Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 9

‘Kimbia Uasherati!’

‘Kimbia Uasherati!’

“Kwa hiyo, muue viungo vya mwili wenu vyenye kuwa katika dunia kuhusiana na uasherati, uchafu, tamaa kubwa ya ngono yenye haizuiliwe, tamaa yenye kuumiza, na pupa, yenye kuwa ibada ya sanamu.”​—WAKOLOSAI 3:5.

1, 2. Namna gani Balaamu alijaribu kuletea hatari watu wa Yehova?

MUVUAJI wa samaki anaenda nafasi kwenye anaweza kupata aina ya samaki yenye anapenda kukamata. Anachagua chambo cha kutumia na anatupa ndoano mu maji. Anangojea kwa uvumilivu, na wakati samaki inakula chambo anaikamata kupitia ndoano na kuileta ku inchi kavu.

2 Vilevile, watu wanaweza kunaswa. Kwa mufano, Waisraeli walikuwa karibu kuingia mu Inchi ya Ahadi wakati walipiga kambi katika maeneo tambarare ya Moabu. Mufalme wa Moabu aliahidi mwanaume mwenye kuitwa Balaamu kama atamupatia feza mingi ikiwa analaani Waisraeli. Mwishowe, Balaamu alipata njia yenye ingefanya Waisraeli wajiletee laana wao wenyewe. Alichagua chambo kwa uangalifu. Alituma vijana wanamuke Wamoabu mu kambi ya Waisraeli ili washawishi wanaume Waisraeli.​—Hesabu 22:1-7; 31:15, 16; Ufunuo 2:14.

3. Namna gani Waisraeli walinaswa mu mutego wa Balaamu?

3 Chambo chenye Balaamu alichagua kilifanya kazi? Ndiyo. Maelfu ya wanaume Waisraeli walifanya “uasherati na mabinti wa Moabu.” Walianza pia kuabudu miungu ya uongo, kutia ndani Baali wa Peori, mungu mwenye kuchukiza wa ngono. Matokeo ni kuwa, Waisraeli 24 000 walikufa kwenye mupaka wa Inchi ya Ahadi.​—Hesabu 25:1-9.

4. Juu ya nini maelfu ya Waisraeli walifanya uasherati?

4 Juu ya nini Waisraeli wengi vile walinaswa mu mutego wa Balaamu? Walikuwa wanafikiria tu kupata furaha yao ya kichoyo, na walisahau mambo yenye Yehova alikuwa amewafanyia. Waisraeli walikuwa na sababu mingi za kuwa washikamanifu kwa Mungu. Alikuwa amewakomboa kutoka mu utumwa wa Misri, aliwapatia chakula mu jangwa, na aliwafikisha kwa usalama ku mupaka wa Inchi ya Ahadi. (Waebrania 3:12) Lakini, walishawishiwa kufanya uasherati. Mutume Paulo aliandika hivi: “Na tusifanye uasherati, kama vile wamoja kati yao walifanya uasherati, . . . wakaanguka.”​—1 Wakorinto 10:8.

5, 6. Mambo yenye ilifanyika mu maeneo tambarare ya Moabu inaweza kutufundisha nini?

5 Ulimwengu mupya uko karibu sana. Kwa hiyo, kwa njia fulani tuko kama Waisraeli ku mupaka wa Inchi ya Ahadi. (1 Wakorinto 10:11) Leo, katika ulimwengu mwenye tunaishi, watu wanatawaliwa sana na ngono kuliko vile Wamoabu walikuwa. Ni mwepesi watu wa Yehova wapatwe na ile jambo. Kwa kweli, chambo chenye Ibilisi anatumia kunasa watu wengi zaidi ni uasherati.​—Hesabu 25:6, 14; 2 Wakorinto 2:11; Yuda 4.

6 Ujiulize hivi, ‘Nitachagua kupata furaha ya kichoyo yenye itafanya muda mufupi tu, ao nitachagua kuishi milele kwa furaha mu ulimwengu mupya?’ Hauone kama ni muzuri kujikaza sana kutii amri ya Yehova: “Mukimbie uasherati”?​—1 Wakorinto 6:18.

UASHERATI NI NINI?

7, 8. Uasherati ni nini? Juu ya nini ile ni jambo nzito?

