Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 4

Juu ya Nini Tuheshimie Mamlaka?

Juu ya Nini Tuheshimie Mamlaka?

“Muheshimie watu wa namna zote, mupende ushirika muzima wa ndugu, mumuogope Mungu, mumuheshimie mufalme.”​—1 PETRO 2:17.

1, 2. (a) Ni muongozo wa nani tunapaswa kufuata? (b) Tutazungumuzia maulizo gani katika sura hii?

WAKATI ulikuwa mutoto, bila shaka kulikuwa wakati wenye wazazi wako walikuomba ufanye jambo fulani lenye haukupenda kufanya. Ulipenda wazazi wako na ulijua kama unapaswa kuwatii. Lakini, pengine haukupenda sikuzote kuwatii.

2 Tunajua kama Baba yetu, Yehova, anatupenda. Anatuhangaikia na anahakikisha kama tuko na kila kitu chenye tuko nacho lazima ili tufurahie maisha. Anatupatia muongozo wenye tuko nao lazima ili tupate matokeo ya muzuri. Wakati fulani, anatumia watu wengine ili kututolea muongozo. Tunapaswa kuheshimia mamlaka ya Yehova. (Mezali 24:21) Lakini juu ya nini wakati fulani haiko mwepesi kwetu kukubali muongozo? Juu ya nini Yehova anatuomba tufuate muongozo? Na namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia mamlaka?​—Ona Mafasirio Ingine ya 9.

JUU YA NINI HAIKO MWEPESI?

3, 4. Namna gani watu waliingia mu hali ya kukosa kukamilika? Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kukubali muongozo kutoka kwa wengine?

3 Sisi wanadamu, tuko na muelekeo wa kuasi. Ile imeonekana wazi tangu wakati mwanaume na mwanamuke wa kwanza, Adamu na Eva, walifanya zambi. Hata kama waliumbwa wakamilifu, waliasi mamlaka ya Mungu. Tangu ile wakati, wanadamu wote wanazaliwa wakiwa wenye hawakamilike. Hali yetu ya kukosa kukamilika ni sababu moja yenye inafanyaka ikuwe nguvu kwetu kukubali muongozo kutoka kwa Yehova na kwa wanadamu. Sababu ingine ni kwamba wanadamu wenye Yehova anatumia ili kututolea muongozo, wao pia ni wanadamu wenye hawakamilike.​—Mwanzo 2:15-17; 3:1-7; Zaburi 51:5; Waroma 5:12.

4 Juu hatukamilike, tuko na muelekeo wa kuwa na kiburi. Kiburi kinafanya ikuwe nguvu kwetu kukubali muongozo. Kwa mufano, katika Israeli ya zamani, Yehova alichagua Musa ili aongoze watu Wake. Mwanaume mwenye kuitwa Kora, mwenye alikuwa amemutumikia Yehova kwa miaka mingi, alifikia kuwa na kiburi na alimukosea Musa heshima sana. Hata kama Musa alikuwa anaongoza watu wa Mungu, hakuwa mutu mwenye kiburi. Kwa kweli, anazungumuziwa kuwa mutu munyenyekevu zaidi mwenye aliishi wakati huo. Lakini Kora alikataa muongozo wa Musa. Alichochea hata watu wengi sana wamuasi Musa kama yeye. Ni nini ilimupata Kora na watu wengine wenye waliasi? Waliuawa. (Hesabu 12:3; 16:1-3, 31-35) Mu Biblia, muko mifano mingi yenye kuonyesha kama ni hatari kuwa na kiburi.​—2 Mambo ya Nyakati 26:16-21; ona Mafasirio Ingine ya 10.

5. Namna gani watu fulani walitumia mamlaka yao mubaya?

5 Pengine umekwisha kusikia maneno, “Mamlaka inaharibu.” Tangu zamani, wanadamu wengi wametumia mamlaka yao mubaya. (Soma Muhubiri 8:9.) Kwa mufano, Sauli alikuwa mutu muzuri na munyenyekevu wakati Yehova alimuchagua ili akuwe mufalme wa Israeli. Lakini aliacha kiburi na wivu vikomae ndani ya moyo wake, na ile ilimuchochea amutese Daudi, mwanaume mwenye hakuwa na kosa. (1 Samweli 9:20, 21; 10:20-22; 18:7-11) Kisha, Daudi alikuwa mufalme, na alikuwa mumoja wa wafalme wazuri zaidi wa Israeli. Lakini, kisha muda fulani, hata Daudi alitumia mamlaka yake mubaya. Alilala na Bat-sheba, bibi ya mwanaume mwenye kuitwa Uria, na kisha alijaribu kuficha zambi yake kwa kutuma Uria aende kuuawa ku vita.​—2 Samweli 11:1-17.

