilitia ndani kutolea miungu kinywaji kitakatifu.’ Walifanya vile kwa “kubadilishana maneno ya kutakia wengine mambo ya muzuri, ni kusema, kwa kufanya sala ya mufupi yenye maneno ‘maisha ya murefu!’ ao ‘ukuwe na afya ya muzuri!’” Wakati wa zamani, watu walizoea kuinua bilauri yao ili kuomba baraka kutoka kwa miungu yao. Lakini Yehova hatoake baraka vile.​—Yohana 14:6; 16:23.

“ENYI WENYE KUMUPENDA YEHOVA, MUCHUKIE MAMBO YA MUBAYA”

21. Ni aina gani zingine za sikukuu zenye Wakristo wanapaswa kuepuka?

21 Wakati unapenda kuamua kama utafanya sikukuu fulani ao hapana, ufikirie ni tabia ao mawazo gani yenye kuchochewa na ile sikukuu. Kwa mufano, sikukuu na karamu fulani kubwa-kubwa zinatia ndani dansi yenye kuchochea mwenendo muchafu, kunywa kupita kiasi, na hata uasherati. Sikukuu za vile zinaweza pia kuchochea watu wapende ngono ya wanaume kwa wanaume ao ya wanamuke kwa wanamuke ao kuchochea watu wapende sana taifa lao. Kama tunajiingiza mu sikukuu za vile, tunachukia kabisa mambo yenye Yehova anachukia?​—Zaburi 1:1, 2; 97:10; 119:37.

22. Ni nini inaweza kumusaidia Mukristo kuamua kama atafanya sikukuu fulani ao hapana?

22 Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu sana ili kuepuka sikukuu yoyote yenye inamushushia Mungu heshima. Mutume Paulo aliandika hivi: “Ikuwe munakula ao munakunywa ao munafanya jambo lingine lolote, mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Wakorinto 10:31; ona Mafasirio Ingine ya 29.) Ni kweli kwamba, haiko sikukuu zote njo ziko na uhusiano na uasherati, ibada ya uongo, ao upendo wa taifa. Kama sikukuu fulani haivunje kanuni za Biblia, tunapaswa kuamua peke yetu ikiwa tutaifanya ao hapana. Ni lazima pia tufikirie matokeo ya uamuzi wetu juu ya wengine.

UMUHESHIMIE YEHOVA KUPITIA MANENO NA MATENDO YAKO

23, 24. Namna gani tunaweza kueleza uamuzi wetu kuhusu sikukuu fulani kwa watu wa familia wenye hawako Mashahidi?

23 Pengine haufanyake tena sikukuu zenye kumushushia Yehova heshima. Lakini watu fulani wa familia yako wenye hawako Mashahidi wanaweza kuwaza kama hauwapendi tena ao haufurahie tena kuwa pamoja nao. Pengine wanawaza kama sikukuu njo wakati tu watu wa familia wanakuwa pamoja. Kwa hiyo, unaweza kufanya nini? Kuko njia mingi zenye unaweza kutumia ili kuwahakikishia kama unawapenda na kama unawaona kuwa wa maana. (Mezali 11:25; Muhubiri 3:12, 13) Unaweza kutafuta nafasi ingine na kuwaalika ili upitishe wakati pamoja nao.

24 Kama watu wa jamaa yako wanapenda kujua sababu gani haupendi tena kufanya sikukuu fulani, unaweza kutafuta habari mu vichapo vyetu na ku jw.org, zenye zinaweza kukusaidia uwafasirie sababu zenye kukuchochea usifanye zile sikukuu. Usizungumuze nao mu njia yenye itawafanya wajione kuwa hawajue kitu ao usiwakaze wakuwe na mawazo kama yako. Saidia watu wa familia yako waelewe kama kuko mambo mingi yenye ulifikiria na yenye ilikuchochea ukamate uamuzi wako. Ukuwe mwenye kutulia, na ‘maneno yako yakuwe yenye kupendeza sikuzote, yenye kukolezwa chumvi.’​—Wakolosai 4:6.

25, 26. Namna gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wapende kanuni za Yehova?

25 Ni jambo la lazima sisi wote tuelewe waziwazi sababu zetu za kipekee zenye zinatuchochea tusifanye sikukuu fulani. (Waebrania 5:14) Kusudi letu ni kumufurahisha Yehova. Na kama tuko wazazi, tunapaswa kukamata wakati wa kusaidia watoto wetu waelewe na wapende kanuni za Biblia. Wakati wanaanza kumuona Yehova kuwa mutu wa kweli kabisa, wao pia watapenda sana kumufurahisha.​—Isaya 48:17, 18; 1 Petro 3:15.

26 Yehova anafurahi wakati anaona namna tunafanya nguvu yetu yote ili kumuabudu mu njia safi na kwa unyoofu ao kwa uaminifu. (Yohana 4:23) Lakini watu wengi wanawaza kama mutu hawezi kuwa munyoofu kabisa katika ulimwengu huu wenye kukosa unyoofu. Je, ile ni kweli? Tuzungumuzie basi ile jambo mu sura yenye kufuata.

^ fu. 3 Unaweza kupata habari kuhusu sikukuu fulani mu Index des Publications Watch Tower, na mu kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova na ku jw.org.