7 Leo, watu wengi hawana haya na wanazarau waziwazi sheria za Mungu juu ya ngono. Mu Biblia, uasherati ni ngono kati ya watu wawili wenye hawaoane kulingana na Maandiko. Inatia ndani ngono ya wanaume kwa wanaume ao ngono ya wanamuke kwa wanamuke na ngono kati ya watu na wanyama. Ngono inaweza kufanywa kwa kutumia viungo vya uzazi, kupitia kinywa, mukundu, ao kugusa viungo vya uzazi vya mutu mwingine ili kuamusha hamu ya ngono.​—Ona Mafasirio Ingine ya 23.

8 Biblia inaonyesha wazi kama mwenye anaendelea kufanya uasherati, hawezi kubakia mu kutaniko. (1 Wakorinto 6:9; Ufunuo 22:15) Zaidi ya ile, mutu mwenye kufanya uasherati anapoteza heshima yake mwenyewe na watu wengine hawawezi kumuaminia. Sikuzote uasherati unaleta matatizo. Kwa kawaida unafanya mutu asumbuliwe na zamiri na mara mingi unatokeza mimba yenye mutu hapendi, matatizo mu ndoa, magonjwa, na hata kifo. (Soma Wagalatia 6:7, 8.) Ikiwa mutu anachukua wakati wa kufikiria matokeo ya uasherati, pengine hawezi kupenda kuwa mwasherati. Lakini mara mingi mutu anafikiriaka tu kutimiza tamaa yake mwenyewe wakati anakamata hatua ya kwanza yenye kuongoza ku uasherati. Mara mingi ile hatua ni pornografia.

PORNOGRAFIA​—HATUA YA KWANZA

9. Juu ya nini pornografia ni yenye hatari?

9 Pornografia iko na kusudi la kuamusha tamaa ya ngono. Leo, pornografia inapatikana fasi yote​—mu magazeti, vitabu, muziki, vipindi vya televizyo, na pia ku Enternete. Watu wengi wanawaza kama pornografia haina hatari, lakini kwa kweli ni yenye hatari sana. Inaweza kufanya mutu akuwe mutumwa wa ngono na akomalishe tamaa zenye kupita mipaka. Wakati tu mutu anakuwa na tabia ya kuangalia pornografia, anaingia mu njia yenye inaweza kuongoza kwenye tabia ya kupiga punyeto (ao, kugusa-gusa viungo vya uzazi ili kuamusha hamu ya ngono), matatizo mu ndoa, na hata kufanya ndoa ivunjike.​—Waroma 1:24-27; Waefeso 4:19; ona Mafasirio Ingine ya 24.

Ni jambo lenye hekima tukuwe waangalifu wakati tunatumia Enternete

10. Namna gani kanuni yenye kuwa mu andiko la Yakobo 1:14, 15 inatusaidia kuepuka uasherati?

10 Ni jambo la maana tuelewe namna uasherati unaweza kutuvutia. Fikiria onyo hili lenye kuwa mu andiko la Yakobo 1:14, 15: “Kila mutu anajaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe. Kisha tamaa, wakati imepata mimba, inazaa zambi; na zambi, wakati imetimizwa, inaleta kifo.” Kwa hiyo, wakati mawazo ya mubaya inaingia mu akili yako, achana nayo bila kukawia. Ikiwa unaona picha chafu bila kutazamia, angalia pembeni! Funga ordinatere, ao badilisha programu yenye uko unafuata. Usiruhusu tamaa za mubaya mu maisha yako. Kama unaziruhusu, zinaweza kuwa zenye nguvu sana hivi kwamba inaweza kuwa nguvu kuzizuia.​—Soma Matayo 5:29, 30.