JUU YA NINI TUNAHESHIMIA MAMLAKA YA YEHOVA?

6, 7. (a) Upendo wetu kwa Yehova unatuchochea kufanya nini? (b) Ni nini itatusaidia kutii hata wakati haiko mwepesi kufanya vile?

6 Tunaheshimia muongozo wa Yehova juu tunamupenda. Kwa kuwa tunamupenda Yehova kuliko kitu kingine ao mutu mwingine yeyote, tunapenda kumufurahisha. (Soma Mezali 27:11; Marko 12:29, 30.) Tangu wakati wanadamu wa kwanza Adamu na Eva walikuwa mu bustani ya Edeni, Shetani amependa watu wakuwe na mashaka juu ya mamlaka ya Yehova. Ibilisi anapenda tufikiri kama Yehova hana haki ya kutuambia jambo la kufanya. Lakini tunajua kama huo ni uongo. Tunaunga mukono maneno haya: “Unastahili, Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.”​—Ufunuo 4:11.

7 Wakati ulikuwa mutoto, bila shaka uliombwa kutii wazazi wako hata wakati wenye haukupenda kufanya vile. Vilevile, tukiwa watumishi wa Yehova, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kutii. Lakini, juu tunamupenda Yehova na kumuheshimia, tunafanya nguvu yetu yote ili kumutii. Yesu alituachia mufano. Alimutii Yehova hata wakati haikuwa mwepesi ao hata wakati alikuwa mu hali yenye haifae. Njo maana angeweza kumuambia Baba yake hivi: “Mapenzi yako ndiyo yatendeke, hapana yangu.”​—Luka 22:42; ona Mafasirio Ingine ya 11.

8. Ni njia gani fulani Yehova anatumia ili kutuongoza? (Ona kisanduku “ Sikiliza Mashauri.”)

8 Leo, Yehova anatumia njia mbalimbali ili kutuongoza. Kwa mufano, ametupatia Biblia. Ametupatia pia wazee wa kutaniko. Tunaonyesha kama tunaheshimia mamlaka ya Yehova wakati tunaheshimia wale wenye anatumia ili kutuongoza. Kama tunakataa musaada wao, ni kama vile tunamukataa Yehova. Wakati Waisraeli walimukataa Musa, Yehova alikamata ile jambo kwa uzito. Aliona kama ni yeye njo wamekataa.​—Hesabu 14:26, 27; ona Mafasirio Ingine ya 12.

9. Namna gani upendo utatuchochea kufuata muongozo?

9 Wakati tunaheshimia mamlaka, ile inaonyesha pia kama tunapenda ndugu na dada zetu. Waza juu ya jambo hili: Wakati kunakuwa musiba wa asili, mara mingi kikundi cha kutoa musaada kinatumika pamoja ili waweze kuokoa watu wengi zaidi kadiri inawezekana. Ili kikundi hicho kitumike muzuri, mutu fulani anapaswa kukipanga na kila mutu wa kikundi hicho anapaswa kufuata muongozo. Lakini, ni nini itatokea ikiwa mutu mumoja anakataa kufuata muongozo na kufanya tu mambo yenye anapenda? Hata kama iko na nia ya muzuri, kukataa kufuata muongozo kunaweza kuletea wenzake magumu, pengine hata kuwafanya waumie sana. Vilevile, kama tunakataa kufuata muongozo kutoka kwa Yehova na kutoka kwa wale wenye amepatia mamlaka fulani, wengine wanaweza kuteseka. Lakini wakati tunamutii Yehova, tunaonyesha kama tunapenda ndugu zetu na kama tunaheshimia mupango wa Yehova.​—1 Wakorinto 12:14, 25, 26.

10, 11. Tutazungumuzia nini sasa?

10 Kila jambo lenye Yehova anatuomba kufanya ni kwa faida yetu. Wakati tunaheshimia mamlaka mu familia, mu kutaniko, na wakati wakubwa wa serikali wanatuomba kufanya jambo fulani, sisi wote tutapata faida.​—Kumbukumbu la Torati 5:16; Waroma 13:4; Waefeso 6:2, 3; Waebrania 13:17.

11 Kuelewa ni juu ya nini Yehova anatuomba tuheshimie wengine kunaweza kutusaidia tufanye vile. Tuzungumuzie mingi zaidi juu ya namna tunaweza kuonyesha heshima mu sehemu tatu za maisha yetu.

KUHESHIMIA MAMLAKA MU FAMILIA

12. Bwana anaweza kufanya nini ili kuonyesha kama anaheshimia mamlaka?

12 Yehova alianzisha familia na alipatia kila mutu mu familia daraka fulani. Wakati kila mutu mu familia anaelewa mambo yenye Yehova anamutazamia afanye, mupango wa familia utatumika muzuri na kila mutu mu familia atapata faida. (1 Wakorinto 14:33) Yehova amemufanya bwana kuwa kichwa cha familia. Ile inamaanisha kuwa Yehova anatazamia bwana ahangaikie na kuongoza bibi na watoto wake kwa upendo. Kwa hiyo, bwana anapaswa kutoa hesabu kwa Yehova kufuatana na namna anawahangaikia. Bwana mwenye kuwa Mukristo ni mwema na mwenye upendo na anatendea familia yake kama vile Kristo anatendea kutaniko. Wakati bwana anafanya vile, anaonyesha kama anamuheshimia Yehova.​—Waefeso 5:23; ona Mafasirio Ingine ya 13.

Wakati anahangaikia familia yake, baba Mukristo anamuiga Kristo

13. Namna gani bibi anaweza kuonyesha kama anaheshimia mamlaka?

13 Bibi Mukristo iko pia na daraka la maana na lenye kuheshimika. Anasaidia bwana yake kadiri anatumika kwa bidii ili kuwa kichwa muzuri wa familia. Yeye pamoja na bwana yake, wako na daraka la kuzoeza watoto. Njia moja yenye anatumia ili kufundisha watoto wake wakuwe wenye kuonyesha heshima ni mufano wake mwenyewe. (Mezali 1:8) Anaheshimia bwana yake na anaunga mukono maamuzi yake. Hata kama hakubaliane na bwana yake juu ya jambo fulani, anaeleza mawazo yake kwa upole na heshima. Wakati mwanamuke Mukristo ni mwenye kuolewa na mutu mwenye haiko Shahidi, iko na magumu ya pekee yenye anapambana nayo. Lakini ikiwa anaendelea kutendea bwana yake kwa upendo na kwa heshima, pengine siku moja bwana yake pia atapenda kumujua Yehova na kumuabudu.​—Soma 1 Petro 3:1.

14. Watoto wanaweza kufanya nini ili kuonyesha kama wanaheshimia mamlaka?

14 Yehova anaona watoto kuwa wa maana sana, na zaidi sana wako na lazima ya kulindwa na kupewa muongozo. Wakati watoto wanatii wazazi wao, ile inafurahisha wazazi wao. Na jambo la maana zaidi, wakati wanatii wanaonyesha kama wanamuheshimia Yehova na wanamufurahisha. (Mezali 10:1) Mu familia mingi, watoto wanalelewa tu na muzazi mumoja. Ile inaweza kuwa jambo ngumu sana kwa muzazi huyo na kwa watoto. Lakini wakati watoto wanatii na kuunga mukono mama yao ao baba yao, maisha ya familia inaweza kuwa muzuri zaidi. Hata hali ikuwe namna gani, hakuna familia yenye kukamilika. Lakini kila familia inaweza kuwa na furaha ikiwa kila mutu mu familia anafuata muongozo wa Yehova. Ile inamuletea Yehova heshima, Mwenye alianzisha familia zote.​—Waefeso 3:14, 15.

KUHESHIMIA MAMLAKA MU KUTANIKO

15. Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunaheshimia mamlaka mu kutaniko?

15 Yehova anatuongoza kupitia kutaniko la Kikristo, na amepatia Yesu mamlaka yote juu ya kutaniko. (Wakolosai 1:18) Yesu pia amepatia “mutumwa muaminifu na mwenye busara” daraka la kuhangaikia watu wa Mungu wenye kuwa hapa ku dunia. (Matayo 24:45-47) Leo, “mutumwa muaminifu na mwenye busara” njo Baraza Lenye Kuongoza. Baraza Lenye Kuongoza linatutolea kila kitu chenye tuko nacho lazima kwa wakati wenye kufaa ili kutusaidia tuendelee kuwa na imani yenye nguvu. Wazee, watumishi wa huduma, na waangalizi wa muzunguko wanategemeza makutaniko yenye kuwa mu dunia yote na wanafuata muongozo wa Baraza Lenye Kuongoza. Ndugu hao wote wako na daraka la kutuhangaikia. Wanatoa hesabu kwa Yehova kufuatana na namna wanatimiza daraka hilo. Kwa hiyo, wakati tunaheshimia wanaume hao, tunamuheshimia Yehova.​—Soma 1 Watesalonike 5:12; Waebrania 13:17; ona Mafasirio Ingine ya 14.