11. Namna gani Yehova anaweza kutusaidia wakati tuko na mawazo ya mubaya?

11 Yehova anatujua muzuri zaidi kuliko vile tunajijua sisi wenyewe. Kwa hiyo, anajua ni kwa kiasi gani hatukamilike. Lakini anajua pia kama tunaweza kupata ushindi juu ya tamaa za mubaya. Yehova anatuambia hivi: “Kwa hiyo, muue viungo vya mwili wenu vyenye kuwa katika dunia kuhusiana na uasherati, uchafu, tamaa kubwa ya ngono yenye haizuiliwe, tamaa yenye kuumiza, na pupa, yenye kuwa ibada ya sanamu.” (Wakolosai 3:5) Hata kama haiko mwepesi kufanya vile, Yehova anatuonyesha uvumilivu na atatusaidia. (Zaburi 68:19) Ndugu mumoja kijana aliangukia mu tabia ya kuangalia pornografia na kupiga punyeto. Marafiki wake wa ku masomo waliona ile mambo kuwa ya kawaida wakati mutu iko anakomaa, lakini alisema hivi: “Iliharibisha zamiri yangu, na nilianza kuishi maisha ya uasherati.” Alitambua kama alipaswa kuzuia tamaa zake, na kwa musaada wa Yehova, aliweza kuachana na tabia yake. Kama uko na mawazo machafu, umuombe Yehova “nguvu zenye kupita zile za kawaida” ili uendelee kuwa na mawazo yenye kuwa safi.​—2 Wakorinto 4:7; 1 Wakorinto 9:27.

12. Juu ya nini tunapaswa ‘kulinda moyo wetu’?

12 Sulemani aliandika hivi: “Linda moyo wako kuliko vitu vyote vyenye unalinda, kwa maana ni mule munatoka chemchemi za uzima.” (Mezali 4:23) “Moyo” wetu ni mutu mwenye tuko kwa ndani, ule mutu mwenye Yehova anaona. Mambo yenye tunaangalia inaweza kutuchochea kwa njia yenye nguvu. Yobu, mutu muaminifu, alisema hivi: “Nimefanya agano pamoja na macho yangu. Basi namna gani ninaweza kumukazia bikira uangalifu kwa njia yenye haifae?” (Yobu 31:1) Kama Yobu, tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu mambo yenye tunaangalia na kufikiria. Na kama muandikaji mumoja wa zaburi, tunasali hivi: “Geuzia mbali macho yangu ili yasiangalie mambo yenye hayana mafaa yoyote.”​—Zaburi 119:37.

DINA ALIKAMATA UAMUZI WENYE HAUNA HEKIMA

13. Dina alichagua marafiki wa namna gani?

13 Marafiki wetu wanaweza kutuchochea sana, ikuwe mu njia ya muzuri ao ya mubaya. Kama unachagua marafiki wenye kufuata kanuni za Mungu, wanaweza kukusaidia ufanye pia vile. (Mezali 13:20; Soma 1 Wakorinto 15:33.) Mambo yenye ilimufikia Dina inaweza kutusaidia kuona kama ni jambo la maana sana kuwa waangalifu wakati tunachagua marafiki. Alikuwa mumoja wa watoto wanamuke wa Yakobo, kwa hiyo alikomalia mu familia yenye ilimuabudu Yehova. Dina hakuwa na mwenendo muchafu, lakini alifanya urafiki wa karibu pamoja na vijana wanamuke Wakanaani wenye hawakumuabudu Yehova. Wakanaani walikuwa na mawazo yenye ilikuwa tofauti sana na ya watu wa Mungu juu ya ngono na walijulikana kuwa watu wenye mwenendo muchafu. (Mambo ya Walawi 18:6-25) Wakati Dina alikuwa na marafiki zake, alikutana na kijana mwanaume Mukanaani mwenye kuitwa Shekemu. Ule kijana mwanaume alimutamani. Shekemu alionwa kuwa kijana mwanaume “mwenye kuheshimiwa zaidi” mu familia yao. Lakini hakumupenda Yehova.​—Mwanzo 34:18, 19.

14. Ni nini ilimupata Dina?

14 Shekemu alifanya jambo lenye lilionekana kuwa la kawaida na lenye kukubalika kwake. Kwa kuwa alimutamani Dina, ‘alimukamata’ na “kumulala kinguvu.” (Soma Mwanzo 34:1-4.) Ile kosa ilikuwa njo mwanzo wa matukio yenye kufuatana yenye iliumiza Dina na familia yake yote.​—Mwanzo 34:7, 25-31; Wagalatia 6:7, 8.

15, 16. Tunaweza kufanya nini ili kuwa na hekima?

15 Haiko lazima tufanye makosa kama ya Dina ili tuelewe kama kanuni za Yehova kuhusu mwenendo ni za muzuri kwetu. “Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.” (Mezali 13:20) Ujiwekee muradi wa kuelewa “njia yote ya mambo ya muzuri,” na utaepuka kujiletea wewe mwenyewe maumivu na mateso.​—Mezali 2:6-9; Zaburi 1:1-3.