16. Juu ya nini tunaweza kusema kama wazee na watumishi wa huduma wanawekwa na roho takatifu?

16 Wazee na watumishi wa huduma wanasaidia ndugu na dada mu kutaniko wabakie waaminifu na waendelee kuwa katika umoja. Ni kweli kwamba, ni wanadamu wenye hawakamilike kama sisi. Sasa, namna gani wanachaguliwa? Ndugu hao wanapaswa kutimiza sifa zenye kuwa mu Biblia. (1 Timoteo 3:1-7, 12; Tito 1:5-9) Yehova alitumia roho yake takatifu ili kusaidia waandikaji wa Biblia wafasirie sifa hizo. Wazee wanasali kwa Yehova ili awapatie roho yake takatifu wakati wanachunguza ni nani anapaswa kuwekwa kuwa muzee ao mutumishi wa huduma. Ni wazi kuwa, makutaniko yote iko chini ya muongozo wa Yesu na Yehova. (Matendo 20:28) Wanaume wenye wamewekwa ili kututegemeza na kutuhangaikia ni zawadi kutoka kwa Mungu.​—Waefeso 4:8.

17. Ili kuonyesha heshima, dada anapaswa kufanya nini wakati fulani?

17 Wakati fulani kutaniko linaweza kukosa muzee ao mutumishi wa huduma ili kutimiza kazi fulani. Ndugu wengine wenye kubatizwa wanaweza kuendelea kusaidia, lakini ikiwa hakuna hata ndugu mumoja, dada anaweza kutimiza kazi yenye kwa kawaida inatimizwa na ndugu mwenye kubatizwa. Mu ile hali, anapaswa kuvaa kitu fulani ili kufunika kichwa chake, pengine kitambaa ao kofia (chapeau). (1 Wakorinto 11:3-10) Kwa kufanya vile, anaonyesha kama anaheshimia mupango wa Yehova kuhusu ukichwa, mu familia na mu kutaniko.​—Ona Mafasirio Ingine ya 15.

KUHESHIMIA WAKUBWA WA SERIKALI

18, 19. (a) Waroma 13:1-7 inatufundisha nini? (b) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia serikali?

18 Leo, Yehova anaruhusu serikali zikuwe na mamlaka fulani, na tunapaswa kuwaheshimia. Wanapanga inchi na maeneo mwenye watu wanaishi ili waweze kutumika muzuri na wanatolea watu kazi zenye wako nazo lazima. Wakristo wanatii muongozo wenye kuwa mu Waroma 13:1-7. (Soma.) Tunaheshimia “mamlaka zenye kuwa kubwa” na tunatii sheria za inchi ao eneo kwenye tunaishi. Sheria hizo zinaweza kuhusu familia yetu, biashara, ao vitu vyetu vya kimwili. Kwa mufano, tunalipa kodi (ao, taxes) na kutoa habari zenye serikali inatuomba. Lakini tunapaswa kufanya nini ikiwa serikali inatuomba kufanya jambo fulani lenye linapingana na sheria za Mungu? Mutume Petro alisema hivi: “Tunapaswa kumutii Mungu kuwa mutawala kuliko wanadamu.”​—Matendo 5:28, 29.

19 Ikiwa ni lazima tukuwe mbele ya mukubwa fulani wa serikali, kama vile muamuzi ao polisi, kila mara tunapaswa kuwa wenye heshima. Wakristo wenye ni vijana wanaheshimia walimu wao na wafanyakazi wengine ku masomo. Ku kazi, tunaheshimia mukubwa wetu wa kazi, hata kama wafanyakazi wengine hawafanye vile. Wakati tunafanya vile, tunaiga mutume Paulo, mwenye aliheshimia wenye mamlaka hata kama wakati fulani haikuwa mwepesi. (Matendo 26:2, 25) Hata kama wengine hawatutendee muzuri, tunaendelea kuwaonyesha heshima.​—Soma Waroma 12:17, 18; 1 Petro 3:15.

20, 21. Ni mambo gani ya muzuri yenye inaweza kutokea wakati tunaheshimia wengine?

20 Mu dunia yote, watu wanaendelea kupunguza tabia yao ya kuonyesha wengine heshima. Lakini watu wa Yehova wako tofauti. Tumeazimia kuheshimia kila mutu. Tunafuata muongozo huu wa mutume Petro: “Muheshimie watu wa namna zote.” (1 Petro 2:17) Wakati tunaheshimia wengine, wanaona hilo. Yesu alituambia hivi: “Muache mwangaza wenu uangaze mbele ya watu, ili waone matendo yenu ya muzuri na wamutukuze Baba yenu.”​—Matayo 5:16.

21 Wakati tunaonyesha heshima mu familia yetu, mu kutaniko letu, na mu sehemu zingine za maisha yetu, mufano wetu unaweza kuchochea wengine watamani kujifunza juu ya Yehova. Na wakati tunaonyesha wengine heshima, tunaonyesha kama tunamuheshimia Yehova mwenyewe. Kwa kufanya vile, tunamufurahisha Yehova na tunaonyesha kama tunamupenda.