16 Tunaweza kuwa na hekima kwa kujifunza Neno la Mungu, kusali kwake mbele ya kukamata maamuzi, na kufuata mashauri ya muzuri kutoka kwa mutumwa muaminifu na mwenye busara. (Matayo 24:45; Yakobo 1:5) Ni kweli kwamba, kama vile unajua, sisi wote ni wazaifu na hatukamilike. (Yeremia 17:9) Lakini utafanya nini kama mutu fulani anakuonya kama uko mu hatari ya kufanya uasherati? Utakasirika, ao utakubali kwa upole musaada wake?​—2 Wafalme 22:18, 19.

17. Toa mufano wenye kuonyesha namna mashauri ya Mukristo mwenzetu inaweza kutusaidia.

17 Kwa mufano, fikiria hali hii. Nafasi kwenye Dada fulani anatumikia, mwanaume mumoja anaanza kupendezwa naye kwa njia ya pekee na anamuomba waende pamoja ili kufanya matembezi. Ule mwanaume hamutumikie Yehova, lakini anaonekana kuwa mutu muzuri na mwema. Dada mwingine anawaona wakiwa pamoja na kisha anamupatia mashauri juu ya ile jambo. Ule dada wa kwanza atatenda namna gani? Atajitetea, ao ataona ile mashauri kuwa yenye hekima? Pengine ule dada anamupenda Yehova na anapenda kufanya mambo ya muzuri. Lakini kama anaendelea kufanya matembezi na ule mwanaume, je, iko ‘anakimbia uasherati’ ao iko “anategemea moyo wake mwenyewe”?​—Mezali 22:3; 28:26; Matayo 6:13; 26:41.

UJIFUNZE KUTOKANA NA MUFANO WA YOSEFU

18, 19. Fasiria namna Yosefu alikimbia uasherati.

18 Wakati alikuwa kijana, Yosefu alikuwa mutumwa katika Misri. Kila siku, bibi ya bwana wake alimuomba wafanye ngono, lakini Yosefu alijua kama ni mubaya kufanya vile. Yosefu alimupenda Yehova na alipenda kumufurahisha. Kwa hiyo, kila wakati ule mwanamuke alijaribu kumushawishi, Yosefu alikataa. Kwa sababu alikuwa mutumwa, hangeweza kumuacha bwana wake. Siku moja wakati bibi ya bwana wake alijaribu kumukaza ili afanye naye ngono, ‘alikimbilia inje.’​—Soma Mwanzo 39:7-12.

19 Hali ingekuwa tofauti kabisa ikiwa Yosefu angeacha mawazo machafu ikuwe mu akili yake ao ikiwa angeendelea kuwaza-waza ule mwanamuke. Lakini Yosefu aliona urafiki wake na Yehova kuwa wa maana sana kuliko jambo lingine lolote. Aliambia ule mwanamuke hivi: “Bwana wangu hakunikataza kitu chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe uko bibi yake. Kwa hiyo ninaweza namna gani kufanya ubaya huu mukubwa na kwa kweli nimutendee Mungu zambi?”​—Mwanzo 39:8, 9.

20. Ni nini inaonyesha kama Yehova alifurahia uaminifu wa Yosefu?

20 Hata kama Yosefu alikuwa mbali na familia yake na mbali na kwao, sikuzote alikuwa muaminifu kwa Mungu, na Yehova alimubariki. (Mwanzo 41:39-49) Yehova alifurahia uaminifu wa Yosefu. (Mezali 27:11) Inaweza kuwa nguvu kupinga uasherati. Lakini kumbuka hii maneno: “Enyi wenye kumupenda Yehova, muchukie mambo ya mubaya. Analinda uzima wa washikamanifu wake; anawaokoa katika mukono wa waovu.”​—Zaburi 97:10.

21. Namna gani ndugu mumoja kijana alimuiga Yosefu?

21 Kila siku, watu wa Yehova wanaonyesha kwa uhodari kama ‘wanachukia mambo ya mubaya’ na kama ‘wanapenda mambo ya muzuri.’ (Amosi 5:15) Hata kama uko na miaka gani, unaweza kuwa muaminifu kwa Yehova. Ku masomo, imani ya ndugu mumoja kijana ilijaribiwa. Kijana mumoja mwanamuke alimuambia kama atalala naye kama anamusaidia wakati wa mashindano ya hesabu. Ule ndugu alifanya nini? Alitenda kama Yosefu. Anasema hivi: “Nilikataa ombi lake mara moja. Kwa kubakia muaminifu, nililinda heshima yangu na nilifanya wengine waendelee kuniheshimia.” ‘Furaha’ yoyote ya muda yenye kuletwa na uasherati, mara mingi inaongoza kwenye maumivu ya moyo. (Waebrania 11:25) Sikuzote, kumutii Yehova kunaleta furaha ya kweli.​—Mezali 10:22.

KUBALI MUSAADA WA YEHOVA

22, 23. Namna gani Yehova anaweza kutusaidia hata kama tunafanya zambi nzito?

22 Shetani atajaribu kutumia uasherati ili kutunasa, na inaweza kuwa nguvu kabisa kuepuka ile jaribu. Kila mumoja wetu anaweza kuwa na mawazo ya mubaya wakati fulani. (Waroma 7:21-25) Yehova anaelewa ile jambo na anakumbuka kama “tuko mavumbi.” (Zaburi 103:14) Kwa hiyo, itakuwa namna gani ikiwa Mukristo anafanya zambi nzito ya uasherati? Je, hakuna tena tumaini? Hapana. Ikiwa Mukristo huyo anatubu kikweli, Yehova atamusaidia. Mungu iko “tayari kusamehe.”​—Zaburi 86:5; Yakobo 5:16; soma Mezali 28:13.

23 Yehova anatupatia pia “zawadi katika wanadamu,” ni kusema, wazee wenye kutupenda na kutuhangaikia. (Waefeso 4:8, 12; Yakobo 5:14, 15) Alitupatia wazee ili watusaidie kuwa tena na uhusiano wa muzuri pamoja naye.​—Mezali 15:32.

TUMIA “AKILI YA MUZURI”

24, 25. Namna gani “akili ya muzuri” inaweza kutusaidia kuepuka uasherati?

24 Ili tuweze kukamata maamuzi ya muzuri, ni jambo la lazima tuelewe kama sheria za Yehova zinatuletea faida sana. Hatupendi kuwa kama ule kijana mwanaume mwenye kuzungumuziwa mu Mezali 7:6-23. Alikosa “akili ya muzuri,” kwa hiyo alinaswa mu mutego wa uasherati. Kuwa na akili ya muzuri ni zaidi ya kuwa na akili yenye mutu anazaliwa nayo. Wakati tuko na akili ya muzuri, tunajikaza kuelewa mawazo ya Mungu na kutenda kulingana nayo mu maisha yetu. Kumbuka hii maneno yenye hekima: “Kila mutu mwenye anapata akili ya muzuri anajipenda mwenyewe. Kila mutu mwenye anapendezwa sana na utambuzi atapata mafanikio.”​—Mezali 19:8.

25 Uko hakika kabisa kama kanuni za Mungu ni za muzuri? Unaamini kabisa kama kuzifuata kutakuletea furaha? (Zaburi 19:7-10; Isaya 48:17, 18) Kama haujakuwa hakika, kumbuka mambo yote ya muzuri yenye Yehova amekufanyia. “Muonje na muone kwamba Yehova ni mwema.” (Zaburi 34:8) Utafikia kuona kama kadiri unafanya vile, ni vile utamupenda Mungu zaidi. Penda mambo yenye anapenda na uchukie mambo yenye anachukia. Ujaze mawazo ya muzuri mu akili yako​—mambo ya kweli, ya haki, yenye kuwa safi, yenye kustahili kupendwa, na tabia za muzuri. (Wafilipi 4:8, 9) Tunaweza kuwa kama Yosefu mwenye alipata faida kutokana na hekima ya Yehova.​—Isaya 64:8.

26. Tutazungumuzia nini mu sura zenye kufuata?

26 Ikuwe haujaoa ao kuolewa, ao uko mwenye kuoa ao kuolewa, Yehova anapenda ufurahie maisha na ukuwe na furaha. Sura mbili zenye kufuata ziko na habari zenye zinaweza kutusaidia kufanya ndoa yetu ikuwe na furaha.